PETE YA KIKE Sehemu Ya 26 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Sunday, February 2, 2020

PETE YA KIKE Sehemu Ya 26







Sasa mama kafika mapokezi shadya hayupo, mana ndio alitegemea ampe shadya apeleke mana ndio kazi yake akiwa kama sekretari,... Sasa mama kila akitaka kiweka hapo mezani kwa shadya, nafsi inamsuta kwanini asipeleke mwenyewe, lakini kila akifikiria kibarua chake kimepatikana kwa njia ya ujanja ujanja, mana mwisho wa umri ni 35 sasa yeye ana miaka 58,..mbona atatukanwa na mtoto mdogo, na mbaya zaidi anaweza kumharibia shadya kibarua chake mana yeye ndio kafanya ile hali ya vyeti feki,.. Mama suria aliamua kupeleka, kama ni kufa kwa kibarua wacha kife kuliko kutopeleka documents za watu,... Sasa kwa mara ya kwanza mama anakwenda kukutana na mtoto wake wa kumzaaa,.. Mama hajui kama anafanya kazi kwenye kampuni ya mtoto wake, na hata mtoto hajui kama mama yake anafanya kazi hapo, na wote wamemisiana mpaka raha,... Surian akiwa ofisini kwake ghafla mlango unagongwa....
"ngo, ngo, ngo, ngo, ngo"
Ilisikika sauti kugongwa kwa mlango, na surian naye akajibu kwa kumkaribisha aliegonga mlango
"karibu, ingia ndani"

ENDELEA.......

Mama surian alikuwa na uoga juu ya kukutana na boss uso kwa uso, kwani kanuni na taratibu za kampuni hiyo, hairuhusu mfanyakazi kuanzia miaka 36, yaani miaka 35 ndio mwisho wa mwajiriwa kuomba kazi, kwani sheria ya kampuni hio ni kuanzia miaka 18 mpaka 35 mwisho, hivyo ukiwa na umri zaidi ya miaka 35 basi kazi hutopata,.... Sasa mama surian ana miaka 58 na boss hajui kama kwenye kampuni yake kuna mfanyakazi mwenye umri mkubwa,

Sasa mama surian akiwa hapo mapokezi anajishauri namna ya kuingia ndani ili kuweza kufikisha Documents hizo ambazo amepewa na kiongozi wa idarani apeleke kwa boss baada ya kiongozi husika kupata haja ya ghafla na kushindwa kutimiza wajibu wake ipasavyo,...

Mama surian alifikiria mno na kupata jibu, kwa namna nyingine....
"ile namba, nilisikia ni sauti ya mtoto wangu, na ni namba ya boss huyu huyu, sasa hapa ndio nafasi yangu ya kwenda kumuona"
Alijiongelea mama huyo huku akishika mafaili hayo na kuusogelea malango wa kuingilia ofisini kwa boss surian...

Sasa ile anataka kugonga tu, mara shadya katokea...
"heee heee heee we mama wewe, hivi umedhamiria kuingia huko ndani"
Aliuliza shadya huku mama alijisikia kufanya kosa kubwa japo sio kosa lake,..
"samahani mwanangu, ni kweli nimepewa hizi karatasi nilete huku kwa boss, sasa nimekuja sijakukuta, je ningefanyeje mimi jamani mwanangu"
Aliongea mama huyo tena huku akilengwa na machozi kana kwamba alitamani hata kulia
"yaani ungeingia,.. Sisi wote tusingelikua na kazi, mana mimi ndio nimefanya majambozi ukaingia, leo ikijulikana mimi nitakuwa sina kazi mama... Haya lete nikusaidie, wewe kaendelee na kazi"
Aliongea shadya ama Cecilia kuwa mama huyo akaendelee na kazi tu,.. Lakini mama ilimuuma sana kwani kakosa nafasi ya kwenda kumuona huyo boss, mana unaambiwa hajawahi kuonekana toka kampuni kufunguliwa, zaidi ya juzi alipotoka na hakutembea sana akarudi ofisini kwake,..

Sasa huku ndani ofisini kwa surian akiwa katulia hakuwa na kazi ni kama alikuwa akizisubiri tu hizo faili ambazo zilitakiwa kuletwa toka idarani,....

ghafla mlango unagongwa....
"ngo, ngo, ngo, ngo, ngo"
Ilisikika sauti kugongwa kwa mlango, na surian naye akajibu kwa kumkaribisha aliegonga mlango
"karibu, ingia ndani"

Huku nje mama akawa anajivuta kuondoka ili asije kuonwa na boss,.. Lakini sasa ile anajivuta kuondoka, ghafla alishtuka kana kwamba kuna kitu kaona,.. Mapigo yake ya moyo alimwenda mbio ghafla tu huku akiwa kama haamini au ana hisia fulani hivi,... Mama surian aliondoka lakini kichwa chale bado kilikuwa na mawazo ya ghafla,... Alirudi kazini kwake na kuendelea na kazi, lakini kila wakati anarudisha picha ya kile alicho kiona..

Sasa kumbe wakati ule shadya anaingia ofisini kumbe mama aliona kichwa cha boss kupitia ule mwanya wa mlango, pale pembeni kabisa kwenye vile vishikizo vya mlango,.. Mama surian aliona kisogo cha boss na kukifananisha na kisogo cha mtoto wake, hivyo ndicho kinacho muumiza kichwa, na kila akilinganisha matukio yote, ni kama anamuona surian, ila hana uhakika na hilo,....
"yaani kichwa kama cha mtoto wangu"
Alijisemea mma surian bila kujua kumbe kweli ni mtoto wake,... Lakini hajui na mtoto pia hajui kama mama yake yupo hapo kwani vyeti alivyotumia mama, vina mkanganyiko wa habari zake,... Wakati huo huo asha alikuja kwa mama yake kumjulia hali mana hakawii kupata mshtuko,.. Asha alimkuta mama yake akiwa katika dimbwi la mawazo mengi akikiwaza kisogo cha boss,...
"mama mbona una mawazo hivyo"
Aliongea asha huku mama akishtuka na kuendelea kufanya usafi
"asha umefuta nini huku... Ukionwa na viongozi wako itakuwa tabu"
Aliongea mama asha akiwa anapenda sana mtoto wake asichezee kazi kwani hawana wanacho kitegemea zaidi ya kazi hio,
"mama nimekuja msalani tuu"
"haya ingia basi kisha urudi ndani"
"sawa, ila una mawazo sana mama angu"
"asha?? Ni kweli kama ulivyo hisi... Unajua nilipeleka makaratasi yaliotoka huko ndani kwenu, nilipeka ofisini, lakini katika hali ya mlango kufunguliwa niliweza kuona kidogo cha boss... Asha?? kile kisogo ni kama cha kaka yako surian, yaani vile vile"
Aliongea mama surian huku asha nae akiendelea kuchanganya matukio
"sasa mama, ina maana kaka surian ndio mwenye hii kampuni? Mana ile namba ni sauti yake... Kichwa umesema ni chakwake... Atakuwa yeye mama"
Aliongea asha huku mama akikataa..
"hapana asha,.. Surian hawezi kuwa na utajiri huu ashindwe kuja nyumbani... Hebu ingia msalani uende kazini"
"sawa, lakini mama... Nina wasiwasi na hilo mama"
"asha, we humjui surian upendo wake kwetu?.. Leo awe na hali hii atuangalie kweli?? Hapana, mimi nina imani sio surian wangu"
Aliongea mama huku asha akiingia ndani kujisaidia... Kwa sasa maisha yao sio magumu sana kwani wanafanya kazi, hivyo mahitaji kwao ni kama kawaida...

Kesho yake ikiwa ni siku ya wafanyakazi kupewa mishahara yao, hivyo siku hio boss hua hakai kwani hakuwi na kazi kutokana na msongamano wa kila mmoja aingie ofisini kusaini mshahara wake,.. Hivyo mpaka wafanyakazi 500 waishe ni siku nzima itaishia hapo, hivyo siku ya leo bosa kaleta mishahara ya wafanyakazi wake kisha akaondoka, hivyo meneja akishirikiana na shadya wakiwa wanatoa mishahara kwa wenzao...

"Leo nataka tutembee mjini unionyeshe mji wenu"
Ilikuwa ni sauti ya jini maimati akimtaka mumewe amtembeze katika mji huo,
"ila sitembei kwa mguu"
Suria alijibu kuwa hatembei kwa miguu mana mkewe anapenda kutembea kwa miguu,..
"sawa, mana hupendi kutembea kwa miguu"
"sipendi kwasababu gari ipo, yanini tuumie"
"sawa babaa..."
Ikiwa ni majira ya saa sita za mchana

Huku kwa faima akimalizia kuhudumia wateja wake... Tariki alionekana kuwepo nje ya duka hilo, na siku hio alikuwa na furaha sana kwani katoka kupokea mshahara muda sio mrefu, hivyo hapo alipo ana furaha ya hali ya juu na kila siku yeye humdanganya faima kuwa ana pesa, kumbe hakuwa na lolote juu ya hilo

Baada ya faima kumaliza huduma kwa wateja, alitoka nje ili kwenda kupata lanchi kwani ilikuwa ni mchana wa saa sita,
"umefuata nini hata riki"
Faima alimuuliza riki kuwa alifuata nini hapo kazini kwake,...
"faima? Mbona umebadilika ghafla? Wakati ulikuwa unaelekea vizuri"
"haijalishi... Enhee nilikupa mtihani wangu na kukwambia ukiuweza basi naweza kukufikiria juu ya hilo"
Aliongea faima kuwa kuna mtihani alimpa lakini bado hajautimiza, na mtihani alio mpa ni riki alete picha ya boss wake,....
"skia faima... Kama wewe ni wangu basi ni wangu tu,... Namba ya boss wangu ninayo hapa wasap, japo sijui unataka ya nini... Kama ni pesa hata mimi ninazo, hivyo sioni haja ya kutaka namba au picha ya boss wangu... Mi najua hukutaka picha, najua ulitaka namba. Sasa simu yangu hii hapa... Chukua namba zake"
Riki aliongea mengi huku akiwa hana amani kwani anajua faima anapenda wanaume wenye pesa, kumbe faima kasikia kuwa boss wa kampuni hio ni surian, hivyo ndio mana akamtuma riki alete picha ya boss wake....
"riki unanikosea heshima... We huoni kuwa tunafanya biashara za nguo za dini, na hio kampuni inahusika na mavazi hayo"
Aliongea faima huku akiwa kashika simu ya riki ambayo ina namba za meneja sadiki,...
"basi yaishe... Tafuta hapo nimeandika boss sadiki"
Aliongea riki kisha faima akafungua WhatsApp, na kuanza kukagua
"mbona namba zako nyingi huku WhatsApp unasevu herufi tu"
Aliongea faima baada ya kukuta herufi tu katika listi ya WhatsApp,..
"umesema umesevu nani"
"boss Sadiki... Angalia alfabeti za mwanzo baada ya Alfabeti A"
Aliongea riki huku faima akianza mwanzo,... Lakini sasa akiwa anashuka chini,.. Ama kweli unambiwa chako ni chako tu,.. Faima alijikuta anabonyeza herufi A ambayo ndio namba ya surian,.. Lakini hapo hajajua kama ni surian,..
"sio hio,... Huyu ni mjomba wake asha huyu"
Aliongea kuwa huyo ni mjomba wake asha...
"asha yupi huyo... Mtumeeeee.... Surian wangu jamani Uuuuuuuuuwiiiiiiii"
Aliongea faima baada ya kifungua ile picha,... Sasa riki akashangaa
"wewe huyu ni mjomba wake aisha, na hata juzi nilimuona mjini"
Riki aliongea hayo lakini faima hakumsikiliza, kwani alikuwa akilia kwa furaha ya hali ya juu...
"sasa unalia nini"
Aliuliza riki huku faima akiichukua ile namba, mana picha tu ilitosha..
"riki, ahsante sana... Huyu ndio mchumba wangu, na ndio inasemekana anamiliki hio kampuni... Na huyu ndio surian wangu huyu"
Aliongea faima huku riki akibaki mdomo wazi kwani haamini kuwa kamletea faima mchumba wake...
"ina maana, mbona sikuelewi faima"
"huyu sio mjomba wake aisha, huyu ni mdogo wake kabisa... Shika simu yako, afu mazoea sitaki"
Aliongea faima kisha akaingia zake dukani kuhudumia wateja... Riki haamini macho yake kwa alicho kifanya,... Sasa riki akaona ngoja arudi kule kampuni akapate uhakika kwa asha....
Wakati huo riki anaondoka kwa hasira, faima alikuwa anahudumia huku machozi ya furaha yakimtoka...

Tukija huku kampuni ambako baadhi ya wafanyakazi wanamalizia malizia kupewa mishahara yao,.. Watoa mishahara ni wawili, shadya anatoa mshahara, na Sadiki anasainisha... Kwahio mfanyakazi unapitia kwa saidiki unasaini kisha unakwenda kwa shadya kuchukua kibunda.... Sasa sadiki alilishangaa jina moja hapo kwenye listi....
"ZUWENA RASHIDI SURIA analipwa laki nne"
Alijisemea sadiki huku akimuangalia huyo mama.....
"we mama si unafanya usafi wa vyoo"
"ndio baba"
Mama surian alijibu kwa huruma kana kwamba sadiki hajui kuwa kuna mgeuzano wa vitengo na mishahara yake...
"shadya??"
"abee boss"
"huyu mama si anafanya usafi kule public toilets"
"ye.. Ye.. Ye. yesi boss"
"sasa inakuwaje analipwa laki nne, mshahara wa msimamizi wa idarani kabisa"
Aliongea meneja huku shadya akitetemeka,... Mana meneja yuko juu na shadya ni sekretari tu..
"labda boss ndio kampangia mwenyewe, mana mishahara yote kapanga boss mwenyewe"
Aliongea shadya kana kwamba, Meneja hajaju kwanini mama mwenye umei huo anafanya kazi hapo,... Na hakuhoji ishu ya umri mana anaju kuwa hata boss anajua kuwa kuna mfanyakazi mwenye umri mkubwa....
"hapana... Sidhani kama boss anaweza kulipa mfanyakazi wa usafi mshahara wote huu"
Aliongea meneja huyo huku akiwa kama anakazia,.. Na anajua kabisa huyu ni mama yake asha hivyo anataka kufanya fitina kwasababu asha kamkataa kimahusiano....
"lakini boss ndio kaamua kumlipa hivyo,... Hivyo mi naona tumpe tu boss"
Shadya aliongea kumtetea mama surian, lakini sadiki akagoma huku akitoa simu na kusema..
"hapana... Wacha nimpigie,.. Huu uchumi umebana sana hatuwezi kulipa mfanya usafi wa vyoo mshahara wote huu.... Ngoja nimpigie huu mshahara tuupange upya"
Aliongea sadiki huku akilitafuta jina la boss surian.... Wakati huo mama surian analengwa lengwa na machozi kwasababu hana la kusema juu ya hilo, mana hakuingia kwa vyeti vyake, na mbaya zaidi umri wake ndio tatizo la kazi yake... Shadya haamini macho yake kwa kile sadiki anacho kwenda kukifanya...
"boss sadiki, tumlipe tu mwezi huu kisha mwezi ujao tutampunguzia"
"hapana... Afu wewe inaonekana unalijua hili swala... Ngoja boss apokee simu"






No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa