PETE YA KIKE Sehemu Ya 6 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Saturday, February 1, 2020

PETE YA KIKE Sehemu Ya 6









BAADA YA SIKU NNE KUPITA

AFTER FOUR DAYS AGO

Zikiwa ni siku nne zimepita lakini ni siku tano toka kuingia kwa majini wawili, yaani shaimati (shamimu) na maimati (maimuna).. Hivyo wamebakiza siku mbili warejee katika dunia yao, iwe wamepata au wamekosa lakini wanatakiwa kurudi baada ya siku saba walizo pewa na malikia wao Murati sabaha ambaye anataka KIJAKAZI WA KIUME kwa ajili ya Kutunza bustani yao,.. Lakini Murati sabaha anataka mwanaume ambaye hajawahi kufanya mapenzi mana hata wao wote hawajawahi kufanya mapezi...

ENDELEA.............

Wanaume ambao hawajawahi kufanya mapenzi duniani, ni wengi sana tena sana.. Lakini sasa wengi wetu hua tunajichua, yaani majini hawa hawataki mwanaume mpiga nyeto,.. Hata kama hajawahi kufanya mapenzi lakini hawamtaki mana kajichafua kwa akili yake... Ila kama umejichafua kupitia ndoto basi wewe wanakutaka mana sio akili yako... Hivyo kama yupo mwanaume ambaye hajawahi kufanya mapenzi toka kuzaliwa kwake na hajawahi kujichua.. Basi aje tanga huku anatafutwa kwa udi na uvumba

Wakati huo surian yupo shuleni akifundisha wanafunzi wake katika kipindi chake cha dini, yaani masomo ya dini husika... Lakini katika lile lile dawati la mwisho alionekana maimati akiwa kakaa, lakini hakukua na mwenye uwezo wa kumwona...
Surian kila akiokota chaki kwenye kiboksi anaona pete,... Na hio pete ndio hio suria anatakiwa aivae, lakini sasa tatizo ni kwamba pete yenyewe ni ya kike.... Na suria yeye anajua ni pete ya mmoja kati ya wanafunzi wake humo darasani,...
"hii michezo yenu hii.. Sasa mumecheza mpaka mumesahau pete kwenye kiboksi cha chaki"
Aliongea mwalimu surian huku akiendelea kuandika,.. Leo Pete haipo chini bali ipo ndani ya kiboksi cha chaki... Na hio pete ni maalum kwa ajili ya surian,... Baada ya kipindi chake kuisha, surian hua anafundishaga watoto wa madrasa kule msikitini pale anapo pata muda.. Hivyo akaona ngoja achukue chaki moja,.. Lakini katika hali ya kichukua alibeba na ile Pete lakini hakuona kama kaibeba ile Pete.. Akaweka katika mguko wake wa suruali akijua kaweka chaki, japo ni chaki kweli lakini imeambatana na ile PETE YA KIKE ambaye anatakiwa kuivaa mwanaume huyo alie onekana msafi katika mkoa wote huo wa Tanga...

Ilipofika mida ya kutoka kazini, surian alipanda baiskeli yake kisha huyoo akaondoka zake,... Hapo sasa maimati karidhika kuona pete ile ipo mfukoni mwa surian... Maimati hakuendelea kumfuatilia, alielekea sehemu yao ambayo wamefikia na wala hahangaiki kitafuta mtu kwani nia yake ni kirudi mikono mitupu kwa Murati sabaha na kumwambia duniani hakuna mwanaume msafi

Sasa huku jirani na nyumba ya akina surian katika mti mmoja ulio acha kivuli kizuuri sana alionekana shaimati akiwa katika hali ya kibinadamu na anaonekana na kila mtu anapewa salamu kama kawaida, na anaitikia kama kawaida, hivyo huezi jua kama ni jini..
"leo lazima niongee na surian... Namshawishi kuna kazi nzuri nje ya nchi atalipwa milioni 10 kwa wiki... Lazima akubali, mana najua akifika kule hawezi kurudi hivyo ni lazima afuate sheria, kanuni na matakwa ya himaya yetu"
Alijiongelea huyu jini shaimati huku akitafuta maneno ya kumrubuni.. Mana anao uwezo wa kumchukua bila kuongea naye, lakini Taurati yao ni hivi... Anatakiwa amrubuni kwa njia ya kibinadamu mana yeye ni binadamu, ila kama suria angelikua ni jini basi angerubuniwa kwa njia ya kijini jini..... Sasa shaimati anaandaa maneno ya kuongea pindi surian anapotokeza kwenye kona...

Sasa huku surian kapitia msikitini kuweka ile chaki moja ambayo kaichukua kule shule kwa ajili ya kuja kufundisha watoto madrasa hapo msikitini.... Sasa alipotoa, alishangaa kuona pete...
"ina maana hii pete ya mwanafunzi niliibeba"
Alijisemea mwalimu surian huku akimpa mtoto chaki akaweke pale ubaoni kwao... Surian hakuona kama kuna tatizo, aliirudisha ile pete katika mfuko wa suruali yake.. Kisha akaanza kupekecha baiskeli na kuondoka, lakini kila akikaa kwenye kiti cha baiskeli ile pete inamchoma choma kana kwamba inamghasi kukaa vizuri katika kiti...
"aahhhh jamani hiii pete.. Nitaitupa mimi aahh"
Aliongea suria huku akiitoa pete ile
"sema ni pete ya mwanafunzi wangu.. Wacha niivae ili kesho nimpe, japo sijui ni ya mwanafunzi yupi"
Aliongea suria kisha akaivaa ile pete kwa hiari yake,... Lakini ni kwasababu imemghasi kukaa katika baiskeli.. Sasa lipo ivaa tu, maimati kapata ishara kuwa pete imevaliwa katika kidole cha surian,..

ILANI YA WAHALIFU WA KIMTANDAO

TAHADHARI SANA KWA WEWE UNAYE UZA KAZI HII KATIKA MITANDAO YAKO YA KIJAMII...

HATUA KALI ZITACHUKULIWA KWA KIFUNGU CHA UKIUKWAJI WA SHERIA ZA MITANDAO, KWA KOSA LA KUHUJUMU KAZI ISIO YAKWAKO..

NDUGU MSOMAJI, HAKIKISHA ANAEKUUZIA SIMULIZI HII NI MMILIKI HALALI MWENYE NAMBA HII, +255714419487... LAA SIVYO NAWE NI MMOJA KATI YA WAHUJUMU WA KAZI ZA WATU, KATIKA MITANDAO YA KIJAMII.....

KWA WALE NDUGU ZANGU WA KUPOSTI KWENYE KURASA ZAO,
HAKIKISHA, UNAPATA IDHINI KUTOKA KWA MMILIKI HUSIKA KWA SIMU NO, +255714419487 WhatsApp
ILI UPEWE MAELEZO, VIGEZO, NA MASHARTI YA KUPOSTI KWENYE UKURASA WAKO WOWOTE ULE..

JIEPUSHE KUKOPI KAZI HII BILA IDHINI YA MMILIKI HUSIKA

TAFADHALI SANA HATUPO KWA AJILI YA KUPELEKANA PABAYA KISHERIA.....

TUWE MAKINI NA KAZI ZA WATU KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

Sasa shaimati bado kasimama kwenye ule mti.. Akamuona surian kwa mbaaali sana anakuja mbio huku akiwa anaendesha baiskeli.. Sasa shaimati akaona kwa ule mwendo wa baiskeli anaokuja nao surian hatoweza kumsimamisha... Hivyo alinyoosha kidole chake na kuifanya tairi ya nyuma kuwa na pancha...
"ayaaaaaa... Misumari hii imetoboa tairi yangu aiseee"
Aliongea suria baada ya kuona tairi ya nyuma haina upepo,... Sasa kwakua nyumbani sio mbali alianza kukokota baiskeli.. Sasa surian akaingiza mkono mmoja mfukoni ili watu wasione ile pete mana ni pete ya kike, watu wakiona itakua aibu..
"samahani kaka.... Kwanza Asalam Aleykh"
Shaimati alianza mambo yake, yaani hapo haruhusiwi kutumia nguvu za kijini...na ndio maana wakatumwa hawa kwasababu wana asili mbili...
"waaleykh msalam dada kheri"
"kheri, za kazi"
"aahh salama tu"
"inaonekana unafanya kazi nzuri eee"
"kawaida tu dada yangu"
Shaimati alianza kumsifia kiasi fulani
"ni kazi gani kwani..."
Kwa kawaida mtu ukiulizwa sana unaweza kushangaa lakini surian hakua mchoyo wa kusema...
"mimi ni mwalimu..."
"aahhh mi nikajua upo wizara fulani hivi ya fedha"
"hahahha hapana dada yangu"
"ila binafsi ningependa tuzungumzie swala la maendeleo... Vipi Naweza kupata walau muda tuongee"
"hapana, sina muda"
"ok.. Mana kuna kazi nje ya nchi.. Mshahara ni milioni kumi kwa wiki"
Aliongea shaimati lakini Swalehe hakuonekana kushtuka kwa hilo
"Kiukweli sihitaji kazi za nje.. Mana kwa sasa nina kazi hivyo nimetosheka na kipato changu"
Aliongea surian kisha akawa anaondoka...
"sasa kaka"
Shaimati aliendelea, lakini surian aliutoa ule mkono wenye pete na kumwambia kwa vitendo huku akisema
"Samahani dada nimechoka sana.. Naihitaji kukoga niwahi msikitini.. Hivyo utaniwia radhi"
Aliongea suria kisha akawa anaondoka,... Sasa shaimati kaiona ile pete, ndio akajua kiumbe ndio mana alikua hataki ni kwasababu ya hio pete...
"ina maana maimati kampa pete?? Shiiiit.... Ujinga gani huu, ina maana nimemkosa?"
Aliongea shaimati lakini ghafla akitabasamu huku akiangalia chini..

Sasa huku ndani surian anaingia, anapishana na dada yake... Mara simu ya surian ikaita
"haalo habari yako"
Ilisikika sauti ya mwanaume mmoja
"salama nani mwenzangu"
"naitwa shabani kisu, ni afisa mwajiri katika kampuni ya MOON VISION ENTERTAINMENT, wewe ndio surian Rashidi Kingazi"
"ndio mimi mkuu... Vipi nimepata kazi"
"acha presha kijana... Utaitwa kesho kwenye intaviu, na boss kasema atakulipa mshahara kwa Mwezi Ni shilingi milioni 3"
Aliongea afisa huyo, surian alifurahi
"haaaaaaa milioni tatu"
"ndio... Kesho saa nne tutakupigia simu"
"sawa boss"
"haya, nikutakie siku njema"
"nawe pia boss"
Simu ilikata, wakati huo asha kashika kiuno akiskiliza swala la milioni tatu
"dada.. Nimepata kazi mpyaa.. Naachana na kazi ya ualimu mimi"
"hongera kwa hilo.... Sasa na hii pete ya kike vipi jamani we surian"
Asha kaona ile pete
"aahh achana nayo"
Suria aliingia zake ndani, asha nae akaachana na ndugu yake.. Sasa ile asha kutoka akakutana na shaimati
"Afadhali umetoka... Njoo njoo haraka"
Shaimati alimwita asha na asha hakusita mana ni marafiki wakubwa kwa sasa...
"kwani ulikuja muda sana..."
"hapana... Sasa skia, mdogo wako nimeongea nae... Lakini nasikitika kua sintokua nae"
Aliongea shaimati huku asha akiuliza
"kwanini sasa jamani shamimu"
"mdogo wako kumbe ni shoga"
Shaimati aliongea hivyo, huku asha akikasirika
"shamimu naomba tuheshimiane.. Kama umemtongoza kakukataa basi, isiwe sababu ya kumtukana"
"hapana aisha... Mdogo wako kavaa pete ya kike... Kama sio shoga, basi inamletea sifa mbaya sana.. Wewe uliona wapi mwanaume akavaa PETE YA KIKE?"
Aliuliza shaimati kisha asha akajibu
"kweli sijawahi kuona.. Lakini sidhani kama ni sababu ya kumwita ndugu yangu hilo jina"
"ashaaaa.. Labda kweli hana hio tabia.. Lakini ile pete... Inamfanya aonekane hivyo... Mimi naomba ukaichukue, mi nampenda mdogo wako... Watu wanamchukulia hivyo akiwa na ile pete... Hebu wahi"
Aliongea shaimati huku asha nae akianza kukubali,...
"lakini, mimi siwezi kuingia chumbani kwake"
"ashaaaaa... Mdogo wako sio shoga lakini watamuona ni shoga"
"sawa lakini pete ipo kidoleni mwake mimi naichukuaje"
"sikia sasa... Hawezi kwenda kuoga na pete... Wewe mvizie kaenda kuoga, ichukue pale mezani kwake"
Aliongea shaimati na yote hayo ni ili ile pete isivaliwe na surian tena..
"sasa mimi sijawahi kuingia chumbani kwake bwana shamimu"
Sasa shaimati kuona asha anazidi kuwa mgumu, alitoa kitita cha pesa kama laki mbili hivi kisha akampa...
"nampenda sana mdogo wako... Chukua hii pesa, fanya hio kazi... Nampenda mdogo wako kweli asha"
Aliongea shaimati huku asha akiwa haamini,... Na keshazipokea zile pesa
"sasa ile pete nikuletee wewe au"
"hapana, vaa wewe tu, mana ni ya kike ile"
Aliongea shaimati kisha asha akaondoka muda huo huo kuingia ndani ili akaiibe ile pete ya suria..

Sasa huku ndani, suria anaingia bafuni huku anacheza kaswida (nyimbo za Kiislamu).. Alikua katika furaha kubwa kwa kuitwa kazi, na wakati huo ana taulo tu.. Anaingia bafuni huku anacheza... Lakini sasa suria kasahau kuvua ile pete, sasa asha kuangalia anaona pete ipo kidoleni,.. Sasa hapo kichwa moto mana anapenda hela kuliko maelezo, suria aliingia bafuni, sasa ile anaanza kuoga anagundua ana pete kwenye kidole, na huezi kuoga na pete kidoleni mana itakuchubua chubua au kukugasi wakati wa kuoga... Sasa wakati huo asha kaduaa, mana kapewa hela lakini pete haipo, na huezi kumvua mtu... Sasa huku bafuni suria kaishika ile pete huku akisema...
"ayaaaaa kumbe sijavua hili lipete"
Aliongea kwa sauti mpaka asha akasikia,... Sasa asha huku anaomba hio pete ivuliwe mana hata akivua hawezi kuiacha huko bafuni, bali ataiweka mahali...

Sasa huku kwa maimati akiwa katulia, ghafla akapata ishara kuwa pete imevuliwa,... Kwa ishara hio aliona kuna umuhimu wa kwenda alipo surian... Maimati akajiandaa kuruka ili akaangalie kulikoni pete ivuliwe,.. Lakini kabla hajaruka, akapata ishara tena kua, pete imevaliwa, hivyo akaahirisha kwenda






No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa