PETE YA KIKE Sehemu Ya 25 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Sunday, February 2, 2020

PETE YA KIKE Sehemu Ya 25




"kweli ni yeye mbona"
Alijisemea tena huku akifungua ile picha na kuiangalia kwa mara nyingine tena, na kuhakikisha ni yeye mjomba wake,... Tariki alikimbia mbio mpaka kazini na kumkuta asha ndio anapanda basi kwenda nyumbani
"asha asha.... Mjomba ako nimemuona kule mjini, twende ukamuone"
Aliongea tariki na kumfanya asha atetemeke, mana sio mjomba wake kama alivyo mwambia tariki, bali ni mdogo wake kabisa....
"unasemaje tariki"
"twende sasa unapoteza muda"
"tariki unasema kweli"
"bwana wewe, twendeeeeeee"
Asha alijikuta analia kabla hata ya kumuona mdogo wake wa damu aliosingiziwa kumuua,... Na lazima awe yeye kwasababu tariki asingelimjua kama sio ile namba alio mpa,....
"sasa unalia nini asha... Twende ukamuone mjomba wako"
Sasa asha akiwa anazidi kulia kwa furaha huku wafanyakazi wakimwangalia,.. Ghafla geti dogo linasukumwa, kana kwamba kuna mtu au watu wanaingia.... Wafanyakazi hawaamini kwa kile wanachokiona, hata asha mwenyewe haamini macho yake.......

ENDELEA........

Wakati huo tariki akiwa anaingia ndani ya geti kuja kumpa taarifa asha kuwa kamuona mjomba wake ambaye alimpa namba ili amuone kupitia WhatsApp, lakini asha hakupata nafasi ya kumwona, hivyo riki alimuona kwenye picha na pia akamuona live bila chenga,...

"unajua nini mke wangu"
Aliongea surian huku wakiwa wanatoka kula lakini mke haonekani kama kawaida yake,...
"sema"
"sasa hivi pale getini patakuwa na watu wengi,... Nataka nisionekane nikiwa naingia"
Aliongea surian mana anajua huo ni muda wa wafanyakazi kutoka kwenda majumbani, hivyo macho yatakuwa mengi sana kwake,
"kwani unamwogopa nani babaa"
"wewe mbona huonekani, kwani unamwogopa nani"
Surian alimuuliza mkewe,... Ndipo mke akamshika surian sikio, hivyo wote wakawa hawaonekani, ila wao wanaona...
"sasa kwakua wewe hawakuoni, nataka nawe usiwaone"
"aaahhh sasa si nitajikwaa"
"hapana, nami nataka usiwaone"
Aliongea maimuna akimtaka surian afunge macho kwani kama haonwi basi naye asiwaone,... Sasa wakawa wanafanya kama mchezo wa mke na mume kufumbana macho yao kwa kutumjia mikono yao, hivyo walikuwa wakipeana zamu,... Ukimzima mwenzio macho basi hakikisha unamwongoza njia ilio sahihi asipaamie mtu.... Sasa walipofika getini wakiwa na mchezo huo huo, ikafika zamu ya surian kufumbwa macho,.. Na wakati huo hawaonekani wote,... Sasa wafanyakazi huku ndani walishangaa geti ndogo imefunguliwa kisha akafungwa, sasa wafanyakazi wakawa wanashangaa mbona geti imejifungua na kujifunga, na hakuna mtu alie ingia.... Hayo ni mawazo yao wao, lakini kumbe ni surian na mke wake ndio wameingia, na kwakua hawaonekani, wafanyakazi walistaajab mana hakuna alie ingia lakini wapo walio ingia ndani ya kampuni,... Surian na mkewe waliingia mpaka ofisini huku wakifanyiana baadhi ya utani wa hapa na pale,...

Huki nje watu wakasahau swala la geti kujifungua na kujifunga....
"twende ukamuone mjomba wako"
Aliongea riki lakini asha hakutaka kwasababu juzi juzi aliitiwa kwenda kumuona surian kule TANGA BITES, lakini akapotea ghafla na kuto muona, hivyo anaona hata akienda huko hawezi kumuoa,... Na kama sio surian kushikwa sikio na maimuna, basi asha angemuona kwasababu alikuwa pale pale mlangoni, na kama sio mchezo wao wa kufumbana macho, basi surian angemuona dada yake,.... Asha hakutamani kwenda huko mjini kati kwenda kumwona ndugu yake,.. Mana hatomuona zaidi ya kuumia moyo wake,... Tariki aliondoka zake huku akiwa na hasira mana kachelewa kwenda kwa faima kisa kumwita asha akamwone mjomba wake,... Kampotezea muda mwingi sana...

ILANI YA WAHALIFU WA KIMTANDAO

TAHADHARI SANA KWA WEWE UNAYE UZA KAZI HII KATIKA MITANDAO YAKO YA KIJAMII...

HATUA KALI ZITACHUKULIWA KWA KIFUNGU CHA UKIUKWAJI WA SHERIA ZA MITANDAO, KWA KOSA LA KUHUJUMU KAZI ISIO YAKWAKO..

NDUGU MSOMAJI, HAKIKISHA ANAEKUUZIA SIMULIZI HII NI MMILIKI HALALI MWENYE NAMBA HII, +255714419487... LAA SIVYO NAWE NI MMOJA KATI YA WAHUJUMU WA KAZI ZA WATU, KATIKA MITANDAO YA KIJAMII.....

KWA WALE NDUGU ZANGU WA KUPOSTI KWENYE KURASA ZAO,
HAKIKISHA, UNAPATA IDHINI KUTOKA KWA MMILIKI HUSIKA KWA SIMU NO, +255714419487 WhatsApp
ILI UPEWE MAELEZO, VIGEZO, NA MASHARTI YA KUPOSTI KWENYE UKURASA WAKO WOWOTE ULE..

JIEPUSHE KUKOPI KAZI HII BILA IDHINI YA MMILIKI HUSIKA

TAFADHALI SANA HATUPO KWA AJILI YA KUPELEKANA PABAYA KISHERIA.....

TUWE MAKINI NA KAZI ZA WATU KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

Huku ofisini mke na mume wanakusanya vitu vyao ili waondoke, lakini surian kwake mda bado kabisa
"mi naona tangulia tu, nikute chakula kitamu"
"afu mume wangu skuizi una kademu wewe"
Aliongea maimuna huku surian akitabasamu
"si bora ningelikuwa nako ningefurahi kwelikweli"
"Jamaaaaani suri, ina maana ukipata kademu unaniacha"
"weeeeeee, nikuache wewe, nani kasema"
"mbona sasa unanitisha jamani... Yaani ndoa za utotoni zina tabu.. Bira tungelikuwa na umri mkubwaaa"
Aliongea mke wa suria ambaye ni jini, lakini ndani ya ndoa na mume wake haruhusiwi kutumia asili ya jini, mana huyo mume wake ni binadamu wa kawaida,...

Muda ulipofika surian na mkewe waliondoka ikiwa ni pamoja keshaondoka, yaani surian ni mfanyakazi wa mwisho kutoka, kana kwamba kesha zoea kuto onekana mapema hivi, yeye na ndani... ndani na yeye

Asha akiwa nyumbani kwao akiandaa mambo ya usiku, mama haamini kama simu yake imeingia maji,... Lakini kila akiikumbuka ile sauti anajiskia raha lakini pia maumivu juu yake, kwani kaongea na mtoto wake na asijue alipo,.. Kwa sasa wote hawana simu, ni baba peke yake...
"hebu nipeni hio namba nimpigie huyo mtu"
Aliongea mzee Rashidi, mana kuumwa kwa mkewe kumetokana na sauti ya surian
"hapana baba asha, acha kwanza akili yangu itulie, kama yupo yupo tu"
Aliongea asha huku akipika chakula, na yeye anajua leo alikuwa amuone ndugu yake,... Sasa hisia za mapenzi hakuna kwani ana tetesi juu ya ndugu yake kuwa mmiliki wa ile kampuni

Baada ya siku kadhaa kupita ikiwa ni siku ya jumatatu ya wiki nyingine, kazi ilikuwa ikilindima kama kawaida oda zilimiminika na kufanya wafanyakazi waongezwe mara dufu, kwani kazi Iliweza kwenda vizuri,...

Siku hio ilikuwa ni mwisho wa wiki ya mwezi huo hivyo yupo kiongozi wa kike aliopewa kazi ya kuandika wafanyakazi ambao hawajafika, kwani kesho ni siku ya kupokea mishahara,... Na siku hio mama suria yupo kazini kama kawaida yake

Tukirudi huku kwa faima tunamwona akiwa na dada yake
"hivi dada? wewe ndio unampa nguvu tariki"
Faima alimuuliza dada yake zamina, mana zamina Alianza tabia ya kumkuadia mdogo wake,....
"kwani tariki ana ubaya gani, kijana wa watu ana hela, ina maana bado unampenda huyo mzimu wako"
Aliongea zamina akimaanisha kuwa faima anampenda mtu aliofariki dunia,
"skia dada, surian yupo hai na yupo mjini"
"nani kakwambia kama surian yupo mjini, tayari kesha oza hata mfupa wake kuukuta ni bahati sana"
"hata kama, lakini ipo siku surian nitamuona tu"
"labda kwenye ndoto lakini sio kwa macho yako... Mkubalie tariki faima jamani"
Aliongea zamina, kwani anamjua tariki ana hela kumbe nae ni choka mbaya,
"kwanza hata sijamuona huyo tariki mwenyewe, kama siku nne hivi sijamuona"
"sasa wewe si humtaki, kila akija mtoto wa watu unamkatisha tamaa, Angalia na uzuri wako Fey unapotea bure"
"bwana weeee, nina mchumba wangu, hao wanaume wako utajua nao mwenyewe"
"shauri yako... Kesho namwambia aje mara ya mwisho, na unapoteza mume hivyo"
"yule sharobaro yule"
"ana hela yule acha ujinga fey"
"sitaki bwana, kwani si hata wewe ni mwanamke"
"fey, unanitukana ivyo ujue"
Zamina alishikwa na hasira kwa maneno ya mdogo wake kumwambia kuwa hata yeye ni mwanamke hivyo Anaweza kumkubalia vilevile...
"dada, hebu nenda nyumbani, ukumbuke hapa ni dukani kwa watu"
"sawa,... Ila ngoja tu"
Zamina alikasirika sana, na hata fey kachoka kutongozeshwa kwa wanaume, mana dada yake ni mtu wa kudanga tu na wanaume hivyo anataka na mdogo wake awe kama yeye, na fey hapo alipo mzimaaaaaa ana bikra yake, na hio alimtunzia surian, lakini mpaka leo suria haonekani....

Sasa tukija huku MICCO yule dada kiongozi alikuwa akipeleka zile documents ambazo kaambiwa aziandae kwa niaba ya kuwalipa wafanyakazi mishahara yao, hivyo amletee takwimu ya wafanyakazi wapo wangapo, kwa maana kuna walio ingia na walio toka kwa kuacha kazi, na idadi hio anaijua dada msimamizi mkuu wa idara zote,.. Sasa akiwa anatoka na documents hizo, haja ilimbana kana kwamba asingeweza kufika ofisini kwa boss kwasababu ana tumbo la kuendesha... Sasa kila akiangalia mtu ampe apeleke haoni,... Mara kamuona mama usafi ambaye ni mama yake surian,...
"we mama hebu peleka hizi documents kwa boss"
Aliongea dada huyo kisha akawa anaingia chooni haraka haraka
"jamani mwanangu, kule siruhusiwi kufika"
Mama surian alilalamika kuwa kule haruhusiwi kufika kwani hata kazi yenyewe kapewa kiujanja ujanja, leo aende mpaka ofisini kwa boss na umri huo ambao hautakiwi kwenye kampuni ya MICCO,..
"we mama vipi, kama hutaki kazi useme, peleka haraka basi"
Dada Aliongea kwa hasira mno kwani ana cheo kikubwa katika idara za ndani, hivyo ana sauti kwa baadhi ya wafanyakazi... Sasa mama kaona kuliko aharibu kibarua chake bora apeleke tu kama ni kukosa kazi basi

Pale mapokezi shadya hayupo kaelekea kujisaidia katika vyoo vyao vya ofisini,.... Mama surian kaambiwa apeleke kwa boss, afu boss mwenyewe ni suria ambaye ni mtoto wake wa Kumzaa,.. Lakini hawajuani mpaka leo kuwa wanafanya kazi kampuni moja,... Sasa mama kafika mapokezi shadya hayupo, mana ndio alitegemea ampe shadya apeleke mana ndio kazi yake akiwa kama sekretari,... Sasa mama kila akitaka kiweka hapo mezani kwa shadya, nafsi inamsuta kwanini asipeleke mwenyewe, lakini kila akifikiria kibarua chake kimepatikana kwa njia ya ujanja ujanja, mana mwisho wa umri ni 35 sasa yeye ana miaka 58,..mbona atatukanwa na mtoto mdogo, na mbaya zaidi anaweza kumharibia shadya kibarua chake mana yeye ndio kafanya ile hali ya vyeti feki,.. Mama suria aliamua kupeleka, kama ni kufa kwa kibarua wacha kife kuliko kutopeleka documents za watu,... Sasa kwa mara ya kwanza mama anakwenda kukutana na mtoto wake wa kumzaaa,.. Mama hajui kama anafanya kazi kwenye kampuni ya mtoto wake, na hata mtoto hajui kama mama yake anafanya kazi hapo, na wote wamemisiana mpaka raha,... Surian akiwa ofisini kwake ghafla mlango unagongwa....
"ngo, ngo, ngo, ngo, ngo"
Ilisikika sauti kugongwa kwa mlango, na surian naye akajibu kwa kumkaribisha aliegonga mlango
"karibu, ingia ndani"






No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa