PETE YA KIKE Sehemu Ya 29 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Sunday, February 2, 2020

PETE YA KIKE Sehemu Ya 29





Sasa tukija huku kwa surian, katika chumba ambacho kalazwa fey,... Faima alizinduka na kuanza kushangaa chumba ambacho kalazwa kikiwa na dhahabu kila kona, faima aliona mlango wa kutokea kisha akaufuata mlango huo, yaani alikuwa ni mtu wa kushangaa jengo hilo kwani lilijengwa kwa dhahabu, na kama mnakumbukwa kuwa jengo hili, lilishushwa tu kutokana na nguvu za maimuna,... Nyakati hizo ikiwa ni saa mbili usiku, surian alitoka hapo sebuleni na kuingia chumbani kuchukua laptop, hivyo ule wakati wa kuingia chumbani, faima alipita hapo sebuleni akitafuta wahusika wa jengo hilo,...

Mke wa suria akiwa jikoni anaandaa maakuli ya jioni, faima alisikia hali ya mkaango katika chumba fulani,... Akafuatilia mpaka jikoni kaingia,... Maimuna akahisi kuwa yupo mtu anaingia na sio mumewe,... Na wakati huo faima bado hajafika jikoni, maimuna ni jini wazuri na hua hawazuru au hazuru mtu... Faima alishtuka kuona mwanamke anakaanga vitu vyake jikoni,...
"shikamoo dada"

ENDELEA.........

Hakuna kitu kibaya mwanamke aolewe halafu akutane na mke mwenzie ambaye hata dosari na mume hawana,... Ila kwa kibongo Bongo hawa wanawake wangekutana hivi lazima ngumi zingerindima, lakini kwakua muna ni jini hivyo hatakiwi kuwa na chuki dhidi ya binadamu ambaye hana hatia naye,..

Faima alifika jikoni na kumkuta muna ambaye ndio mke wa surian,
"Shikamoo dada"

Faima alimsalimia mwanamke mwenzie ambaye huenda akawa lika lake au kazidiwa kidogo....
"safi tu, karibu"
Huezi amini muna hakuwa na chuki na fey kwani kagundua ni msichana ambaye hana tabia mbaya na kitu kilicho mfanya muna asimchukie fey, ni kwamba fey bado ni bikra, hivyo ni msichan msafi kuliko wasafi wote, hivyo fey ana uwezekano wa kuwa jini kutokana na hali alio nayo mana kuna majini ambao hupewa nguvu kutokana na tabia na usafi wao,... Usafi sio usafi wa kuoga, bali ni usafi wa kuwa na bikra ukiwa mtu mzima, kana kwamba umeepuka ushetani mwingi sana katika dunia ya leo,... Hivyi hata surian angelikubali kubadilika kuwa jini, ingeliwezekana kwasababu alikuwa ni mwanaume Msafi,... Sasa kitu ambacho muna kampenda fey ni kwasababu ni bikra na hakumchukia kwa lolote lile...

"ahsante dada,... Samahani wewe ni nani"
fey alimuuliza muna kuwa yeye ni nani,...
"mimi Naitwa maimuna au maimati.. Ni msichana mwenye asili mbili, ni binadamu na ni jini... Ni mke wa surian"
muna hakutaka kumficha kwasababu hata yeye fey hakujificha baada ya kumuona surian,...
Faima alishtuka sana baada ya kuskia kuwa ni mke wa surian,.. Yaani hakushtuka kuwa ni jini, bali kashtuka kuwa ni mke wa surian,... Muna alishangaa kuona fey anadondosha machozi mfululizo.
"kuna tatizo fey"
"lipo tatizo, dada"
"unahitaji utatuzi juu ya hili"
"sina jinsi dada... Nimesha kosa haki yangu,. Surian nampenda sana, nahisi hata nikifa nitakufa naye"
Aliongea faima huku akilia,... Muna alishtuka sana kuskia hivyo...
"kwanini msinge oana"
"alikuwa anajipanga na maisha, ndio ghafla akapotea, toka siku hio ndio nimemuona leo"
Aliongea faima huku akiendelea kulia
"kahio bado unahitaji kumuona"
"Kiukweli sio kumuona tu, hata kunioa nataka..... Dada? Nipe nafasi nami nijivunie kuwa naye"
Muna alishtuka sana kuskia hivyo, mana ni ujasiri wa hali ya juu sana
Mana fey keshaambiwa kuwa huyo ni jini lakini bado tu anatamani aolewe na surian angalau awe mke wa pili,
"hapana, Utanisamehe fey.... Siwezi kuolewea mke wa pili... Kama unahitaji kumwona umwone tu, lakini kwa hilo, haiwezekani"
Aliongea muna huku akiligeukia jiko na kuendelea kupika...
"naomba unielekeze njia ya kumuona surian, niwe namuona tu"
Fey aliumia sana baada ya kusikia kuwa haiwezekani kuolewa na suria kwa sasa, lakini fey hakukata tamaa mana hawezi kumuacha surian kamwe,. Hivyo fey akaomba awe anamuona tu,..
"una maana gani kusema hivyo fey"
"naomba hata niwe nafanya kazi humu niwe namuona tu"
Aliongea fey kuwa apewe hata kazi za za ndani ili awe anamuona tu surian,... ni ujasiri wa hali ya juu ambao fey anao....
"una maana gani kusema hivyo"
"hata kunipa kazi hapa sawa tu"
"hapana,.. Kukupa kazi ndani ni ngumu, labda kiwandani"
Aliongea muna huku akiwa bize katika kupika,.. Fey alitoka jikoni hapo na kutaka kutoka....
"Unakwenda wapi fey"
Muna alimuuliza lakini fey hakujibu lolote,.
Lakini fey alipokuwa anatoka, alimwona surian pale sebuleni... Waooo huezi amini alishindwa kutoka na kumkimbilia surian... Sasa suria kushtuka mara fey huyo,...

Yalionekana machozi ya muna yakidondoka baada ya kuona surian kamkumbatia fey,... Kumbe muna naye roho inamuuma sana kwani fey ndio mwanamke wa kwanza katika moyo wa surian,...
"we fey, tulia basi"
Aliongea surian huku akijitahidi kumtoa, kana kwamba fey anafanya makusudi kwasababu keshakataliwa na hawezi kupata nafasi ya kuwa na surian,....
"suri?? Hebu amua moja... Kama sipo moyoni mwako nijue kabla"
Aliuliza faima huku suria akiwa hana jibu sahihi la kumpa....
"fey, nina mke naaa"
"najua, una mke na ni jini... Lakini jua kuwa moyoni mwako bado nipo nawe upo na hutokaa kutoka... Nimejitunza mpaka leo, na hata sinioe lakini naomba uitoe hii bikra"
Muna alishtuka kuskia hivyo, kitu kilichomfanya aje mpaka pale walipo
"fey, naomba ujieheshim tafadhali sana,.. Nimekuona ni mstarabu sana hivyo naomba uutumie ustarabu wako vyema"
Aliongea maimuna huku akiwa Siriasi kweli,...
"samahani dada... Lakini jua kuwa ni moyo ndio unanisukuma kulitaka hilo"
"ni sawa, ila wanaume wapo wengi,.. Bikra alio nitoa basi inamtosha sana"
Aliongea maimuna kisha akageuka kuelekea jikoni, ikiwa chakula tayari kimesha iva.. Muna alianza kuleta mboga, kabla hajatua fey kanyanyuka na kukimbilia jikoni kuleta chakula.... Kiukweli hakuta kitu cha raha kama kujiamini, na yote hio ni upendo wa kweli toka moyoni, hivyo muna kalenda mboga, na fey kaleta chakula
Muna alijikuta anafurahi tu katika moyo wake, kwani ni ujasiri wa hali ya juu ambao fey anao..... Fey alimaliza kitenga kila kitu mpaka maji ya kunywa, na bila uoga naye akakaa na kula bila wasiwasi,... Yaani kaamua liwao na liwe kama muna ni jini muuaji basi auwawe tu kwa niaba ya penzi....

Kesho yake fey kaamka asubuhi sana kabla ya muna kuamka,... Kawasha jiko kisha akawa anapika chai,... Yaani fey anaililia nafasi ya kazi ya hapo ndani, ili aweze kumwona surian hata kwa macho tu....

Muna anaamka anakuta kila kitu kipo mezani, afu kakaa hapo akisubiri wenyeji waamke,... Yani muna alijikuta anampenda fey licha ya kumchukia kwakua analihitaji penzi la mume wake,..
"kwahio ina maana kwamba unataka kuwa House Girl kwa nguvu"
"dada? Nampenda sana surian, nipo tayari kufa kwa ajili yake... Na ukae ukijua kuwa dini yetu inaturuhu kuwa wake wawili kwa mume mmoja,.. Nitakuheshim vile utakavyo"
Aliongea fey huku muna akiwa haamini maneno ya huyo msichana mwenzie,...
"maneno yako wala siwezi kiyaweka akilini fey, mimi ni mke halali wa surian"
"najua, na mimi pia ni mchumba wa kwanza wa halali kwa surian,.. Umeninyang'anya surian wangu"
Mara surian alitokea akiwa kavalia kikazi, kana kwamba keshaoga, sasa hapo anywe chai aondoke, na wakatili huo ni saa 12 za asubuhi...

Masaa kadhaa mbele ikiwa ni saa nne asubuhi surian akiwa kazini baada ya jana kito kuka kwakua ilikuwa ni siku ya kutoa mshahara, hivyo leo kazini kama kawaida.... Surian alipiga simu kwa shadya na kuwataka vikao kati yake na sadiki kutokana na hali ya jana kwa mfanyakazi yule mwenye umri mkubwa alipewaje kazi hapo MICCO, kikao kiliitwa na boss surian

Tukija huku kwenye jumba la dhahabu, ambalo linamilikiwa na jini maimuna,...
"afu wewe ulikuwa unauza duka la nguo"
Aliongea muna baada ya kuachwa wote nyumbani na surian kajua hapo hakuna ugomvi mana muna anapenda sana mwanamke mwenye bikra kwani kaepuka vishawishi vingi mno,....
"ndio, na hata wewe pia sio mgeni kwangu"
"kama vile twajuana.... Ila kwa mume tafadhali sana"
"sawa,... Ila mimi nataka kazi tu"
Fey alikubali kumkosa surian lakini hio ni akili anaitumia,....
"labda ujaribu kujitahidi sana"
Aliongea muna tena kwa kucheka cheka kama watu walio marafiki zaidi, kumbe ni watu wenye kugombea mwanaume mmoja....
"kikubwa nina furaha sana kumuona surian, na nitakuja kumuona kila wakati... Leo wacha na familia yangu ikajue furaha yangu juu ya kukutana na surian"
Aliongea fey huku akiamka na kutaka kuondoka....
"sawa karibu tena"
Yaani kwa sasa wapo kama marafiki, lakini ni mahasimu wawili wakubwa sana....
"na nitakuja tu"
Aliongea fey kisha akaondoka, lakini alipofika nje, aliliangalia sana jengo hilo ili akija baadaye asilisahau,.. Yaani nje ni jengo la kawaida sana lakini ndani kumejaa dhahabu kila kona

Faima kwa furaha kwanza akapitia kwa akina asha mbako ni kwa akina surian,....
"yaani we mtoto nikikuona namkumbuka mwanangu"
Aliongea mama yake suria baada ya kumuona fey, akiwa na maana hajui lolote juu ya mtoto wake,...
"Shikamoo mama"
"marahaba ujambo mwanangu"
"sijambo... Asha kaenda wapi"
Fey alimuuliza mama huyo
"asha siku hizi ana kazi.... Kapata kazi kwenye kampuni moja hivi inaitwa MICCO"
Aliongea mama huku fey akijibu kuwa
"oohhh nilijua tu,..."
"ulijua nini"
"si anafanya kazi kwa ndugu yake"
"unasemaje wewe"
"ila mama.... Kwanini umekubali surian aoe jini, huezi amini mimi sina nafasi tena... Ila nina furaha kwa kumuona"
"fatuma, una maana gani... Hio ndoto uliota saa ngapi"

Wakati huo huku kazini, sadiki na shadya ndani ya kikao, siria ya surian kuwepo mjini imeanza kujulikana
"shadya, sina maswali mengi sana kwa sadiki, mana hata yeye alipitia katika uchambuzi wako... Hebu niambie, huyo mfanyakazi alipataje kazi hapa"
Shadya aliulizwa na boss wake,
"ni kweli boss,... Kiukweli yule mama alilia sana, hivyo nikajikuta namuonea huruma,... Nilichokifanya nilitumia picha za mdogo wangu, na jina nikalitumia la huyo mama... Na pia ilishangaza kumpangia mshahara mkubwa.. Na pia kwakua hukutaka mfanyakazi mwenye umri mkubwa, nikafanya mabadiliko ya wafanyakazi, yule aliotakiwa kufanya usafi chooni nikamuweka idarani, na yule wa idarani nikamweka chooni kwakua huendagi kule, hivyo ni ngumu kumuona... Kiukweli naomba unisamehe boss na nitakubaliana na adhabu yeyote itakayo jitokeza"

Shadya Aliongea kwa huzuni akionyesha ukweli juu ya huruma yake kwa mama huyo, bila kujua ndio mama wa surian, hivyo surian kamfukuza mama yake mzazi katika kampuni yake,...
"kwahio umeleta huruma kwenye kampuni za watu"
"samahani boss, sikujua kama itakuja kujulikana"
"kwanini huyo mama asingeleta mtoto wake"
"Kiukweli boss, mwanzo yule mama alisema hana mtoto... Na ana hali mbaya sana ndio nikashawishika kumsaidia,... Ila baade mtoto wake alikuja kuomba kazi, nakumbuka siku ile ulitoka... Hivyo mpaka sasa mtoto wake yupo idarani"
Aliongea shadya tena kwa kujiamini kwani kama kazi inakufa basi ife, na kama ipo basi iwepo tu...
Wakati huo sadiki katulia tu akisikiliza kwani hahusiki kwa jambo hilo,...
"kwahio hii familia unaonekana umeipendelea sana... Haya na huyo mtoto wake analipwaje"
"analipwa laki mbili na nusu"
"elimu yake?"
Surian aliuliza elimu ya msichana huyo
"ni kidato cha nne felia"
"haaaaaa... Yaani kidato cha nne felia analipwaje laki mbili na nusu??"
"aliomsajiri ni boss sadiki"
Aliongea shadya kuwa yeye hahusiki kumpangia mshahara mfanyakazi huyo...
"sadiki?? Sasa kama mtu alio feli analipwa laki mbili je yule mwenye levo nzuri ya elimu alipwe kiasi gani.. Mana hio laki mbili analipwa mtu mwenye levo ya elimu nzuri, sasa kwanini unamlipa mshahara mkubwa kiasi hicho"
Aliongea surian huku akiwa anaanza kukasirika kwani aliona wafanyakazi wanaongeza mishahara kwa mapenzi yao
"samahani sana boss,... Nitalibeba jukumu hilo kama kosa langu, na nipo tayari kumpunguzia mshahara wake hivi punde"
"sio kupunguza tu, pia kitengo abadilishwe... Akae kitengo cha mama yake,... Afu nasema hivi sitaki ujinga na kazi. Kama hamtaki kazi mseme"
Aliongea boss surian huku akikasirika sana...
"tusamehe boss, tunahitaji kazi"
"haya mara moja nisiwaone hapa... Na huyo mfanyakazi apelekwe chooni, kulingana na elimu yake"
"sawa boss... Sasa alipwe kiasi gani"
"laki na nusu inamfaa kwake"
"sawa boss"

Sadiki alilichukua jukumu lile la kwenda kwa asha kisha akaanza kumtia Jamba jamba ya hapa na pale, wakati huo asha yupo bize na kazi...
"mfanyakazi hodari... Haya niambie jibu langu lipo wazi"
Aliongea sadiki huku asha akibinua mdomo,
"mschiuuuuuiu (msunyo).. Huna hadhi ya kuwa nami, kama umeweza kumfukuzisha kazi mama yangu,.. Utawezaje kuwa nami"
Aliongea asha huku sadiki akianza kusema
"yaani unanisunya mimi.... Sasa kwa taarifa yako, kuanzia leo nakulipa laki na nusu, na kitengo chako, kuanzia leo ni chooni, kama hutaki acha kazi"
Aliongea sadiki huku wafanyakazi wengi wakisikitika kwani idara aliopo asha ni kubwa kuliko...
"sitaki kazi yako... Huezi kunipa kazi kwa kunitongoza..."
Aliongea asha huku wafanyakazi wakiguna kuashiria kuwa kumbe sadiki ana tabia ya kitongoza Wafanyakazi,....
"asha kwanini usiende kusema kwa boss"
Aliongea mmoja wa wafanyakazi wenzake, waliompa ushauri huo...
"hapana, wacha niache kazi"
"hapana wewe... Nenda kashtaki kuwa sadiki kakushusha cheo kwasababu kakutongoza ukakataa, nenda acha ujinga wewe"
Aliongea rafiki wa asha ambaye anafanya nae kwenye idara moja,... Kweli asha akashawishika kwenda kwa boss kusema, lakini sha nia ya kukubali swala hilo ni ili akamjue boss wa kampuni hio mana anasikia ni ndugu yake kabisa....
"wewe Unakwenda wapi"
"usiniulize"
"we asha rudi huko hamruhusiwi kuingia"
Aliongea sadiki kwani anaogopa kwa ushauri aliopewa na rafiki zake,...
Asha alipata kichwa cha kwenda ofisini kwa boss...
"we asha vipi tena"
Shadya alimuuliza asha baada ya kumwona asha yupo mlangoni
"nina shida na boss, haiwezekani boss sadiki anipeleke chooni kisa nimemkatalia kuwa naye"
Aliongea asha huku shadya akishangaa
"haaaaaaaaaaaaaaaaa, asha, unasema kweli"
"ndio, nimemkatalia sasa amekuja kunishushia mshahara wangu na kunibadilishia kitengo"
"lakini asha, hicho kitengo na mshahara, ni swala la boss mwenyewe na sio sadiki"
Aliongea shadya huku asha akitamani hata kufungua ule mlango bila ruksa,...
"sawa, lakini jua kuwa sadiki ana tabia ya kututongoza wafanyakazi wa idarani"
"haaaaaaaaa, kweli asha?"
"ndio... shadya"
Shadya aliamka na kugonga mlango..
"nani?"
Boss aliuliza, lakini asha alishtuka kuskia hio sauti
"ni mimi shadya... Yule dada anataka kukuona"
"dada nani huyo"
"yule mwenye mama yake aliokuwa mfanya usafi kule toilets"
"ana shida gani"
Suria aliuliza lakini asha akaona kwa hali hio hakutokuwa na ruksa.... Asha akapayuka kwa sauti na kusema
"boss?? Boss sadiki kanitongoza"
Aliongea asha, sasa sadiki alisikia sauti hio mbona ni kama ya dada yake.... Na ni kweli alikuwa ni yeye, hivyo surian kwa furaha alijikuta anatoka nje...
"suuuuuuriaaaaan"
Asha alipayuka na kumkumbatia mdogo wake kabisa.... Shadya kabaki mdomo wazi,... Mara sadiki katokea.... Alishangaa kukuta asha kakumbatiwa na surian
"haaaaaaaaaa.... Uh nnh uuuh aahh uuun"






No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa