KITUMBUA CHA KIHINDI SEHEMU YA 22 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Wednesday, February 5, 2020

KITUMBUA CHA KIHINDI SEHEMU YA 22





ILIPOISHIA..
“Hii kazi inaelekea ni ngumu Ashura, wacha nikamridhishe bosi” Zawadi alizungumza.
“Kwahiyo unataka kusema mimi siwezi kikazi?” Ashura akahoji kwa msisitizo.
“Unaweza Ashura, lakini tambua kuwa hujawahi kuua mtu wewe” Zawadi alieleza.
“Unafikiri nitaanza lini kama sio leo? Ngoja na mimi nikamthibitishie bosi kuwa niko vizuri kikazi” Ashura alizungumza kwa kujiamini.

ENDELEA...
“Ok utaua, lakini wacha mshenzi huyu nikammalize mwenyewe” Zawadi alizungumza kwa msisitizo.
“Basi twende sote” Ashura akatoa wazo.
“Hapana Ashura, wewe baki na kikosi kazi ukiandae kwaajili ya mapambano. Kama kazi itakuwa ngumu basi tutawafahamisha mje kutoa msaada mara moja” Zawadi alieleza.
“Lakini Zawadi…” Ashura alitaka kuzungumza kitu lakini kabla hajamaliza Zawadi alimkatisha.
“Hakuna cha lakini Ashura, Hii ni mbinu moja wapo ambayo tunaitumia katika wakati kama huu. Kuwa makini” alizungumza Zawadi na kuondoka haraka pamoja na vijana wengine watatu huku wakimuacha Ashura mwili wake ukichemka kwa hamu ya kutaka kuua. Roho yake ilikuwa imekwisha mbadilika na kusikia harufu ya damu ya binadamu imemtawala kwenye tundu za pua yake. Alirusha ngumi kwa hasira na kupiga ukuta. Aliamini kuwa hakuwa ametendewa haki na rafiki yake kwa kukatazwa kwenda kufanya mauaji yale kwa mkono wake.
*****
Kule hospitali kwa Bi.Fahreen, Rachna na Magosho walikuwa wamejawa na furaha baada ya kumuona mama yao amerejewa na fahamu kwa mara nyingine. Rachna akiwa ameketi kwenye kitanda alichokuwa amelala Bi.Fahreen, Magosho alikuwa amekaa kwenye kiti kidogo pembeni mwa kitanda kile. Mkono wa kulia wa Bi.Fahreen ulikuwa kwenye viganya vya mikono ya Magosho vikisuguliwa suguliwa taratibu.
Kitendo cha Magosho kumsugua sugua Bi.Fahreen kiganja chake cha mkono kilimfanya mama yule kuhisi hali fulani ya ahuweni ndani ya moyo wake. Hata hivyo alipopeleka macho kumtazama binti yake Rachna alihisi dukuduku kubwa limemkaba moyoni. Alitamani kumrukia na kumrarua kwa meno lakini hakuwa na uwezo huwo masikini ya Mungu. Jamani nyie acheni tu, mapenzi haya!
Rachna hakuelewa chochote kilichokuwa kikiendelea baina ya mama yake na dereva wao Magosho. Alichokuwa anakijua yeye ni kwamba Magosho kuchua mkono wa Bi.Fahreen hakikuwa kitu kibaya kwasababu ni kama mtu na mwanawe. Hata hivyo Magosho alikuwa ameushika mkono wa Bi.Fahreen kwa lengo la kumfariji kama mama yake mzazi na si vinginevyo.
Bi.Fahreen alikuwa akijitahidi kukwepesha macho yake kumtazama binti yake na badala yake muda mrefu aliyatuliza macho yake usoni mwa Magosho. Alihisi damu zikitereza kwenye mishipa yake kiulaiini. Alitamani sana wasaa ule wangekuwa wenyewe wawili tu maeneo yale ili apate angalau busu kutoka kwa kijana yule aliyetokea kuukonga mtima wake. Akainua macho yake na kumtazama binti yake.
“Rachna” Aliita Bi Fahreen kwa sauti kavu lakini iliyokuwa imelegea kutokana na kitendo cha Magosho kumsugua sugua kiganja cha mkono wake.
“Yes Mom” Rachna aliitika kwa heshima na bashasha.
“Nenda kwa home letea mimi majuisi” (Nenda nyumbani ukaniletee juisi) alisema Bi.Fahreen pasipo kumtazama Rachna usoni.
“Oh! Juisi ya nini Mom?” alihoji Rachna kwa hamasa. Alifurahi sana kusikia mama yake alikuwa anahitaji kula.
“Pinaple” (Juisi ya Nanasi) Bi.Fahreen alijibu kwa ufupi.
Rachna aliinuka kwa hamasa kubwa na kumshika Magosho begani.
“Twende basi Goso” alizungumza Rachna kwa sauti ya kutokea puani kama vile mgonjwa wa mafua.
Bi.Fahreen aliposikia maneno ya binti yake alihisi maumivu makali mithili ya mtu aliyekuwa amechomwa mkuki kwenye moyo wake. Alifumba macho kwa sekunde kadhaa kuyasikilizia maumivu yale kutoka moyoni na kuenea sehemu mbalimbali za mwili wake. Racha akagundua utofauti aliokuwa nao mama yake.
“Whats rwong Mom?” (Nini tena mama?) Rachna alihoji huku akimsogelea haraka sana mama yake na kumuwekea kiganja cha kushoto shavuni.
“No thing wrong, just go” (hakuna kitu we nenda) Bi.Fahreen alizungumza huku akiutoa mkono wa binti yake kutoka kwenye shavu lake.
“Ok, Goso subiria mimi hapa” Rachna alizungumza na kuondoka huku akiamini amemuwacha Magosho kuhakikisha usalama wa afya ya mama yake kipenzi.
Rachna alipowapa kisogo tu Bi.Fahreen alikunja sura na kuvuta midomo yake kwa nyodo na hasira kuonesha wazi kumchukia binti yule aliyewahi kuishi ndani ya tumbo lake la uzazi kwa takribani miezi sita.
“Kwanini unafanya hivyo Bi.Fahreen?” Magosho alihoji Baada ya kugundua kuwa Bi.Fahreen hakuwa sawa kwa binti yake.
“Shut up!” Bi.Fahreen alipaza sauti kwa Hasira kumtaka Magosho anyamaze.
Magosho akatii amri na kukaa kimya. Alikuwa akimtazama mke wa bosi wake kwa macho ya tahadhari.
“Veve Goso tazama mimi?” Bi. Fahreen alizungumza kwa jazba.
Magosho aligeuza shingo na kuangalia pembeni huku mikono yake ikiwa ingali imekamatia kiganja cha mama yule wa kihindi.
“Kwanini veve iko matesa mimi?” alihoji kwa hasira Bi. Fahreen.
“Kwani nimefanya nini mama?”Magosho akahoji kwa umakini mkubwa.
“Kwanini veve iko magawa penzi kwa matoto yangu Rachna?” alihoji mama yule kwa umakini.
“Mnh mama! Mbona hakuna kitu kama hicho” Magosho akazungumza kwa mshangao. Ni kweli kabisa hakuwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na binti wa mama yule pamoja na uzuri aliokuwa nao.
“Sasa baba ya matoto yangu iko jua kila kitu” Bi Fahreen alizungumza kwa sauti ya msisitizo.
“Lakini mama hakuna kitu kinachoendelea kati yangu mimi na Rachna, tunaishi kama kaka na dada tu na hakuna cha zaidi” Magosho alijaribu kuzungumza ukweli mbele ya mwanamke yule aliyekuwa anaugua ugonjwa wa wivu.
“Kama iko kweli matembea na matoto yangu au hapana kweli, leo veve kufe” Bi. Fahreen alizungumza huku akijaribu kuchomoa mkono wake kutoka kwenye vianja vya Magosho bila ya mafanikio kwasababu Magosho aliuzuia mkono ule.
“Hapana jamani mnanionea bure mimi, hata sijawahi kumtongoza dada Rachna mimi” masikini Magosho aliendelea kujitetea kwa msisitizo.
“Mimi penda veve Gosoo lakini veve umisa mimi. Ondoka hapa mara moya, Mr. Nakeshwar kuje toa roho yako saa hii" Bi. Fahreen alizungumza kwa tahadhari kwasababu alikuwa akimfahamu vyema mume wake. Hakuwa na masihara kwa kibwengo yeyote yule aliyethubutu kuchezea maisha ya binti yake Rachna. Kitu kibaya zaidi ni kwamba bwana huyo alipata taarifa kuwa Magosho huyo huyo alikuwa akidokoa asali ya mtima wake.
Ghafla mlango wa wodini ulifunguliwa kwa nguvu na Mr.Nakeshwar aliingia huku akiwa ameongozana na watu wane akiwemo Zawadi na vijana wengine watatu.
Magosho alishituka na kuuachia mkono wa Bi.Fahreen haraka. Mr.Nakeshwar hakuweza kuamini macho yake kwa kile alichokuwa amekikuta pale. Yale aliyokuwa ameyasikia kutoka kwa rafiki yake Mansoor yalithibitika moja kwa moja. Hakuona sababu ya kuuliza.
“The dog is that one” (mbwa mwenyewe ni huyo hapo) Mr. Nakeshwar alizungumza kwa hasira huku akinyoosha kidole kwa Magosho.
Zawadi alisogea hadi pale kwa Magosho na kumuonesha ishara ya kuinuka kwa kidole chake cha kati huku amemkazia macho kijana yule.
Magosho alishangazwa sana na tukio lile lililokuwa likiendelea mbele ya macho yake. Alikuwa anamfahamu vizuri sana Zawadi. Msichana yule alikuwa wamekulia katika mtaa mmoja na kipindi cha utotoni walikuwa wakicheza pamoja. Pia alimfahamu Zawadi kwasababu alikuwa ni shoga mkubwa wa mdogo wake Ashura. Mara nyingi walipokuwa sokoni wakiuza vitumbua walipenda kukaa pamoja. Kwa ufupi ni kwamba alishangazwa sana na kuona msichana yule akiwa ameongozana na Mr. Nakeshwar. Mbaya zaidi alikuwa akimuonesha dharau. Magosho alitaka kuhoji kitu.
“Shssss” Zawadi alimnyamazisha kwa kuweka kidole mdomoni mwake na kumtolea macho kwa ukali zaidi.
Magosho alitii amri na kunyamaza kimya huku katika akili yake akiwa amejawa na maswali yaliyokosa majibu.
Zawadi akaonesha msisitizo wa kumuamuru Magosho kuinuka pale alipokuwa ameketi. Pasipo kujishauri alijiinua kwa kusitasita huku moyo wake ukiwa umejawa na wasiwasi pamoja na hofu.
“Usitucheleweshe we kunguni” Zawadi alizungumza huku akivuta hatua kumkaribia Magosho.
Zawadi alivuta mkono wake wa kushoto na kumtandika Magosho kofi moja takatifu sana maeneo ya shavuni karibu kabisa na shingoni. Magosho aliinama na kuweka mkono kwenye shavu kusikilizia maumivu ya pigo lile murua.
Dharau ile ilimuumiza sana Magosho, aliinuka na kurusha ngumi nzito kwa Zawadi lakini mwanamama yule aliiona na kuinyaka ikiwa hewani kabla haijatua kwenye pua yake ambayo ilikuwa imelengwa kung’olewa na Magosho. Haraka sana Zawadi alijibu shambulizi lile kwa kurusha ngumi yake ikamtwanga Magosho shavuni. Magosho alipepesuka na kudondokea kwenye kitanda alichokuwa amelala Bi.Fahreen.
“Uuuwiiiii!” Bi.Fahreen alitoa ukulele wa woga kama vile yeye ndiye aliyekuwa amepokea pigo lile kutoka kwa Zawadi.
“Kimya, Malaya kuba veve, iko ona raha tembea penzi na matoto dogo!” Mr.Nakeshwar alipaza sauti kumwambia mke wake. Kauli ile ilitosha kumfanya Magosho kutambua sababu ya hukumu ile aliyokuwa akipewa na mtoto wa kike.
Zawadi alimfuata Magosho pale kitandani akamshika shingoni na kumvuta juu. Alimuinamisha na kumtandika vigoti vitatu mfurulizo vya usoni. Magosho kama mtoto wa kiume hakutaka kushindwa kirahisi namna ile. Aliinuka na kumvaa Zawadi kwa hasira. Zawadi alimpisha na kumsukuma kwa teke takatifu la mgongoni. Magosho akapepesuka hadi alipokuwa amesimama Mr. Nakeshwar.
Mzee yule wa kihindi alimsukumia Magosho kwa baunsa wake ammoja ambaye alikuwa amesimama pembeni. Baunsa yule alitanua mikono yake na kuikutanisha pamoja kwa nguvu sana, akabana kichwa cha Magosho katikati ya mikono ile.
“Mama N a k u f a a a a  !” Magosho alitoa ukulele wa maumivu makali yaliyotokana na kichapo kile. Sauti za ajabu ajabu zilikuwa zikisikika kwenye masikio yake. Machoni alikuwa akiona vitu Fulani fulani vilivyokuwa vikikatiza huku vikiwakawaka na kuzima kama nyota za mbingu ya saba.
ITAENDELEA



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa