PETE YA KIKE Sehemu Ya 30 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Sunday, February 2, 2020

PETE YA KIKE Sehemu Ya 30







"sawa, lakini jua kuwa sadiki ana tabia ya kututongoza wafanyakazi wa idarani"
"haaaaaaaaa, kweli asha?"
"ndio... shadya"
Shadya aliamka na kugonga mlango..
"nani?"
Boss aliuliza, lakini asha alishtuka kuskia hio sauti
"ni mimi shadya... Yule dada anataka kukuona"
"dada nani huyo"
"yule mwenye mama yake aliokuwa mfanya usafi kule toilets"
"ana shida gani"
Suria aliuliza lakini asha akaona kwa hali hio hakutokuwa na ruksa.... Asha akapayuka kwa sauti na kusema
"boss?? Boss sadiki kanitongoza"
Aliongea asha, sasa sadiki alisikia sauti hio mbona ni kama ya dada yake.... Na ni kweli alikuwa ni yeye, hivyo surian kwa furaha alijikuta anatoka nje...
"suuuuuuriaaaaan"
Asha alipayuka na kumkumbatia mdogo wake kabisa.... Shadya kabaki mdomo wazi,... Mara sadiki katokea.... Alishangaa kukuta asha kakumbatiwa na surian
"haaaaaaaaaa.... Uh nnh uuuh aahh uuun"

ENDELEA.........

Sadiki alipatwa na kigugumizi baada ya kukuta kumbatio zito baina ya suria na asha ambao ni mtu na dada yake baada ya kumisiana kwa muda mrefu,.... Asha wakati huo anaangua kilio, kwani haamini kama leo kamuona mdogo wake ambaye ameshukiwa kumuua kwa ajili ya mali,...

Shadya na Sadiki wakiwa mashahidi wa kumbatio hilo, na wasijue watu hao wana uhusiano gani... Baada ya kumbatio surian naye machozi yalimtoka kwa kuto waona ndugu zake kwa muda mrefu,... Sadiki na shadya bado kimya kilitawala juu yao,.. Surian alimchukua asha na kuingia naye ofisini kwake,..

"mbona sielewi"
Aliuliza sadiki huku akiwa na wasiwasi,..
"hata mimi sielewi"
Shadya naye alimjibu sadiki, mana hakuna ambaye anafahamu hilo...
"mungu wangu, isijw kuwa ni mpenzi wake"
Aliongea sadiki huku akikaa kwa kalio moja kwa uoga wa hali ya juu
"na asha kasema ulimtongoza, na kukukatalia kwake, ndio sababu ya kumfukuza mama yake... Sasa kama atamwambia mpenzi wake,.. Kazi huna boss"
Aliongea shadya akidhani kuwa surian na asha ni mtu na mpenzi wake,
"shadya usiseme hivyo jamani"
Sadiki Aliongea huku akiwa kasimama mana kiti hakikaliki wala kusimama hakusimamiki,
"sina maana kuwa ufukuzwe kazi, ila ulionyesha tamaa boss"

Huku ofisini surian na dada yake walikuwa wakisimuliana maisha yalivyokuwa mpaka sasa
"surian mdogo wangu, ulikuwa wapi... Dada yako naambiwa nimekuua jamani"
Aliongea asha huku machozi ya furaha yakiendelea kumtoka kwa kasi mana haamini kama leo kamuona mdogo wake,...
"dada, ni maisha tu... Mi nadhani utajua tu"
Surian naye machozi ya furaha yalimtoka kwani ni miezi sita kama sio saba, toka kupotea kwake,.. Wakati huo huku mapokezi sadiki anajinyea nyea kwa kujua labda asha ni mpenzi wa surian,...
"surian, hebu twende kwa mama, mana yeye ndio anaumwa kila siku juu yako... Japo naye kafanya kazi hapa na kafukuzwa juzi tu"
Aliongea asha huku surian asiweke hata ubishi wa chembe moja...
"ina maana kwamba mama ndio alikuwa akifanya usafi wa choo"
"ndio, kwani ulikuwa hujui"
"hapana.."
"ndio hivyo, mama alikuwa akifanya usafi wa chooni na hajui kama wewe ndio mmiliki wa hapa"
Surian alilia sana na kushikwa na hasira,
"shadyaaaaaaa"
Siku zote surian anapigaga simu kwa shadya, lakini leo kaita kwa mdomo tena kwa sauti kubwa,
"abeee boss"
"njooo"
sadiki na shadya roho ziliwapasuka huku kila mmoja akichanganyikiwa juu ya uitaji wa boss kuwa mkali na wa hasira...
"abee boss"
"shadya?? Kwanini mama yangu umpangie chooni aisee"
Alifoka surian huku shadya akitetemeka kwa uoga
"bo... Bos.. Bos... Samahani sana,... Kwanza sikujua kama ni mama yako, na pia kigezo kikuu cha kampuni yetu, hairuhusu mfanyakazi mwenye umri zaidi ya miaka 35.... Hivyo yule mama aliniomba na kuniomba.... Boss? Niliingiwa na huruma kutokana na maelezo ya maisha yake yalivyo, hivyo nikaamua kumtangenezea vyeti feki ili apate kazi aweze kuilisha familia yake... Nilitafakari nitamueka wapi ili usimuone kwakua ana umri usiotakiwa hapa kwenye kampuni.... Boss? Nisamehe sana... Niliona huna muda wa kwenda public toilets, nikaona huko kunamfaa kwakua hutokwenda mara kwa mara.... Na jina lake ulilifanya kulipwa mshahara mkubwa sana, na sikuweza kuukata mshahara wake mpaka alipokuja kuacha kazi.... Boss? Nisamehe, sikujua kama ni mama yako"

Shadya aliongea ukweli wote huku akilia kwa uoga wa hali ya juu.. Huko mapokezi sadiki anahangaika, moja haikai mbili haikai...
Surian alimsikiliza shadya kwa umakini wa hali ya juu, alijua hana kosa....
"rudi ofisini kwako"
Aliongea surian huku shadya asiamini kuwa kaambiwa arudi kazini kwake....
"ahsante boss"
Alishukuru shadya huku asha akimtaka mdogo wake waondoke waende kwa mama yao....
"twende kwa mama surian,.. Utamuua mama etu.."
Surian alikuwa na mipango ya kwenda kwao wiki hio hio, lakini siku hio kakubali kwenda kabla ya siku husika ambayo kaipangilia kwenda...
"twende dada...."
Asha na mdogo wake surian walitoka na kupanda gari ya kifahari,... Wafanyakazi wanashangaa asha leo kapanda gari ya boss.... Waliondoka kwenda kwao

"enheee... Mbona mimi hajaniita"
Aliuliza sadiki baada ya boss kuondoka
"we acha tu.... Ni kesi kubwa unayo"
Aliongea shadya, sadiki nae presha juu...
"shadya acha utani dada angu"
Sadiki mpaka kamuita shadya dada, kwa uoga...
"sasa skia balaaa... Kumbe yule mama ni mama yake mzazi, na huyu asha ni dada yake wa kuzaliwa naye"
Shadya alimwambia Sadiki kuhusu asha na yule mama
"ati unasemaje shadya??"
"asha ni dada yake.. Na yule mama, ni mama yake mzazi"
"mungu wangu weeee......kumbe nimemfukuza mama yake boss"

Wakati huo huo huku nyumbani kwa surian, yaani kule kwa mke wake.... Kama ilivyo kwa viumbe ambavyo sio binadamu halisi hua wanajifungua kwa muda mfupi,... Binadamu hukaa miezi tisa... Jini wabaya (mashetani) hukaa miezi miwili mpaka na nusu... Na hawa majini wazuri, wao hukaa miezi minne mpaka mitano... Maimuna miezi mitano ilishafika, na ndio maana hakuwa wakwenda kazini japo mimba yake haionekani sana kwasababu ni miezi mitano tu, na pia wao sio binadamu kwamba atachoka kama ilivyo kwa binadamu.. Na hata kujifungua kwao hawaelekei hospitalini,... Bali hurudi ujinini kujifungua,.... Na siku hii ya leo shaimati alikuja nyumbani kwa maimuna baada ya maimuna kutoa taarifa ya kujifungua kwake, na hawa kama ilivyo wana ugomvi lakini hawapigani...
"maimati twende sasa hivi"
Aliongea shaimati kwani kisheria atatakiwa kujifungulia ujinini, na kama kuna kurudi kwa mume basi atarudi na mtoto wake...
"hapana shaimati, wacha mume wangu aje ndio tuondoke usiku wa leo"
"maimati, huyo ni binadamu tu, hawezi kuvuruga taratibu zetu"
"shaimati, nenda nitakuja mwenyewe"
maimuna kaamua kumfukuza shaimati kwani shaimati katumwa na uongozi wao aje kumchukua maimati lakini maimati kakataa kuondoka kwa siku hio mpaka surian aje...

Tukija huku kwa mama yake surian akiwa na faima, mama alishtuka sana baada ya faima kumwambia mama mkwe wake kuwa surian kaoa jini....

"ila mama.... Kwanini umekubali surian aoe jini, huezi amini mimi sina nafasi tena... Ila nina furaha kwa kumuona"
"fatuma, una maana gani... Hio ndoto uliota saa ngapi"

Aliuliza mama huyo huku akizani labda anadanganya kuhusu uwepo wa surian na kuoa jini...
"mama, mbona surian yupo na hata asubuhi kaenda kazini..."
"anaishi wapi kama umemuonac
Mama aliuliza huki akilengwa na machozi mana ni miezi saba sasa hamuoni mtoto wake, na wala hajui yupo wapi kwa sasa...
"kuna nyumba moja hivi anaishi, ila mkewe ni jini"
Aliongea faima huku naye roho ikimuuma kwani atakuwa hana nafasi tena ya kuolewa na surian...
"nipeleke nikamuone mwanangu.. Nina shida na mwanangu"
"sawa mama... Lakini, na mimi vipi ina maana ndoto za kuolewa na surian zimeishia njiani mama"
"wewe twende kwanza"
Mama surian alivaa haraka haraka ili apelekwe huko ambako surian anaishi.... Mama keshavaa sasa akiwa anafunga mlango, ghafla aliona gari moja ya kifahari inasogelea jengo lao,...
"enheee ndio huyo hapo... Hilo ndio gari analotumia"
Aliongea faima kwakua anajua na alisha wahi kulipanda gari hilo...
"we faima? Mbona sikuelewi"
Mama akiwa katoa macho, aliona mtu wa kwanza kushuka ni asha... Mama katulia tu... Mara surian anashuka,... Mama haamini leo kwa mara ya kwanza toka kupotea kwake anamuona kwa macho yake...

Mama surian anapoteza fahamu kwa kitendo cha kumuona mtoto wake,.. Haraka haraka surian na dada yake pamoja na faima wanambeba mama na kumueka kwenye gari, moja kwa moja mpaka hospitalini,....
"dada? Baba kaelekea wapi"
Surian alimuuliza dada yake, mana wakati akiingia pale kwao baba yake hakuwepo..
"baba nadhani yupo msikitini, mana ndio mtunza hazina wa msikiti"
"hebu nipe namba yake"
Basi asha alimpa mdogo wake namba ya baba yake na kumpigia
"Hallow mzee, Asalam Aleykh"
Surian alimsalimia baba yake
"heeee, wa.. Waleykh... Waleykh msalam, upo wapi mwanangu"
"nipo hospitali hapa mama kapoteza fahamu"
Aliongea surian na baba yake alijua tu sababu ya mkewe kupoteza fahamu kwani hata sauti ya surian tu ilimfanya apoteze fahamu,...
"nakuja sasa hivi"
Simu ilikata baada ya mzee Rashidi kutaamka ujio wake hapo hospitali..

Ilipofika saa saba mchana mama asha alizinduka, jicho la kwanza lilipita kwa surian,... Mama Alianza kulia huku akiamka
"mama, pumzika Kwanza mimi nipo tu"
"surian mwanangu, ulikuwa wapi baba"
Mama alimuuliza mtoto wake huku akilia sana,
"mama? Ni stori ndefu sana..."
Alisema surian huku akiwa kakaa katika kitanda alicho lazwa mama yake
"ni nini tatizo? Dada yako kapewa kashfa nzito juu yako...."
Wakati huo baba katulia tu nae furaha ilimjaa katika moyo, surian ni mtoto waliimpenda kuliko hata asha,
"jamani, kama matibabu tayari, tuondokeni ili kusiwepo na gharama zaidi"
Aliongea baba yake suria huku suria akisema kuwa
"hakuna shaka baba"
Basi baada ya baba yao kusema hivyo waliona ni bora waondoke, kwani mama huyo hakuwa na ugonjwa wowote zaidi ya kupoteza fahamu....

"haya baba, nsikia umeoa jini"
Alisema ZUWENA ambaye ndio mama mzazi wa surian na asha...
"ati nini?? Mama asha?? Unasema suria kaoa nini"
Baba alidakia juu kwa juu baada ya kusikia mtoto wake kaoa jini...
"muulize mtoto wako si huyo hapo"
Wakati huo surian anaendesha gari kurudi nyumbani...
"wazazi wangu, mtajua hayo yote, wacheni tufike nyumbani, kisha nikamchukue mke wangu muje mumuone"
Aliongea surian lakini mama na baba walisema kuwa
"hapana, yaani kama huyo mwanamke ni jini sisi hatumtaki, hatuwezi kukupoteza kwa mara nyingine tena"
Ni maongezi ya wazazi hao wakikataa ndoa ya wawili hao baina ya binadamu na jini... Wakati huo faima katulia kimyaaaaa...
"tena kama inawezekana naomba twende sasa hivi huko kwa mkeo... Wewe ni binadamu huezi ukaoa jini.. Na umekubali vipi?"
Aliongea mama yake asha huku mzee Rashidi akisema
"twendeni huko huko... Mana hata leo hatutaki uondoke katika himaya yetu"
Aliongea mama yake asha,... Lakini ghafla asha akadakia
"surian, si uwasikilize wazazi lakini"
Kiukweli suria alikuwa katika wakati mgumu sana kwa wakati huo... Mana anajiuliza Ataanzaje kumkana maimati, japokuwa kweli ni jini... Suria aligeuza gari kuelekea nyumbani kwake ambako mkewe ndipo alipo...

"halafu na elimu ya dini ulio nayo, imewezekana vipi ukafanya ujinga kama huo suria"
Mzee Rashid aliongea tena kwa hasira, kana kwamba pamoja na dini elimu zote alizopewa, lakini kakubali kuoa jini.
"baba,... Labda niwaambie kwa ufupi kuhusu suala hilo"
"sio kwa ufupi, nataka kujua sababu ni nini, kama ni magari rudisha gari za watu"
Wazazi walikuja juu kwa tatizo la suria kuoa jini, kiumbe ambaye sio jamii yake,...

"baba.... Siku hio nilichukuliwa na kuambiwa nakwenda kupewa kazi nchini dubai,... Kwa vile nilikuwa sina kazi nilikubali, na siku ile nilikuja kuwaaga lakini sikuwakuta, hivyo niliondoka na kutegemea kurudi.. Lakini kumbe haikuwa dubai bali ni ujinini,... Baada ya muda ndio nikafahamu kuwa nipo ujinini na sio dubai... Nilipendwa na jini kiongozi kwa tamaa, akawa na mimi kwa njia za ndoto, lakini yupo alionipenda kwa dhati kabisa na kunipa kinga... Hivyo yule jini akakosa uwezo wa kunifuata, hivyo akatumia njia ya kawaida ambayo kwao ni makosa... Jini yule aligeuka kuwa shetani kwa kuzini na mimi... Ndipo nikapewa taarifa ya kupendwa na jini huyo alionipa kinga,.. Nilishindwa kukataa kwakua nipo ndani ya himaya ya watu,.. Lakini nikaahidi nikija huku duniani nitaachana nae,.. Sasa nilipokuja huku nikamwambia nataka nije kuwaona, lakini yeye akasema katika masharti yao ni mpaka zipite siku saba ndio nije nae,.. Mara zikaongezeka tena,... Zilipoisha ndio nikapanga wiki hii nije nyumbani lakini kabla siku hazija fika ndio leo nikakutana na dada asha... Alafu pia  wazazi wangu?? Kwa hali ilivyokuwa ngumu, nikashindwa kumuacha kwakua alikuwa na mali nyingi sana.. Sasa nina kosa gani hapo wazazi wangu"

Suria alimaliza kuongea lakini ghafla faima kadakia
"kwahio mimi ndio basi"
Aliuliza faima lakini wazazi wakasema
"sisi hatumjui huyo jini.. Twende mkapeane talaka"
Aliongea mzee Rashid huku suria akiwa na wasiwasi juu ya hilo...

Walifika lakini suria ana wasiwasi kuingia ndani,....

Sasa huku ndani shaimati bado yupo,
"we maimati, nahisi nje kuna group la watu"
Aliongea shaimati huku maimati akisema
"najua toka wanaanza kuja... Na najua nia yao"
"nia gani tena"
"familia yake hainitaki"
"na suria nae ana maamuzi gani"
Kabla hajajibu, mama na baba na faima na asha waliingia ndani huku surian akiwa nyuma kabisa....
Maimati na shaimati hawakutaka kujificha (kuto onekana)....
"eti nyie jini ni nani hapa"
Mzee Rashid Aliuliza huku maimati na shaimati wakiangaliana...
"sisi sote hapa ni majini"
Walijinu wote wawili maimati na shaimati.... Ghafla surian ndio anaingia huku akiwa mpole sana... Yani haamini kama leo anatenganishwa na mke wake... Sasa asha alishtuka kuskia ni majini mana asha ana urafiki na shaimati...
"hata wewe pia ni jini?"
"ndio"
Ghafla mama akaingilia kati na kusema
"sasa nataka nimjue mke wa mwanangu surian"
"ni mimi... Shikamoo mama"
Aliitika maimuna na kumsalimia
"marahaba.... Kumbe majini manajua hata kusalimia"
"mama, sisi hatuna tofauti nanyie, ni uwezo tu ndio tumekusudiwa nao"
"sawa.... Sasa mwanangu,? Nimepata taarifa juu ya ndoa ya wewe na mtoto wangu wa kiume, tukiwa kama wazazi wa mtoto wake,... Tumekaa na kujadili swala hili kua, hatukubaliani na ndoa hio, kwani wewe ni kiumbe na huyu ni binadamu, hio ndio sababu ya kuikataa ndoa hio"







No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa