JE HAYA NI MAPENZI!! 33: - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Monday, February 17, 2020

JE HAYA NI MAPENZI!! 33:





Akamshtua yule dereva na kumuuliza,
"Mbona hunipeleli huko ofisini?"
"Hatuendi ofisini ndio, kuna mahali nakupeleka"
"Ni wapi huko?"
Yule dereva hakujibu ila alianza kucheka.
Sabrina akamuangalia na kumshangaa yule dereva kisha akamuuliza tena,
"Mbona unacheka wakati mi niko serious nakuuliza jamani!"
Ila bado yule dereva hakumjibu kitu Sabrina na kumfanya aweze mambo mengi zaidi bila ya jibu.

Ile gari ikafika mahali furani na kusimama kisha yule dereva akashuka na kwenda kumfungulia mlango wa gari Sabrina ili naye ashuke,
"Tumefika mama, teremka"
Kwa uoga Sabrina akashuka ili kujua kitu ambacho ameletwa huko, yule dereva akamwambia Sabrina
"Kwa kifupi Sabrina nimekuleta hapa kwa jambo moja kubwa muhimu ila sio kama Sam amenituma kweli ila nilikwambia vile ili uweze kukubali kuja nami hapa"
"Sasa kwanini ukanidanganya kuwa Sam amekutuma?"
"Nimesha kujibu hilo Sabrina, unajua wazi kuwa ningekwambia ukweli usingekubali wewe. Nakuomba ufatane nami sasa, ni jambo la muhimu sana Sabrina"
Kwakweli Sabrina alijisikia vibaya kwa kuongopewa na hakujua kuwa yule kijana ana lengo nae lipi.
Yule kijana akamwambia Sabrina kuwa amngoje pale nje ili waingie wote.
Sabrina akaona kuwa ni kheri aondoke eneo lile.
Sabrina akatoka pale kwenye gari na kuongoza kwenye barabara kisha akasimamisha bodaboda na kuelekea kazini huku akiwa na mawazo mengi kichwani mwake.

Alipofika ofisini akamlipa yule wa bodaboda na kuingia ofisini ingawa alikuwa tayari ameshachelewa.

Sabrina aliingia ofisini huku mawazo mengi yakimtawala hata kujieleza kuwa kwanini amechelewa hakuwa na jibu la kuandika.
Sabrina alikaa ofisini ila mawazo yake yote hayakuwepo pale na kumfanya afanye kazi za pale ofisini kinyume na utaratibu uliopo.
Akafatwa na bosi msaidizi na kuulizwa,
"Mbona umechelewa sana leo, na kwanini umeharibu kazi kiasi hiki?"
Yule bosi msaidizi akamtolea Sabrina zile faili alizoharibu na kumfanya Sabrina kukaa kimya na kujiona wazi kuwa ana makosa kweli na hakuwa na cha kujitetea kwahiyo akabaki kimya tu na kumchukiza yule dada ambaye alikuwa ndiye bosi wake msaidizi.
"Huwa unafanya ujinga sababu unajua wazi Sam atakutetea ila leo hayupo huyo Sam wako, na haya makosa lazima niyafikishe mbali ndio nadhani utaelewa umuhimu wa kazi"
Sabrina aliendelea kuwa kimya tu  huku akimuangalia huyu dada na kumfanya huyu dada achukie na kuondoka.
Sabrina akaona kuendelea kwake kubaki pale ofisini ni sawa na kujiongezea matatizo kwahiyo akaenda kuomba ruhusa ili arudi nyumbani ila walimkatalia kuondoka na kumfanya achukie zaidi.

Jeff aliamua kwenda kwa yule mwalimu wake ili kuweza kupata ushauri, uzuri ni kwamba alimkuta akiwa hana watu wengi na kuona kuwa hapo atapata nafasi ya yeye kuzungumza na mwalimu wake huyo kama alivyomuahidi,
"Eeh Jeff niambie tatizo lako"
"Tatizo langu madam ni mapenzi"
"Mapenzi!! Yamefanyaje kwani?"
"Kwanza madam niambie mapenzi ni nini?"
Joy akacheka kwanza kisha akamjibu Jeff,
"Mapenzi ni kama mti au majani, huota popote"
"Kwamaana hiyo mtu yeyote anaweza akapendwa na kupendwa?"
"Ndio maana yake hiyo Jeff"
"Je mapenzi yanajali umri, kabila, pesa na kiwango cha elimu?"
"Nimekwambia mapenzi ni kama mti huota popote, kwamaana hiyo mapenzi ya kweli hayajali umri, kabila, elimu, pesa wala muonekano ila yanajali moyo unavyohisi na kuumia kwa yule umpendae. Vipi Jeff je kuna mtu umempenda?"
"Tena sana ila nashindwa kumwambia sababu yeye ni mkubwa kwangu, natamani angetambua hisia zangu, angejua ninavyoumia na kuteseka juu yake. Natamani angejua upendo uliopo ndani yangu kwake"
"Mmmh ni nani huyo aliyepata bahati hiyo Jeff?"
"Yupo mdada madam, ni mzuri, anavutia na kupendeza. Huwa siwezi kusahau siku aliyorudi nchini na kunikumbatia!"
Jeff alitulia na kuwa kama mtu anayevuta hisia na kukumbuka kitu fulani, Joy alikuwa akimuangalia tu na kugundua kuwa kweli huyu kijana kuna mtu anampenda kweli.
"Alinikumbatia vizuri sana sijapata kuona, huwa sisahau kabisa. Mimi ndiye nilikuwa mtu wa kwanza kukumbatiwa naye siku hiyo kabla ya watu wote. Alinifurahia sana, hajui tu jinsi kumbatio lake linavyonipa hisia kali hadi leo. Siwezi kumsahau kwakweli, sitaki kumpoteza jamani. Nisaidie madam, nifanye nini ili aweze kuzisoma hisia zangu?"
"Hebu nitajie kwanza kuwa huyo mwanamke ni nani?"
"Hapana madam, sitaweza kukutajia jina lake kwa sasa ila muda ukifika nitamtaja"
Joy akajaribu kumwambia Jeff njia ambazo aliona kuwa itakuwa rahisi kwa huyo mtu kumuelewa Jeff, kisha Jeff akamuaga mwalimu wake huyo na kuondoka.

Sabrina bado alikuwa na kisirani pale kazini, alitamani muda wa kazi uishe mapema aondoke kwani alihisi wazi kuwa watu wa ofisini ndio waliofanya ule mpango wa kumdanganya kuwa yule dereva katumwa na Sam kumfuata kumbe ni njama zao za kumchelewesha kazini    tu siku hiyo ili wapate sababu ya kugombana nae.
Sabrina hakuwa na raha siku hiyo na aliona ni vyema akitoka hapo basi aende nyumbani kwao akatulize mawazo yake.
Muda wa kutoka ulipofika, Sabrina hata hakuaga siku hiyo bali alitoka na kuondoka zake, na moja kwa moja alienda nyumbani  kwao.

 Alimkuta mama yake kama kawaida na kumsalimia, moja kwa moja Sabrina alianza kumueleza mama yake jinsi alivyochukizwa siku hiyo
"Yani leo kazini wamenikera balaa"
"Nini tena mwanangu?"
Sabrina akamuelezea mama yake kilichomtokea siku ya leo tangu alipotoka nyumbani kwake,
"Mwanangu ndio mambo yalivyo katika dunia, kuwekeana wivu na kinyongo ndio kawaida katika kazi. Vumilia tu mwanangu"
Joy akampa moyo binti yake na kumfanya kurudi katika hali ya kawaida na kuwa na furaha tena.
"Ngoja nikamuone na dada Sakina mama"
"Sawa mwanangu"
Sabrina akainuka na kwenda nyumbani kwa Sakina.

Alipofika alimkuta Sakina akiwa amelala na kumuamsha pale alipolala,
 "Dada, dada"
Sakina akashtuka sana kutoka usingizini,
"Kheee Sabrina utaniua mwenzio, umenishtua halafu nilikuwa naota ndoto mbaya sana"
"Ndoto gani hiyo dada?"
"Yani sijawahi kuota ndoto ya namna hii kwakweli, eti nimeota Jeff ameoa"
Sabrina akacheka na kumshangaa Sakina,
"Sasa hiyo ndio ndoto mbaya? Kwahiyo hutaki wakwe wewe! Hutaki mwanao aoe?"
"Sio hivyo Sabrina, tatizo ni kwa mwanamke niliyeota kuwa ameolewa na mtoto wangu"
"Mwanamke gani huyo hadi useme ni tatizo?"
"Ni mtu mzima, yani nimeota kuwa Jeff kamuoa mwanamke ambaye ni mkubwa kwake, kwakweli sijaipenda hii ndoto jamani"
Sabrina akacheka tena na kumuuliza Sakina,
"Inamaana Jeff kaanza mahusiano na masugar mamy? Mbona hiyo ndoto yako siielewi dada!"
"Yani nikigundua kuwa kuna mwanamke mtu mzima anaisumbua akili ya mwanangu hadi anawakataa watoto wenzie huyo mwanamke atanitambua nakwambia, atataja majina  yangu ya utoto nakwambia."
"Ila una uhakika kama Jeff anatoka na mwanamke mtu mzima?"
"Sina uhakika ila mbona anakataa wasichana wazuri wanaomtaka? Hebu niambie vizuri huko kwako anatulia kweli nyumbani?"
"Anatulia ndio ila sijui muda ambao sipo nyumbani kama anafanyaga upuuzi"
"Basi nakupa kazi Sabrina, tafadhari mchunguze mwanangu. Ongea nae kwa ukaribu ili ujue kama kuna kitu kinamsumbua, najua wewe hawezi kukuficha"
"Usijali kwa hilo dada yangu"
Wakaongea vitu mbali mbali na kujikuta wakikumbuka mambo yaliyopita hapo nyuma,
"Tena umenikumbusha Sabrina, hivi yale matatizo yako yaliisha mdogo wangu?"
"Yapi hayo dada?"
"Yale ya kipindi kile, si unakumbuka ulikatazwa kulala na mwanaume yeyote yule, si unakumbuka!"
"Nakumbuka ndio"
"Vipi umewahi kulala na wanaume wangapi? Na kile kinyama kilichokuotaga vipi kilitoka?"
"Dah ni historia ndefu dada yangu, ila kwa kifupi sijawahi kulala na mwanaume yeyote   yule"
"Hebu nieleze vizuri, imekuwaje hadi leo usilale na mtu kweli!"
"Naogopa kuwaua watu wasio na hatia dada yangu. Ngoja nikusimulie kidogo ilivyokuwa. Wakati nipo chuo nilienda hospitali na kufanyiwa operesheni kile kinyama kikatolewa. Nimeogopa kulala na mwanaume yeyote tangia kipindi kile, ni kweli wakati nipo chuo nilifatwa na vijana wengi sana ila kuna kitu nilifanya ambacho kimekuwa ni doa kwangu hadi leo"
"Kitu gani hicho mdogo wangu?"
"Pale chuoni nilijitangazia kuwa nimeathirika kwa virusi vya ukimwi kwahiyo watu wote waliosoma pale wanajua mimi nimeathirika na kufanya vijana wengi wanikwepe kama ukoma"
Sakina alimsikiliza sana Sabrina na kumuonea huruma kwa tatizo lake,
"Sasa itakuwaje kwa kijana Sam?"
"Sijui kwakweli ila nampenda, najua Mungu atanisaidia kwa hili. Hata hivyo Sam ni kijana mwenye pesa labda ataweza kunipeleka mahali pazuri kuweza kutibiwa"
Wakaongea mengi sana, mwisho wa  siku Sabrina akamuaga Sakina na kuondoka kisha akapita nyumbani kwao na kumuaga mama yake ili kuianza safari ya kurudi kwake,
"Ila mbona muda umeenda sana mwanangu! Leo si ungelala hapa hapa tu jamani"
"Acha tu nirudi kwangu mama, hata usijali kitu"
Joy akambembeleza mwanaye ila ikashindikana na kuamua kumpa tu ruhusa ya kuondoka halafu Sabrina akaondoka na kwenda nyumbani kwake.

Alipofika muda ulikuwa umeenda sana, Jeff alimfungulia mlango Sabrina
"Mbona leo umechelewa sana mamy?"
Sabrina akamueleza alikopita baada ya kutoka kazini, na kwenda kukaa kwenye kochi. Kisha akamwambia,
"Mama yako leo kanichekesha sana, eti amekuotea wewe umemuoa mtu mzima basi akachukiaje huyo"
Sabrina aliongea hayo huku akicheka na kumfanya Jeff naye atabasamu na kumuuliza,
"Kwani kuna ubaya gani mi nikimuoa mtu aliyenizidi umri ikiwa nampenda?"
"Weee usitake kumuua mama yako kwa presha, hataki kabisa kusikia huo upuuzi"
"Kwani kuna ubaya gani mamy? Mbona kuna wanaume wazee kabisa na wanaoa mabinti wadogo! Kwani mi nikioa mtu mkubwa kuna ubaya gani jamani!"
"Kwamaana hiyo ndio unanihakikishia hapa kuwa ndoto ya mama yako ni ya kweli, na wewe umepata sugar mamy! Eeh hebu niambie vizuri nikuelewe Jeff"
Jeff alimuangalia Sabrina na kutamani kumwambia ukweli ila akasita na kubakiwa na kigugumizi, wakati huo Sabrina nae aliendelea kumdadisi
"Niambie mwanangu, mi ndio msiri wako jamani. Au kuna mwingine?"
"Hakuna mwingine zaidi yako mamy"
"Basi niambie ukweli toto yangu jamani"
Jeff akatabasamu tu na kumuangalia Sabrina kisha akambadilishia mada
"Nikuwekee chakula mamy?"
"Najua unaipotezea mada tu huna lolote"
Sabrina akainuka na kwenda chumbani kwake kwaajili ya kupumzika.

Kesho yake Sabrina akajiandaa kwaajili ya kwenda kazini, na alipofika kazini akakutana na barua kwenye meza yake na kushangaa kuwa ile barua kawekewa   ya nini.
Akakaa kwenye kiti na kuifungua, akashangaa kukuta barua ikiwa imeandikwa kuwa amesimamishwa kazi kwa muda usiojulikana
"Mungu wangu, hivi wananifanyia yote haya sababu Sam hayupo au ni nini? Mbona haya kwangu ni mambo ya ajabu jamani!"
Sabrina hakutaka kubishana na mtu kwa muda huo kwahiyo akabeba mkoba wake na kuondoka huku kichwa chake kikiwa kimejaa mawazo.

Jeff akiwa nyumbani kwa Sabrina, alitawaliwa na wazo moja tu, wazo la kutaka kumwambia Sabrina ukweli ila hakujua ni kwa jinsi gani ataweza kumwambia ukweli huo.
Wakati Jeff akiwaza hayo akashangaa kumuona Sabrina amerudi nyumbani kwa muda wa mapema kiasi kile.
"Mbona leo mapema mamy?"
"Ofisini kwetu kimenuka, yote hii sababu Sam hayupo tu"
Jeff akamuangalia Sabrina alivyokuwa akilalamika hadi pale alipoenda kukaa.
"Ila mamy, mi nina ujumbe wako"
"Ujumbe gani huo?"
"Nakupenda sana, tena sana"
Sabrina akamuangalia Jeff na kucheka.

Itaendelea



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa