KOVU LA MOYO 14 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Friday, February 7, 2020

KOVU LA MOYO 14




Angelo alimvuta Jonas mpaka kwake na akumuuliza ilimtoka ngumi moja takatifu mpaka katika Sura ya Jonas, ngumi ambayo ilimpeleka Jonas mpaka chini na kuumuka kama ngano iliyotiwa amila kwa wingi.
Angelo alitaka kuendelea kumfuata Jonas ili akamshikishe adabu, lakini robby alimzuia na kumkamata ipasvyo ili amuepushe Shetani.
Jonas baada ya kuinuka ndio alikuwa kama amemeza cd iliyokuwa imejaa matusi na alikuwa ameifungulia mtaa mzima akimtukana Angelo na mwenzake Poshie, na kuwafanya wapita njia waliokuwa wanapita maeneo hayo wasimameme na kutaka kujua nini kinachoendelea ....
Kauli za Jonas zilizidi kumchefua Angelo na hasira zikazidi kumpanda mwishowe akaponyoka na kumkimbilia Jonas ... Alifika na kumrukia miguu miwili ya kifua na kabla Jonas hajainuka Angelo alimfikia na kumkalia na akawa anampa ngumi za uso mithili ya Mike Tyson yupo ulingoni anapambana .... "Angelo muache utamuumiza, tafadhali nakomba mpenzi wangu achana naye tuondoke" ... Poshie alipiga kelele akimsihii mpenzi wake aache maswala ya ugomvi na waondoke eneo hilo ... Robby akishirikiana na baadhi ya watu waliokuja kuamulia ugomvi, waliweza kumshika Angelo na kumtoa pale alipokuwa amemkalia Jonas na akimpa ngumi za haja ...
Jonas aliinuka pale chini na kutaka aachiwe ili akapambane na Angelo huku mdomo ukiwa umepasuka na ukitoka damu kwa wingi ...
Hakuna aliyetaka kumachia na walimkamata ipasavyo, na baada ya kuona ameshikwa sana Jonas aliamua kuendelaza matusi yake akiwatukana kama hana akili nzuri.
"Sijui unafanya mambo gani Angelo? Badala ya tuangaikie maswala yako kwanza, unaenda kuyachokoza mengine sasa kama akienda polisi unafikiri itakuaje?" ... Robby alichukia na kumsema Angelo huku wakiwa wanaondoka pale kwenye ugomvi ... "Labda umwambie wewe Robby anaweza kukuelewa mana wewe ndio Rafiki yake mkubwa. Tatizo la Angelo yeye kila siku bado anajiona mdogo na hataki kubadilika sijui kwanini" ...."Ukisema hivyo Poshie utakuwa unakosea! Inamana wewe umefurahia kwa matusi aliyokuwa anatumwagia yule mpuuzi?" .... "Sijafurahia lakini pia sijafurahia na wewe kwa upuuzi wako wa kwenda kupigana na mpuuzi kwa sababu waote mmeonekana wapuuzi mbele ya watu ambao walikuwepo pale, kwani we ungenyamaza na tukondoka pale inamana matusi yake yangetutia vidonda? ... Poshie alimwambia Angelo huku akiwa amechukia kwa swala ambalo Angelo ametoka kulifanya pale.
Baada ya kina Angelo kuondoka eneo lile, wale Watu waliokuwa wamemshika Jonas walimuachia na kuondoka zao .... Jonas aliokota kipande cha mti na alikuwa akiwakimbilia wakina Angelo walipokuwa wameelekea ....
"Angelo anakuja huyooo" ... Poshie alipiga kelele, baada ya kumuona Jonas akija mbio huku akiwa amelenga kumpiga Angelo na ule mti ... Angelo aligeuka nyuma na kumkwepa Jonas ambaye alikuwa ameshanyanyua juu mti ili ampige Angelo lakini kwa bahati mbaya baada ya Angelo kumkwepa, ule mti ulitua kichwani kwa Poshie .... "Buuuuuuu!!" ... Poshie alikuwa akiyumba nakwenda kuliangukia tumbo. Robby alimuwahi na kumdaka lakini akatereza na Poshie akamuangukia Robby mpaka chini Pwaaaaaa!! ...."Poshieeeeeeeeeeeee" .... Angelo alipiga kelele na kumkimbilia mpenzi wake ili kwenda kumtazama kama bado alikuwa mzima ...... "Poshie amka mpenzi wangu, tafadhali Poshie usife bado nakuitaji amka" .... Angelo alimtikisa huku akimuamsha Poshie lakini wapi Poshie hakuwa hana kauli hata kidogo.
Damu zilikuwa zikimmwagika kwa wingi Poshie kiasi ambacho Roby alianza kupatwa na wasiwasi akihisi labda Poshie atakuwa amekufa.
Hakuna kitu kibaya kama kuona damu ya mtu aswa unapohisi kuwa utakuwa umemuua mwenzako bila ya kukusudia, Jonas alikuwa ameshikwa na butwaaa na kujikuta akitetemea akiamini lazima Poshie atakuwa amekufa ... "Unaona umeua, Jonas unaona umeua" ... Robby alimwambia Jonas huku akimfuata alipo. Jonas alistuka na kuzidi kuogopa, hakutaka kuendelea kusubiri alikurupuka na kukimbia eneo lile
****
Walipata msaada kwa wasamalia wema na wakamkimbiza Poshie Hospital na akapata kitanda ..."Angelo wewe ni mtu mkubwa sasa na karibuni unatarijia kuitwa Baba, hivyo unatakiwa ubadirike sana kutoka katika maisha yako ya zamani ili kuingia katika maisha mapya. Kwasasa wewe hautakiwi uishi kwa kujifikiria wewe mwenyewe bali unatakiwa uishi kwa kuifikiria familia yako yani wewe, mkeo na mtoto wako. Kosa moja ambalo utakalolifanya basi kaa ukijua unaweza kuigharimu familia yako kwa kosa lolote unaloweza kulifanya. Nafikiri mfano umeuona leo" ...
Usiku huo Hawakulala hata lepe moja la usingizi badala yake Robby aliutumia usiku huo kumpa kichen party bila vyombo Angelo {Kumfunda bila sherehe} ... Angelo alimuomba sana msamaha rafiki yake na kumuakikishia kwamba jambo hilo halitokuja kujirudia tena katika maisha yake.
*****
Asubuhi kulipokucha waliandaa chai chumbani kwa Robby ili wampelekee mgonjwa wao. Robby alitoka nje ili kumvizia Mama yake ili hasimuone Angelo na wakafanikiwa kutoka salama katika chumba cha Robby na wakaelekea Hospital.
Baada ya kufika Hospital walistuka baada ya kumkuta Jonas akiwa na Poshie huku Poshie akiwa amepata faham na wakiongea na akiwa amemletea Poshie mtoli na alikuwa akila.
Japokuwa Robby alimuhusia sana Angelo jana usiku lakini Angelo alichukia kumkuta Jonas akiwa na mkewe ..."Umefuata nini hapa" ... "Angelo lini utabadilika mpenzi wangu? Yani Badala ya kuniuliza mimi kwanza hali yangu wewe unashikiria maswala ya ugomvi tu, basi gombaneni tena mniue kabisa" .... Poshie aliongea kwa uchungu huku akilia na Angelo alimuomba sana msamaha Mpenzi wake ... "Jonas amekuja hapa kwa niaba yako na yangu pia amekuja kutuomba msamaha na amesema amejifunza kutokana na makosa, istoshe yupo tayari kutusaidia" .... Jonas aliwapigia magoti na kuwaomba msamaha kisha akawaambia .... "Kuna chumba kinapangishwa kule bondeni kwa Tsh 15,000 Mwenyewe alikuwa anataka kodi ya mwaka mzima ambayo ni 180,000. Mimi katika akiba yangu, nilikuwa na Tsh 1,00,000 nilikuwa nataka kuwasaidia je mtakuwa na hiyo ya kuongezea hili mlipie pale mpate kwa kujishikiza" ...
Angelo hakuamini hata kidogo kwa maneno ambayo ameyaongea Jonas alimshukuru sana kwa moyo wake wa huruma na kuombana msamaha ... Robby aliamua kutoa simu yake ili ikauzwe na wapate kiasi cha kuongezea ... Poshie pia aliamua kutoa simu yake ili nayo iuzwe na wapate pesa ya kuongezea katika kodi.
Robby, Jonas pomoja na Angelo walitoka hospital na kuelekea mtaani ili wakauze simu na wapate kiasi cha kuongeea pale katika kodi ...
Walifanikiwa kuiuza simu ya Robby kwa Tsh 50,000 na simu ya Poshie kwa Tsh 30,000 na wakaongzea na ile pesa aliyokuwa nayo Jonas na ikafikia Tsh 180,000 .... Haraka walitoka pale na kuelekea kule kwenye chumba na walikuta tayari kimeshapata mpangaji.... Nguvu ziliwaishia na wailikaa chini huku wakiwa wamechoka kabisaa.
Mchana ulipofika walitoka na kuelekea Hospital na kukuta Poshie akiwa ameruhusiwa lakini walikuwa wanadaiwa kiasi cha Tsh 50,000 pale Hospital na kuna dawa za kiasi cha Tsh 10,000 walitakiwa kununua....
NINI KITAENDELEA? ...



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa