JE HAYA NI MAPENZI!! 76: - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Wednesday, February 19, 2020

JE HAYA NI MAPENZI!! 76:



Muda huo huo simu ya Sabrina ikaanza kuita,
akamsikia Sam akisema kwa ukari
"Pokea hiyo simu Sabrina na uweke loudspeaker"
Sabrina alipoiangalia ile simu akaona ni namba ya
nchi za nje, moja kwa moja akapatwa na hisia kuwa
mpigaji atakuwa ni Jeff na kumfanya atetemeke
zaidi.
Sabrina akiwa ametawaliwa na uoga, akashtuliwa tena na sauti kali ya Sam,
"Pokea hiyo simu Sabrina, ole wako ikatike"
Sabrina aliipokea ile simu huku akitetemeka sana na kuiweka sauti kubwa kama alivyoamriwa na Sam.
Moja kwa moja upande wa pili ukaanza kuongea,
"Shikamoo Mamdogo"
Sabrina hakuamini masikio yake kuwa ni Jeff kamsalimia hivyo na kujikuta akijibu kwa kutetemeka,
"Marahaba"
"Kheee mamdogo kimya kabisa tangu nimeondoka, huwa nawasiliana na bamdogo tu. Unaendeleaje lakini?"
"Naendelea vizuri"
"Vipi mdogo wangu Cherry hajambo? Nimekakumbuka sana hako katoto"
"Hajambo"
"Mbona unanijibu kwa mkato hivyo mamdogo? Una matatizo gani au unaumwa?"
"Hapana siumwi"
"Sasa mbona unaongea kwa kupooza kiasi hicho? Utakuwa unaumwa wewe, ngoja nitampigia simu bamdogo nimuulize. Mi nilikuwa nakusalimia tu, wasalimie wote hapo"
"Haya"
Kisha ile simu ikakatika, Sabrina bado hakuamini   kama aliyekuwa akiongea nae kwa muda huo alikuwa ni Jeff kweli, bado alikuwa kaduwaa kuwa imekuwaje Jeff akaongea kistaarabu kiasi kile.
Akamuona Sam akishusha ile bastora yake na muda kidogo simu ya Sam nayo iliita, naye aliipokea kwa kuweka sauti kubwa, mpigaji alikuwa ni Jeff yule yule.
"Shikamoo bamdogo"
"Marahaba, hujambo"
"Sijambo, muda mfupi uliopita nimeongea na mamdogo anaonekana kupooza sana sijui anaumwa?"
"Aah usijali, nipo nae hapa"
"Sawa basi mi nilikuwa nawasalimia tu"
Kisha akaagana nae na kukata simu.
Sam akamuangalia Sabrina kisha bila ya kusema chochote akaenda chumbani.

Mama wa Sabrina akamkaribisha mumewe ndani, na kumfanya ashangae ule ujio wa James pale.
Kitu pekee alichokijua Deo kuhusu James ni kuwa baba mzazi wa mkwe wao Joy ila alisahau kabisa kama huyu James ndiye aliyekuwa mwalimu wa kwaya wa mke wake.
Kwahiyo alipomuona hapo hakushangaa sana na kujua kuwa amepita kusalimia  ukizingatia wameshaweka kama undugu kwa watoto wao kuoana.
Deo akamsalimia James pale na kumkaribisha bila kujua jambo lililompeleka James pale nyumbani kwake.
Mama wa Sabrina alijifanya kwenda jikoni kumuandalia mumewe na kumfanya James aage na kuondoka zake.

Sabrina hakuamini kama amepona kweli, pia hakujua kwanini Sam alimnyooshea bastora,
"Inamaana leo ndio ingekuwa mwisho wangu, maisha gani haya ya kuishi roho juu juu kiasi hiki?"
Alikuwa pale pale akisikitika.
Muda kidogo Sam alitoka chumbani huku akiwa amembeba yule mtoto wao mdogo Cherry na kufika nae sebleni kisha kukaa nae karibu na Sabrina, na kuanza kusema,
"Nampenda sana huyu mtoto, siku zote mshukuru huyu mtoto Sabrina kwani huyu mtoto ndiye aliyeokoa maisha yako. Ulipata mimba kwa kubakwa ndio, hilo sijakataa wala kupinga. Ila swali linaloisumbua akili yangu kwasasa ni kuwa hiyo mimba nyingine uliyonayo ni ya nani? Najua hapo hukubakwa na baba wa mtoto unamjua vilivyo, nataka kujua ni nani huyo?"
Kisha akainua kichwa chake na kumtazama Sabrina ambaye aliinamisha kichwa chini tu, na kumfanya Sam aendelee kuongea,
"Najua hili swali huwa ni gumu sana kwako, tafadhari Sabrina. Nahitaji kujua mwenye hiyo mimba, nakupa siku mbili uniambie muhusika wa hiyo mimba"
Sabrina alikuwa akitetemeka kwa aibu tu wakati akiambiwa maneno hayo na mumewe.
Walitulia pale mpaka muda wa kulala ulipofika na kulala.

Kulipokucha kama kawaida, Sam aliondoka na kwenda kazini ila Sabrina alifungiwa ndani kama alivyofanyiwa jana yake.
Njiani Sam alikuwa akiwaza tu, kwani mwanzoni alikuwa na hisia za uhakika kabisa kama muhusika ni Jeff lakini jana ile simu ya Jeff ilimshangaza kwani aliamini kuwa lazima wangeongelea mambo ya kimapenzi ambayo yangempa hasira zaidi Sam na kumfanya atende kile alichokitarajia.
Lakini kilichomshangaza ni yale mazungumzo yao yaliyoonyesha kuwa Jeff hana hatia hata kidogo kwani alikuwa akimuheshimu sana Sabrina.
Sam hakupata jibu na kumfanya ajipe matumaini ya kuendelea kuchunguza huku akijilaumu kwa kile kitendo chake cha kumnyooshea bastora Sabrina.
"Nampenda sana, ningewezaje kumuua? Sabrina ana sura ya upole, siku zote anaonekana kuwa hana hatia ingawa anafanya makosa, nawezaje kummaliza Sabrina? Nawezaje kummaliza mtoto mdogo malaika wa Mungu asiye na hatia Cherry? Ooh Mungu nisaidie nisije rudia tena kile kitendo na kujiku......."
Akashtuka gafla na kufunga breki mbele ya mtu yani ilikuwa bado kidogo tu amgonge, alishuka upesi kwenda kumuomba msamaha ambapo alimkuta kajawa na hasira na uoga wa kugongwa.
Kumuangalia vizuri alikuwa ni yule yule Neema, wakati huo Neema nae alishangaa kumuona kuwa ni Sam.
"Kumbe ni wewe Sam ulitaka kuniua tena?"
"Tafadhari nisamehe Neema, yani hata sijui nina matatizo gani"
Ikabidi watoke pale na kuingia kwenye gari ya Sam na kuacha watu walioanza kukusanyika katika eneo lile.

Sam hakwenda moja kwa moja ofisini bali alipita kwenye baa ya karibu ili kupata supu na Neema.
Walifika na kukaa na kuagiza,
"Nisamehe bure Neema, kwakweli hata sijui kuna nini kati yetu maana si jambo la kawaida hili"
"Na kweli si jambo la kawaida maana ni mara ya pili hii unataka kunigonga. Mi nahisi kuwa kuna kitu kipo kati yetu"
"Inawezekana, ila nisamehe sana"
Wakanywa supu pale, kisha wakainuka ili Sam ampeleke Neema alipokuwa anaelekea na yeye kwenda ofisini kwake.

Sabrina nyumbani bado alikuwa na mawazo ya kutosha kabisa, na kikubwa alijiuliza kuhusu Jeff hakuamini kabisa kama Jeff ndiye aliyeongea nae jana.
Moja kwa moja akachukua simu yake na kuingia kwenye mtandao wa facebook kuangalia kuwa Jeff atatoa hoja gani.
Na alipoingia tu akashtuliwa na ujumbe toka kwa Jeff ambaye humo alijiita Prince J.
"Hellow, jana usiku   nimeota. Huwezi amini mamy ila nimekuota kuwa tupo pamoja tukifurahia mapenzi yetu"
Sabrina akaamua kumuuliza Jeff,
"Hivi ni wewe kweli uliyenipigia simu jana mchana?"
"Wow, upo hewani mamy. Ni mimi ndio kwani kuna tatizo gani?"
"Nimekushangaa, mbona jana umeongea kwa ustaarabu sana?"
"Nilikumiss sana, muda kidogo kuna roho ikaniambia nikupigie simu. Ulipopokea nikahisi kama kuma mtu anasikiliza maongezi yetu ndiomana nikaongea vile. Kiukweli mimi nakupenda sana, na kuna kitu muhimu sana kati yetu ingawa wewe hutaki kukubali wala kuamini hilo"
Sabrina alisoma meseji hii mara mbili mbili na kuhisi kuwa huenda kuna kitu kweli kati yake yeye na Jeff, kisha akamuaga ila kabla hajafunga ukaingia ujumbe wa mwisho kutoka kwa Prince J naye akimuaga pia,
"Nakupenda sana, milele nitaendelea kukupenda haijalishi kitu mimi nitakupenda siku zote"
Sabrina alifunga simu yake na kujifikiria, hii ndio aina ya upendo alioutaka yeye kwani siku zote upendo wa Sam juu yake hakuuelewa kabisa kwahiyo alihitaji huu upendo anaouhisi upo kwa Jeff tu.

Sakina sasa akaamua kufunga safari na kwenda tena kwa yule mtaalamu wake ili kujua mambo yake yameishia wapi.
Alimkuta na kuanza kumuulizia,
"Nimekuja kukushukuru mtaalamu na pia unisaidie mkwe wangu arudi nyumbani"
"Usijali, mkweo lazima arudi hata usiwe na wasiwasi. Tena atarudi siku sio nyingi"
"Sawa nashukuru baba, vipi kuhusu swala la yule mdogo wangu?"
"Yule mdogo wako namsaidia sana, mwambie aje nimtengeneze. Namuhurumia sana, amezungukwa na watu wabaya, jitahidi uje nae nimsaidie kwa karibu zaidi."
"Sawa nitakuja nae hakuna tatizo hata usijali"
Yule mtaalamu akampatia Sakina dawa zingine za kuweka ndani ya nyumba yake ili azidi kuwa salama.
Kisha Sakina akaondoka zake.

Sakina akiwa njiani akashangaa gari ikisimama mbele yake na dereva kushuka, alikuwa ni Sam na kumfanya asimame na kuanza kusalimiana nae.
"Panda kwenye gari nikupeleke shemeji"
Sakina hakusita na kupanda kwenye gari ya Sam kisha safari ya kwenda nyumbani kwake.
"Hivi umeongea na Jeff shemeji? Anakusalimia sana"
"Ni jana tu hapo katoka kunipigia simu, huwa nafurahi sana shemeji"
"Vipi umemfatilia na mkwe wako Dorry?"
"Ndio niliongea nae akasema atakuja"
"Usijari, mi nitamfata na kumleta. Unatakiwa kumpenda sana yule binti, mtu kaamua kubeba mimba ya kijana wako bila tatizo unatakiwa kumpenda sana"
"Hata hivyo nampenda sana, yani hapa natamani huyo mjukuu wangu azaliwe leo kesho jamani. Natamani sana kubeba damu ya mwanangu kwenye mikono yangu"
Wakaongea mengi hadi walipofika nyumbani kwa Sakina ambapo Sakina alishuka na kumuaga Sam.
Wakati Sam anaondoka aliamua kumpigia simu Dorry na kumsihi kuwa arudi kwavile mambo yote yapo sawa.
"Huku hakuna tatizo Dorry, jitahidi tu urudi ili mtoto wako alelewe huku"
"Sawa nimekuelewa"
Kisha akakata ile simu.

Dorry alizidi kumshangaa Sam kwani ukweli wote aliujua ila bado alimsisitiza kuwa arudi kwakina Jeff ili mtoto wake akalelewe kule,
"Lazima Sam atakuwa na mipango binafsi tu, maana sio kitu rahisi eti yeye afurahie tu kuona mtu analea mimba isiyo muhusu"
Alifikiria sana lakini aliona ni jambo jema katika kumsaidia yeye malezi ya mimba na mtoto.

Deo akiwa ametulia pale nyumbani kwake na kumuuliza mke wake kuhusu watoto wao.
"Vipi huyu Sabrina hajui kama nimekuja nini? Maana naona leo siku inapita bila ya yeye kuja kuniona. Maana katika wanangu wote huyu ndio kiboko yao kwa kunipenda"
"Nilimpigia simu jana ila hakupokea, nimemtumia na ujumbe lakini hajajibu natumaini atakuja tu hata usiwe na wasiwasi"
"Wasiwasi lazima, nimewakumbuka wanangu. Wajukuu na kila kitu"
Kisha akafikiria kidogo na kuuliza,
"Na yule mkwe wetu jana alifata nini?"
"Alipita kusalimia tu"
"Mbona akaondoka aliponiona?"
Mama wa Sabrina aliamua kubadilisha mada, kwani alijua kitakachoendelea hakitakuwa sawa kabisa.

Sabrina alitulia akingoja muda ufike na Sam arejee,
"Sijui leo kutakuwa na tukio gani jipya"
Akatazama tumbo lake na kusema,
"Eeh mimba wee, siku nitakapokuzaa nitapumua kwakweli maana sina raha kabisa. Najutia yote niliyoyatenda nyuma"
Sam nae akawa amewasili na kumkuta Sabrina akiongea peke yake pale.
Alimuuliza swali moja tu,
"Umekula?"
"Ndio nimekula"
"Basi vizuri"
Kisha Sam akaenda zake chumbani na kulala.

Sabrina alibakia pale pale sebleni peke yake kwani muda huo hata mtoto wao naye alikuwa ameshalala.
Sabrina akajikuta akipitiwa na usingizi pale kwenye kochi.
Wakati amelala, akajiwa na njozi.
Akajiona anaolewa tena, kumuangalia mwanaume anayemuoa alikuwa ni Jeff tena sura yake ikiwa imejawa na furaha sana.
Sabrina nae alikuwa amejawa na furaha, Jeff akamsogelea na kumwambia.
"Siamini kama leo nakuoa mwanamke wa maisha yangu"
Sabrina akatabasamu, Jeff akamsogelea ili ambusu Sabrina mdomoni mara akatokea Sam karibu yao.
Hapo hapo Sabrina akashtuka na kujiona kuwa bado yupo sebleni.

Sam akiwa amelala, akashtuliwa na mlio wa simu yao.
Kuangalia mpigaji kwa usiku ule alikuwa ni Neema.
Sam hakutaka kupokea ile simu na kuicha iendelee kuita tu.
Alitazama mule chumbani bila kumuona Sabrina, aliamua ainuke ili aende sebleni kumfata.

Sabrina pale sebleni baada ya ile ndoto, akajikuta akikaa na kuchukua simu yake moja kwa moja na kuingia kwenye mtandao wa kijamii ili kumwambia Jeff kuhusu alichoota.
Alipoingia tu akakutana na ujumbe toka kwa Prince J ukionyesha umetumwa muda sio mrefu,
"Yani huwezi amini mamy, nimetoka kukuota muda sio mrefu eti tunaoana"
Sabrina akashangaa kuwa inakuwaje ameota ndoto moja na Jeff.
Kabla hajajibu chochote, akashangaa kumuona Sam mbele yake
"Nipe hiyo simu Sabrina, tena usibonyeze chochote"
Sabrina aliona sasa mwisho wa ujanja wake umefika.

Itaendelea

JE HAYA NI MAPENZI!! 77:

Sabrina akashangaa kuwa inakuwaje ameota ndoto
moja na Jeff.
Kabla hajajibu chochote, akashangaa kumuona Sam
mbele yake
"Nipe hiyo simu Sabrina, tena usibonyeze chochote"
Sabrina aliona sasa mwisho wa ujanja wake
umefika.
Mwili wote ulimuisha nguvu Sabrina ukizingatia pale alikuwa akiwasiliana na Jeff kwa njia ya meseji, na ubaya zaidi yalikuwa ni maneno ya kimapenzi.
Kilichomuumiza kichwa zaidi ni ile picha ambayo alitumiwa na Jeff wakiwa wote kitandani kuwa Sam akiiona je itakuwaje.
Sabrina akataka kumpa simu Sam ili liwalo na liwe, ila nafsi yake nyingine ikamshauri kitu na kumwambia kuwa asikubali kushindwa kirahisi namna ile.
Alichokifanya Sabrina ni kuibamiza chini ile simu kisha na yeye kuanguka.
Sam alimuangalia Sabrina na kutikisa kichwa, akataka kumfata pale chini ila akasita na kuamua kumuacha pale pale na kurudi chumbani.

Sam alikaa chumbani na kusikitika sana, kama kawaida yake akaanza kumuweka Sabrina kwenye kundi la wanawake wasiokuwa na akili.
Aliona wazi kuwa alikosea sana kumuoa Sabrina,
"Ni kheri nisingemuoa tu, mambo gani haya ya kuishi na mwanamke asiyekuwa na akili? Mwanamke gani huyu wa kubwaga simu na kujifanyisha kuzimia ili nisimseme kwa makosa yake? Ni wazi alikuwa akiwasiliana na mwanaume, sijui cha kufanya kwa huyu kiumbe kwakweli"
Sam aliwaza sana na kujilaza pembezoni mwa kitanda kwani akili yake ilishavurugika kwa wakati huo.

Kulipokucha kama kawaida, aliinuka na kwenda kuoga bila ya kujali kuhusu Sabrina.
Alimaliza na kuvaa, ila alipoangalia kitandani akagundua kuwa Sabrina bado yupo sebleni, akatikisa kichwa chake na kumfanya azidi kumpunguza akili Sabrina.
Alipomaliza kuvaa akamuona mtoto wao kitandani akiwa ameamka huku akicheza cheza, akaamua kutoka mule chumbani ili akamshtue Sabrina kuwa mtoto alishaamka tayari.
Ila kufika sebleni akashangaa kumuona Sabrina akiwa pale pale chini, akatikisa kichwa,
"Hivi huyu mwanamke ana akili kweli?"
Akamsogelea na kumpiga teke kumuonyesha kwamba hataki ujinga kwa wakati huo.
Ila ile teke lilifanya kama kumsogeza Sabrina kidogo.
Sam akashangaa na kushtuka baada ya kuona damu pale ambapo kililala kichwa cha Sabrina na kumfanya ainame haraka kumchunguza.
Ni kweli kwenye sura ya Sabrina kulijaa damu na ilionekana ikimtoka mdomoni.
Sam hofu ikamjaa na huruma pia, aliamua kumbeba Sabrina juu juu na kutoka naye nje hadi kwenye gari yake huku akimuamuru mlinzi wao afungue geti kwa haraka.
Geti lilifunguliwa kwa haraka sana, kisha Sam akaondoa gari kwa kasi na kusahau kuwa kuna mtoto wamemuacha ndani ya nyumba yao.

Safari ilikuwa moja kwa moja hadi hospitali ambapo Sabrina alikuja kuchukuliwa upesi kama mgonjwa mahututi na kupelekwa moja kwa moja kwenye chumba cha daktari kwa matibabu.
Sam alitulia nje akingoja majibu huku akijikuta kuongea peke yake, daktari alimuita ili kumuhoji kidogo kuhusu kilichompata mkewe.
"Kwani imekuwaje Mr. Sam?"
"Kwakweli daktari sielewi, sijui kama alianguka au ilikuwaje"
"Wewe niambie tu unavyo  elewa wewe"
"Ninachokumbuka ni kuwa, mimi nilienda kulala na kumuacha mke wangu sebleni. Nilipoamka asubuhi sikumuona chumbani na kuamua kwenda kumuangalia sebleni. Ndio hivyo nikamkuta yupo chini na damu zimetapakaa"
Daktari akasikitika kwa kutingisha kichwa kisha akamwambia Sam,
"Pole sana Bwana Sam"
Sam akashtuka na kuuliza kwa tahamaki,
"Vipi tena, mke wangu amekufa?"
Daktari alimuona Sam akinyong'onyea kabisa na gafla akaanguka na kupoteza fahamu.
Daktari akawa na kazi mbili sasa ya kumshughulikia Sabrina na kumshughulikia Sam.

Sakina akiwa nyumbani kwake, alijikuta akitaka kwenda nyumbani kwa Sabrina ili kumshauri zaidi kuhusu swala la kwenda kwa mtaalamu.
Akajaribu kuipiga simu yake ila haikupatikana,
"Atakuwa kwake tu, naenda hivyo hivyo"
Sakina akajiandaa na kuanza safari ya kwenda nyumbani kwa Sabrina.

Sakina alifika na kumkuta yule mlinzi akiwa getini kama kawaida,
"Sabrina yupo ndani?"
"Sijui, inawezekana yupo"
"Yani hujui kama yupo au hayupo? Kheee mnaishije humu?"
"Tunaishi kawaida tu, ila mzee asubuhi aliondoka kwa kasi sana, nadhani alikuwa akiwahi ofisini. Mama atakuwepo tu ndani"
Sakina akaingia na kuanza kuifata nyumba ilipo, kadri alivyozidi kusogea akasikia sauti ya mtoto inayoonekana alilia sana na inaelekea kukauka.
Sakina akashangaa kuwa iweje Sabrina amuache mtoto alie kiasi kile.
Alipofika mlangoni akagonga ila mlango haukufunguliwa na kujaribu kuita ila hakuitikiwa.
Akajaribu kufungua mlango na kuona ukifunguka hata kushangaa kuwa kumbe mlango ulikuwa wazi.
Alitembea hadi sebleni na kuona zile damu pale chini, akashtuka na kushangaa.
Aliposikilizia sauti ya mtoto akagundua kuwa ile sauti inatokea chumbani.
Akasogea na kugonga kisha kuita ila hakuitikiwa na kumfanya ajipe ujasiri wa kufungua mlango na kuingia.
Alimuona mtoto kitandani akionekana kulia sana hadi kuanza kukaukiwa na sauti.
Alimchukua na kumbeba mgongoni ila bado hakuelewa kilichotokea, aliamua kutoka na mtoto tu ili kwenda nae nyumbani kwake.

Wakati anatoka getini, mlinzi hata hakuwa na habari yoyote ila Sakina nae alitoka bila hata ya kumuaga wala kumuuliza chochote na kuondoka zake.
Alifika kwake na kumtafutia maziwa kwanza mtoto yule kisha kumnyeshwa ambapo alikunywa na kulala kisha Sakina akaanza kumkorogea uji.
Alijikuta akijiuliza maswali bila ya majibu,
"Kweli utajiri hauna maana, mlinzi kama yule anafaida gani ndani? Mlinzi asiyejua kama bosi wake yupo au hayupo? Na huyu Sabrina kapatwa na nini? Simu yake haipatikani wala mumewe hapokei simu. Hawa watu wanajielewa kweli? Unamuachaje mtoto mdogo kama huyu ndani peke yake?"
Alisikitika sana huku akiendelea kukoroga ule uji ili akishtuka ampe kisha aende kwa mama wa Sabrina kumuhabarisha.

Mama wa Sabrina na mumewe wakiwa nyumbani bila wasiwasi wowote wala taarifa yoyote.
Alishangaa kupigiwa simu na kuambiwa kuhusu hali ya mtoto wao na mkwe wao.
Ile simu iliwafanya waondoke pale nyumbani kwa haraka kuelekea hospitali.

Walifika hospitali na kukuta Sam ameshazinduka kwa muda huo kwa huduma aliyopewa, ila hawakutaka kumsumbua kwanza kwa kumuuliza maswali kwahiyo wakaacha apumzike kidogo.
Wakamuuliza daktari kuhusu mtoto,
"Mmh hawajaja na mtoto hapa"
Wakajiuliza kwa haraka haraka kuwa mtoto atakuwa wapi na jibu lao likawaelekeza kuwa lazima ameachwa nyumbani,
"Maskini mjukuu wangu ameachwa peke yake"
Ikabidi wajihimu ili kwenda kumuangalia mtoto.

Walifika kwa nyumbani kwa Sam, kama kawaida mlinzi aliwafungulia mlango na moja kwa moja wakaingia ndani tena bila ya kumuuliza chochote kile.
Ila ndani hawakukuta mtoto na kufanya watoke na kwenda kumuuliza mlinzi,
"Eti mtoto yuko wapi?"
"Mtoto! Si yupo na mama yake"
"Hivi akili yako ni nzima kweli? Unajua mama yake alipo"
"Si yupo ndani"
Ikabidi wamueleweshe kuwa yupo hospitali ila mlinzi alikuwa akishangaa tu,
"Sio unashangaa, mtoto yuko wapi?"
"Nimekumbuka, atakuwa ameondoka na yule dada wa mama mwenye nyumba"
"Dada wa mama mwenye nyumba? Yupi huyo, kwani kulikuwa na msichana wa kazi humu?"
"Hapana, ila aliyekuja kumchukua ni yule dada kabisa wa mama"
"Kivipi mbona hueleweki?"
"Namaanisha dada wa Sabrina, yule dada yake kabisa"
"Sabrina ana dada? Dada yupi? Tuna mtoto mmoja tu wa kike huyo dada ni dada yupi? Anaitwa nani?"
"Jina lake limenitoka ila linafanana na jina la mama humu"
Wakafikiria kwa haraka haraka na kuhisi kuwa huyo mtu lazima atakuwa Sakina tu kisha wakaondoka mahali pale.

Sakina alipompa yule mtoto uji, alijikuta akimuangalia sana hata hisia zake zikampeleka mbali.
Akakumbuka kipindi Jeff alivyokuwa mdogo, alivyokuwa akimlisha, anavyofanya. Alijikuta akiguna tu,
"Mmh ila huyu mtoto kafanana na mwanangu jamani, yani kila kitu kama mwanangu Jeff kasoro tu huyu ni wa kike ila kafanana sana na mwanangu"
Alikuwa akimuangalia sana na kuona kamavile amembeba Jeff mdogo,
"Sijui Dorry akijifungua mtoto atafanana na mwanangu kama hivi! Mmh duniani wawili wawili ila kwanini mtoto wa Sabrina ndio afanane kiasi hiki na mwanangu Jeff?"
Alijiuliza sana ila mwisho wa siku aliamua kukubaliana tu na hali halisi kuwa mtoto yule ni wa Sam na Sabrina.
Wakati akifikiria hayo, walifika wazazi wa Sabrina na kumkuta Sakina akimpa uji yule mtoto.
Wakashukuru sana pale na kuamua kumuaga Sakina kwani waliamini kuwa sasa mtoto yupo kwenye mikono salama.
"Yani nilijaribu kuwapigia lakini simu iliita tu bila ya kupokelewa"
"Kuchanganyikiwa mwanangu yani simu tumeacha nyumbani"
Basi Sakina akawaaga pale ili waweze kuwahi kumuona Sabrina.
Wakati wanatoka, wakapishana na Dorry ambaye alikuwa anaingia nyumbani kwa Sakina, akawasalimia pale kisha na wao kuondoka.

Dorry alitulia kidogo na kumsalimia Sakina ambapo alifurahi sana kumuona.
Ila alimshangaa yule mtoto,
"Mtoto wa nani huyo mama?"
"Mtoto wa mdogo wangu huyu, mzuri eeh!"
"Ndio ni mzuri, kafanana na Jeff huyo balaa"
Sakina akamuangalia yule mtoto tena na kutabasamu.
"Ni kweli kafanana na Jeff hata mi nimeliona hilo mwanangu."
"Kwani Jeff kafanana na nani kwenye ukoo wenu? Maana damu yake itakuwa kali sana kumfananisha ndugu yake namna hii"
Sakina akaguna kidogo na kusema,
"Natumaini hata huyo mjukuu wangu atafanana nae kwa vizuri sana maana damu ya mwanangu ni kali kwakweli"
Dorry akaitikia kwa kutikisa kichwa na kumfanya Sakina amuangalie kwa jicho la wasiwasi kidogo kisha kuendelea na mambo mengine.

Hali ya Sabrina haikuwa nzuri sana, na wote walikuwa wakingoja majibu ya daktari kuhusu hali yake.
Daktari hakuwaambia moja kwa moja na kufanya wazidi  kusubiri.
Kwavile Sam alikuwa tayari anajitambua, wazazi wa Sabrina waliamua kutumia nafasi hiyo kumuuliza kilichotokea ila aliwajibu kama ambavyo alimjibu daktari alipoulizwa kuhusu swala hilo.
"Sasa sijui tatizo ni nini hapo. Haya mambo ni makubwa sana"
Wakapeana moyo na kuendelea kusikilizia hali ya Sabrina.

Sakina akiwa pale nyumbani na Dorry muda kidogo akapigiwa simu na mtoto wake na kumfanya afurahi sana,
"Tena leo nipo na Dorry hapa"
"Aah sawa ila hana umuhimu kwangu"
"Hana umuhimu kivipi wakati ana mzigo wako!"
"Mzigo wangu? Mzigo gani?"
Sakina akapewa ishara na Dorry kuwa asiseme chochote, alibadilisha mada ila hakuelewa kwanini amemzuia kusema,
"Mbona umekaa kimya mama? Achana na Dorry huyo hanihusu. Ila naomba nikuulize, mbona mamdogo Sabrina hapatikani?"
Sakina aliamua kumueleza Jeff hali halisi ilivyo na kuhusu mtoto wa Sabrina kuwa yupo nae pale.
"Maskini mamdogo jamani, ndiomana jana moyo uliniuma sana. Tafadhari mama kaa vizuri na huyo mtoto Cherry"
"Usijali mwanangu"
Kisha simu ikakatika, Sakina aliamua kumuuliza Dorry kuwa kwanini hataki Jeff aambiwe ukweli kuwa ana mimba yake,
"Mama, nataka kumfanyia Jeff surprise. Nataka siku akirudi twende uwanja wa ndege na mwanae kumpokea"
Sakina akatabasamu na kuona kuwa Dorry yupo sahihi.

Shangazi wa Sabrina naye aliitumia siku hii kwa kumuita James ambaye ni kaka wa Sabrina kwa lengo la kumkomesha wifi yake.
"James, unaniamini mimi?"
"Ndio nakuamini shangazi"
"Basi kwa ufupi tu, mimi ni shangazi yako jina yani sio kwa damu. Na yule baba yako nae ndio hivyo hivyo"
"Sikuelewi shangazi! Unamaana gani?"
"Deo sio baba yako mzazi"
James alijikuta akishtuka sana na kujishika kifuani na muda huo huo akaanguka chini.

Wazazi wa Sabrina wakiwa pale hospitali, daktari aliwaita pamoja na Sam ili kuwaambia hali ya Sabrina ilivyo.
"Jamani, nina habari mbaya kidogo ya kuhusu Sabrina"
Wote wakashtuka kusikia habari mbaya.

Itaendelea

JE HAYA NI MAPENZI!! 78:

Wazazi wa Sabrina wakiwa pale hospitali, daktari
aliwaita pamoja na Sam ili kuwaambia hali ya
Sabrina ilivyo.
"Jamani, nina habari mbaya kidogo ya kuhusu
Sabrina"
Wote wakashtuka kusikia habari mbaya.
Mama wa Sabrina akamkazia daktari macho kamavile anamtishia kama akitoa habari mbaya.
Daktari akapumua kidogo na kumuangalia mama wa Sabrina kisha akasema,
"Sio mbaya sana jamani ndiomana nimesema kidogo. Msiniangalie kwa macho makali kiasi hicho"
"Basi tuambie daktari"
"Kwasasa Sabrina ameamka, ni jambo la kumshukuru Mungu ila tatizo ni kuwa amepoteza kumbukumbu yani kwakifupi hajui chochote kuhusu yeye wala nani"
Wote wakapumua kidogo, kisha Sam akauliza,
"Kwani kwa uchunguzi wako daktari umegundua kuwa tatizo ni nini?"
"Inaonekana alivyoanguka aliumia maeneo ya kichwani ndiomana kumbukumbu zimepotea. Kwahiyo mtakapoingia kumuona mchukulieni kama alivyo na mjitahidi kumuelekeza yale ya msingi ili iwe rahisi kwa yeye kurudisha kumbukumbu zake."
Wakakubaliana pale na daktari kisha akawapeleka kwenda kumuona Sabrina.
Na kweli walimkuta akiwashangaa tu, kwavile na giza nalo liliingia wakaamua wamuache apumzike kwanza.
Wakaongea na daktari na kuona kuwa ni vyema waje kesho kwaajili ya kumuelekeza kuhusu familia yake.
Kwahiyo wakaaga na kuondoka pale hospitali.

Moja kwa moja kabla ya kwenda kokote, sam alihitaji kumuona mtoto wake kuwa anaendeleaje, kwahiyo wote wakaelekea nyumbani kwa  Sakina.
Walifika na kumkuta Sakina akiwa amembeba mtoto yule mgongoni.
"Yani katoka kuamka muda sio mrefu utafikiri amenusa kuwa mnakuja. Karibuni sana"
Sam alimchukua mwanae, kisha wakamueleza hali ya Sabrina na kumshukuru kisha kumuaga.
Ila Sakina akamwambia mama wa Sabrina,
"Si mtaondoka kesho asubuhi?"
"Ndio, kesho asubuhi"
"Basi tutaenda wote, na msihangaike chakula cha mtoto mi nitakiandaa"
Wakakubaliana pale kisha kuondoka na kumruhusu Sam kuelekea kwake, na wao kurudi na mtoto nyumbani.

Sam akiwa njiani kwenda kwake, akajiwa na mawazo ya gafla kuwa kwanini Sakina anaonekana kujali   sana kuhusu yule mtoto.
"Au anajua kama ni mjukuu wake? Mmmh inawezekana anaujua ukweli yule ila sidhani"
Alijifikiria sana na kujipa maswali sana kuhusu Sakina kujua ukweli kuhusu Sabrina na Jeff.
"Mmh! Nadhani hajui, maana angejua basi lazima angeropoka kwangu"
Alienda na mawazo hivyo hadi nyumbani kwake.
Alipofika tu nyumbani kwake, akamkuta yule mlinzi getini na kumuona mdada aliyemzoea pale pale.
Mdada huyo alikuwa ni Neema.
Sam aliingiza gari yake ndani kisha akashuka na kwenda kumsalimia Neema pamoja na kumkaribisha.
"Karibu sana Neema"
Kisha akaongozana nae hadi ndani kwake.
Neema akashtuka kuona ile damu chini pale na kumuuliza Sam kilichotokea.
Sam akamueleza kama alivyowaeleza wazazi wa Sabrina na daktari, Neema akasikitika sana kisha akachukua maji na dekio na kusafisha pale sebleni.
Muda wote Sam alikuwa akimuangalia tu Neema anavyojishughulisha.
Alipomaliza, Sam akamshukuru na kumwambia,
  "Asante Neema"
"Aah usijali, ni lazima nikusaidie. Wewe ni rafiki yangu bwana"
Kisha akamuuliza,
"Hivi umekula kweli?"
Sam akatikisa kichwa kuonyesha kwamba bado hajala.
"Basi ngoja nikaangalie cha kuandaa nipike ule"
"Hapana Neema, usihangaike juu ya hilo. Acha tu tukale kwenye hoteli"
"Hapana, leo utakula nitakachokuandalia mimi"
"Hapana Neema"
Ikabidi Neema asimlazimishe sana na kukubaliana nae kwenda kula hotelini.

Muda kidogo waliondoka pale na kwenda hotelini kula.
Wakati wanakula, Neema akasema tena,
"Ila mi sijapenda kuja kula huku wakati kwako pale una jiko. Ila sio tatizo ipo siku nitakuandalia"
Walipomaliza kula, Sam aliamua kumrudisha kwanza Neema nyumbani kwake kisha yeye kurudi kwake.

Ingawa ilikuwa ni usiku tayari, ila Neema alihitaji sana japo ushauri tu kuhusu Sam.
Na moja kwa moja usiku ule ule akaenda kwa rafiki yake Rose, mtu aliyemuamini kuliko wote.
"Nipe ushauri rafiki yangu tafadhari maana haya mambo yananishinda"
"Kwahiyo wewe unampenda sana huyo mwanaume hadi unatamani uwe mke wa pili!"
"Ndio nampenda sana ila kila ninachofanya imekuwa ni kawaida tu yani haiwi vile ninavyotaka mimi"
"Usijali, nitakupeleka kwa mtaalamu matata huko juu, ila twende kesho alfajiri sawa!"
"Sawa, ila hata yule wa mwanzo alikuwa matata, mbona limefanikiwa lile dili la mwanzo"
"Kwahiyo mkewe kalazwa kweli?"
"Ndio, kwisha khabari yake na kumbukumbu kapoteza"
"Wow, hiyo ni hatua nzuri sasa. Kilichobaki ni rahisi, kumdaka tu huyu mwanaume na huyo mkewe akirudiwa na fahamu anashangaa kuwa tayari upo mke mwenza. Kwani mtaalamu mwanzoni alisema itakuwaje hadi mke alazwe?"
"Mtaalamu alisema kuwa, popote yule mwanamke atakapoanguka hata kama akianguka kidogo basi ndio hapo hapo ugonjwa utampata. Na ndivyo ilivyokuwa kwa huyu mke wa Sam"
Wakafurahi kwa ule ushindi wa awali na kusubiri ushindi wa pili sasa utakaowezesha Sam kuwa upande wao.

Sam alirudi nyumbani na kumfikiria mkewe Sabrina, pia alifikiria kuhusu Neema,
"Huyu ndio mwanamke sasa, anajua kusafisha nyumba na kumjali mwanaume. Ila ndio hivyo nishaoa tayari"
Aliamua kwenda kulala sasa.
Wakati amelala akajiwa na njozi, akamuona Sabrina akiwa sebleni pale, akamuona alivyoanguka.
Mara gafla akaona kitu kama upepo kikimnyanyua Sabrina na kumponda tena pale chini.
Sam akashtuka sana kutoka usingizini huku akitetemeka na kujiuliza kama kuna ukweli wowote kwa kitu alichokiota.
"Mungu wangu, mtoto wa Sabrina tumboni atakuwa mzima kweli? Huo upepo je ni nini? Au mauzauza yangu tu!"
Hakuweza kulala tena, hadi kunakucha.
Asubuhi na mapema alidamka na kuelekea hospitali kumuona Sabrina.

Alipofika aliwakukuta wazazi wa Sabrina wakiwa na Sakina nao wamefika muda sio mrefu.
Aliwasalimia pale kisha wakaongozana wote kwenda kumuona Sabrina ambaye bado hakuwa na fahamu kabisa, kwahiyo wote kwake aliwaona ni wageni.
Walijaribu kukaa nae karibu na kumwambia baadhi ya mambo, wakampa mtoto wake amshike kidogo.
"Mmh! Mimi nina mtoto? Aah mnanitania nyie"
Wakamsikitikia kwani Sabrina hakujielewa kabisa.
Wakamuuliza daktari uwezekano wa kurudi nyumbani na Sabrina,
"Huyu tutamruhusu kesho au keshokutwa, ngoja tuangalie hali yake kwanza"
Basi wakakaa pale na kuondoka huku wakipanga kurudi jioni, ila Sam hakuondoka alikuwa pale pale hospitali kumuangalia Sabrina.

Muda kidogo Sam akapigiwa simu na Neema,
"Vipi Sam umekula?"
"Hapana, bado sijala"
"Basi usijali, leo nimekuandalia chakula kizuri sana. Naomba ufike kwangu tafadhari"
Sam hakutaka kukataa kwani akaona kuwa atamfanya Neema ajihisi vibaya na kuamua kwenda nyumbani kwa Neema.
Na alipofika tu akaandaliwa chakula na Neema na kuanza kula huku wakibadilishana mawazo.
"Inaonekana unampenda sana mkeo Sam"
"Ni kweli nampenda sana na sitegemei kumpenda mwanamke mwingine yeyote kama ninavyompenda Sabrina"
"Hongera zake maana ni wanaume wachache sana wenye upendo wa namna hiyo"
Sam akatabasamu, kisha akamuaga Neema kuwa anarudi hospitali kumuangalia Sabrina.

Sam alipoondoka tu, Neema akaenda tena kwa rafiki yake Rose.
"Mbona kama dawa haijafanya kazi dada?"
"Kwanini?"
"Sam alikuja, kala kile chakula nilichomuwekea dawa ila cha kushangaza kaniaga na kuniambia kuwa anarudi hospitali kumuangalia mkewe"
"Usijali mdogo wangu, kila kitu taratibu. Hebu tuangalie hadi kesho, kama ikibuma tuwasiliane na yule mtaalamu maana alituahidi wazi kuwa ile dawa inafanya kazi haraka sana"
Wakakubaliana kusubiri hadi kesho yake.

Sam akiwa njiani kuelekea hospitali, gafla akaona moyo wake kuwa mgumu kwenda.
"Aah ngoja nirudi nyumbani tu, hata hivyo sioni umuhimu wa kwenda"
Kwahiyo Sam akageuza gari na kuanza safari ya kurudi nyumbani kwake.

Wazazi wa Sabrina walirudi hospitali jioni ile ila Sam hakwenda.
"Atakuwa amepumzika kidogo tu maana huyu kijana ana moyo sana"
Mama wa Sabrina akajipa matumaini juu ya hilo.
Kisha wakazungumza na daktari ambaye aliwapa uhakika wa Sabrina kuruhusiwa kesho.
Baada ya hapo wote wakarudi nyumbani.

Shangazi wa Sabrina bado alikuwa na James yule kaka wa Sabrina nyumbani kwake, kwani alipoanguka mwanzoni alimpa huduma ya kwanza na kisha kukaa nae pale nyumbani kwake.
"Shangazi, naomba leo niondoke kwani najua hata mke wangu atakuwa na mawazo na mimi"
"Sawa, ila pole kwa huo ukweli niliokupa. Sikukusudia kukuumiza ila nilitaka tu uujue ukweli mwanangu James"
"Nashukuru shangazi na nimeamini kuwa siri ya mtoto anayo mama ingawa hujanitajia kuwa baba yangu mzazi ni nani"
"Hilo kamuulize mama yako, ila kama atashindwa kukutajia basi mi nitakupeleka hadi kwa baba yako mzazi"
Basi James akamuaga  tena shangazi yake pale na kuondoka.

Alifika kwa mkewe akiwa na mawazo sana, hata Joy akapatwa na mashaka juu ya hali ya mumewe.
"Hujaonekana siku mbili hapa, si kawaida yako James ndiomana shangazi aliponipigia simu na kusema nisiwe na mashaka upo kwake nikaamini hilo. Leo umerudi ila ukiwa umejawa na mawazo. Nini tatizo mume wangu? Niambie mimi pengine naweza kukusaidia"
"Hapana Joy usijali, kila kitu huenda kwa ngazi. Kwahiyo muda ukifika nitakwambia tu ukweli, ngoja nipate uhakika kwakweli"
"Sasa mimi ndio mwandani wako, usiponiambia mimi utamwambia nani tena? Tafadhari James niambie ukweli mume wangu"
James akafikiria sana na kuona wazi kuwa atakaposema ukweli basi atakosa raha zaidi kwani hakujua mkewe nae angemuongezea kwa maneno yapi, kwahiyo alikazana kumwambia kuwa atamwambia ukweli muda ukifika ingawa Joy naye alijipanga kuendelea kumbembeleza hadi amwambie ukweli wa mambo yanayomfanya awe na mawazo kwa kiasi kile.

Sam akiwa nyumbani kwake, alishangaa kichwa chake kutawaliwa na picha ya Neema. Mawazo yake yote kuwazia uzuri wa Neema,
"Huyu mwanamke mzuri, umbo lake la kuvutia, anajua kujali na sifa zake zote ni nzuri. Kwanini nisiwe na huyu mimi? Kwanini muda huu namuwaza sana?"
Akafikiria kisha akalala.
Kulipokucha asubuhi na mapema, Sam akaenda kuoga na kujiandaa kwenda hospitalini kumuangalia Sabrina.
Mara gafla moyo wake ukasita na kuwa mgumu,
"Kwani nikienda mimi ndio atapona? Hapana, madaktari watamsaidia pale. Ngoja niende kwenye kazi yangu"
Sam akaondoka na kwenda kazini.

Wazazi wa Sabrina walipoenda hospitali walishangaa kwa kutokumuona Sam kabisa ile asubuhi, na walipompigia simu iliita tu bila ya kupokelewa.
"Sijui kapatwa na matatizo? Itabidi tukitoka hapa uende ukamuangalie baba Sabrina"
Walikubaliana juu ya hilo kisha daktari naye akawapa ruhusa ya kurudi na Sabrina nyumbani kwao.
Walirudi nyumbani kisha baba wa Sabrina kwenda kumuangalia Sam nyumbani kwake na ofisini kwake kama atakuwepo.

Muda kidogo, baba wa Sabrina alirudi nyumbani.
"Umempata Sam?"
"Mmh yule kijana nahisi akili yake haipo sawa kwa leo, hebu tumuache kwanza"
"Kwani imekuwaje?"
"Nimempata, nimemkuta kwenye ofisi yake ila majibu aliyonipa mmh tutajadili siku nyingine"
Mama wa Sabrina alibaki kushangaa tu kwani hakuelewa kama Sam anaweza kuwa na majibu mabaya kiasi cha kumuudhi vile mkwe wake.

Sakina naye alienda kwa wakina Sabrina ili kumsalimia Sabrina na kuangalia hali yake.
Kwahiyo yale mazungumzo kuhusu Sam akayasikia kidogo na kusema lazima kutakuwa na kitu maana yeye mawazo yake yalikuwa yakimtuma kwenye ushirikina tu.
Kwahiyo hakukaa sana pale na kuwaaga.
Alipofika kwake napo akajiandaa upesi upesi na kumuaga Dorry kuwa atarudi badae.
Safari yake ilikuwa ni moja kwa moja kwa mtaalamu,
"Leo siendi  kule ana watu wengi sana yule. Ngoja niende kwa huyu wa bondeni hadi nijue leo maana siwezi kulala na hili dukuduku"
Wakati anakaribia kufika likamjia wazo kuhusu mtoto wa Sabrina kuwa kwanini kafanana na Jeff.
"Mmh! Au Sabrina alichepuka na kutembea na shemeji zangu! Ngoja nikaulize na hili pia."
Sakina alifika na kuingia moja kwa moja kwa mtaalamu.
Kisha kukaa,
"Eeh eleza shida yako mama"
"Kwanza kabisa, kabla ya yote niangalizie kama huyu mtoto wa Sabrina ni wa mumewe kweli"
Mtaalamu akacheka, kisha akasema,
"Yule mtoto si wa mumewe"
"Mmmh amezaa na nani sasa?"
"Ni damu yako"
Sakina akashtuka na kumuangalia kwa makini yule mtaalamu.

Itaendelea



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa