KITUMBUA CHA KIHINDI SEHEMU YA 15 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Wednesday, February 5, 2020

KITUMBUA CHA KIHINDI SEHEMU YA 15






ILIPOISHIA
Magosho aligeuza shingo yake kumtazama Bi.Fahreen ambaye siku zote alikuwa anapenda amuite mpenzi, au baby hasa wawapo wenyewe wawili. Na alichukia sana kuitwa mama. Kosa hilo ndilo ambalo Magosho alikuwa amelifanya.
“Usinitazame, umeniitaje?” Bi.Fahreen alisisitiza swali lake huku ametoa macho.

ENDELEA
“Basi Bosi nisamehe” Magosho ilimbidi atunge jibu la kumpa mama yule aliyekuwa na balaa.
“Enhee iko namna hiyo, mimi bosi yako bhanaa” Bi.Fahreen alijibu huku akitingisha kichwa kujifanya kuwa alikuwa anataka Magosho amuite Bosi. Kumbe alikuwa amejisahau kama walikuwa na mtu mwengine mle ndani ndani ya gari.
“Iko ona toto yangu vhevhe?” alihoji bi Fahreen kwa kujibaraguza.
“Ndio bosi nimemuona, mmefanana sana” alisema Magosho huku akipangua gia na kukata kona.
“Kweli?”
“Kweli bosi. Inaonekana na wewe kwenye ujana wako ulikuwa moto” Magosho alizungumza na kukanyaga mafuta huku akipishana na magari mengine.
“Kwanini iko sema ivo vhevhe Goso?”
“Kwa kweli dada Rachna ni mrembo sana” alisema Magosho huku akimtupia jicho Rachna kupitia kwenye kile kioo kidogo. Alimuona Rachna alivyo vutiwa na kauli ile kiasi cha kumfanya aachie tabasamu zito la furaha. Magosho akajikuta akifarijika sana baada ya kumona binti yule akitabasamu kutokana na maneno yake.
Kwa upande wa Bi.Fahreen kauli ile haikuwa imembariki kabisa. Alishindwa kujizuia kuonesha kukasirika kwake.
“Veveee! hiyo toto yangu chezea mimi, hapana chezea toto yangu” alizungumza Bi.Fhreen huku akimuoneshea kidole cha onyo  Magosho. Magosho alimtupia Bi.Fahreen jicho la wizi, alipoona mambo yameharibika ikammbidi awe mpole.
“Kama mama alikuwa mkali hivyo kwa binti yake, je huyo Mr.nakeshwar angekuwaje?” alijiuliza Magosho alipokuwa akikatiza mitaa ya kariakoo.
****
Ashura akawa ameduwaa pale kwenye kochi akishindwa kutafakari kale kamchezo ka rafiki yake na yule mwanaume wa kihindi. “Shauriyako, mjini shule” aliyakumbuka maneno ya Rafiki yake Zawadi alipokuwa akiingia chumbani na brifkesi iliyokuwa imejazwa pesa.
“Ni nani ambaye hapendi utajiri hapa duniani?” Ashura alijiuliza pale alipokuwa amekaa. “Hakuna ambaye hapendi utajiri, kama ni hoja ya kupika vitumbua hata mimi naweza kupika, sasa kwanini naichezea bahati hii? Haiwezekani” Ashura aliendelea kujiuliza maswali na kujijibu mwenyewe.
Baada ya Ashura kujiuliza maswali na kujipatia majibu yaliyomridhisha, akafanya maamuzi ambayo mwenyewe aliyaona yalikuwa na busara.
“Shost….” Sauti ya zawadi ilimgutusha Ashura kutoka kwenye lindi la mawazo. Ashura aliinua macho kumtazama rafiki yake ambaye alifika pale sitingrum na kuketi kwenye kochi la jirani na pale alipokuwa ameketi yeye.
“Mkataa pema pabaya panamuita” alizungumza Zawadi huku akijiweka vizuri kwenye kochi.
Ashura ahakutia neno lolote zaidi ya kutulia na kumsikiliza kwa umakini rafiki yake yule muuza vitumbua vya kihindi.
“Unayakumbuka vizuri maisha yangu ya nyuma?” alihoji Zawadi huku akiwa amemkodolea macho shoga yake. Ashura akaitikia kwa kichwa huku akimtazama Zawadi kwa umakini wa hali ya juu.
“Kama ningekuwa mgumu wa kuelewa kama wewe, kamwe nisingefikia hapa nilipo” alizungumza Zawadi kwa kujiamini.
Ashura aliinamisha kichwa chini kwa sekunde kadhaa kama vile alikuwa akiyapima yale maneno ya Zawadi kumbe jibu alikuwa nalo kitambo tu.
“Zawadi” aliita Ashura alipoinua shingo kumtazama Zawadi.
“Nakusikiliza”
“Nimeamua kufanya biashara pamoja nawe” alisema Ashura.
Zawadi hakuzungumza neno lolote baada ya kusikia maneno yale kutoka kinywani kwa Ashura. Hakutegemea kama binti yule mwisho wa siku angetamani kuthubutu kuungana naye katika biashara yake ya kuuza vitumbua vya kihindi. Akabaki ameduwaa akimkodolea macho rafiki yake yule.
“Ndio, nimeamua kufanya biashara ya kitumbua cha kihindi” Ashura akazungumza kwa msisitizo huku naye akimkodolea macho Zawadi.
“Kwanini unanitania zawadi?” alihoji Zawadi kwa mashaka ya kauli ile ya Ashura.
“Zawadi, unafahamu mimi siomtu wa kona kona, kama sitaki kitu nakuchana. Sasa nikuongopee ili iweje” Ashura alizungumza kwa msisitizo huku akilini mwake
“Kweli shost?” Zawadi alionesha kuhmaki baada ya kuthibitisha ukweli wa maneno ya Ashura.
“Amini nakwambia shoga yangu” Ashura alijibu kwa kujiamini.
“Wooow! umasikini tupa kuleee!” Zawadi alipaza sauti kushangilia huku akipaga makofi kwa furaha.
Ashura akawa anacheka kwa jinsi ambavyo shoga yake huyo alivyo onekana kuwehuka kutokana na majibu aliyo yatoa.
“Aaah! Jigiji!-Jigiji! Jigiji-jigiji-jijgiji” Zawadi alikuwa akiimba huku akikata viuno na mkono mmoja ameubandika kichwani na mwingine kiunoni.
Ashura alikaukia kucheka kiasi cha kushika mbavu zake kutokana na maumivu aliyo yapata kwa kucheka kwake.
“Zawadi shoga yangu kumbe bado hujakua wewe!” Ashura alizungumza huku akiendelea kucheka.
“Nimefurahi sana kuona shoga yangu unauaga umasikini”
“Jamani Zawadi asante kumbe unanipenda hivyo?”
“Alaaa! kwanini uteseke wakati najua jinsi ya kukusaidia? Haya nifuate nikuelekeze kazi mama” alizungumza Zawadi huku akipiga hatua kuondoka pale sebleni.
Waliingia kwenye chumba kimoja kilichokuwa na ukubwa wa wastani. Ndani ya chumba kile hapakuwepo na kitu kingine zaidi ya meza moja tu katikati iliyokuwa na ukubwa wa wastani. Juu ya meza ile iliyokuwa imetandikwa kwa kitambaa kisafi cheupe palikuwa na vitabu viwili. Walivua viatu na kuingia peku.
Mazingira ya chumbani mle yalimtatanisha sana Ashura. Alichokuwa anakifahamu yeye kazi ile ilikuwa ikifanyika jikoni. Sasa akashangaa analetwa kwenye chumba kilichokuwa kisafi kupita maelezo.
“Tunapikia humu hivyo vitumbua?” alihoji Ash ura baada ya kuona mambo hayaelewiki.
“Kuwa mpole shost, simama hapo geukia kule mbele” Zawadi alitoa maelekezo.
Ashura alifanya kama ambavyo mwenyeji wake alivyokuwa akimuamuru.
“Ok, unaona nini hapo mezani?” Alihoji Zawadi kwa umakini mkubwa.
“Vitabu” Ashura akajibu kwa ufupi.
“Unavifahamu?”
“Ndiyo, ni Biblia na Msahafu” Ashura alijibu baada ya kuviangalia vitabu vile kwa makini.
“Wewe unaamini katika kitabu gani kati ya hivyo?” Zawadi alihoji.
“Mimi ni muislamu, unadhani nitaamini kitabu gani?” Ashura alitoa jibu kwa kuuliza swali.
“Haya kichukue” alisema Zawadi.
Ashura alishituka kidogo baada ya kupewa yale maelekezo na rafiki yake yule. Akatulia na kukiangalia kitabu kile kwa kitambo kisha akamgeukia Zawadi na kumtazama kwa makini.
“Vipi mbona unasita? Chuku kitabu cha Quran hicho nikwambie cha kufanya” Zawadi akazungumza kwa msisitizo.
“Siwezi” Ashura aligoma kufanya vile alivyoagizwa na zawadi.
Jibu lile halikumridhia kabisa Zawadi. Hakutegemea kama angekumbana nalo kutoka mdomoni mwa Ashura. Akahisi kupandwa na ghadhabu dhidi ya tabia na mienendo ya rafiki yake yule.
Zawadi alikunja uso kwa hasira baada ya kusikia Ashura amegoma kugusa kile kitabu cha Quraan tukufu.
“Kwanini huwezi kukigusa?” Zawadi alihoji huku amekunja sura.
“Sipo tohara.” Ashura akajibu kwa upole.
Kauli ile ya Ashura kwamba hakuwa tohara ilimfariji Zawadi kwa kiasi fulani. Wasiwasi na hofu dhidi ya uamuzi wa Ashura vikapungua.
“Unaweza kujitoharisha, au unakikwazo?” Zawadi alihoji kwa umakini mkuwa.
“Sina kikwazo chochote naweza kujitoharisha”
“Ok njoo huku” Zawadi alizungumza na kutoka mle chumbani.
Waliingia chumba cha jirani ambacho kilikuwa na mabomba mengi ya maji. Ashura alipoyaona hakujiuliza afanye nini kwasababu alikuwa anafahamu wajibu wake. Alijitoharisha kisha wote wawili wakarejea kwenye kile chumba kilichokuwa na vitabu. Ashura alikichukua kile kitabu cha Quraan na kukishika kwa unyenyekevu.
“Kishike kwa mkono wa kulia na ukiinue juu” Zawadi aliagiza.
Ashura akafanya kama alivyoagizwa na shoga yake huku akiwa haelewi kilichokuwa kinataka kuendelea pale.
“Fuatisha maneno haya nisemayo” Zawadi aliagiza.
“Sawa” Ashura ilimbidi akubali tu ingawa hadi kufikia wakati ule alikuwa amekwisha poteza matumaini ya kufanya shughuli ile ya kuuza vitumbua kutokana na mfumo wake kuwa mrefu.
Hivyo vitumbua vya kupika kwa kutumia vitabu vya dini ni vitumbua vya aina gani? Akajipa moyo na kufuata maelekezo aliyokuwa anapewa na yule mwalimu wake wa kmfundisa mapisi ya kitumbua ca kihindi.
“Sema Emwenyezi mungu” Zawadi alizungumza.
“Ee Mwenyezi Mungu” Asura akafuatia.
“Mimi Ashura Machaku”
“Mimi Ashura Machaku” Ashura akamfuatisha.
“Nikiwa na akili yangu timamu, naapa kwamba nimeingia katika biashara hii kwa hiyari yangu mwenyewe, pasipo kulazimishwa wala kushurutishwa na mtu. Nitatenda yale yote ambayo kazi hii itanitaka kutenda pasipo ubishi wala kusita. Naahidi kuwa nitatunza siri zote za kazi hii. Nitakuwa tayari hata kutoa uhai wangu ili kutunza siri hii. Ee Mwenyezi mungu nisaidie” Ashura alifuatisha maneno yote hayo kama ambavyo Zawadi alimtaka kufanya na mwisho alirejesha mezani kile kitabu cha Quraan.
“Sasa shost utajiri ni wako” alisema Zawadi huku akitabasamu.
“Lakini shoga biashara yenyewe ndiyo ina mlolongo mrefu hivi?” Ashura akahoji kwa mashaka.
“Ah si unajua tena kila kazi ina kanuni na taratibu zake”
“Na hizi ni kanuni za kupika hivyo vitumbua?” alihoji Ashura kwa umakini.
“Sio vitumbua bali sema Vitumbua vya kihindi” Zawadi alimsahihisha Ashura.
“Sio vitumbua vya kihindi, bali sema Kitumbua cha kihindi” Ashura naye akamsahihisha Zawadi.
“Woow! umekwishaiva, sasa twende zetu huku” Alisema Zawadi na kutoka mle chumbani. Waliingia kwenye kile chumba kilichokuwa na mabomba mengi ya maji.
“Vipi tunajitoharisha tena?” Ashura alihoji baada ya kuona anarudishwa tena chumbani mle.
“Hapana” Zawadi alijibu huku akisogea pale kwenye bomba ambalo alilitumia Ashura kujitoharishia. Alilikamata bomba lile na kulivuta kwanguvu huku Ashura akiwa amesimama pembeni akimtazama. Shughuli ile iliendelea kwa sekunde kadhaa na mwisho pale kwenye lile bomba pakafunguka kama vile mlango pakawa pana pango.
“Heee!” Ashura alihamaki baada ya kuona tukio lele.
“Twende zetu” Zawadi alizungumza kisha akajichomeka kwenye lile pango lililofunguka.
Moyo wa Ashura ulisita kuingia kwenye pango lile ambalo ndani kulikuwa hakuonekani kitu kutokana na kiza kinene kilichokuwa kimetanda. Zawadi akiwa ndani ya lile pango aligeuka na kumchungulia Ashura ambaye alikuwa bado amesimama pale nje.
INAENDELEA



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa