KITUMBUA CHA KIHINDI SEHEMU YA 20 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Wednesday, February 5, 2020

KITUMBUA CHA KIHINDI SEHEMU YA 20






ILIPOISHIA..19
 Mtoto Vashal alipofokewa na kusukumwa ikabidi ajiongeze na kutoka nduki kuingia ndani na kumuacha mwanamke yule aliyekuwa mkali kama mbogo pale barazani.
            Vijana wale wawili walipoteremka tu Rachna alimsogelea Magosho na kumshika mkono, wakawa wanatembea huku wameshikana mikono. Bi.Fahreen alipowaona akasimama ghafla kutaka kuwavaa wawili wale waliokuwa wamedhamiria kuumiza moyo wake.

ENDELEA…20
Bi. Fahreen alipokuwa akivuta hatua kuwafuata Magosho na Rachna alihisi kizunguzungu kikali kikimtawala na kushindwa kuhimili mikiki. Pumzi zilimuishia na kudondoka chini kama mzigo ‘Puuu!’.
            “Gosooo help! help! faster” Rachna alimkimbilia mama yake na kumuinua shingo kisha akamuweka kwenye mapaja yake.
            “Mom!…Mom!.....Iko nini tatizo?” Rachna alipaza sauti kumuita mama yake huku akiwa na wasiwasi na hofu kubwa. Hata hivyo Bi.Fahreen alionekana kuwa na hali mbaya kuliko mbaya.
Magosho na Rachna walisaidiana na kumpakia kwenye gari kisha zoezi la kuelekea Hospitali ilifanyika kwa haraka. Rachna alionekana kuchanganyikiwa baada ya kiona hali ya mama yake jinsi ilivyokuwa. Alikuwa akiwapenda sana wazazi wake na hakutamani kuwaona wakiteseka hata kidogo.
Kwa msaada wa Magosho, Bi.Fahreen alilazwa kwenye hospitali moja ya private iliyokuwa inafahamika kwa jina la ST.METHEW ambayo ilikuwa inapatikana maeneo ya Posta pale jijini Dar.
            Baada ya masaa mawili hali ya Bi.Fahreen ilianza kutengemaa. Mr.Nakeshwar alikuwa pembeni yake akimliwaza mke wake kipenzi, laadhidhi wake nyonga mkalia ini. Rachna na Magosho hawakuwepo muda huwo.
            “Hello my wife how are you?” (Vipi mke wangu unaendeleaje?) alihoji Mr.Nakeshwar kwa sauti iliyojaa upendo na huruma.
            “Am fine my husband, what is going on?” (nipo vizuri mume wangu, vipi nini kinaendelea?) alihoji Bi.Fahreen kwa taabu huku akizunguusha macho yake kuangalia mazingira ya pale hospitalini.
            “Just relax my lovely wife,I will inform you every thing letter” (Pumzika kidogo mke wangu, baadae nitakufahamisha kila kitu) alisema Mr.Nakeshwar kwa ile sauti yake ya kubembeleza.
 Bi. Fahreen alijaribu kuvuta kumbukumbu lakini hakuweza kukumbuka juu ya kilichotokea hadi kufikia hatua ile ya kulazwa hospitalini pale, tena mkononi akiwa na drip la maji na glucose.
            Baada ya dakika kadhaa Rachna alifika hospitalini pale akiwa ameongozana na Magosho. Kama ilivyokuwa kawaida ya Rachna kila alipokuwa anatembea alipenda sana kumshika mkono Magosho.
            “Mom iko mapata nafuu?” alizungumza Rachna kwa furaha kubwa baada ya kumkuta mama yake amezinduka.
Kwa mapenzi aliyokuwa nayo binti Rachna kwa mama yake yule, akajikuta amepatwa na furaha ya kupitiliza. Alimfuata Magosho na kumkumbatia kwa lengo la kufurahia ahuweni aliyokuwa nayo mama yake kipenzi. Alimbusu Magosho kwenye mashavu yake mara kadhaa huku akicheka kwa furaha masikini ya Mungu. Hakika lilikuwa ni jambo la furaha na lililokuwa limejaa Baraka za Mungu.
Jamani jamani nyie! Kumbe kitendo kile cha Rachna kumkumbatia Magosho na kummiminia mvua ya mabusu kutokana na furaha, kilikuwa ni kitendo cha hatari sana kwa afya ya Bi.Fahreen.  Hali ya Bi. Fahreen ikabadilika tena na kuwa mbaya, Alikuwa akipumua mfurulizo huku akitoa macho utafikiri alikuwa katika harakati za kuachanisha roho na mwili.
            “Emergence! Call nurse” (mwite nesi kuna dharula) Mr.Nakeshwar alipaza sauti kuomba maada.
“N u r s e !..... N u r s e!.....Help…..N u r s e” Rachna naye alipaza sauti huku akikimbia kuelekea kwenye chumba cha manesi kuweza kupata msaada wa haraka.
****
         Ashura aliendelea kuwa na hamu kubwa ya kuweza kufahamu kile kilichokuwa kinaendelea kule chini ya ngazi. Macho ya Ashura yaliweza kushuhudia chumba kilichokuwa na eneo moja pana sana. 
Ashura hakuweza kuamini alichokuwa anakiona mbele ya macho yake katika eneo lile pana. Kulikuwa na vijana kama kumi na mbili hivi waliokuwa wameshiba kwa mazoezi ya viungo. Lakini walikuwa kama vile wanapigana kwa kurushiana ngumi na mateke mazito.
 “Huuuu!..... Haaaa!..... Huuuu!.... Haaaa!” vijana wale walikuwa wakipiga kelele kila walipokuwa wakirushiana ngumi na mateke.
 “Zawadi ni nini hiki, kwanini wanapigana?” alihoji Ashura kwa sauti ndogo lakini iliyokuwa imejaa hofu na mashaka.
 “Shsss tulia! Hawapigani hawa wanafanya mazoezi” Zawadi akamtuliza Ashura kwa sauti ndogo na Ashuara akatii amri.
Wakasogea hadi sehemu moja ambako vijana wawili walikuwa wakipambana na mtu mmoja. Walipofika tu vijana wale wakaacha kupambana na kutoa salamu kwa Zawadi kwa kuinama kidogo na mikono yao wakiwa wameibandika kifuani.
 Zawadi akanyoosha mkono kama vile alikuwa anaomba kitu Fulani kutoka kwa vijana wale. Mmoja wa wale vijana alimletea grops za kupigania, wenyewe sijui wanayaitaje, yale ambayo wanayavaa mkononi mabondia wakati wakapigana ulingoni.
Zawadi alivaa grops zile kisha akampa Ashura ishara ya kusogea pembeni, akawaita vijana kwa ishara huku akibonyea kidogo huku amekunja ngumi na miguu yake akiipishanisha kwa kuruka ruka kidogo. Vijana wote watatu wakakunja ngumi na kumsogelea Zawadi taratibu.
 Ilikuwa ni kama vile picha ya kichina kwa Ashura kwani alishangaa shoga yake alivyokuwa akipambana na vijana wale walioonekana kushiba mazoezi. Vijana walijitahidi kurusha ngumi na mateke lakini Zawadi aliyaona na kupangua kisha akawa anawatwika yakwake takatifu. Baada ya dakika chache vijana wote watatu walikuwa chini hoi bin taaban. Hawakutamani kumsogelea tena zawadi.
 Zawadi alimgeukia Ashura ambaye alikuwa angali kwenye mshangao. Alitoa tabasamu na kumkonyeza. Ashura alikuwa kama vile amegandishwa kwenye barafu. Hakujibu wala hakutikisika. Aliendelea kumshangaa rafiki yake yule ambaye siku hiyo alikuwa ameamua kumuonesha mambo ya kushangaza.
 “Vipi unaweza?” alihoji Zawadi huku akitabasamu huku akivua zile gloves na kuzitupa pembeni.
Ashura aliendelea kumtazama pasipo kutikisika wala kuzungumza neno lolote lile. Nafikiri kati ya mambo yote aliyoyaona siku hiyo, lile la shoga yake Zawadi kupambana na wanaume watatu walioshiba na kuwashinda kilimshangaza zaidi.
 “We Ashura!” Zawadi aliita kwa sauti huku akimpigia makofi karibu na usoni.
Ashura alishituka kama vile mtu aliye gutushwa kutoka usingizini. Zawadi naye akatulia akimshangaa rafiki yake kwa jinsi alivyokuwa.
 “Kumbe ndivyo ulivyo?” alihoji Ashura kwa sauti ya tahadhari.
 “Yeah, vipi unaweza?” Zawadi akahoji huku akijifuta jasho kwa taulo dogo lililokuwemo ndani mle.
 “Mnh! sijui hata kukunja ngumi” Alijibu Ashura.
 “Nenda bwana kidogo tuu ukajaribu!”
 “Niende wapi, we Zawadi niende wapi?” Ashura alihoji huku ametoa amacho kwa msisitizo.
 “Nenda ukanitwangie wale vijana wawili pale” Zawadi alizungumza huku akimuoneshea Ashura vijana wawili waliokuwa wakirushiana ngumi karibu na pale walipokuwa.
 “We Zawadi wewe, Muogope Mungu!” alizungumza Ashura kwa msisitizo.
 “Wale wachovu tu hawatakusumbua” Zawadi alizungumza huku akiachia tabasamu la masihara.
 “Thubutu! Hunipeleki popote” Ashura akazungumza kwa msisitizo.
 “Usijali utajua tu na pengine ukawa mkali kuliko hawa wote” Zawadi alizungumza huku akiwaoneshea kidole wale watu waliokuwemo mle ndani.
 Ashura alizunguusha macho kuwatazama vijana wale waliokuwa bize na mazoezi.
 “Sasa hawa nao kwanini wako hapa?”
 “Hawa ni vijana wa bos Nakeshwar”
 “Wao wanafanya kazi gani?”
 “Hawa ni walinzi wa biashara zetu. Huwa hawachelewi kutoa uhai wa mtu mzembe ama anayejaribu kuingilia biashara zetu” alisema zawadi.
 “Kwahiyo nawewe unaweza kuua?” Ashura akahoji kuhamaki.
 “Kama kuna mtu atakayejaribu kunitia hatarini sioni dhambi kummaliza yeye kabla ya yeye kunimaliza mimi” alisema Zawadi kwa kujiamini.
 “Mnh!”
 “Usigune, hata wewe inabidi uwe vizuri kwaajili ya usalama wako kwasababu watu kama sisi tunasakwa kwa udi na uvumba na serikali mbalimbali hapa duniani” Alisema Zawadi kwa msisitizo.
Ashura alizidi kuona ugumu na uhatari wa biashara ile ambayo awali aliiona ni rahisi na salama. Akapumua kwanguvu kuashiria ugumu wa kazi.
****
Mr.Nakeshwar alikuwa amechanganyikiwa kutokana na kubadilika kwa hali ya mke wake. Akiwa nje alikuwa akitembea tembea hapa na pale. Alikuwa hajisikii kukaa wala kusimama. Daktari alikuwemo wodini akiendelea kumtibia mke wake kwa uangalifu zaidi.
Magosho alikuwa ametumwa kumpeleka Rachna benki kuchukua pesa kwaajili ya matibabu ya Bi.Fahreen. Hivyo wodini pale alikuwepo Mr.Nakeshwar pekeyake. Baada ya dakika kadhaa mlango wa wodi ile ulifunguliwa na Daktari akatoka.
 “Vipi Dokta?” Alihoji Mr.Nakeshwar huku akiwa ametoa macho.
 “Anaendelea vizuri mzee usihofu” Daktari alizungumza kwa upole.
 “Naweza kumuona?”
 “Anatakiwa kupumzika kwa muda mrefu” alisema Daktari kwa umakini mkubwa.
 “No Dokta, ruhusu mimi maone muke yangu mara moya!”
 “Ok. Nakupa dakika tano” Daktari alizungumza kisha akaondoka na kumuacha Nakeshwar akiingia wodini.
Bi.Fahreen alikuwa amerejewa na fahamu ingawa hali yake haikuwa ya kuridhisha.
 “Muke yangu!” aliita Mr.nakeshwar.
Bi.Fahreen aligeuza shingo na kumtazama mume wake pasipo kutoa sauti yake.
 “Vipi my wife?”
 “Niko vizuri”
 “Kwani tatizo iko nini muke yangu?”
 “Rachna”
“Racha iko tuma kwa benki kuchukua some money”
“Goso?”
“Goso iko peleka Rachna kwa benki” Mr.Nakeshwar alieleza pasipo kufahamu kuwa maelezo yake yale yalikuwa yakimuumiza sana mke wake.
“My God!” Bi.Fahreen alizungumza huku akionekana kupoteza amani.
“Kwani iko nini my wife?”
“That is a huge mistake” (umefanya kosa kubwa sana) alisema Bi.Fahreen huku sura yake ikionekana kujawa na hofu kubwa.
“What mistake?” (kosa gani?)
“Goso is a problem” (Magosho ni tatizo)
“How?” (kivipi?)
“Goso iko tembea na Rachna” alitamka Bi.Fahreen kwa ghadhabu.
“What?” (nini?) Mr.Nakeshwar alihamaki.
“Yes, Goso iko chezea matoto yetu Rachna” Mwanamke yule aliendelea kutapika maneno ya uchonganishi.
“Are you sure?” (una uhakika?)
“Hundred percent” (asilimia miamoja)
“Shit! he must be perished” (shenzi! ni lazima afe) Mr.nakeshwar alizungumza huku akitetemeka kwa hasira.
ITAENDELEA



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa