PETE YA KIKE Sehemu Ya 5 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Saturday, February 1, 2020

PETE YA KIKE Sehemu Ya 5






"wewe, mbona leo sikuelewi?... Hii ndio kazi tuliotumwa huku duniani... Leo nataka nimjue kama ana sifa.. Afu wewe hutaki una maana gani"
Aliuliza shaimati na kuachana na suria.. Wakati huo suria keshaingia kwao...
"ni kweli shaimati... Huyo mwanaume ni Msafi, ila nilisha mwona tokea asubuhi.... Ana sifa zote za kuishi ndani ya himaya yetu... Lakini sifa alizonazo huyo mwanaume, hata mimi nazitaka... Hivyo sipo tayari nimpeleke kwa murati sabaha... Tafadhali sana shaimati... Naomba tutafute MWANAUME MSAFI mwingine, ila sio Surian"
Aliongea maimati tena kwa kumuomba shaimati
"maimati, hivi una akili wewe... Hivi umejisahau kuwa upoje... Yule ni binadamu na wewe ni jini... Inawezekanaje kwa hilo"
"nikifuata taratibu zote.. Naweza kuwa nae"
"hata kama... Lakini huyu mwanaume ni lazima afike kwenye himaya ya Murati sabaha... Na nitampeleka mimi kama wewe hutaki"
"sasa tutaona... Mimi na wewe nani zaidi.... Surian haendi popote"

ENDELEA.......

Katika dunia hii kila kiumbe kimeumbwa na hisia zake na matamanio yake, hata wadudu hutamaniana kama ilivyo kwetu sisi binadamu, na hisia za mapenzi anazo kila kiumbe kilichopo duniani.. Maimati akiwa nusu mtu, nusu jini amejikuta akiangukia katika penzi la mwanadamu, lakini rafiki yake alikataa juu ya swala hilo la maimati kumpenda binadamu ingali binadamu huyo ana sifa za kuishi katika bustani yao huko chini ya bahari ambako ndiko makazi ya watu hawa yaliko... Shaimati hakubaliani na maimati katika swala la kumwacha suria dunia,....

"sasa tutaona... Mimi na wewe nani zaidi.... Surian haendi popote"
Aliongea maimati kisha akapotea pale pale katika mazingira ya kutatanisha, shaimati alibaki pale akiendelea kumsubiri suria ili aweze kumshawishi waondoke wote, mana hairuhusiwi kuondoka nae bila makubaliano na kama hataki basi hatakiwi kuondoka, hivyo utumike uongo wowote ule ilimradi akubali, yaani kikubwa asilazimishwe kuondoka

Shaimati alikaa sana hapo nje lakini suria hakutoka nje, kwani hanaga tabia za kutoka nje pale afikapo nyumbani.....
"mwanangu? Mbona leo umechelewa sana kuja nyumbani"
Mama yake surian alimuuliza mwanaye baada ya kurudi jioni sana mida ya saa kumi na moja..
"mama? Mimi nimepeta kazi ujue"
Aliongea surian ama suria au sua, vyovyote utakavyo mwita sawa tu..
"umepata kazi?"
Alidakia dada yake surian aitwaye asha
"ndio dada, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema zake"
Alimjibu dada yake kwa uzuri tu kisha asha akamuuliza mdogo wake
"ni kazi gani umepata"
"ualimu"
"boooo, nikajua kazi ya maana kumbe ualimu?... Mama? Ina maana kumsomesha kooote huko Kapata kazi ya ualimu?"
Aliongea aisha huku akibinua mdomo, kana kwamba kapata kazi ya kishamba ambayo haiendani na elimu yake alio nayo, na ni kweli surian ana elimu kubwa sana na hakupaswa kuwa mwalimu... Yaani alitakiwa kuajiriwa serikalini tena ngazi za juu sana.. Na kima cha mshahara wake kilitakiwa kiwe kuanzia milioni 5 kwenda mbele... Lakini kapata kazi ya ualimu ambayo analipwa laki tatu na elfu sabini...
"asha mwanangu.. Mbona huna furaha na maendeleo ya ndugu yako"
"sio sina maendeleo mama.. Mmemsomeshaaaaaaaaaa.... Sasa mbona hata ukimuomba hela ya vocha hapo hana"
"sasa si alikua hana kazi hamani"
"hana kazi eeee??... Mtajibeba na elimu zenu za juu... Mwana PHD"
Aliongea asha kisha akaondoka zake mana alikua kashika chupa ya mafuta ya kula, kana kwamba anakwenda dukani....
"surian mwanangu... Achana na dada yako si unamjua? Au bado hujamzoea tu"
"wala tu sina shida nae... Afu mama? Ina maana vile alivyo vaa ndio anakwenda dukani vile"
"heeeeee... Tena vile kavaa vizuri sana vile... Kuna saa nyingine mpaka nampa kanga hapa nje ili asipite mbele ya baba yake.. Vile?? Vile mbona kava vizuri sana pale"
Aliongea mama yake asha huku suria akizidi kutikisa kichwa
"mamaaaa.... Yaani vile ndio kavaa vizuri vile"
"hebu nenda kaoge ule"
"lakini mama, dada mnamleaje lakini mama"
"surian?? Ina maana dada yako humjui wewe?"
"mi najua unamwachia tu ni kwasababu anawapa wapa visent sent"
Aliongea surian kana kwamba asha ndio anatoa pesa ya kula pale baba yao anapokua kakosa, mana asha anamiliki saluni hapo mjini mjini, hivyo hakosi pesa...

Sasa huku barabarani, shaimati alimwona asha, akitoka kwenye ile nyumba,.. Shaimati anamkumbuka sana asha mana alisha msitili kimavazi bila asha kujua,... Na shaimati hapendi kuona hali ile.. Hivyo pale pale akamvisha hijabu katika mazingira ya ajabu... Hivyo watu wanaona asha kavalia hijabu lakini asha akijiangalia anajua ana kasketi kafupi...
"Asalam Aleykh dada"
Shaimati alimsalimia asha... Na wakati hua inakwenda saa 12 kasoro za jioni..
"Waleykh msalamu mambo"
"poa.. Naona Unakwenda dukani"
"enheheh ndio, nakwenda kuchukua mafuta ya kula"
Alijibu asha, na hapo bado hajui kama anazungumza na jini, na shaimati kavalia hijabu kisha kapiga ushungi wake,...
"ila we mzuri"
Shaimati alimsifia asha huku asha akitabasamu kusifia na mwanamke mwenzie.. Unajua wachilia mwanaume kumsifia mwanamke kuwa yeye ni mzuri... Kuna mengi yamemvutia au kaamua tu kumwambia ni mzuri.. Lakini mwanamke akimwambia mwanamke mwenzie ni mzuri basi inakua kuna ukweli kiasi na hata anae ambiwa mzuri hujiskia vyema, japo alitamani kuambiwa na mwanaume.... Sasa tabu ni kwa wanaume kuambiana ni mahensam,.. Utasubiri sana kuskia mwenzio kakwambia wewe ni hensam,.. Hatusemagi wanaume hua tunavungaga tu.. Huezi kumsifia mwanaume mwenzio eti ni hensam... Ila jamaa atajisemea mwenyewe tu kua DUUU JAMAA NI HENSAM YULE
lakini haji kusema WEWE NI HENSAM..

"kweli?"
"haaaa... Sasa nikudanganye kwani mimi mwanaume"
"kwani mwanaume akimwambia mwanamke ni mzuri, kamdanganya"
"huenda asimdanganye au akamdanganya,.. Na pia huenda akamwambia ni mzuri kwa umbo... Au kifua, hivyo wanaume hawasemi mzuri mwili mzima.. Bali kuna kipande cha mwili kakipenda hivyo labda hawezi kusema una umbo zuri, au una kifua kizuri, au una sura nzuri... Hawezi kichambua lakini atasema kwa ujumla wewe ni mzuri, lakini kuna sehemu kailenga"
Aliongea shaimati na kumteka asha kwa yale maneno yake...
"haaaaaa, basi mimi sijuagi... Kumbe wanaume hawapendagi mwili mzima"
"tena sio kupenda bali kutamani"
"heeee dada unaniacha hoi"
"usijali... Mimi natamani uwe rafiki yangu, sjui unaitwa nani"
Shaimati aliongea hivyo na kumuuliza jina lake, lakini sio kuwa halijui bali kaamua tu kumuuliza...
"haina shida.. Mimi naitwa asha.. Ni mtoto wa kwanza katika familia ya kawaida sana"
"waooooo... Mimi Naitwa shamimu, ni mtoto wa tatu katika familia yetu.. Vipi kwenu mmezaliwa wangapi"
Shaimati au shamimu alimuuliza asha kuwa kwao wamezaliwa wangapi...
"Kiukweli tupo wawili tu.. Nina mdogo wangu wa kiume anaitwa surian"
"waoooo... Kumbe una ndugu wa kiume"
"yes"
Aliongea shaimati, japo anajua kila kitu lakini hakutaka kumwonyesha kuwa anajua hilo.... Asha alifika dukani akanunua mafuta kisha wakawa wanarudi....

"kaka yako ni mkubwa eee"
Shaimati alikua na maswali mengi sana ili tu kujenga mazoea na asha kwa urahisi wa kumpata suria, ili huyo huyo asha amrubuni mdogo wake kwa njia yoyote ile...
"yes, ni mkubwa.. Ana miaka 23 sasa"
"waoooo, basi mwambie mimi nina 20"
Aliongea shaimati ili kumwonyesha asha kua keshazimika na mdogo wake
"mmmhhh shamimu, ina maana ushampenda mdogo wangu"
"nikipata muda wa kuongea nae... Sitasita kumwambia"
Aliongea shaimati huku akishusha tabasamu zito mno... Asha hajui kuwa huyo ni jini
"waooo basi napenda pia uje kuwa wifi yangu"
"eti eee"
"ndio"
Asha alifika kwao kisha akamuaga shaimati
"shamimu? Nimefika na hapa ndio nyumbani... Afu subiri nikuitie surian"
"ah ah Noo Noo... Mwache kwanza.. Nafikiria kachoka kwa kiasi fulani"
"sawa wifi, kesho basi"
"ok poa"
Sasa ile asha anafunga tu mlango, huku nje shaimati kapotea pale pale...

Sasa huku ndani,.. Surian katoka kuoga, sasa alikua akivaa saa yake, lakini kwa pembeni ya ukuta alikuwepo maimati akimtazama huku akizidi kumpenda surian... Wakati huo surian anaharakisha kuvaa ili awahi msikitini kuswali swala ya magharibi.. Suria alitoka na maimati akafuata nyuma... Kana kwamba hamuachi... Surian alipoingia msikitini, maimati alipotea mana kahakikisha anaingia sehemu salama kabisa....

Sasa huku katika kambi yao ambayo wamefikia wao wawili..
Maimati alimkuta shaimati akiwa katulia, tena kavalia mavazi meupee ambayo ndio waliokuja nayo toka baharini....
"mpaka sasa nimefanya mawasiliano na Murati sabaha, nimemwambia kuna msafi tumempata"
Aliongea shaimati kama kumwelezea maimati
"lakini shaimati.. Mbona unafanya haraka hivyo? Mimi nimekuomba tutafute mwingine"
Aliongea maimati kana kwamba bado anazidi kumwomba ili watafute mwanaume mwingine lakini sio suria
"sikiliza maimati... Lazima twende na matakwa ya Murati sabaha..."
"hapana...ivi wewe shaimati huna hisia za kimapenzi"
"ninazo ila sihitaji mwanaume mana hakuna mwanaume atakaye timiza sifa ninazo taka"
Aliongea shaimati kana kwamba naye anapenda lakini ana sifa zake ambazo anataka...
"sifa gani wewe unataka"
Maimati alimuuliza ili aweze kujua
"nataka mwanaume ambaye hajasoma kabisa... Yaani kama kasoma sana, basi awe kaishia darasa la saba tu basi... Na awe msafi"
Aliongea shaimati huku maimati akitikisa kichwa,...
"Kwa sasa huezi kupata mwanaume kama huyo, labda zamani... Mana zamani watu hawakua wakisoma sana... Lakini sasa hivi watu wanataka mpaka PHD, leo unasema unataka ambaye hajasoma... Na kama kasoma basi awe kaishia darasa la saba"
"ndio"
"mmmhhh Masharti yako magumu sana... Lakini yote tisa.. Surian tumuache shaimati"
Maimati alizidi kumwomba mwenzie kuwa suria wamwache kama alivyo...
"maimati... Mimi sihitaji kuishi duniani... Kwanza duniani kunatia kichefuchefu... Wanawake wanasagana.. Wanaume ndio usiseme... Mimi sitaki kabisa. Sitaki kuishi huku.. Hebu tumchukue huyo aliopatikana tuondoke zetu"
"kweli surian haondoki shaimati..."
"mimi nasema hivi surian ataondoka"
Walibishana lakini uzuri ni kwamba hawa hawapigani ila ili mmoja aonekane mshindi basi ni lazima wapimane nguvu kwa kutumia akili..
"sawa.. Tutajua... Na nahitaji niwasiliane na Murati sabaha,.. Kua tunaona wanaume wasafi ambao wanajichua tu"
"heeeee... Maimati?? Unataka kupeleka uchafu kwenye bustani yetu... Yaani hatakiwi mwanaume alio fanya mapenzi, au alio jitoa manii zake kwa njia ya mkono ama njia yeyote ile kama katumia akilia yake"
Aliongea shaimati,... Shaimati Kiukweli hajui kitu kuhusu mapenzi japo wote hawajui.. Yaani hawa wasichana wawili wote ni mabikra, hawajui mapenzi lakini maimati kapenda, hisia zimemjaa kwa kumuona surian...
"kwahio"
"mimi naona usisumbuke kuwasiliana nae"
Aliongea shaimati, jini asiejua kupenda, mwenzie kapenda lakini hataki kujua swala hilo...

BAADA YA SIKU NNE KUPITA

AFTER FOUR DAYS AGO

Zikiwa ni siku nne zimepita lakini ni siku tano toka kuingia kwa majini wawili, yaani shaimati (shamimu) na maimati (maimuna).. Hivyo wamebakiza siku mbili warejee katika dunia yao, iwe wamepata au wamekosa lakini wanatakiwa kurudi baada ya siku saba walizo pewa na malikia wao Murati sabaha ambaye anataka KIJAKAZI WA KIUME kwa ajili ya Kutunza bustani yao,.. Lakini Murati sabaha anataka mwanaume ambaye hajawahi kufanya mapenzi mana hata wao wote hawajawahi kufanya mapezi...

Itaendelea...............






No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa