KITUMBUA CHA KIHINDI SEHEMU YA 18 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Wednesday, February 5, 2020

KITUMBUA CHA KIHINDI SEHEMU YA 18





ILIPOISHIA
Wasiwasi na hofu vilizidi kumtawala Ashura na taratiibu akajikuta akiingiwa na majuto ya kujiingiza kwenye shughuli kama ile pamoja na kwamba ilikuwa na dalili zote za kumtajirisha kwa muda mfupi.

ENDELEA…18
****
Rachna alikuwa akiendelea kufuta macho yake huku akiwa ametawaliwa na tabasamu. Wakati huwo Bi.Fahreen ambaye alikuwa amejawa na hasira juu ya binti yake huyo alikuwa bado amesimama mlangoni pale.
“Karibu mom” Rachna alimkaribisha mama yake.
“Itia mimi Gosoo” alizungumza Bi.Fahreen kwa sauti kavu ambayo haikuwa yakwake kutokana na hasira alizokuwa nazo.
“Mnh! Mom, Goso iko furahisa mimi bhanaa” Rachna alizungumza kwa sauti ya kudeka pasipo kufahamu kuwa mama yake alikuwa amejawa na hasira juu yake.
“Veve iko chizi sana! mimi iko sida na Goso halafu veve leta jhinga jhinga yako hapa!” Bi.Fahreen alishindwa kuizuia hasira yake na kujikuta akimfokea binti yake ambaye alikuwa akimpenda kuliko kawaida.
“Basi mom, samehe mimi” Rachna alijikuta akiwa mpole ghafla. Aligundua kuwa mama yake alikuwa amekasirika.
“Hapana chelewesa mimi tena, itia Goso bhanaa” Bi.Fahreen alizungumza kwa hasira zaidi.
“Gosooo!” Rachna alipaza sauti kumuita Magosho ambaye alikuwa chumbani kwake akisikiliza majibizano yale kati ya Rachna na mama yake.
“Naam” Magosho aliitika kwa sauti ya chini iliyokuwa imajaa woga na wasiwasi.
“Kuje huku mom iko sida” alisema Rachna huku akiwa amegeukia chumbani kwake ambako Magosho alikuwemo.
Magosho alikurupuka na kutoka nje kwa wasiwasi akihofu kukutana na sura ya Bi.Fahreen. Rachna aliingia chumbani na kuwaacha mama yake na Magosho wamalizane.
“Naam mama” Magosho aliitika mara tu alipofika pale nje
Bi.Fahreen alimtazama kuanzia chini hadi juu kisha akatoa pumzi ndefu kuashiria kuwa alikuwa amejawa na hasira ndani ya moyo wake. kengere ya hatari ikagonga kwenye ubongo wa Magosho, akafahamu wazi kuwa alikuwa amekwisha zua balaa.
“Kuje huku” Bi.Fahreen alizungumza huku akiondoka kuelekea nje.
Pasipo kujishauri Magosho alimfuata mke wa bosi wake nyuma.
Bi.Fahreen alifika nje na kusimama barazani huku akionekana dhahiri kuwa alikuwa na hasira.
“Hivi veve Goso iko taka kufe?”
“Kwanini mpenzi”
“Iko naanza lini hiyo tabia?” alihoji Bi.Fahreen
“Tabia gani?”
“Hapana uliza mimi swali! veve iko toa penzi kwa toto yangu?” alihoji Bi.Fahreen huku sura akiwa ameikunja kwa hasira.
“Hapana mpenzi, tulikuwa tunapiga stori tu” Magosho alijaribu kujitetea.
“Napiga stori kwa chumba ya toto yangu?” Bi.Fahreen alihoji kwa hasira.
Swali la Bi.Fahreen lilimfanya Magosho kutulia kimya na kutafakari cha kujibu. Wakati huo Rachna alitoka chumbani na kusimama mlangoni. Alikuwa akiwatazama mama yake na Magosho walivyokuwa wakiangaliana kama majogoo. Bi.Fahreen alipomuona mwanae akajikuta akishiwa pozi.
“Hapana leta tena jhinga yako, nenda shule kachukue toto yangu” Bi.Fahreen alibadilisha maongezi mara tu alipobaini kuwa Rachna alikuwepo jirani na mahali pale.
“Sawa mama” Magosho alijibu na kuingia ndani kuchukua funguo za gari.
Alipokuwa anatoka aliwakuta Rachna na mama yake bado walikuwepo pale nje wakizungumza mambo yao ambayo yeye hakuyafahamu.
“Gosooo” Rachna alimuita Magosho alipokuwa anatoka nje.
Magosho alisimama na kugeuka nyuma kumtazama Rachna ambaye alikuwa anamuita.
“Ngoje mimi twende vote” alizungumza Rachna huku akivuta hatua kumfuata.
Magosho aliposikia maneno yale akajikuta akiishiwa na nguvu. Alimtazama Bi.Fahreen
ambaye alikuwa akimkata jicho la kumuonya kufanya kile ambacho Rachna alikuwa anakitaka.
“Lakini dada Rachna we ungepumzika tu, ngoja mimi nikamchukue mtoto” Maosho alizungumza kwa tahadhari baada ya kubaini kuwa Bi. Fahreen hakuwa amebariki safari ile.
“Goso taka nyima mimi safari veve?” alizunumza Rachn huku akimuelekeza kidole Magosho.
“Hapana Rachna my baby veve pumzike bhanaaa, hii Goso ipo hapa kwa kazi hiyo” alizungumza Bi. Fahreen kwa msisitizo ili kumshawishi binti yake asiongozane na Magosho.
“No Mom, mimi iko penda sana Goso, acha sindikize yeye” Jamani nyie binti yule alizungumza maneno makali kwa mama yake pasipo kuelewa kama alikuwa anautesa mtima wa mwanamke wa watu.
“Veve Rachna iko bisi sana mashiku izi” alizungumza Bi. Fahreen kwa ukali kidogo.
“Gosooo leo mimi endesa motukaa, vhevhe kae pembeni ya mimi” alizungumza Rachna na kumshika mkono Maosho kumvuta kuelekea kulipokuwa kumepaki gari.
Magosho alisita kuondoka lakini kutokana na lazima na machachari ya Rachna akajikuta akivuta hatua kuelekea kwenye gari huku wakimuacha Bi. Fahreen akiwakodolea macho kwa mshangao.
Kitendo kile cha Rachna kutaka kuondoka na Magosho kilizidi kumchanganya Bi.fahreen. Wivu ukamjaa na kuanza kutetemeka kwa hasira. Alibakia akiwatazama vijana wale wawili jinsi walivyokuwa wakiondoka.
Ndugu msomaji laitani Rachna asingekuwa mtoto wake wa kumzaa, nafikiri siku hiyo ndiyo ilikuwa mwisho wa maisha yake binti yule. Kijasho chambaamba kilikuwa kikimtiririka masikini mama wawatu. Kumbe wivu ni kitu hatari kiasi kile, Duuh! Ndugu msomaji omba sana katika maisha yako ugonjwa huu hatari wa wivu usije ukakupata mana unaweza ukafa kibudu ilhali unapumua.
Kwakuwa Rachna alikuwa ni mtu wa matani muda wote, alizidi kummaliza mama yake kwa kumshika kiuno Magosho wakati wanatembea.
“My God! Hii toto kuwe setani sasa!” alihamaki Bi. Fahreen huku akipeleka mkono wake kifuani kushika mapio ya moyo wake.
Masikini ya Mungu Rachna hakuwa na maana yoyote ile mbaya, tabia yake ya ucheshi na kupenda utani ndiyo iliyokuwa ikimmaliza mama yake kipenzi. Hakufahamu kabisa kama Magosho alikuwa ni baba yake wa mpango wa kando.
Magosho alielewa hali halisi aliyokuwanayo Bi. Fahreen kwa wakati ule, lakini angefanya nini sasa wakati Rachna hakuelewa kitu na ndiye aliyekuwa akifanya vituko mbele ya mama yake. Magosho akajikaza na kujichekesha mbele ya macho ya Rachna lakini ndani ya moyo wake kulikuwa na hofu na mashaka makubwa dhidi ya Bi. Fahreen.
Wakitembea huku wakicheka na kugongeana mikono Magosho na Rachna waliingia kwenye gari ndogo na safari ya kuelekea shuleni kwa mtoto Vashal ikaanza.
Kule nyuma Bi.Fahreen alizidi kuishiwa nguvu, na kwambaali akajikuta akimchukia binti yake Rachna ingawa alikuwa akimpenda kuliko maelezo.
Magosho aliendesha gari huku akilini mwake akiwaza namna ambavyo angekuja kujitetea kwa Bi.Fahreen mwanamke ambaye alikuwa ametawala uhuru wake. Kwa kiasi fulani alianza kujihisi mtumwa wa mapenzi. Kidogokidogo akaanza kujutia maamuzi yake ya kukubali kulala na mwanamke yule ambaye alikuwa sawa kabisa na mama yake mzazi.
Rachna ambaye alikuwa ameketi pembeni mwa Magosho alikuwa akimtazama dereva wao jinsi alivyokuwa akibadili gia na kukanyaga mafuta. Hakika aliridhika kabisa na kumsifu kimoyomoyo mwalimu aliyemfundisha kuendesha gari kijana yule hodari wa kuongoza gari lile.
Rachna aliinua macho yake na kumtazama usoni Magosho kwa makini ili kuendelea kuthibitisha umahiri wa dereva wa mama yake. Lakini Rachna alibaini hali tofauti kwenye sura ya Magosho.
“Gosoo” aliita Rachna kwa sauti ya chini.
Magosho hakuitika wala hakugeuza shingo kumtazama binti yule wa kihindi. Alikuwa amesikia vizuri wito ule lakini moyo wake ulisita kutoa ushirikiano wowote ule. Alihofia sana kupoteza kibarua chake kwa mambo ya kipuuzi kama yale aliyokuwa ameyafanya Rachna.
“Vhevhe Gosoo!” Rachna aliita tena kwa sauti.
Magosho hakuitika bali aligeuza shingo yake na kumtazama Rachna kisha akarudisha macho yake kutazama mbele.
“What is the problem?” (Tatizo nini) Rachna alihoji kujua kama kulikuwa na tatizo.
Magosho alitingisha kichwa kuonesha kuwa hakukuwa na tatizo lolote ambalo lilikuwa likimkabili.
“Sasa mbona iko ivo, au Mom iko kosea vhevhe?” Rachna akahoji kwa sauti iliyokuwa imejaa mashaka.
“Hapana dada Rachna nipo sawa tu” Magosho alizungumza huku akibana mafuta na kubadilisha gia kwenye tuta la barabarani.
****
Mawazo ya woga yalimjaa Ashura kila lipokuwa anakumbuka kesi za vijana wa kitanzania kuvuma kukamatwa na madawa ya kulevya nje na ndani ya nchi. Alimtazama Zawadi kwa hasira kwasababu ndiye aliyekuwa anamshawishi kufanya biashara ile.
“Haiwezekani” alisema Ashura kwa sauti ya msisitizo.
“Kipi kisichowezekana?” Zawadi alihoji huku macho yake akiwa ameyafinya kidogo kuonesha umuhimu wa swali lake.
“Mimi siwezi kufanya biashara haramu” Ashuara alizungumza kwa msisitizo
“Nahisi una wazimu we binti”
“Kama ningekuwa na wazimu ningekubali kufanya biashara za ajabu ajabu kama hizi” alizungumza Ashura kwa kujiamini.
“Kwahiyo unachokitaka hasa ni kipi?” Zawadi alihoji kwa sauti iliyojaa kiburi
“Nahitaji kutoka humu kwenye hili pango lenu” alisema Ashura.
“Pango la nani?” alihoji Zawadi kwa mkazo.
“Sijui mimi, ninachotaka ni kutoka humu” Ashura aliendelea kuzungumza kwa msisitizo.
“Umechelewa Ashura, tayari umeshafahamu ziri za kitumbua cha kihindi. Hivyo hili pango linakuhusu kwa namna moja ama nyingine” Zawadi akaeleza kwa msisitizo.
“Thubutuuu!, Zawadi kumbe hunifahamu vizuri wewe!” Ashura akazungumza kwa vitisho ili kumshawishi Zawadi aweze kumuacha Huru.
“Kwahiyo unataka kusemaje Ashura?” Zawadi akahoji kwa msisitizo mkubwa huku akijitikisa na macho yake akiyachezesha kwa dharau na kebehi.
“Naondoka, wewe endelea na vitumbua vyako vya kihindi” alizungumza Ashura kwa msisitizo.
“Okay, unaweza kuondoka” Zawadi alijibu taratibu lakini kwa sauti iliyokuwa imejaa gadhabu.
Ashura alibinua midomo yake kwa hasira kisha akavuta hatua kuanza safari ya kurudi kule walipotokea. Ni kweli kabisa pesa alikuwa anazihitaji lakini anaufahamu vizuri mziki wa watu wanaokamatwa kwa uhalifu wa madawa ya kulevya.
Zawadi alisimama huku mikono yake ameikumbatia kifuani na kumtazama jinsi ambavyo Ashura alivyokuwa akiondoka kwa kiburi. Aliachia tabasamu na kutikisa kichwa kwa masikitiko.
ENDELEA…



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa