PETE YA KIKE Sehemu Ya 8 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Saturday, February 1, 2020

PETE YA KIKE Sehemu Ya 8





Suria aliegemeza baiskeli yake kwenye geti lao la mabati kisha akawa anakimbilia kule walipo achana na shaimati, au shamimu kama anavyo mjua yeye. Lakini wakati huo shamimu anamuangalia tu huku akicheka.... Suria alikua anawahi huku akiwaza maneno alio yasema shaimati kua
"hapana... Twende leo, kesho tunarudi rasmi kuwaaga wazazi"
Aliyakumbuka maneno ya shamimu, na shamimu akatokea mbele yake kama vile hakumuona.....
"dada? ... Dada?... Dada.?... Nipo tayari, twende sasa"
Shaimati alifurahi sana huku akicheka katika moyo wake,... Leo ikiwa ni siku yao ya sita toka siku wanaingia duniani,... Lakini shaimati anailazimisha safari ili suria asije kupata kinga ya pete...

Sasa huku kwa maimati kakaa kwa kutulia akivizia pete ivuliwe, ili ampe suria aivae... Na kesho wakiondoka waondoke bila mwanaume msafi, lakini bila kujua leo shaima anaondoka na suria... Mwanaume aliopendwa na jini mwenzie....

ENDELEA.......

Kila kiumbe kilicho umbwa kwa mikono ya Mwenyezi Mungu hapa duniani, kina hisia za kimapenzi kwani hata wadudu wenyewe wana hisia za mapenzi, sisimizi, viroboto, chawa, kupe, nzi, mbu.. Hao ni baadhi ya wadudu na wao wanafanya mapenzi kulinga na hisia ambazo wameumbwa nazo, sasa itakuwaje kwa upande wa majini?.. Ni jambo lisilo pingika kua maimuna alijikuta anampenda kijana surian ama suria,.. Na suria ndio mwanaume pekee ambaye katimiza vigezo ambavyo Murati sabaha anavitaka,.. Na maimuna na mwenzie shamimu wametumwa kuja duniani kutafuta mwanaume msafi, sasa mwanaume huyo waliompata na maimuna nae kampenda na hataki aende kwa Murati sabaha, lakini hapo hapo shamimu anataka surian aende kwa Murati sabaha,...

Ikiwa ni siku ya sita toka kuja kwao duniani,.. Kesho ni siku yao ya saba siku ambazo hawatakiwi kupitisha, hivyo kesho ilikua ni safari yao ya kurudi ujinini, wawe wamepata au hawajapata, lakini leo shaimati yupo safarini na suria... Katika ufukwe mmoja mkoani tanga, shaimati alifika akiwa kavalia mavazi meupe, hayo ni macho ya shaimati, lakini kwa upande wa suria yeye anaona kama uwanja wa ndege, unaona sasa tofauti iliopo hapa... Shaimati yeye kama yeye, anaona yupo katika fukwe za bahari na ndivyo ilivyo, lakini suria yeye anaona kama yupo katika kiwanja cha ndege,... Hivyo suria kapigwa kiini macho mana akiona wanaingia katika maji atauliza huku ni wapi na hatakiwi kujua mana hata kule ujinini hutojua ni wapi, sasa shaimati na surian wanaingiza miguu kwenye maji, lakini surian yeye anahisi kupanda ndege ya kuelekea dubai,... Ndani ya ndege kweli kuna abiria lakini ni kiini macho ili surian asijue anakwenda wapi kupitia maji,...

Sasa kitendo cha shaimati kugusa maji,.. Na kule maimati kapata ishara kuwa mbona jini mwenzie anarudi nyumbani ingali siku bado,... Pale pale akafanya mawasiliano na jini mwenzie...
"shaimati, kuliko waenda leo"
Aliuliza maimati huku shaimati akicheka sana....
"hahaha, hahahaha... Ahahaha... Hahahah.. Hahahaha.... Nimeamua kuondoka leo"
Aliongea shaimati, lakini maimati alipata mashaka kutokana na vicheko alivyokuwa akicheka shaimati
Maimati hakutaka tena kusubiri pete ivuliwe na asha hivyo, ndani ya sekunde chache, maimati alionekana katika fukwe za bahari akiwa anafuata nyuma mana alihisi ni lazima shaimati anakwenda na surian....

Kweli aliwakuta njiani kutokana na usafiri wao wanao utumia, lakini suria yeye anajua yupo katika ndege kuelekea dubai kufanya kazi,...
"shaimaaaaaaaat"
Maimati aliita kwa hasira kubwa baada ya kumuona suria akiwa sambamba na shaimati, na mbaya zaidi walishavuka mipaka ya ujinini na duniani,.. Kuna mahali binadamu hata uzamie vipi huezi fika.. Na hapo ndio himaya ya mipaka yao... Huko chini kuna viumbe vya kila aina, amaki wa ajabu ajabu.. Na pia kuna maisha mengine utafikiri ni duniani, lakini huku majumba yao yote ni ya kifahari, yaani yaliojengwa kwa matofali ya dhahabu, yaani nyumba imesimama kwa madini tu,... Kumbuka hata madini yote duniani yanamilikiwa na majini, na ndio mana kuna mahali mpaka mtu afe ndipo madini yatoke,.. Hapo ujue kuna jini mchafu, lakini mahali kuna jini msafi au mzuri, hapo hapahitajiki kafara lolote, zaidi ya juhudi za mchimbaji (nikimaanisha kwenye migodi)...
"nilikwambia... Surian anakwenda lakini huamini"
Aliongea shaimati wakati huo maimati yupo kwa mbele, lakini haonekani, hivyo suria pia hajui kama shaimati kuna kitu anaongea nacho, yaani anahisi maisha ni ya kawaida...
"ni sawa, umeshinda... Lakini utajua kwanini sitaki suria aje huku... Najua ipo siku nawe utapenda,... Ahsante sana"
Aliongea maimati kwa hasira sana, lakini pamoja na kukataa kwake surian asije huku, naye alijiunga katika safari hio ili Murati sabaha asijue kuwa maimati alikua tofauti nae, sasa hapo suria ndio anamuona maimati kama vile abiria ambaye amepanda ndege hio,.. Na kama unakumbuka kule duniani, suria alimuona maimati mara moja tu pale wakati alimkosa kosa kumgonga kwa baiskeli, kuanzia pale maimati hakuonekana mbele za suria, japo alikua nae sambamba kila hatua,

Nani alikwambia safari ya majini huchukua muda,... Ndani ya dakika chache tu, wapo katika himaya yao, lakini surian yeye anajua safari ndeefu kumbe hata dakika mbili hakuna,.. Sasa kama kawaida shaimati hakutaka kuipoteza taswira ya mji wa dubai,... Hata mazingira yalikuwa kama dubai, hio yote ni kumfanya surian asijue lolote,.. Lakini wao wakiangalia mandhari yao, wanaona mapango makubwa makubwa... Lakini surian akiangalia mandhari hio, naona maghorofa makubwa makubwa tena ya thamani sana,.. Sasa kumbe macho yake yanapo ona ndivyo anavyo ona... Lakini nyuma yake surian, ni mapango makubwa wanayapita majani mzuri sana, miti, wanyama wa kila aina.... Lakini hata akigeuka haoni msitu wala mapango, na akigeuka kuangalia nyuma, na kule mbele yake ni msitu afu nyuma yake anaona jiji la dubai... Akirudisha macho mbele, anaona ni jiji vile vile, kwahio hapo macho yake yalipo angalia ndipo yanapo ona, hivyo anacho kiona mbele sicho kilichopo nyuma yake... Nadhani mumenielewa ndugu wasomaji wangu...

Ndani ya falme ya majini Murati sabaha na wafuasi wake wengi sana, wakiwa katika hali ya kufurahia ujio huo,... Surian anashangaa kumbe dubai kuna warembo kiasi hicho, watoto weupe haoni mweusi hata mmoja, mpaka sasa surian anajua yupo dubai, kumbe yupo ujinini kwenye falme za majini huko chini ya bahari,...
"hakika mumeifanya kazi vyema kabisa... Maimati na shaimati, hongereni sana"
Aliongea Murati sabaha malikia mkuu wa kaya yao,.. Japo yupo kuu zaidi lakini katika jimbo hilo mkuu ni sabaha, na yeye ana asili moja tu ya ujini hana asili mbili.... Jamani kna aina 360 ya majini, na majini wengine ni watu kama akina maimati na shaimati, ikiwa na maana kuwa wapo majini walioshiriki tendo la ndoa na binadamu hivyo kupata mtoto mwenye asili mbili, na ndivyo ilivyo kwa wazazi wa shaimati na maimati
"Murati sabaha? Sedutu potie santuu dubai rikati"
Shaimati alimwambia Murati sabaha kuwa
"Murati sabaha? Mtu huyu anajua tupo dubai kikazi"
Hapo nimekutafsiria kwa lugha yao walio itumia ili surian asijue chochote, kwahio hata Murati sabaha kuskia hivyo akatumia njia hio hio kumkaribisha suria
"waoooo kijana karibu dubai, hii ndio himaya ya Murati sabaha"
Aliongea Murati sabaha huku surian akikaribia ndani, lakini hapo kwenye huo mtaa, kuna majumba ya kweli, hivyo surian hakuwa akiona kiini macho tena, ila akitoka mbali ya hapo ndipo ataona kiini macho.. Alishangaa nyumba nzima imejengwa kwa dhahabu, yaani hata kiti alicho pewa akalie kilikuwa ni dhahabu tupu, yaani hakuna mbao wala chuma hapo ndani.... Kama unavyojua majumba ya kifalme yalivyo, sasa hii ni falme ya majini... Wakili wenyewe wa madini yote yatokayo chini... Kama kuna dini linatoka juu, basi hilo sio lao... Ila yale madini yote yachimbwayo... Wamiliki ni hawa.. Sasa kwanini kila kitu kwao kisiwe dhahabu.. Surian alibaki kushangaa lakini yupo jini mmoja aliokua akiumwa na roho kwa kitendo cha suria kuja katika falme za majini.... Maimati hana raha kabisa kwani hakupenda surian aje huku kwani kampenda awe mume wake, na akija huku uwezekano hakuna na ndio mana hakutaka aje huku...
Shaimati alitoka nje na kumsalimia maimati kama kumkejeli, lakini maimati alitulia tu kwani shaimati hajajua uchungu wa mapenzi...

Huku duniani katika saluni ya asha, dada yake surian, akiwa bado anapiga hela kwa wateja walio miminika,... Marafiki wa asha wanajiuliza asha kagusa wapi,
"hivi amina,.. Unajua bado sielewi"
"ulizani ni wewe tu fatu... Jana si tulikaa pale wateja hakuna tena asha akawa analalamika kweli kodi inafika ajui atalipa na nini, hebu ona leo wateja walivyo wengi, afu huezi amini kapandisha bei ya saluni lakini ona wateja walivyo jaaa..."
Aliongea amina ambaye ni rafiki wa karibu wa asha...
"lakini amini.. Inaonekana hata mavazi yake yamechangia wateja kuja... Hebu ona toka afungue saluni, sikuwahi kumuona akiwa na hijabu... Leo kavaa"
"enheee...danga lake lilee, linamfuata"
"heee, sasa asha atatoka kweli"
"asitoke kwa nini, mbona kila siku anatoka nae, anakwenda kubinjuliwa anarudi"
Walikua ni marafiki wa asha wakiwa wanajadili mabadiliko ya asha, msichana mwenye mavazi ya kichefu chefu,.. Sio kichefuchefu kua mavazi yametoboka lahasha... Bali ni mavazi yasio stahili mbele ya jamiii, anaweza hata kuvaa kanga bila hata chupi, na akatembea mtaani, sasa imagen na umbo lake... Afu avae hivyo.... Ndio mana wengi hushangaa pale asha anapo vaa kiheshima mana sio staili yake ya uvaaji...

Kwanza jamaa kashangaa kuona mavazi ya asha,... Duuuu.. Mpaka akasita kwenda pale saluni... Kisha akaamua kwenda
"oohhh asalam aleykh"
Alikuwa ni mpenzi wake na asha kaja kumtembelea kam ilivyo oda ya kila siku...
"waaleykh msalam hali vipi"
Watu walishangaa asha ndio wa kupokea salamu hio... Lakini pamoja na hayo asha aliitikia huku akiwa bize sana ikiwa ni mishele ya saa 11 za jioni lakini wateja hawakauki, yani mpaka asha kachoka sasa
"vipi leo, naona upo bize sana mamii"
"yes, kwa leo sina time na jambo lolote, labda tuangalie wiki ijayo"
"wiki ijayo.... Asha ivi umetumia akili kwa kusema wiki ijayo"
"sasa we huoni nipo bize"
Asha alimjibu mpenzi wake kwa hasira, kwani alikuwa yupo bize sana
"ni sawa, lakini wasaidizi si wapo"
"nimesema siondoki hapa"
Duuuuu asha leo alikua mkali hata kwa mpenzi wake,.. Yaani ukiwa na hio pete, utaanza kuvichukia vitendo ulivyokua ukivifanya,... Tena ndio utakua mstari wa mbele kufundisha wenzio ambao wana tabia za ajabu

Baada ya masaa mawili akafunga saluni, huku wateja waliobaki wakiahidi kurudi kesho ili kufanya sevisi ya nywele zao... Asha akakaa chini na wasaidizi wake kisha akaanza kuhesabu hizo pesa....
"eeehh mungu ahsante... Leo nimeingiza milioni na laki mbili"
Aliongea asha huku akiwa haamini,.. Na hapo akili ya asha inawaza kuanza kufanya ibada, yaani hio pete ni kiboko unapata riziki na bado inakulazimisha kufanya yalio mazuri kwa mungu na kwa binadamu wenzako... Basi asha aliwalipa wale wasaidizi wake ile laki mbili yote na wasaidizi walikuwa watano... Kama unavyojua shughuli za saluni ya kike ina vitu vingi vya kufanya hivyo ukiwa mwenyewe utapata tabu pale wateja wanapokua wengi,... Leo asha hakupanda haisi, kachukua taxi kabisa mpaka nyumbani... Ikiwa ni mida ya saa moja hivi

Alimkuta mama yake hana raha kabisa,
"Shikamoo mama"
Asha alimsalimia mama yake, lakini kabla mama hajaitikia... Mara baba yake suria kafika
"mama asha, huyo suria bado hajarudi tu"
Baba alimuuliza mkewe kuwa suria hajarudi...
"kwani huko msikitini hayupo"
"sijamuona na kule shule uliko sema kaenda, nimeenda nimeambia huyo mtu hajafika"
Aliongea baba yake asha huku asha akiingilia kati na kusema
"nyie mnamtafuta suria,... Yaani mtu mzima na akili zake mnamuwazia baba.... Sawa lakini baiskeli yake si ile pale"
Aliongea asha lakini mama yake akasema
"baiskeli niliikuta hapo nje..."
"lakini mama na baba... Yule ni mtu mzima atakuja tu... Au mpigieni simu"
"simu yake haipatikani, na hajawahi kuzima simu... Hapo ndipo tunapokua na mashaka"
Aliongea baba yake asha huku asha akivuta kumbukumbu fulani anayo ijua...
"enheeeeee, safi nimekumbuka"
Aliongea asha huku mama na baba wakipumua kuona Afadhali asha kajua surian kaenda wapi...
"kaenda wapi kwani"
Aliuliza mama huku wakiwa makini kumsikiliza asha
"jana nilimsikia suria kwa masikio yangu mawili...."
Aliongea asha huku akiwashtua wazazi wake kana kwamba labda suria kabadilika tabia...
"kasema nini mdogo wako? Hebu sema"
"jana jioni suria aliiiii"
Sasa asha kila akitaka kuongea uongo anashindwa, kwasababu ile pete haitaki uongee uongo bali inataka uongee ukweli,.. Sasa asha alitaka kumchomekea mdogo wake kisa anapendwa na wazazi, sasa pete haitaki uongo...
"sasa aliiii aliii nini"
Mama huyo alimwambia mwanae hivyo, kwani hajui hapo aliposema aliii kumbe hio pete ndio imemzuia kuongea uongo.. Sasa asha baada ya kuona anashindwa kuongea uongo, aliamua kuongea ukweli halisi ambao anaujua yeye kuhusu mdogo wake..

Je? Ni ukweli gani asha anaujua kuhusu mdogo wake??








No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa