KITUMBUA CHA KIHINDI SEHEMU YA 19 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Wednesday, February 5, 2020

KITUMBUA CHA KIHINDI SEHEMU YA 19





ILIPOISHIA..18
Zawadi alisimama huku mikono yake ameikumbatia kifuani na kumtazama jinsi ambavyo Ashura alivyokuwa akiondoka kwa kiburi. Aliachia tabasamu na kutikisa kichwa kwa masikitiko.

ENDELEA…19
Ashura alitembea kwa haraka sana ili kutoka ndani ya pango lile ambalo alikwisha baini kuwa lilikuwa ni pango la uhalifu. Ndani ya moyo wake alipanga kwenda kutoa siri ile kwa jeshi la polisi ili kutokomeza shughuli zile.
Alipofika kwenye kile chumba cha kwanza walichoingilia alikuta makabati yako wazi na pesa zikiwa zinaonekana. Alisimama kwa sekunde kadhaa akizitazama pesa zile ambazo Zawadi alimueleza kuwa zilikuwa ni za kwao wawili. Alikumbuka hali halisi ya maisha yake yeye na kaka yake Magosho, akajiona ni upunguani wa akili.
Pamoja na kwamba hali ya woga ilikuwa imemtawala juu ya biashara ile iliyokuwa inapigwa vita kila kulipokucha na serikali pamoja na vyombo vya dini lakini maburungutu ya pesa yaliyokuwa yanamtazama kwa tabasamu la bashasha akajikuta akipatwa na tamaa ya kumiliki pesa zile.
“Potelea mbali bwana! kwani mie ndio nitakuwa wa kwanza kufanya biashara hii?” alijiuliza mwenyewe moyoni. Aligeuka na kurudi kule alikokuwa amemuwacha Zawadi amesimama.
“Zawadi” aliita Ashura kwa sauti ya upole na unyenyekevu.
“Vipi umesahau nini?” Zawadi alijibu kwa jazba huku akimtazama Ashura kwa jicho la dharau na kebehi.
“Hakuna nilichokisahau shoga”
“Kumbe?”
“Sina kipingamizi tena”
“Kipingamizi cha nini?”
“Nipo tayari kufanya biashara” Ashura alizungumza huku akiwa amemkazia macho zawadi usoni. Zawadi alitoa tabasamu lililoonekana wazi kuwa lilikuwa limejaa dharau na kebehi.
“Biashara gani?” alihoji Zawadi huku akijitikisa kwa nyodo.
“Ya kitumbua cha kihindi”
“Hata kama usingekuwa tayari ni lazima ungefanya tu” Zawadi alizungumza huku akiendelea kujitingisha tingisha na mikono yake ikiwa ingali kifuani.
“Ningefanya kivipi?”
“Unakumbuka kama ulikwisha kula kiapo cha kufanya kazi pamoja nasi?”
“Ah! hakukuwa na sababu ya kupeana viapo, ila kwakuwa imekwishatokea hakuna tatizo” alijibu Ashura kwa kujiamini.
Zawadi alichukua lile sinia la vitumbua na kuelekea nalo upande wa kushoto ambako Ashura hakuwahi kufika. Waliingia kwenye chumba kimoja kilichokuwa kimejaa brifkesi za kila saizi na kila rangi kwenye makabati.
Zawadi alichukua brifkesi ndogo na kuanza kupanga vile vitumbua. Ashura aliendelea kumsoma rafiki yake yule ambaye alikuwa akimfundisha kazi. Kitendo kile kilikuwa kigeni machoni mwa Ashura. Hakuwahi kuona vitumbua vinahifadhiwa kwenye brifkesi kama noti ama nguo.
Zawadi alipomaliza kupanga vitumbua vile kwenye ile brifkesi aliinua shingo kumtazama Ashura ambaye alikuwa amesimama pembeni yake akimtazama kwa makini.
“Unaona mzigo huu?” Zawadi alihoji huku ameinua ile brifkes kwa mkono wake wa kulia.
Ashura akaitikia kwa kichwa kuonesha kuwa alikuwa ameiona.
“Mzigo huu unathamani ya dola za kimarekani  ‘Bilioni moja na ushee’” alisema Zawadi na kumfanya Ashura kushituka.
“Unasema!….”
“Habari ndio hiyo mama”
“Mnh! kwakweli wacha vijana wa kitanzania wanyongwe huko china” alizungumza Ashura huku ameweka kiganja cha mkono wake wa kuume kifuani.
“Wanaokamatwa ni wazembe. Sisi tuko vizuri mama” Zawadi akazungumza kwa kujiamini.
“Sasa huo mzigo unakwendaje sokoni?” Ashura alihoji kwa udadisi mkubwa.
“Huu unasafirishwa kwenye makontena ya vyakula kama vyakula vya kawaida”
“Haviharibiki?”
“Sio rahisi, ule unga umechanganywa na kemikali maalumu za kuzuia vyakula visiharibike hata kama vikikaa miaka kumi” alisema Zawadi.
“Duh!  ama kweli mmekamilika” Ashuara alitamka.
“Si hivyo tu mama, mzee mwenyewe ameshikilia serikali hapa kiganjani” alisema Zawadi.
“Mnh! Serikali hii?” Ashura akahoji kwa kuhamaki.
“Wewe ukijua la kulia, wenzako wanahamia la kushoto”
“Unataka kusemaje?”
“Kila kukicha, mzee na kamati yake wanawaza mbinu za kujilinda na kuishi kwa usalama” Zawadi alieleza.
“Kwahiyo hatuwezi kukamatwa?”
“Tutakamatwaje sasa? Mwenyewe umeona kila siku watu wanashikwa lakini hakuna hata mtu mmoja aliyekamatwa kwenye mtandao wetu” Zawadi alieleza.
“Mnh, unaanza kunitia moyo” alisema Ashura.
“Tupo vizuri kila idara mama. Njoo huku nako uone mambo yetu” Zawadi alizungumza huku akiondoka na brifkesi ya vitumbua mkononi. Kama ilivyokuwa kawaida Ashura alimfuata kwa nyuma.
Waliingia sehemu moja iliyokuwa na kiuchochoro chembamba sana. Walipenya kwenye kiuchochoro kile kilichokuwa kirefu na kutokea sehemu moja iliyokuwa na mawe mengi makubwa. Juu kulikuwa na kitu kama tundu la darini.
Zawadi alipanda kwenye mawe na kudandia pale juu kama ngedere kisha akajivutia kwa ndani. Alipoingia aligeuka na kunyoosha mkono kwa Ashura ambaye alikuwa amesimama chini akimuangalia.
Ashura alinyoosha mkono wake na kuukamata mkono wa Zawadi. Alivutwa na kudondokea ndani mle.
Kilikuwa ni chumba kidogo mno kilichokuwa kimetawaliwa na kiza kinene. Zawadi alipowasha tochi wakaona ngazi iliyokuwa ikiteremka chini kwa upande mwingine.
“Twende huku” alisema Zawadi huku akiteremka ngazi zile.
Ashura alifuata nyuma bila kipingamizi chochote. Waliteremka ngazi nyingi sana “hadi walipokaribia kufika chini wakasikia sauti za watu wakizungumza kwa makelele.
“Nani hao Zawadi?” Ashura alihoji kwa wasiwasi.
“Vijana hao wapo kazini”
“Vijana?” Ashura akahoji kwa wasiwasi.
“Ndio vijana wa kazi” Zawadi alijibu huku akiendelea kushuka ngazi.
Mwanga wa taa uliokuwa ukitokea chini uliashiria kuwa safari yao ilikuwa imekaribia kufika ukingoni. Na dalili zilionesha kuwa kule walikokuwa wanaelekea kulikuwa na mwanga wa kutosha. Ashura akawa anatembea huku akikodolea macho yake mbele kwa hamu kubwa ya kuona kile kilichokuwa kinaendelea kule chini.
****
Hasira za Bi.Fahreen zilishindwa kuzuilika ndani ya moyo wake. Ghafla alijikuta akiwachukia vijana wale wawili yaani Magosho na binti yake Rachna. Sababu kubwa ya chuki ile ilikuwa ni mapenzi. Aliamini kwa asilimia zote kuwa binti yake Rachna alikuwa akitoka kimapenzi na asali wake wa moyo.
Bi.Fahreen alishindwa kufanya kitu chochote kile tangu Magosho alipoondoka nab inti yake. Alihisi viungo vya mwili vikimnyog’onyea na kukosa hamu ya kufanya jambo lolote lile. Alisogea kibarazani na kuketi huku akiona dunia ikizunuuka kutokana na wivu ulivyokuwa umemtawala. Alikumbuka bastola ya mume wake na kutamani kuitumia katika kuhakikisha Amani ya moyo wake inapatikana. Ndio, Bi. Fahreen alikuwa tayari kutoa uhai wa mtu ili kulinda Amani na furaha ya moyo wake.
Muungurumo wa gari waliyoondoka nayo Rachna na Magosho ulimgutusha kutoka kwenye lindi la mawazo. Baada ya sekunde kadhaa gari ile ilifunga breki hatua chache kutoka pale barazani alipokuwa amekaa Bi. Fahreen..
Mtoto Vashal aliteremka na kumkimbilia Bi.Fahreen kumkumbatia kwa furaha kama ilivyokuwa kawaida yake siku zote alipokuwa akitoka shuleni. Lakini siku hiyo mambo yalikuwa tofauti kabisa kwa mtoto yule kwani hakuchangamkiwa kama ilivyo kawaida ya mama yule.
“Mom tatizo iko nini?” alihoji mtoto Vashal kwa mashaka.
“Nenda ndani baba” alisema Bi.Fahreen.
“Mr.Nakesh iko piga veve?”
“Vashal, nenda kwa nyumba” alijibu mwanamke yule kwa ufupi.
“No Mom, nani chuza veve?” mtoto Vashal aliendelea kudadisi.
“Vashal mimi iko piga veve, I said nenda kwa nyumba!” Bi.Fahreen alizungumza kwa ukali na kumsukuma Vashal.
Mtoto Vashal alipofokewa na kusukumwa ikabidi ajiongeze na kutoka nduki kuingia ndani na kumuacha mwanamke yule aliyekuwa mkali kama mbogo pale barazani.
Vijana wale wawili walipoteremka tu Rachna alimsogelea Magosho na kumshika mkono, wakawa wanatembea huku wameshikana mikono. Bi.Fahreen alipowaona akasimama ghafla kutaka kuwavaa wawili wale waliokuwa wamedhamiria kuumiza moyo wake.
ITAENDELEA




No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa