JE HAYA NI MAPENZI!! 36: - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Monday, February 17, 2020

JE HAYA NI MAPENZI!! 36:





Jeff alimshika mkono Sabrina mpaka chumbani
kwa Sabrina, kisha akamwambia
"Nenda ukakae pale kwenye kitanda chako
nikuonyeshe"
Sabrina akamuangalia Jeff kwa mshangao na
jicho la hasira.
Halafu akamuuliza kwa mshangao,
"Hivi wewe mtoto una akili!!"
Sam akamuangalia Sabrina na kutabasamu kitendo ambacho kilimkera sana Sabrina,
"Hivi wewe mtoto una kichaa? Yani unaniambia vitu visivyoeleweka halafu nakuuliza jambo unashindwa kunijibu kwanini huku unatabasamu tu. Haya nionyeshe na ukiniletea ujinga wako leo tutaonana wabaya nakwambia. Haya nionyeshe"
Jeff akamuangalia Sabrina kwa upole kisha akaongea kwa utaratibu.
"Sina maana mbaya mamdogo, ila nimekuona ukiwa umechoka sana halafu nakwambia nitakuonyesha kesho wewe unang'ang'ania leo, ndiomana nimekuleta humu chumbani kwako na kukwambia ukakae pale kitandani kwako ili upumzike mamdogo"
Sabrina akacheka na kusema,
"Yani wewe mtoto wewe akili zako sijui huwa zinafikiria vitu gani. Haya nipishe nilale mie"
Jeff akatoka, ila kabla hajafika mbali Sabrina akamuita tena
"Jeff njoo"
Jeff akarudi kwa shauku huku akitamani kujua kuwa kaitiwa kitu gani.
"Na leo kweli nimechoka jamani, naomba unitolee viatu vyangu nimeviacha pale nje"
"Sawa"
Akaitikia kiunyonge na kutoka nje.

Sabrina akiwa chumbani kwake usiku huo, akapigiwa simu na Sam hadi yeye mwenyewe akashtuka kwani akakumbuka wazi kuwa waliahidiana kufanya mazungumzo.
"Mmmh sijui nitamjibu nini jamani!"
Akaiangalia ile simu ambayo iliita hadi kukatika na kuanza kuita tena.
Sabrina akaamua kuipokea, na swali la kwanza toka kwa Sam lilikuwa
"Uko wapi?"
"Nipo nyumbani"
"Unafanya nini?"
"Nimelala"
"Na nani?"
"Mmmh peke yangu"
"Una uhakika?"
"Ndio"
"Haya, usiku mwema"
Kisha akakata simu na kumfanya Sabrina aishie kumshangaa tu,
"Maswali kama polisi, inahusu! Kuwa bosi ndio mpaka kujua njia zangu! Akha! Anipishe mie asinipe shida, yani hata simuelewagi kwakweli maana kama angekuwa ananipenda basi angekuwa ameshaniambia kitambo sana ila anachojua yeye ni kunifatilia tu loh  nishamchoka mie"
Sabrina alikuwa akijiongelea mwenyewe pale kitandani na kulala.
Akajiwa na ndoto kumuhusu Jeff, ndoto iliyomuonyesha kuwa Jeff ana mahusiano na mwanamke aliyemzidi umri.
Aliwaona wakiwa wameongozana, ila Sabrina aliweza kumuona huyo mwanamke mgongoni tu, wakati yule mwanamke anataka kugeuka Sabrina akashtuka na kuanza kujilaumu,
"Kwanini nimeamka bila kuijui sura ya huyo mwanamke? Haiwezekani, mi ndoto zangu mara nyingi huwa ni za kweli. Lazima nikamwambie Da Sakina ili tupambane kuhusu hili janga"
Muda wa kwenda kazini ulikuwa umefika na kumfanya Sabrina ainuke na kujiandaa kabisa.
Alipotoka, alimkuta Jeff akiwa sebleni
"Basi siku hizi hulali wala nini, unamuwaza sugar mamy tu. Hiyo mimama itakutokea puani mtoto wewe"
Sam alifika na kumsikia Sabrina akifoka kwa Jeff kisha akatoka na Sabrina kwaajili ya kwenda kazini.

Wakati wapo ndani ya gari, Sam aliamua kumuuliza Sabrina,
"Mbona  ulikuwa unamfokea yule dogo, kafanyaje kwani?"
"Usimuone vile yule mtoto, anatembea na mimama mikubwa"
"Kwanini sasa kijana mdogo vile anajiharibu?"
"Ndio pakumshangaa hapo, yani kuna mabinti wazuri kweli yeye anakazana na masugar mamy, yani leo nikitoka tu ofisini naenda kwa mama yake kumpa habari"
"Ila Sabrina unajipa mizigo mikubwa bure tu, huyo dogo angerudi kwao ili mama yake awe nae karibu na aweze kumchunguza"
"Ngoja nikashauriane nae juu ya hilo kwanza"
Waliongea mambo mengi ya kumuhusu Jeff hadi pale walipofika ofisini.

Sabrina alifanya kazi yake, na alipomaliza akaona ni vyema aende kupata ruhusa sababu alikuwa na hamu sana ya kuongea na Sakina.
Kwavile ilikuwa ni mwisho wa wiki, hawakushindwa kumpa ruhusa ukizingatia kazi alishazikamilisha.
Sabrina akaondoka pale na kufanya safari ya kwenda kwao.

Moja kwa moja alianza na nyumbani kwao kwanza, na kumkuta mama yake na kaka yake mkubwa.
"Kheee leo kaka James umekumbuka nyumbani!!"
Mama yao akadakia,
"Kaja kunipa khabari kuwa amepata mchumba, kwahiyo Sabrina mwanangu umepata wifi"
"Mmh! Nani huyooo?"
James akacheka, kisha mama yao akajibu tena,
"Kasema atamleta kesho, tena anajina kama langu"
"Joyce!!"
"Ndio, anaitwa Joyce"
Sabrina akamuangalia kaka yake na kumuuliza,
"Mmh sio Joy yule kweli!!"
James akatabasamu na kumjibu dada yake,
"Na wewe acha papara, utamjua kesho"
"Basi kesho nitakuja mapema jamani kumuona wifi"
Huku akitabasamu na kufurahia na wote wakafurahia.
Kisha Sabrina akawaaga kuwa anaenda kuonana na Sakina.

Siku ya leo, Jeff akiwa nyumbani kwa Sabrina akachekecha kichwa chake na kuwaza cha kufanya juu ya Sabrina.
Akapata wazo la haraka, tena la bila kutumia nguvu wala maneno mengi na kuona kuwa wazo hilo ndio litakalomfaa katika mpango wake wa kumpata Sabrina.
"Mungu atanisamehe tu, kwakweli nampenda Sabrina tena nampenda sana  sitaki kumkosa wala sitaki mtu yeyote wa kuyaingilia mapenzi yangu kwake. Mimi ndiye mwanaume pekee nimpendaye kwa dhati, hata kama ni mkubwa kwangu ila nampenda na siwezi kumpenda mwingine zaidi yake"
Aliendelea kupanga mipango yake ili aweze kumpata Sabrina kwani alijua wazi hata kama aseme vipi Sabrina hawezi kumuelewa ukizingatia anamuona kama mtoto wake.

Sabrina alimkuta Sakina na kuanza kuongea nae mawili matatu, kisha akamsimulia ndoto aliyoota kuhusu Jeff na kumfanya Sakina azidi kuchukia kuhusu huyo mama mtu mzima mwenye mahusiano na Jeff bila hata ya kumuona.
"Kwakweli nikimfahamu huyo mwanamke, nakuapia Sabrina nitammeza mzima mzima. Yani wanawake wengine sijui vipi, hawana hata huruma na wanawake wenzao. Kuniharibia katoto kangu Jeff ndio nini? Mtoto mwenyewe ndio huyu huyu kama jicho jamani!"
"Dada, tufanye uchunguzi na tukimjua lazima ajue sisi ni akina nani. Hata kama watu wanasema haifai kumchagulia mtu mchumba sio kwa mtindo huu jamani. Mi nahisi huyo mmama kampa Jeff madawa"
"Itakuwa hivyo tu, ila kumbuka Sabrina mi ni mtoto wa kitanga siogopi kitu na nitamkomesha hilo jimama"
Sakina alikuwa akiongea kwa jazba sana na hasira.
"Ila dada, mi nina wazo"
"Wazo gani hilo?"
"Naona ni vyema Jeff arudi kukaa hapa na wewe ili uweze kumchunguza vizuri sababu mimi muda mwingi nakuwa kazini dada"
"Kweli ni wazo zuri mdogo wangu, ila kama wewe umeshindwa mi nitaweza kweli! Unajua Jeff anakusikiliza sana wewe, kwahiyo mi nakuomba ujaribu kumbana ili akutajie huyo mjaalaana asojua vibaya maana hata nikimfikiria huyo mwanamke kutembea na katoto kangu nahisi kichefuchefu"
"Basi dada mi nitajaribu kumbana nimuulize ila kama ikishindikana basi itabidi tu arudi huku kwako sababu mi sitaweza zaidi kwakweli"
"Hakuna tatizo, ndio kujaribu huko ndugu yangu. Ila lazima tushirikiane kumjua huyo mwanamke."
Sakin a akakubaliana na Sabrina juu ya swala hilo.
Kisha Sabrina akamuaga Sakina na kuelekea tena nyumbani kwao.
"Mi nataka kuondoka mama!"
"Si ungelala hapa hapa leo! Kwanza kesho hakuna kazi, pili ungesubiri tu hadi hiyo kesho umuone wifi yako"
"Usijali mama, Sam alihitaji kuongea na mimi tangia jana ila ratiba zikaingiliana. Ndio leo naenda kuzungumza nae, halafu kuhusu wifi hakuna tatizo kwani kesho asubuhi na mapema nitafika hapa na kumngoja wifi yangu"
Basi Joy hakuwa na jinsi zaidi ya kumruhusu binti yake aende tu huko alikopanga.

Sabrina akaenda kuonana na Sam kwaajili ya mazungumzo ambayo walipanga kuongea jana yake.
Ila alijikuta akiwa eneo la tukio peke yake bila ya Sam kutokea,
"Inamaana ananilipizia ya jana au ni kitu gani? Si angeniambia tu kuliko kunifanyia hivi!"
Ila aliendelea kusubiria na kujipa moyo wa subira kuwa Sam atatokea tu.
Mida iliendelea kupita bila ya Sam kutokea na kumfanya Sabrina ajawe na hasira kwenye moyo wake.
"Kwanini kanifanyia hivi jamani, kwanini Sam lakini!"
Wakati akilalamika hivyo ujumbe ukaingia kwenye simu yake, ulionyesha kuwa umetoka kwa Sam na kumfanya Sabrina aufungue kwa shauku kubwa,
"Samahani Sabrina, ratiba zimeingiliana. Kuna watu muhimu sana natakiwa kuonana nao leo, kwahiyo tutapanga siku nyingine ya kuongea"
Sabrina akavimba kwa hasira, akatamani hata aipasue ile simu yake.
Akainuka kwenye kiti huku moyo wake umejaa hasira na kuanza kuondoka, simu yake ikaita. Sabrina hakutamani hata kuipokea kwakuwa mpigaji alikuwa ni Sam, ila aliona ni vyema aipokee tu
"Geuka nyuma Sabrina"
Sabrina akageuka na kumuona Sam akitabasamu, Sabrina alimuangalia Sam kwa jicho la hasira huku likicheza cheza na kutamani kucheka na kulia kwa pamoja.

Sam alisogea pale alipokuwa Sabrina huku akiendelea kutabasamu,
"Sabrina, twende tukakae tufanye mazungumzo yetu"
"Kwanini Sam umenifanyia hivi jamani!"
"Nilitaka kupima uvumilivu wako Sabrina"
"Ili iweje?"
"Twende tukakae basi kwanza tuzungumze"
Sam akamshika mkono Sabrina na kumpeleka mahali ambako kulikuwa na kiti na kumsihi akae, kisha wakaagiza vinywaji na kuendelea na maongezi.
"Nimegundua kitu kutoka kwako Sabrina"
"Kitu gani hicho?"
"Nimegundua kuwa wewe ni mwanamke mvumilivu sana, una hasira za karibu lakini pia ni mvumilivu"
"Haya, nashukuru kwa hilo ila umenikera sana"
"Nisamehe Sabrina, tena unisamehe sana"
"Poa usijali"
"Nisijali ndio umenisamehe au!"
"Nimekusamehe ndio"
"Sasa Sabrina mi kuna jambo moja kubwa nataka kukuuliza"
"Jambo gani hilo?"
"Nilitaka kukuuliza kuhusu maisha yako Sabrina ila kuna jambo lingine linataka kuingilia kati hapa"
"Niambie basi ni ja mbo gani hilo!"
"Leo ngoja niseme ukweli wa moyo wangu, kwakweli Sabrina nakupenda sana, nakuhitaji, napenda uje kuwa mke wangu. Nakupenda  Sabrina jamani nakupenda sana."
Sabrina hakuamini macho yake wala masikio kwa kile alichokisikia kutoka kwa Sam na kujikuta akiwa kama mtu anayehitaji kusikia zaidi.
"Hivi Sam upo serious kweli?"
"Sabrina, unadhani yote haya nayafanya kwaajili ya nini jamani? Ni sababu ya upendo wangu juu yako Sabrina, nakupenda wewe, sitaki kukukosa. Sitaki uwe mbali na mimi, nakupenda sana Sabrina"
Sabrina hakujua amjibu nini Sam kwa muda huo kwani alihisi akili yake kamavile ikipaa angani, alihisi kama yupo ndotoni vile kwani hakuamini kuwa Sam ndiye aliyekuwa akimtamkia maneno yale.
Sabrina akaamua kumjibu Sam kwa tabasamu kubwa usoni,
"Hata mimi nakupenda Sam, siku zote nilikuwa nikingoja kwa hamu siku ambayo utanitamkia wazi kuwa unanipenda. Sikutaka kuanza kusema kwavile ungenielewa vingine, nashukuru Mungu aliyekufunulia kuniambia ukweli huo Sam. Nami nafurahi sana na kukwambia kuwa nakupenda pia"
Sam aliinuka pale alipokuwa amekaa, kisha akamshika mkono Sabrina na kumuinua halafu akamkumbatia kwa furaha.
Kisha akamnong'oneza sikioni,
"Naomba leo ukalale kwangu Sabrina maana nina mengi ya kuzungumza na wewe"
Sabrina akasita kidogo na kuacha kumkumbatia Sam, kisha akamuomba kwenda msalani.

Alipokuwa maeneo ya msalani, Sabrina akafikiria sana.
"Nikikubali kwenda kulala kwake leo lazima atataka kufanya mapenzi na mimi. Mmh! Siku ya kwanza tu ya kukubaliana nitaonekana malaya ni bora nikatae halafu tutapanga siku nyingine. Na vipi kuhusu matatizo yangu yale je! Nitamdhuru kijana wa watu, bora nikatae halafu nitamuelewesha siku zijazo"
Sabrina akakubaliana na moyo wake na kisha kurudi eneo alilomuacha Sam ili kuendelea na mazungumzo.
"Unasemaje sasa mpenzi, twende ukalale kwangu leo"
"Hapana Sam, nitalala kwako siku nyingine ila sio leo"
"Nina mengi ya kuzungumza nawe Sabrina, nina mengi ya kukwambia. Yani usiku    wa leo nilitaka uwe ni usiku wa mazungumzo tu baina yetu Sabrina, nakupenda jamani"
"Naelewa Sam, ila tupange siku nyingine tafadhari. Hata mi nakupenda"
Sam hakutaka kubishana sana na Sabrina badala yake akamwambia kuwa atamrudisha nyumbani kwake ila kesho atampitia kwaajili ya matembezi.
"Tena kesho naenda nyumbani sababu kaka yangu kapata mchumba anataka atutambulishe"
"Basi itakuwa ni vyema, tutaenda wote ili nami kwenu wakanitambue"
Waliongea kiasi kisha Sam akamrudisha Sabrina nyumbani kwake na kumuaga kwa kumbusu kwenye paji la uso.

Sabrina alipoingia ndani kwake alianza kwa kumuita Jeff,
"Jeff mwanangu leo nina habari njema sana"
Jeff alitoka chumbani kwake ili kumsikiliza Sabrina hiyo habari yake njema,
"Kuanzia leo, Sam ni baba yako mdogo"
Sam alijibu kwa unyonge, ila nae akamwambia kitu kingine Sabrina
"Hongera mamy, ila na mimi nina surprise yako leo"
"Surprise gani hiyo?"
"Leo nimekutengene zea juisi unayopenda kuliko zote duniani"
"Ipi hiyo?"
Jeff akaenda kwenye jokofu na kutoka na glasi yenye juisi na kumpa Sabrina,
"Jeff na wewe, nimeshiba sana leo"
"Jamani mamdogo, ndio hutaki kunywa wakati mi nimepoteza muda wangu wote hapo!"
"Haya lete ninywe kidogo"
Jeff alimkabidhi Sabrina ile juisi kwa furaha.
Sabrina naye aliipokea na kuinywa, muda huo huo Sabrina alijikuta akikaa kwenye kochi na kulala pale pale.

Itaendelea



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa