JE HAYA NI MAPENZI!! 34: - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Monday, February 17, 2020

JE HAYA NI MAPENZI!! 34:





Jeff akamuangalia Sabrina alivyokuwa akilalamika
hadi pale alipoenda kukaa.
"Ila mamy, mi nina ujumbe wako"
"Ujumbe gani huo?"
"Nakupenda sana, tena sana"
Sabrina akamuangalia Jeff na kucheka.
Jeff alitulia na kutaka kumsikiliza Sabrina kuwa atasema kitu gani ila Sabrina hakusema chochote zaidi ya kucheka na kufanya Jeff aulize
"Mbona unacheka mamy?"
"Hivi wewe Jeff asiyejua kama unanipenda nani? Ndiomana umetafuta kisingizio cha kutoka kwenu na kuja kwangu"
Jeff akajiuliza moyoni kama kweli Sabrina amemuelewa vyema upendo anaouzungumzia yeye na kufanya amuangalie tu, kisha akamuuliza
"Kwahiyo unajua kama nakupenda?"
"Ndio najua, tena wewe kunipenda mimi hujaanza leo wala jana. Yani toka upo tumboni mwa mama yako ulikuwa unanipenda mimi, hakuna kitu ambacho mama yako aliweza kufanya bila ya mimi kwahiyo natambua vyema kama wanipenda mwanangu ndiomana jukumu la kukulea sioni kama ni gumu kwangu. Hivi umekula leo?"
Sabrina alikuwa tayari ameshabadili mada muda huo huo na kumfanya Jeff ashindwe kuendelea na pia ashindwe kuelewa kama ameeleweka alichokuwa anakisema au la.
Sabrina aliendelea na habari zingine tena hata kabla Jeff hajamjibu kama amekula au la,
"Yani ile ofisi, ngoja Sam arudi wataipata. Yani wamenitegeshea mtego ili nichelewa kazini halafu wamenitafutia vijisababu vya uongo na kweli ili wanisimamishe kazi dah"
Ikabidi Jeff nae aendane na mazungumzo ya Sabrina tu,
"Si ungemtafuta huyo Sam kwenye simu umwambie"
"Sam hapatikani, angepatikana mbona ningekuwa nimemwambia kila kitu tayari! Yani sina hata raha jamani"
"Pole mamy, mi nipo kwaajili yako"
Sabrina akainuka na kwenda chumbani kwake ambapo alikuwa amejichokea kwa mawazo tu.

Sabrina alikaa sana chumbani kwake akiwaza na kuwazua, mlango wake ukagongwa naye akaenda kufungua alikuwa ni Jeff,
"Chakula tayari, twende ukale upunguze mawazo"
"Kheee Jeff na wewe unakuwa kama mfanyakazi wa ndani, uwe unajipikia chakula chako tu sitaki mama yako akija hapa aseme nakunyanyasa. Na hata kama unaona kazi zako binafsi ni nyingi niambie niajili housegirl, sawa!"
"Hapana tatizo, mie kazi naziweza mamdogo hata usilete huyo housegirl"
Sabrina akatoka chumbani kwake na kwenda sebleni kula.
Wakati Sabrina anakula, Jeff akapigiwa simu na kuongea nayo
"Poa nakuja, nipe kama dakika tano hivi"
Kisha akamgeukia Sabrina na kumuaga,
"Natoka kidogo mamdogo, nitarudi muda sio mrefu"
"Mmmh wapi saivi?"
"Hapo juu kidogo"
"Kufanya nini?"
"Kuna rafiki yangu naenda kuonana nae"
"Kwanini yeye asije hapa?"
"Aaah atakuja siku nyingine"
Jeff akainuka na kuondoka, Sabrina akahisi vitu vingine kabisa juu ya Jeff
"Huyu mtoto huyu, atakuwa ameenda kwa hilo sugar mamy lake na tukiligundua litatutambua maana mtoto mawenge yamemjaa balaa"
Akatamani hata ampigie simu Sakina na kumueleza ila alisubiri apate uhakika kwanza ndio amwambie Sakina.
Akaamua kutulia pale na kuwasha luninga ili kupunguza mawazo.

Wakati ametulia pale sebleni, akapigiwa simu kwa namba ngeni kabisa, Sabrina aliipokea ile simu kwa haraka huku akifikiria kuwa mpigaji atakuwa ni Sam, ila hakuwa Sam bali alikuwa ni Fredy ambaye alimuulizia Sabrina alipo ili akamtembelee
"Nipo nyumbani, karibu tu utanikuta"
"Poa nakuja"
Ile simu ilikatika huku Sabrina akitarajia ujio wa Fredy pale nyumbani kwake.

Sam alirudi kutoka katika safari yake na kuwaza jambo kubwa moja, nalo ni kumwambia ukweli Sabrina kuwa anampenda na anataka kumuoa.
Alikaa na rafiki yake mkubwa aliyeitwa Jose na kushauriana nae juu ya jambo hilo,
"Nataka nimfanyie Sabrina surplise ndiomana nikawaambia wampe ile barua ya kusimamishwa kazi mapema ili arudi nyumbani kwake"
"Sam kwa mipango nakukubali sana"
"Yeah, mimi ndio Sam bhana huwa sibabaishwi na kitu. Nataka pale kwa Sabrina leo tuwe wawili tu ndiomana nikakwambia tuchonge lile dili la kumuondoa yule dogo mahali pale maana ni king'ang'anizi balaa"
Wakafurahi na Jose huku wakipanga namna ya Sam atakavyoingia pale kwa Sabrina na kumfanyia ule mshtukizo ambao Sam amepanga kuufanya kwaajili ya Sabrina.
"Leo lazima lengo langu litimie"
"Usijali Sam, kila kitu kitaenda kama kilivyopangwa"
Sam akajiandaa vizuri ili aende kwa Sabrina, mwanamke pekee aliyeona akimpenda kuliko wote.

Sabrina aliendelea kuungoja ujio wa Fredy ili amsikilize kuwa kaja na jambo gani jipya.
Muda kidogo mtu akabisha hodi, moja kwa moja Sabrina akajua kuwa mtu huyo lazima atakuwa ni Fredy ila alipofungua tu macho yake yakagongana na Japhet
"Kheee Japhet, nini kwangu muda huu?"
"Nimekuja kukutembelea Sabrina"
"Ni nani huyo aliyekuonyesha hapa kwangu?"
"Nilienda ofisini kwenu kuna mtu amenielekeza"
"Haya nakuomba uende, sitaki hata kukuona kwenye macho yangu. Tafadhari Japhet nakuomba uende"
"Naomba unihurumie Sabrina, nahitaji msamaha wako tafadhari. Najua nilikukosea sana"
"Naomba uende"
Sabrina  akataka kufunga mlango ila Japhet akauzuia ule mlango na kumfanya Sabrina ashindwe kuufunga.
Japhet alikuwa kama mtu anayeng'ang'aniza kufanya kitu fulani ambacho Sabrina hakukitaka.
Wakati Japhet aking'ang'aniza hivyo, Fredy nae aliwasili mahali pale na kwajinsi alivyomuona Japhet alijua wazi kuwa anataka kumdhuru Sabrina, alijikuta akimrukia Fredy na kumpiga ngumi ya sura kitendo kilichomfanya Japhet aanguke kwavile hakujipanga.
Kuanguka kwa Japhet kukampa Fredy nafasi kubwa ya kumshambulia, ni Sabrina sasa aliyemtaka Fredy kupunguza hasira zake
"Basi Fredy inatosha"
Fredy alionyesha kuwa na hasira sana kanakwamba ule ugomvi unamuhusu yeye kabisa.
Fredy alisikiliza kauli ya Sabrina na kumuachia Japhet, muda huo Japhet nae akainuka kutoka pale chini na kumuangalia Fredy kisha akamwambia,
"Kumbe ni wewe! Nitakupata tu sehemu"
"Nenda zako, na bado picha itaendelea"
Fredy alijibu kwa jazba sana na kumfanya Sabrina ahisi kuwa Fredy na Japhet wanajuana kutokana na vile vitisho ambavyo walikuwa wakipeana.

Japhet akaondoka kwa hasira kisha Fredy na Sabrina wakaingia ndani, ikabidi Sabrina aende kumletea Fredy maji ili kumtuliza zile hasira kidogo
"Kunywa maji basi Fredy"
"Usijali Sabrina"
Fredy akanywa yale maji kidogo na kupunguza hasira ili aweze kuzungumza kile kilichomleta kwa Sabrina.
"Pole Fredy, nimekuingiza kwenye matatizo hata usiyo husika nayo"
"Usijali Sabrina, yule jamaa ni bwege sana"
"Kwani unamjua?"
"Ndio namfahamu vizuri sana"
"Khee umemfahamia wapi?"
"Nitakwambia tu ila ngoja nipumue kidogo"
Fredy alitulia kwa muda kidogo, Sabrina nae akatulia huku akitafakari mambo mawili matatu.
Wakati Fredy ametulia pale, usingizi nao ukampitia pale pale na kujikuta akilala pale sebleni kwa.
Sabrina akatamani kumuamsha ila akaona kwamba itakuwa ni kumuharibia usingizi wake na kumuacha aendelee tu kulala
pale kwenye kochi.
Huku Sabrina akiendelea na mambo mengine.

Wakati Sabrina akiwa jikoni kwake akasikia mtu akibisha hodi, akajiuliza kuwa atakuwa ni nani maana kama angekuwa ni Jeff basi angefungua tu sababu ana funguo yake.
Yule mtu naye akazidi kugonga na kumfanya Sabrina awaze kuwa Japhet amerudi tena kutokana na kile kipigo alichopewa akahisi kuwa amekuja kulipiza kisasi kwake.
Hofu ikamjaa Sabrina kuwa inawezekana akapigwa.
Akatoka jikoni na kwenda sebleni hadi mlangoni na kuuliza,
"Nani wewe?"
Yule mtu hakujibu bali aliendelea kugonga tu na kumfanya Sabrina azidi kupatwa na hofu. Hivyobasi akaenda hadi alipolala Fredy na kumuamsha,
"Kuna mtu anagonga mlango wangu hata sijui ni nani halafu naogopa kwenda kufungua"
"Usijali, twende wote"
Sabrina akaongozana na Fredy hadi mlangoni, muda huo Fredy alikuwa nyuma ya Sabrina na kujikuta akipatwa na tamaa ya kumshika Sabrina kiunoni.
Wakati Sabrina anafungua mlango, mikono ya Fredy ilikuwa tayari imezunguka kwenye kiuno cha Sabrina, na aliyeingia ndani alikuwa ni Sam.
Alipoona sura ya Sabrina alitabasamu ila alipoona mikono ya Fredy kwenye kiuno cha Sabrina alichukia sana na badala ya kuingia ndani vizuri, alitoka nje na kuanza kuondoka na kumfanya Sabrina amfate kwa nyuma,
"Sam, Sam. Tatizo nini jamani"
"No, siwezi kuzungumza kwasasa."
Sam akaenda na kupanda gari yake na kuiondoka, Sabrina alibaki kaduwaa tu kwani hakumuelewa kabisa Sam na hakuelewa kuwa ni kwanini achukie kiasi kile.
Aliangalia gari ya Sam ikiishia tu,
"Halafu kaja na gari mpya ile, nadhani kanunua nyingine. Dah hata sijui kachukia nini, yani amerudi bila kuniambia na amekuja nyumbani kwangu na kuondoka kwa hasira."
Sabrina akaamua kurudi ndani tu ambapo Fredy alikuwa bado mlangoni huku naye akishangaa kuwa kwanini yule Sam kaondoka tena bila ya salamu wala kuaga.
Sabrina  alipofika pale mlangoni akaingia ndani na Fredy huku akiendelea kujiongelesha mwenyewe,
"Hata sijui kwanini Sam amechukia kiasi kile"
Fredy akamuuliza Sabrina,
"Kwani una mahusiano nae?"
"Hapana, yule ni bosi wangu na rafiki yangu"
"Sasa mbona amechukia vile?"
"Hata sijui ni kwanini"
Sabrina akachukua simu yake na kujaribisha kama namba za Sam zinapatikana ila bado hazikupatikana na kumfanya Sabrina awe na mawazo zaidi.
Fredy akaanza tena kwa kumuongelesha Sabrina,
"Kuna jambo moja tu lililonileta hapa kwako Sabrina"
"Tafadhari Fredy, nakuomba usiniambie kitu chochote kile. Maana akili yangu haipo sawa kabisa hapa."
Fredy hakuwa na la kusema zaidi wala la kufanya na kuamua kumuaga Sabrina ili aende.
"Basi ngoja niende Sabrina, ila kumbuka nakupenda sana. Na hakuna mwanaume anayekupenda kama mimi ninavyokupenda yani hakuna kabisa. Nakupenda Sabrina tena sana"
Sabrina hakumjibu kitu chochote Fredy zaidi ya kumuangalia tu.
Fredy akatoka zake nje na kuondoka.

Sabrina akiwa amebaki mwenyewe ndani, aliwaza sana.
"Huenda Sam naye ananipenda ndiomana kachukia kunikuta na Fredy. Inawezekana ikawa hivyo tu, au ana mambo yake mengine yaliyomfanya achukie. Kwanini jamani, kwanini haniambii ukweli huyu Sam jamani mmh"
Sabrina aliwaza sana bila ya kupata jibu, muda kidogo akawasili Jeff akiwa amechoka sana na kumfanya Sabrina amuulize.
"Vipi tena na wewe?"
"Yani hapa nimechoka mamy balaa, huwezi amini. Mtu aliyenipigia simu amenizungusha mji mzima na mwisho wa siku sijaonana nae wala nini"
"Pole sana, basi mwenzio hapa yamenikuta makubwa leo"
"Makubwa!! Mambo gani hayo?"
Sabrina akaanza kumueleza Jeff tangia ujio wa Japhet, Fredy na Sam ambapo Jeff nae akaonyesha kuchukizwa
"Na bahati yao hawajanikuta haswa huyo wakuitwa Japhet ningemfunza adabu"
"Mmh Jeff wakubwa zako wale"
"Mi mdogo ila nitawashinda"
"Mmmh kivipi"
Jeff akacheka bila ya kumjibu Sabrina na kumuingizia habari zingine.
Ila Sabrina akaendeleza khabari zilezile,
"Sijui kesho niende ofisini ili nikamwambie Sam kuwa nimesimamishwa kazi!"
"Usijisumbue mamdogo, kumbuka huyo Sam ndio bosi mwenyewe kwahiyo wale hawawezi kufanya chochote bila ya maamuzi yake."
"Unamaanisha kuwa Sam ndio kakubaliana nao kuwa mi nisimamishwe kazi?"
"Hiyo ndiomaana yake, wewe tulia kwanza uone kitakachoendelea"
"Mmh wee mtoto, kazi naitaka mie. Unataka nirudi tena kukaa nyumbani! Niombe hela ya mafuta na vipodozi kwa mama! Hapana kwakweli, lazima nibembeleze kazi"
"Sasa utafanyaje"
"Ilimradi Sam amerudi, basi kesho kwenye mida ya saa nne nitaenda ofisini ili nikajaribu tena bahati yangu"
Jeff hakuwa na pingamizi juu ya hilo zaidi ya kukubaliana nae tu.

Sam alikuwa amejawa na hasira, kile kitendo cha kumkuta Sabrina ameshikwa kiuno na mwanaume mwingine kilimuumiza sana.
Alijaribu kukaa na rafiki yake Jose ili kuweza kupata ushauri.
"Kwakweli sijui cha kufanya, roho inaniuma sana."
"Ila Sam, wewe ndiye unayechelewesha mambo. Kwanini usimwambie ukweli yule mtoto?"
"Nina matatizo Jose, sitaki kumchukua tu Sabrina bila ya yeye kujua matatizo yangu. Leo nilijipanga kabisa kumueleza Sabrina kila kitu kuhusu mimi, najua asingekataa ndiomana nikataka kumpa hata lile gari kama zawadi tu"
"Pole sana, najua jinsi gani unaumia ingawa hata mi mwenyewe huwa sijui una matatizo gani ila la msingi ni kumwambia Sabrina ukweli tu. Kuchukia sio suruhisho baina yenu"
"Naona kamavile Sabrina hajatulia, nami nahitaji mwanamke aliyetulia ili aweze kunielewa ni kitu gani nakitaka kutoka kwake"
Jose akajaribu kumuelekeza rafiki yake na kumtuliza zile hasira alizokuwa nazo.

Usiku ulipofika Sabrina alienda kulala, ila akajiwa na ndoto kuwa ameolewa na kumfanya ashtuke na kujiuliza
"Hivi hii ndoto inanijia mara kwa mara kwani mume wangu ni nani?"
Akasikia sauti ya Jeff ikijibu kutoka mlangoni,
"Mimi hapa"
Sabrina akashtuka na kuuliza tena,
"Nani?"
Jeff akajibu tena,
"Mimi hapa Jeff"
Sabrina akainuka ili kuangalia kama kweli anayemjibu ni Jeff.

Itaendelea



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa