KITUMBUA CHA KIHINDI SEHEMU YA 21 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Wednesday, February 5, 2020

KITUMBUA CHA KIHINDI SEHEMU YA 21






ILIPOISHIA
“Yes, Goso iko chezea matoto yetu Rachna” Mwanamke yule aliendelea kutapika maneno ya uchonganishi.
“Are you sure?” (una uhakika?)
“Hundred percent” (asilimia miamoja)
“Shit! he must be perished” (shenzi! ni lazima afe) Mr.nakeshwar alizungumza huku akitetemeka kwa hasira.

ENDELEA….21
Wakati mzee yule wa kihindi alipokuwa akitetemeka kwa hasira, simu yake ya mkononi iliita. Aliitoa mfukoni na kuitazama kujua mpigaji. Aligundua kuwa aliyekuwa anampigia alikuwa Mansoor yule mfanya biashara mwenzie.
“Hallo”
“Yes. Mr.Nakeshwar, Just come faster. Something is wrong” (Ndio Mr.Nakeshwar. Njoo haraka kuna tatizo kidogo) alizungumza Mansoor kwenye simu.
“Where?” (wapi?)
“Cerena Hotel”
“Ok. Five minutes” (Sawa. Nipe dakika tano) Alizungumza Nakeshwar na kukata simu. Alimtazama mke wake kwa sekunde kadhaa kisha akaondoka kwa haraka sana huku akili yake ikionekana kuvurugwa na taarifa za kijana Magosho kuwa na mahusiano ya kimapenzi na binti yake kipenzi Rachna.
Mr.Nakeshwar aliendesha gari kwa mwendo mkali sana. Baada ya dakika tano alikuwa amekwishafika kwenye hoteli ya Serena. Alipoingia tu hakupata shida kumtafuta Mansoor kwasababu alikuwa amekaa kwenye makochi ya pale ghrorofa ya chini. aliongoza moja kwa moja hadi pale alipokuwa ameketi.
“What is the matter?” (Kuna nini?) alihoji Mr Nakeshwar punde tu alipofika.
“Have a seat and calm down” (kaa chini halafu tulia) Mnsoor alizungumza kwa upole.
Mr.Nakeshwar alikaa kwenye kochi na kumsikiliza Mansoor kwa makini ingawa akili yake ikiwa imekwisha chafuka. Alichukia sana kwasababu Magosho alikuwa ni mswahili na wao walikuwa ni wahindi. Hivyo kutokea kwa kitu kama kile kilikuwa ni aibu kubwa sana kwenye familia ya tajiri kama yeye.
“Am sory Mr.Nakesh kwa hili nitakalokwambia. Sina jinsi” alisema Mansoor kwa utaratibu.
“Tafadhali ambia mimi bana kubwa” alisema Nakesh.
“Unafahamu kuwa yule dereva wa mke wako anakuzunguuka?” alizungumza Mansoor kwa umakini mkubwa na kumeza funda la mate.
Mr.Nakeshwar aliowanisha taarifa zile na maneno aliyokuwa ameambiwa na mke wake kule hospitali. Hasira juu ya Magosho ikaongezeka zaidi.
“Yes iko mapata taarifa” alijibu Mr. Nakeshwar huku akionekana kufahamu kila ambacho Mansoor alikusudia kumueleza.
“Umeambiwa na nani?”
“My wife” (Mke wangu) alijibu Mr.Nakeshwar.
“Mke wako?” Mansoor alihoji kwa mshangao huku ametoa macho kwasababu alichokuwa anataka kumuelewa isingewezekana Bi. Fahreen kuzungumza kwa mume wake.
“Yes, ingawa my wife iko gonjwa lakini ambia mimi majinga ya Goso” alizungumza Mr.Nakeshwar huku akiumauma midomo yake kwa hasira.
“Bado unanichanganya Mr.Nakeshwar. Unasema aliyekwambia ni nani?” Mansoor aliendelea kuchanganyikiwa na kuhoji kwa mshangao mkubwa.
“My wife Bi.Fahreen ambaye iko Hospital” alizungumza Mr.Nakeshwar huku akikuna nywele zake kwa hasira.
“Mnh! Huyo mke wako ameanzaje kukwambia jambo hili?” Mansoor alionekana kuzidi kuchanganywa na maneno ya Mr.Nakeshwar.
“That boy must die!” (Yule kijana ni lazima afe) alisema Nakeshwar kwa hasira.
“Sawa, niambie huyo mke wako amekuelezaje?”
“Fahreen told me that Goso iko fanya matoto yangu maakuli” (Ameniambia kuwa Magosho anatembea na binti yangu) alisema Mr.Nakeshwar kwa uchungu.
Taarifa zile zilimshangaza sana Mansoor. Taarifa alizokuwa anampa ni kwamba Magosho anatembea na mke wake. Sasa akashangaa kuwa kijana huyo huyo alikuwa na mahusiano ya kimapenzi tena na Rahna.
 “Unamaana jamaa anakula kuku na watoto wake?”
 “What do you mean Mansoor?” (unamaanisha nini Mansoor?)
 “Ni dharau kubwa sana”
 “Ni kweli lakini iko maanisa nini?”
 “Ni aibu boss”
 “Ambia mimi bhanaa!”
 “Kwa ufupi ni kwamba huyo kijana anatembea na mke wako” alisema Mansoor kwa msisitizo.
 “What!...Nasema nini?.....No!....No!....Hapana wezekana kabisa” Mr.nakeshwar aliinuka juu na kuzungumza huku mikono akiiweka kichwana na kuihamishia kiunoni kabla ya kuitumbukiza mfukoni.
 “Tulia Bwana Nakesh” Mansoor alijaribu kumtuliza.
Mr.Nakeshwar hakumuelewa rafikiyake. Aliondoka kwa mwendo wa spidi kali sana na kumuacha rafiki yake amekaa akimtazama alivyokuwa akitokomea. Vijana wanakwambia kilikuwa kimenuka.
*****

Mazoezi aliyokuwa akipewa Ashura na rafiki yake zawadi yalimfanya kuwa vizuri sana katika sekta ya mapambano. Jitihada alizokuwa nazo zilimfanya kuwa na uwezo mkubwa zaidi ya vijana ambao alikuwa amewakuta pale kambini.
 Ashura akiwa amezunguukwa na vijana sita wakipambana naye kimazoezi, Zawadi alikuwa pembeni akipanga mzigo wa vitumbua vyenye unga wa COCAIN ndani yake. Yalikuwa ni maandalizi ya kupeleka mzigo huwo nchini Afrika kusini.
Kwa kiasi kikubwa sana Ashura alikuwa ameweza kuimudu kazi ile na kuizoea sana. Hakuwa anajilaumu tena kama ilivyokuwa awali. 
 Lango kuu lilifunguliwa kwa mbwembwe na Mr.Nakeshwar akaingia. Watu wote wakiwemo Ashura, Zawadi pamoja na vijana wengine waligeuka na kumtazama. Sura ya Mr. Nakeshwar ilionekana kuto kuwa ya kawaida. Macho yake yalikuwa mekundu mno na mwili wake ulikuwa ukimtetemeka na vinyweleo vimemsimama. Zawadi akatazamana na Ashura kisha wakakonyezana kama ishara ya kupeana tahadhari.
 Mr.Nakeshwar alizunguusha shingo kwenye jumba lile na kuwatazama vijana wake kwa hasira.
 “Keje hapa yote” Mr. Nakeshwar alipaza sauti kwa hasira kuwakusanya vijana wake.
Vijana wote walisogea huku wakiwa wamejawa na wasiwasi kwenye mioyo yao. Hawakuzoea kumuona bosi wao akiwa katika hali kama ile. Ni kweli kabisa Mr. Nakeshwar alikuwa anakasirika lakini hakuwahi kufikia hatua ile.
 “Afrika yote majinga jinga, kuje hapaaa!” Mr. Nakeshwar alipaza sauti kuzunumza kwa kufoka.
 “You!” (wewe!) Mr.Nakeshwar alizungumza huku akionyesha kidole kwa Ashura na Zawadi.
 “Yes Boss” Zawadi na Ashura waliitika kwa unyeyekevu huku wakionekana kuwa na hamu ya kutaka kufahamu sababu ya ujio wa bosi wao akiwa katika hali kama ile.
 “I want some one to be ded by today” (Nataka mtu mmoja auwawe leo hii) alizungumza Mr.Nakeshwar huku akitetemeka kwa hasira na mate yakimtoka mdomoni kama matone ya mvua.
 Zawadi akatazamana na Ashura kwa sekunde kadhaa kisha wakapeana ishara ya kutekeleza agizo lile la bosi wao.
 “Ni kazi rahisi bosi” Ashura alizungumza kwa ukakamavu na kujiamini.
 “Ni nani huyo mtu tumalize kazi bosi?” alihoji Zawadi.
 “Hapana uliza swali nyingi bhanaa! Mimi iko taka maroho sasahivi” alizungumza Mr. Nakeshwar kwa hasira utafikiri waliosababisha hasira zile walikuwemo ndani ya mjengo ule.
Vijana waliposikia Maneno yale kila mmoja alijiweka sawa kwa kuchukua silaha yake na kuiweka kiunoni tayari kwa mapambano.
Mr.Nakeshwar aligeuka na kuanza kuondoka kwa haraka. Ashura alivuta hatua na kutaka kumfuata kwa nyuma lakini Zawadi akamdaka mkono na kumrudisha.
 “Niachie mimi” alisema Zawadi kwa sauti ndogo.
 “No! na mimi nina hamu ya kuua leo” Ashura alimjibu Zawadi kwa msisitizo.
 “Hii kazi inaelekea ni ngumu Ashura, wacha nikamridhishe bosi” Zawadi alizungumza.
 “Kwahiyo unataka kusema mimi siwezi kikazi?” Ashura akahoji kwa msisitizo.
 “Unaweza Ashura, lakini tambua kuwa hujawahi kuua mtu wewe” Zawadi alieleza.
 “Unafikiri nitaanza lini kama sio leo? Ngoja na mimi nikamthibitishie bosi kuwa niko vizuri kikazi” Ashura alizungumza kwa kujiamini.
ITAENDELEA



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa