KITUMBUA CHA KIHINDI SEHEMU YA 17 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Wednesday, February 5, 2020

KITUMBUA CHA KIHINDI SEHEMU YA 17






ILIPOISHIA
Magosho alikamata kitasa cha mlango na kukinyonga tayari kwa kuingia chumbani mle. Sauti ya mtu aliyekuwa anajikohoza ilimgutusha na kumfanya ageuke. Macho yake yalikutana na macho ya Bi.Fahreen ambaye alikuwa ameegemea ukuta huku akimtazama jinsi alivyokuwa amekikamatia kitasa cha mlango wa chumba cha binti yake Rachna.
Magosho akabaki ameduwaa, alishindwa kufungua mlango kuingia na pia akashindwa kuachia kitasa cha mlango ule. Aibu na woga ndivyo vilikuwa vimemtawala kwa wakati ule.

ENDELEA….17
“Gosooo” Rachna alizidi kuita kule chumbani pasipo kuelewa kitu kilichokuwa kikiendelea nje ya chumbani kwake.
Magosho hakuitika bali aliinua macho yake na kumtazama Bi.Fahreen ambaye alionekana kuvimba kwa hasira pale alipokuwa amesimama.
Magosho aliachia kitasa cha mlango wa Rachna kwa aibu huku akitazama chini na kuachia tabasamu ambalo halikuwa na ulazima.
“Shikamoo mama” akasalimia kwa haya huku akikutanisha viganja vya mikono yake na kuvisugua sugua.
Bi.Fahreen aliachia msonyo huku akimtazama Magosho kwa dharau na hasira.
“Dada Rachna aliniita” Magosho alijaribu kujitetea
“Nani iko mama yako?”
“Nisamehe  mpenzi, hakuna kinachoendelea kati yetu” alizungumza Magosho kwa sauti ya chini ili Rachna kule chumbani asisikie maneno yale makali.
Rachna baada ya kuona Magosho anachelewa kuingia alifungua mlango na kuchungulia nje. Alimkuta mama yake amesimama hatua chache akitazamana na Magosho.
“Mom, mimi iko sida na Goso huku kwa chumba yangu” Rachna alizungumza pasipo kufahamu kitu kilichokuwa kikiendelea kati ya watu wale wawili.
“Ooh! No problem my daughter” Bi.Fahreen alijikakamua na kuzungumza huku kwenye uso wake akiwa amevaa tabasamu la bandia. Alimruhusu Rachna kuendelea na shughuli yake na Magosho. Rachna alimshika mkono Magosho na kuingia naye chumbani.
Kule nyuma Bi.Fahreen alipandwa na hasira zilizokuwa zimechanganyikana na wivu. Alikwenda kwenye kochi na kujitupa kama vile mgonjwa mahututi. Akajikuta akichukia sana uwepo wa Rachna ndani mle. Aliona wazi asali yake ilikuwa inaelekea kudokolewa nab inti yake kipenzi.
Rachna alipofika chumbani kwake aliketi kwenye kitanda na kumkaribisha Magosho kwenye kochi.
“Karibu kwa chumba yangu Goso” alisema Rachnakwa ile sauti yake nyororo iliyokuwa ikimmaliza Magosho.
“Kwanini tusiende kukaa sebleni dada Rachna?” Magosho akazungumza kwa sauti iliyokuwa imejaa hofu na mashaka. Wasiwasi wake wote ulikuwa kwa Bi. Fahreen ambaye alimtisha kwa kumtazama kwa jicho kali la onyo na tahadhari kubwa.
“Kae kwa sebule kwani sisi iko geni bhana!” alizunumza Rachna huku akirembua macho yake meupe yaliyokuwa yamepambwa kwa kope ndefu nyeusi.
“Kwahiyo wanaokaa sebleni ni wageni tu?” alihoji Magosho huku akijaribu kukwepesha kidogo macho yake kumtazama mrembo yule aliyekuwa mbele ya macho yake.
“Yes. Iko ivo” alisema Rachna huku akijiweka vizuri pale kitandani.
Kusema ukweli hapakuwepo na jambo lolote baya lililokuwa likiendelea kati ya Rachana na Magosho kule chumbani. Stori za hapa na pale ndizo zilizokuwa zikiendelea. Ucheshi wa Rachna ulimfanya Magosho kuondokewa na uwoga ingawa awali alikuwa na wasiwasi.
Walizungumza na mara kwa mara walikuwa wakiangua vicheko vya sauti huku wakigongeana mikono. Moyo wa Magosho ulijawa na amani baada ya kupata nafasi ya kuzungumza na mrembo yule wa kihindi ambaye alionekana kuwa mcheshi kuliko kawaida. Alisahau kabisa habari na vitisho vya yule mama mtu mzima wa kihindi.
Zile sauti za vicheko vya Magosho na Rachna kule chumbani zilimfikia vizuri sana Bi. Fahreen ambaye alikuwa ameketi kwa gadhabu sebleni. Alijikuta hasira zikimzidi kila alipokuwa akiwasikia watu wale wakicheka kwa furaha kule chumbani.
“Hii Goso iko bure kabisa!” alizunumza Bi. Fahreen kwa hasira huku akijiinua kutoka kwenye kochi na kusimama wima huku ameshika kiuno na midomo ya chini akiiuma kwa meno yake ya juu.
Mwanamke yule wa kihindi alizunguuka zunguuka pale sebleni huku akikuna kichwa chake kwa ghadhabu. Alikuwa akiamini kuwa binti yake alikuwa anaelekea kupora penzi lake kutoka kwa Magosho.
Uvumilivu ulimshinda Bi.Fahreen na kuvuta hatua kuelekea kwenye mlango wa chumba cha Rachna. Alisimama na kutega sikio kusikiliza kilichokuwa kikizungumzwa na wawili wale waliokuwa wamejifungia chumbani mle.
Pale mlangoni Bi. Fahreen aliambulia kusikia sauti za vicheko tu, maneno yaliyokuwa yakizungumzwa hakufanikiwa kuyasikia kwasababu yalikuwa yakizunumzwa kwa sauti ya chini. Hilo ndilo lililozidi kummaliza Bi.Fahreen pale mlangoni na kuhisi tayari binti yake alikuwa ameshafanya mapinduzi ya huba.
Wivu ulizidi kumtafuna mama yule wa kihindi na mwisho uzalendo ukamshinda. Kijana ambaye alikuwa akimpatia huduma takatifu anaona dalili za kumpoteza. Mbaya zaidi alikuwa anampoteza kwenye mikono ya binti yake mwenyewe.
“Haiwezekani” Alisema na kugonga mlango wa chumbani mle.
Mlango ulifunguliwa na Rachna ambaye alikuwa akifuta macho yake kutokana na mchozi yaliyokuwa yamesababishwa na kucheka sana. Bi.Fahreen alipomuona binti yake anafuta macho akajikuta akizidi kuchanganyikiwa na kujawa na wivu zaidi akiamini Magosho alimpa dozi binti yake hadi kumtoa machozi.
****
Zawadi alichukua paketi ya ule unga wa vitumbua alioutoa kwenye tanki na kuupasua kisha akauingiza kwenye karai la mashine moja lililokuwa likifanana na lile la mashine ya kukobolea mahindi lakini lenyewe lilikuwa na mfuniko. Baada ya hapo alichukua maji kutoka kwenye tanki jingine na kuyamimina mle kwenye mashine. Alichukua sukari kiasi cha kilo moja na kuimimina pamoja na yale maji kisha akabonyeza kitufe chekundu kwenye mashine ile na baada ya muda ikasikika ikiunguruma kwa sauti ya chini.
“Ama kweli ni vitumbua vya kihindi” Ashura alizungumza kwa mshangao.
Zawadi hakumjibu kitu chochote bali alikwenda kule kwenye kile chumba walichopita na kurejea na zile pakiti za unga uliokuwa umefanana na unga wa ngano uliokuwepo kwenye kabati.
“Unakumbuka vitu hivi?” alihoji Zawadi huku akimuonesha Ashura paketi zile.
“Sana tu” Ashura alijibu kwa kifupi.
Zawadi alifungua mtambo mwingine uliokuwa pembeni na mashine ile aliyokuwa ameiwasha awali.
“Unaona mashine hii?”
“Ndio…” alijibu Ashura huku akisogea pale alipokuwa amesimama Zawadi.
“Kwanza unaiwasha, halafu unachukua pakiti hizi, unazitumbukiza na nailoni zake” Zawadi alizungumza huku akifanya na vitendo. Kitu kilichomshangaza Ashura ni kile kitendo cha kutumbukiza pakiti za unga ule pamoja na nailoni zake.
“Sasa mbona hutoi hizo nailoni?” Alshura alihoji,
“Unga huu huwa hautolewi kwenye pakiti” Zawadi alizungumza huku akizitumbukiza pakiti zile moja moja mtamboni.
“Kwanini?” Ashura akahoji kwa mshangao.
“Kwasababu hii ndiyo mali yenyewe”
“Kwani ni unga wanini huo?”
“Hii ni COCAIN”
“Cocain!” Ashura alitamka neno lile kwa mshangao.
“Unacho shangaa ni kipi sasa?”
“Cocain si ni madawa ya kulevya?” alihoji Ashura kwa mshangao huku akihisi mwili wake ukiingiwa na baridi ya woga.
“Sasa kama ni madawa ya kulevya wasiwasi wako wewe ni nini?” Zawadi alihoji huku akimalizia kutumbukiza pakiti ya mwisho kwenye mtambo. Alisogea kwenye mashine ya kwanza na kuifunua kama vile kutazama maendeleo ya unga wa awali uliokuwa umechanganywa na maji.
“Njoo uone huku” Zawadi alimuita Ashura ambaye alikuwa ameduwaa kwa mshangao baada ya kuambiwa kuwa unga uliotumika ulikuwa ni madawa ya kulevya.
Ashura alisogea hadi pale na kuchungulia kwenye karai lile. Hapakuwepo na kitu chochote. Akageuza shingo yake na kumtazama Zawadi usoni kwa jicho la udadisi huku moyoni mwake akiwa bado amejawa na hofu
“Ukishaona karai limekuwa tupu unazima mashine” Zawadi alizungumza huku akibonyeza kitufe cha kuzimia kilichokuwa na rangi nyekundu.
akili ya Ashura ilikuwa imehama kabisa kiasi cha kuto kuzingatia kile alichokuwa anaelekezwa. Taarifa ile ya unga wa cocain ilikuwa imemchanganya kabisa.
“Sasa Zawadi…” aliita Ashura kwa sauti ya chini.
“Enhee….”
“Watu wakila hivi vitumbua si watalewa?”
“We wacha maswali bwanaaa, njoo mtamboni” Zawadi alimvuta mkono Ashura hadi kwenye mashine ya pili ambayo ilikuwa bado ikitoa mlio wa muungurumo kuashiria kuwa ilikuwa inaendelea kufanya kazi. Alibonyeza kitufe kingine na mashine ikabadili sauti na kutoa muungurumo mzito lakini nao pia haukuwa wa sauti ya juu.
“Ukisha washa hapa unasubiri dakika kama tano hivi” Zawadi alitoa maelekezo kisha akachukua sinia kubwa na kuliweka mbele ya mashine ile ambako kulikuwa na tundu dogo. Ashura alibakia kimya akimtazama rafiki yake yule ambaye alikuwa akishughulika vilivyo.
“Sasa tayari unaweza kubonyeza hapa” alitoa maelekezo huku akibonyeza mahali alipokuwa anapazungumzia.
Baada ya sekunde kadhaa vitumbua vilianza kudondokea kwenye lile sinia alilokuwa ameliweka kwenye tundu la mashine ile.
“We Zawadi!” Ashura alijikuta akihamaki na kusogea pale kwenye sinia lililokuwa likidondokewa na vitumbua.
“Vipi?” alihoji Zawadi huku akiachia tabasamu la matumini.
“Mbona mchawi hivyo?” Ashula alisema kwa kuhamaki.
“Mambo ya kihindi hayo” alisema Zawadi na kwenda kuzima mashine.
“Imekuwaje hapa?”
“Hapo mambo tayari kwa biashara” Zawadi akaeleza.
“Na ile Cocain imekwenda wapi?”
“Imo humo humo”
“Wapi?”
“Kwenye kitumbua”
“Lakini zawadi una dhambi wewe!”
“Dhambi za nini?”
“Sasa watu wa watu si watalewa wakila hivi vitumbua?”
“Hivyo vitumbua sio vya kula”
“Kumbe?”
“Vya biashara”
“Sasa ukifanya biashara ya chakula maana yake si kitaliwa?”
“Kikate katikati uone” Zawadi alizungumza kwa kujiamini.
Kwa hamasa kubwa Ashura alikimega kitumbua kile kilichokuwa mkononi mwake na kukikodolea macho. Hakuweza kuamini, pakiti ya Cocain ilikuwa ndani ya kitumbua kile.
“Hee!” Ashura alihamaki kwa mshituko.
“Sasa kazi ya vitumbua vyetu ni kusafirisha mzigo huwo” Alizungumza zawadi kwa kujiamini.
“Kuupeleka wapi?” alihoji Ashura
“Tunaupeleka katika nchi mbalimbali za hapa duniani, kama vile China na Afrika Kusini” alisema Zawadi.
Ashura aliposikia maneno yale alishituka sana. Akakumbuka matukio kadhaa yaliyotokea siku za hivi karibuni jinsi serikali ilivyotilia mkazo katika suala la madawa ya kulevya.  Akakumbuka taarifa alizozipata za watu kufungwa jela kifungo cha miaka 30 kwa sababu hiyo hiyo ya biashara ya madawa ya kulevya.
Wasiwasi na hofu vilizidi kumtawala Ashura na taratiibu akajikuta akiingiwa na majuto ya kujiingiza kwenye shughuli kama ile pamoja na kwamba ilikuwa na dalili zote za kumtajirisha kwa muda mfupi.
TUKUTANE



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa