KITUMBUA CHA KIHINDI SEHEMU YA 16 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Wednesday, February 5, 2020

KITUMBUA CHA KIHINDI SEHEMU YA 16






ILIPOISHIA
Moyo wa Ashura ulisita kuingia kwenye pango lile ambalo ndani kulikuwa hakuonekani kitu kutokana na kiza kinene kilichokuwa kimetanda. Zawadi akiwa ndani ya lile pango aligeuka na kumchungulia Ashura ambaye alikuwa bado amesimama pale nje.

ENDELEA …
“Vipi wewe! twende” Zawadi alisisitiza kwa kutumia kiganja chake cha mkono.
Ashura huku akiwa na wasiwasi aliingia ndani ya pango lile kisha Zawadi akaufunga mlango wa pango lile.
Kwakuwa kiza kilikuwa kinene Ashura alishindwa kujua pa kuelekea. Zawadi alimtangulia na kumwambia amshike blauzi na kumfuata kwa nyuma.
Safari ile ya Zawadi na Ashura kwenye lile pango iliwachukua takribani dakika kumi hivi kwa mwendo wa kutambaa na magoti. Ashura alikuwa akitambaa kumfuata Zawadi lakini hofu ya kupoteza uhai wake ilikuwa imemjaa moyoni mwake. Hata hivyo hakukata tamaa na kuendelea kusonga mbele kuzama zaidi ndani ya pango lile.
Walitokea sehemu moja iliyokuwa na chumba kipana kilichokuwa na ukuta uliokuwa umepakwa rangi nyeupe sana. Ndani mle kulikuwa kumezunguukwa na makabati ya ukutani. Chumba kile kilikuwa na mwanga wa kutosha ukilinganisha na kwenye lile pango walimokuwa wakipita.
“Zawadi” Ashura aliita huku akizunguusha macho yake kuangalia mazingira yale.
“Niambie shost” Zawadi aliitika kwa sauti ya upendo pasipo kuwa na tabasamu lolote.
“Hizi ndio kanuni na taratibu za hivyo vitumbua vya kihindi zinaendelea?” Ashura alihoji kwa sauti iliyokuwa imekata tamaa.
“Baada ya dhiki faraja” Zawadi alijibu huku akifungua moja ya kabati lililokuwa mle ndani.
Hadi kufikia wakati ule kitumbua cha kihindi bado kilikuwa ni fumbo kubwa sana kwa msichana Ashura. Pamoja na kwamba alijiingiza kushiriki katika biashara ile tena kwa viapo vya vitabu vitukufu lakini bado hakuwa na mwanga wowote.
“Mungu wangu!” Ashura alihamaki baada ya kuona kilichomo ndani ya lile kabati lililofunguliwa na Zawadi.
Ashura aliweza kushuhudia idadi kubwa sana ya pesa za kitanzania zikiwa zimepangwa ndani ya kabati lile.
“Kawaida sana, Mungu akupe nini tena?” Zawadi alizungumza huku akilifunga kabati lile na kuendea kabati lingine lililokuwa jirani na kulifungua.
“We Zawadi!” Ashura alizidi kuhamaki baada ya kuona mabunda ya noti za dola ya kimarekani yamepangwa kwenye kabati lile.
“Vipi kuna tatizo?” Zawadi alihoji huku akimgeukia Ashura
“Pesa zote hizo ni za nani?”
“Zakwangu mimi na wewe” Zawadi alijibu kwa mkato.
“Kwa lipi hasa?”
“Kitumbua cha kihindi” alijibu Zawadi huku akitabasamu.
“Mnh!”
“Huna sababu ya kuguna njoo uone” alisema Zawadi huku akifungua kabati lingine.
Kilichokuwemo ndani ya kabati lile kilikuwa kigeni machoni mwa Ashura. Kulikuwa na pakiti nyingi sana zilizokuwa zimejazwa vitu vilivyofanana na unga wa ngano.
“Unafahamu hii?” Zawadi alimuuliza rafiki yake huku kimuoneshea zile pakiti.
“Sio ngano hii kweli?” Ashura alijibu huku akibonyeza bonyeza pakiti zile.
“Usijali utafahamu tu”
“Ni kitu gani?”
“Hii ndiyo pesa yenyewe sasa”
“Kwahiyo huu ndio unga wa kupikia hivyo vitumbua vya kihindi?”
“Naweza nikakwambia ndio au hapana”
“Kivipi sasa?”
“Njoo hapa” Zawadi alizungumza na kusogea kwenye kabati jingine refu kuanzia juu hadi chini lililokuwa karibu na lile pango waliloingilia.
Zawadi alipolifungua kabati lile Ashura akabaini kuwa kumbe halikuwa kabati kama alivyo dhani bali ulikuwa ni mlango. Yani kila hatua waliyokuwa wakipitia Ashura alijikuta akipatwa na mshangao. Bado alikuwa kama vile yupo usingizini kwasababu hakuna ambacho aliking’amua juu ya kile kitumbua cha kihindi.
“Twende zetu tajiri wangu” alisema Zawadi huku akiingia kwenye mlango ule aliokuwa ameufungua.
Kama ilivyokuwa kawaida Ashura alimfuata nyuma Zawadi. Walipoingia kwenye mlango ule, wakatokea sehemu moja ambayo ilikuwa na mashine nyingi ambazo Ashura hakuwahi kuziona katika maisha yake tangu alipokuwa amezaliwa.
“Sasa hapa mama ndipo jikoni kwetu” Zawadi alimtambulisha rafiki yake ambaye muda wote alikuwa ni mtu wa kushangaa shangaa. Ashura aliangaza kila kona mle ndani lakini hakuona jiko wala flampeni za kukaangia hivyo vitumbua.
“Jiko lenyewe liko wapi?” alihoji Ashura huku akijaribu kulitafuta mwenyewe.
“Hapa ndipo kila kitu” Zawadi alijibu huku akiwa ameweka mkono wake kwenye moja ya mashine zilizokuwemo mle ndani.
Ashura alisogea na kuishangaa ile mashine aliyoambiwa kuwa ndio kila kitu. Kusema kweli mashine ile ilikuwa haifanani na jiko la aina yoyote ile ambalo alikuwa anayafahamu yeye.
“Sasa hapa ndio unafanyaje?” alihoji Ashura huku akiikagua kwa makini mashine ile.
“Tulia mama” Zawadi alijibu na kuvuta hatua hadi sehemu moja ambayo ilikuwa na vitu kama matanki ya kuhifadhia maji. Aliingiza mkono na kuchomoa pakiti moja iliyokuwa na unga.
“Huu mama ni unga wa kawaida unatokana na mchele” Zawadi alizungumza huku akimuonesha Ashura ile pakiti ya unga aliokuwa ameutoa kwenye moja ya tanki lililokuwemo mle chumbani. Ashura alitulia kama kawaida yake akimsoma kiongozi ama mwalimu wake wa kazi.
****
Magosho alipaki gari kisha akateremka na kuzunguuka kwenye buti la gari ambapo alifungua na kutoa mzigo wa Rachna. Wakati huo Rachna na Bi.Fahreen walikuwa wamekwisha teremka na kuanza kuelekea ndani.
Magosho aliutoa ule mzigo kisha akauweka chini huku macho yake akiwa ameyagandisha kwa mgeni Rachna ambaye alikuwa ameongozana na mama yake.
“Haki ya mungu wallah” Magosho alijikuta akizidi kuchanganyikiwa na mtoto yule wa bosi wake. Alitikisa kichwa kusikitika kisha akavuta pumzi na kuzitoa kwa nguvu. Alimsifu Muumba kwa ustadi mkubwa aliouonesha kwa kumtengeneza Rachna pasipo kumfanyia choyo wala hasira hata chembe.
Bi. Fahreen na binti yake walipokuwa akikaribia kuingia ndani, yule mama wa kihindi aligeuka nyuma na kumfuma Magosho amesimama akiwakodolea macho. Mama yule alikunja sura yake kisha pasipo kuzungumza neno lolote alivuta hatua kurudi nyuma alipokuwa magosho.
Magosho aliisoma hali ya hatari kwenye sura ile ya mwanamke wa kihindi ambayo tayari alikuwa amekwisha kuizoea vya kutosha. Alichofanya yeye ni kuinua begi na kuvuta hatua kuelekea ndani. Wakakutana na Bi. Fahreen njiani.
“Vhevhe Goso, hiyo macho yako mbona hapana tulia leo?” alihoji Bi.Fahreen huku akiwa amemkazia macho Magosho.
“Kwanini unasema hivyo mama?” Magosho alihoji kwa wasiwasi.
“Pumbaaaa, yaani nazidi tibua mimi?”
“Mnh!” Magoshio aliguna kwa msahngao.
“Fyee nini? Iko tamani toto yangu halafu naita mimi mama?” Bi.Fahreen alizungumza kwa hasira huku akiwa amemtolea macho Magoso wa watu.
“Nisamehe kwa kukuita mama, lakini kuhusu kumtazama Rachna hilo sio kweli Bi.Fahreen” Magosho alijaribu kujitetea.
“Shut up! sasa ole yako sikia veve iko chukua toto yangu” Bi.Fahreen alizungumza na kuchukua lile begi kwa hasira kisha akaondoka na kumuacha Magosho ameduwaa kwa mshangao.
****
Onyo alilokuwa amepewa Magosho na Bi.Fahreen lilimfanya kuwa makini wakati wote. Hata hivyo tabia za Rachna zilimfanya Magosho kuwa katika wakati mgumu sana. Rachna alikuwa ni msichana mcheshi na mwenye upendo na watu wote pasipo kujali rangi wala jinsia. Kwa kipindi kifupi sana alikuwa tayariamekwisha kumzoea Magosho kutokana na tabia yake hiyo.
Mara nyingi sana Rachna alikuwa anapenda kuketi pamoja na Magosho hasa anapokuwa nyumbani. Alifanya hivyo pasipo kufahamu kuwa kitendo kile kilikuwa kikimtia hatarini kijana wawatu.
“Gosooo!” ilikuwa ni sauti mwanamke ikimuita Magosho ambaye alikuwa chumbani amepumzika.
“Vhevhe Gosooo!” Sauti ile iliita tena.
Magosho alikurupuka kutoka chumbani akiamini kuwa mtu aliyekuwa akimuita alikuwa ni Bi.Fahreen. Alipotoka tu akakutana na Rachna amesimama hatua kadhaa kutoka mlangoni kwake.
“Ooh! dada Rachna kumbe ni wewe?” Magosho alitamka huku akionekana kuishiwa nguvu.
“Vipi iko lala vhevhe?” alihoji Rachna kwa sauti ya upole.
“Hapana sikuwa nimelala, nilipumzika tu” Magosho alijibu huku akifikicha macho yake kwa vidole vya mikono.
“Kuje huku” Rachna alizungumza huku akivuta hatua kuelekea chumbani kwake.
Magosho alibaki akimkodolea macho binti yule wa kihindi aliyekuwa akitembea kwa nyodo na kudondosha mojamoja.
“Nije wapi sasa dada Rach?” Magosho akahoji kwa mashaka kidogo.
“Kuje kwa chumba yangu” alijibu Rachna pasipo kugeuka nyuma na kuingia chumbani mwake.
Magosho alivuta pumzi ndefu na kuzitoa kwa nguvu. Akajipa moyo kuwa Rachna hakuwa na tabia kama za mama yake Bi.Fahreen kwasababu binti yule alikuwa anajiheshimu sana kuliko mama yake. Hivyo hata kama angekwenda huko chumbani kwake pasingetokea baya lolote.
Tatizo lilikuwa ni kwa Bi.Fahreen ambaye mapema sana alimuonya Magosho kumzoea binti yake huyo ambaye mwenyewe alikuwa ni mcheshi. Hivyo Magosho alikuwa anahofia sana kukutwa na Bi. Fahreen chumbani mle mwa Rachna.
“Gosoooo!” Rachna alipaza sauti kuita.
Magosho akatazama kulia na kushoto kama kulikuwa na mtu anamuona. Baada ya kuhakikisha kuwa hakuwa anaonekana, alivuta hatua hadi pale kwenye mlango wa chumba cha Rachna na kugonga taratibu huku akisikiliza kwa makini kuruhusiwa kuingia.
“Ingia bhanaaa!” Rachna alipaza sauti kutokea ndani ya chumba kile.
Magosho alikamata kitasa cha mlango na kukinyonga tayari kwa kuingia chumbani mle. Sauti ya mtu aliyekuwa anajikohoza ilimgutusha na kumfanya ageuke. Macho yake yalikutana na macho ya Bi.Fahreen ambaye alikuwa ameegemea ukuta huku akimtazama jinsi alivyokuwa amekikamatia kitasa cha mlango wa chumba cha binti yake Rachna.
Magosho akabaki ameduwaa, alishindwa kufungua mlango kuingia na pia akashindwa kuachia kitasa cha mlango ule. Aibu na woga ndivyo vilikuwa vimemtawala kwa wakati ule.



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa