PETE YA KIKE Sehemu Ya 28 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Sunday, February 2, 2020

PETE YA KIKE Sehemu Ya 28






MWANAUME MSAFI

"hapana,... Huku ni V.I.P, lazima uwe na mweza wako... Nashukuru tumekutana"
Sasa kila neno analo ongea faima,.. Maimuna anaumia sana katika moyo na kujiona labda hana haki kwakua yeye ni jini...
"surian mwambie mtu wako kanikalia bwana alaaaa"
Aliongea jini maimati na hapo anaye sikia ni surian peke yake...
"faima vuta kiti ukae"
"mume wangu... Ina maana kwa sasa hutaki niwe karibu yako"
"sina maana hio faima..."
Sasa maimuna anazidi kuumia mana kakaliwa na mwanamke mwenzie afu ni lika lake, na vile faima ana umbo matata, basi na uzito umezidi...
"surian, narudi tena mwambie kanikalia... Na asipo amka nitamuadabisha mana kaingia anga zangu vibaya"
Aliongea jini maimuna kana kwamba kakasirika baada ya kujua huyo ni mke mwenzie ambaye ni binadamu kama surian.... Sasa surian naye anampenda sana faima, kuliko aumizwe ni bora amwambie ukweli
"faima? nimekwambia uchukue kiti kingine mana hapo ulipokalia umemkalia mtu"

ENDELEA........

Katika dunia hii kuna viumbe wengi sana lakini viumbe waliopewa uwezo wa hali ya juu huku duniani, ni pamoja na majini... Na majini hawa wapo wa aina nyingi kuna majini wazuri na majini wabaya, kuna jini maimuna mbaya na kuna jini maimuna mzuri, sasa huyu jini wa suria ni jini mzuri, na huyu maimuna ni jini mwenye asili mbili, na jini mwenye asili mbili ndio mwenye uwezo wa kuonekana na watu au asionekane, ni uwamuzi wake

Sasa maimuna kila kifanya matembezi na mumewe hua hapendi kuonekana na binadamu kwasababu ya uzuri wake kupitiliza na kusababisha watu kumshangaa mwanamke huyo, hivyo ndio sababu ya yeye kuto onekana kwa jamii,... Na kuto onekana kwake hata alipokaa au kusimama pia haionyeshi kuwepo kwa mtu au hata kivuli,...

Leo suria anakutana na mchumba wake wa zamani, akiwa na mkewe katika hali ya kuto onekana wanapata lanchi..... Faima aliweza kumuona mpenzi wake na kumfuata kwa furaha ya hali ya juu,... Bila kujua hapo alipo ana mkewe lakini faima hakuwa na uwezo wa kumuona zaidi ya mumewe ambaye ni surian,... Sasa faima alifikia mpaka kukalia kile kiti ambacho maimuna kakalia, hivyo kwa jinsi maimuna anavyo jiskia ni kuumia kwa kukaliwa kwa juu, na faima yeye anahisi kukaa kwenye kiti bila mashaka... Sasa maimuna anamwambia suria amwambie mtu wake kuwa anamuumiza kwa bile alivyo kaa kwa juu

"faima? nimekwambia uchukue kiti kingine mana hapo ulipokalia umemkalia mtu"

Aliongea suria huku faima akishtuka na kukiangalia kile kiti, alikiona hakina mtu, hivyo akakaa tena lakini wakati faima anakaa tena, maimuna alisha amka na kusimama,...
"mbona hakuna mtu... Ina maana utani wako hujaachaga tu"
Aliongea faima akizani labda ni utani wa surian,.... Na wakati huo maimuna anamuangalia faima kwa hasira mno, mana pia faima sio mgeni sana kwenye macho yake, na hata faima akifanikiwa kumuona maimuna basi pia hatokuwa mgeni katika macho yake yake, kwani walishawahi kuwa wateja wake katika kipindi fulani..

"huyu mtu ni nani wako surian,... Ina maana kumbe ulikuwa na mchumba kabisa"
Aliongea maimuna, kisha surian akajibu
"hapana muna, kalikuwa ni kademu tu"
Alijibu surian kisha faima akasema
"unaongea na nani surian"
Faima aliuliza, kwani alimwona surian anaongea pasina kumwangalia yeye,
"fey, mi naona tutawasiliana kwa wakati mwingine"
Aliongea surian baada ya kuona maimuna kakasirika na anaharakisha kuondoka
 "hapana surian, siwezi kukuacha tena, utaniua hapa hapa lakini lazima twende huko uendako"
Aliongea fey huku akitaka hata kulia kwa jinsi surian alivyo taka,...
Suria alimwangalia maimuna kavimba kwelikweli, licha ya kuwa ni jini lakini roho inamuuma kwakua kakutana na mke mwenzie ambaye alipenda kabla yake,...
"surian, twende nyumbani basi mume wangu"
Aliongea maimuna huku akitangulia kwenye gari na kuingia pale kushoto kwa dereva... Baada ya surian kuona hivyo, alitoa pochi na kutoa pesa kama laki moja na kumpa fey
"shika hii, tutaonana"
Surian alitoa pesa kisha akawa anaondoka..
"sitaki pesa zako surian, nakutaka wewe tu"
Fey alizitupa zile pesa kisha akatangulia kwenye gari ambalo surian alikuwa akilielekea na fey akajua hio ndio gari ya surian,.. Sasa surian akarudi nyuma kuokota ile pesa alio tupa fey,. Wakati huo fey naye kapanda gari na kukaa, hivyi kwa mara ya pili akamkalia maimuna, muna alishikwa na hasira sana..

Surian yeye anaona kila kitu,.. Kiukweli hapo ana mtihani mkali juu ya wanawake hao,.. Suria aliingia kwenye gari na kuona hali halisi jinsi fey alivyo kaa juu ya maimuna...
"muna, mi naona ujionyeshe tu akuone"
Aliongea surian huku fey akisema
"muna ndio nani surian, au unaongea na simu"
Alijibu faima huku surian akiendesha gari kuelekea nyumbani akamwache maimuna kisha amrudishe fey kule alipo tokea...
"siongei na simu, hapo ulipo umekalia mtu fey"
"surian mimi staki utani wako"
Aliongea fey akidhani labda surian anaongea utani, huku muna akisema
"hivi surian, kwanini usingeniambia kuwa una mchumba"
"muna, kukupenda nakupenda... Lakini hata ujinini nilikwambia mke wangu kuwa nina mchumba... Ukaniambia mchumba sio mke"
"ni sawa,... Lakini mimi nilijua msha achana"
"bado, sasa itakuwaje muna,.. Mana sina ugomvi nae"
Aliongea surian huku fey akiuliza
"surian, hio ni simu au unaongea na mimi"
wakati huo wote walikuwa safari kwenda nyumbani, na hapo wamekaribia kufika,. Sasa maimuna akaona bora ajionyenye,... Sasa fey akajikuta anahisi kukaa katika mapaja ya mtu, ikiwa na maana kwamba muna kajionyesha,... Fey aligeuka nyuma na kukutana na msichana mwenzie mzuri kabisa... Ghafla fey alipata mshtuko na kuzimia baada ya kujua kumbe hapo yupo katika himaya isio sahihi... Muna hakumshusha fey katika mapaja yake kwani ingelikuwa ni kumnyanyasa mwanamke mwenzie hivyo fey alipakatwa kama jinsi alivyo kaa awali lakini akiwa kazimia,...
Walifika nyumbani muna alitumia nguvu za kijini kumbeba fey mpaka ndani, na alimpeleka kwenye chumba kimoja kizuri kilichozungukwa na dhahabu, madini ya kila aina... Kitanda chenyewe cha dhahabu, yaani kila kilicho onekana hapo ndani ya mjengo ni pesa tupu...

Huku ICC wateja wamejaa lakini mhudumu hakuna, muuzaji wa duka la jirani alijaribu kumpigia fey simu lakini haikuwa ikipokelewa,.. Ikabidi ampigie boss wake ambaye ndie alie mwajiri fey, mpaka hapo lazima fey aharibu kibarua chake

Huku kwenye daladala mama surian na mtoto wake asha wakiwa na huzuni kubwa baada ya mama huyo kufukuzwa kazi kutokana na umri wake, yaani kilicho mfukuzisha kazi sio mshahara bali ni umri wake...
"mama, wala usiwe na mawazo mama.... Mimi si bado nipo kazini"
Aliongea asha huku akimtuliza mama yake.....
Walifika nyumbani wakiwa na pesa zao na hapo ukichanganya wana kitu kama laki sita hivi na pointi,... Mama alimwangalia sana mtoto wake asha na kumsihi sana
"asha mwanangu, kwa sasa mdogo wako surian tunamsikia tu... Sasa tegemeo letu ni wewe mwanangu... Mimi nilikuwa nina ombi moja kwako"
Aliongea mama huyo, huku asha akimuuliza mama yake
"ni ombi gani mama?, niambie tu"
"asha,... Kwa sasa wewe ni mtu mzima... Unahitaji kuolewa, na katika wanaume wa sasa wanachagua sana aina na heshima za mwanamke... Mimi nakuomba ubadilike mwanangu.. Kua unavaa hivi ili upate mume bora mwanangu"
Aliongea mama huyo huku asha akicheka sana.... Mana kwa sasa asha anavaa kiheshima kwakua pale kwenye kampuni ya MICCO hawahitaji mavazi ya ajabu, yena hususan mkoa wa tanga ulivyo miminika wingi wa imani ya Kiislamu, hivyo mama kamsihi mwanaye kuwa aendelee vivyo hivyo, yaani isiwe hivyo kwa niaba ya kazi, bali iwe ndio tabia yake na awe mwanamke mwenye heshima....
"ahahaha mama, Kiukweli namshukuru mungu toka nilipojua kuwa ninaye mtaka kimapenzi ni ndugu yangu... Mama mpaka leo sitaki tena kudanga wala kutamani mwanaume,.. Mana naona tamaa yangu itanipeleka pabaya... Haya sasa kama sio kujua sauti ya mdogo wangu surian je si ningetembea naye?? Mama?? Mpaka leo nimekoma na sitaki tamaa"
Aliongea asha na kumfanya mama yake kufurahi mara dufu zaidi,... Ni ukweli kua asha kaachana na hali ya kudanga,...
"asha naomba uwe mtoto mwema kwetu, usitulize tena wazazi wako"
"mama, nakili kulikubali hilo, nitawalea kuanzia sasa"
Aliongea asha na wakati huo baba naye anaingia na kukuta mkewe anafuraha mpaka analia, yaani alipoteze ile huzuni yote ya kufukuzwa kazi,...
"vipi jamani mbona furaha hivyo"
Aliuliza mzee Rashidi ambaye ndio baba wa familia hio,....
"we acha tu baba asha... Asalam Aleykh mume wangu"
"waaleykh msalam mke wangu,.. Habari za kazi"
"mmmhh Kiukweli kazi ni mbaya kwa upande wangu.. Kwani imegundulika kuwa nimeingia kinyemela"
Aliongea mama huyo huku baba akishtuka kwa taarifa hizo,
"mungu wangu, sasa itakuwaje mke wangu"
"hakuna tabu, na hapa nilikuwa na furaha baada ya asha kukili kutulea kwani yeye bado yupo kazini"
"asha mwanangu, ni kweli utakuwa nasi"
Mzee Rashidi alimuuliza mtoto wake aliobaki baada ya suria kupotea takribani miezi sita sasa toka kupotea kwake, japo wapo waliosema surian amefariki dunia...
"ndio baba, na naahidi kubadilika kuanzia tabia"
"ahsante sana mungu, mana sikutegemea kama asha utakuja kubadilika mwanangu"
"msijali wazazi wangu, na pia numepata tetesi kuwa ile kampuni anamiliki kaka surian"
Aliongea asha, na swala hilo baba hakuwahi kulisikia kabla na hata asha hawana ule uhakika wa wazi
"unasemaje asha.."
"ndio baba, nimesikia tu, hivyo nitafanya upelelezi kwa hilo"

Sasa tukija huku kwa surian, katika chumba ambacho kalazwa fey,... Faima alizinduka na kuanza kushangaa chumba ambacho kalazwa kikiwa na dhahabu kila kona, faima aliona mlango wa kutokea kisha akaufuata mlango huo, yaani alikuwa ni mtu wa kushangaa jengo hilo kwani lilijengwa kwa dhahabu, na kama mnakumbukwa kuwa jengo hili, lilishushwa tu kutokana na nguvu za maimuna,... Nyakati hizo ikiwa ni saa mbili usiku, surian alitoka hapo sebuleni na kuingia chumbani kuchukua laptop, hivyo ule wakati wa kuingia chumbani, faima alipita hapo sebuleni akitafuta wahusika wa jengo hilo,...

Mke wa suria akiwa jikoni anaandaa maakuli ya jioni, faima alisikia hali ya mkaango katika chumba fulani,... Akafuatilia mpaka jikoni kaingia,... Maimuna akahisi kuwa yupo mtu anaingia na sio mumewe,... Na wakati huo faima bado hajafika jikoni, maimuna ni jini wazuri na hua hawazuru au hazuru mtu... Faima alishtuka kuona mwanamke anakaanga vitu vyake jikoni,...
"shikamoo dada"

Je? Nini kitaendelea hapo baada ya Wake wawili wakutana jiko moja??....






No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa