JE HAYA NI MAPENZI!! 31: - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Monday, February 17, 2020

JE HAYA NI MAPENZI!! 31:






Jeff akainuka na kuzunguka nyuma ya Sabrina,
kisha akamuinamia pale alipokuwa amekaa na
kuinua mkono wake kwa lengo la kutaka kumtoa
Sabrina ule uchafu.
Ila gafla akajikuta akikilaza kichwa chake kwenye
shingo ya Sabrina, wakati Sabrina akitahamaki
hilo alimuona Sam akiwa mbele yao.
Sam akamwita Sabrina kwa nguvu na kwa mshangao,
"Sabrina!!"
Jeff akashtuka na kuinuka kwenye bega la Sabrina, wakati huo Sabrina nae alikuwa kama akijipukuta kwenye nguo yake ili kuweza kukipoteza kile kilichotokea.
Kisha Sabrina akainuka na kumfata Sam alipo ambapo Sam alimvuta mkono Sabrina na kutoka naye nje,
"Unaweza kuniambia chochote?"
"Chochote kuhusu nini? Na mbona umepaniki hivyo?"
"Unajua Sabrina mi simuelewi huyu mtoto unayeishi naye humo ndani! Ni kitu gani kinaendelea kati yenu?"
"Unamaana gani Sam?"
"Sio nina maana gani, nataka kujua kinachoendelea kati yako na huyo kijana wako hapo ndani"
"Kwani wewe unaona nini kinaendelea?"
"Sijawaelewa kwakweli, mnakaa kama wa...."
Sabrina akaingilia kati yale maneno tena hata kabla Sam hajamaliza kusema,
"Naona unataka kunivunjia heshima Sam, inamaana hujui kuwa Jeff ni nani yangu hadi uanze kunihisi vibaya!!"
Sam alikaa kimya akimuangalia Sabrina tu anavyoongea kwa hasisa huku Sabrina naye akiongea kwa ukali kuonyesha kama amekerwa na jinsi alivyohisiwa vibaya na Sam.
"Kwakweli Sam sijapenda ulivyonihisi vibaya"
"Basi yaishe Sabrina, acha kupaniki ila nakuomba uwe makini"
"Makini na nini? Unataka kunivuruga tu"
"Usivurugike,  ila ipo siku utayakumbuka maneno yangu"
"Ila kiukweli hata sikuelewi Sam, yule Jeff ni kama mwanangu tafadhari usinihisi nae vibaya"
"Ok, yaishe basi"
Sabrina akaamua kuweka mazungumzo mengine ili waweze kukatisha yale ya awali.

Muda wote Jeff alikuwa dirishani akiwachungulia Sabrina na Sam huku akitamani kurudisha wakati nyuma na kufanya kama vile Sam hakutokea ni nini kingeendelea na je Sabrina angechukua hatua gani.
Alijikuta akiwaza sana, mara nyingine alijilaumu ila moyo wake ndio uliomsumbua na kumfanya afanye vitu bila ya kufikiria.
Akawaangalia Sam na Sabrina, akawaona wakikumbatiana na kuagana  kisha akamuona Sabrina akija maeneo ya kuingia ndani.
Jeff akatoka pale dirishani na kuingia chumbani kwake.

Sabrina alipoingia ndani akajua kuwa Jeff ameshalala, akamuita
"Jeff, wee Jeff wee hebu njoo"
Jeff akatoka kama mtu aliyetoka kulala kweli,
"Yani muda huu umeshalala!"
"Usingizi huo mamdogo"
"Sasa utoto wako uache, utakosa baba wadogo shauri yako"
Kisha Sabrina akaelekea chumbani kwake na kumuacha Jeff akiwa kasimama huku akimuangalia tu, huku akijiuliza moyoni,
"Eti nitakosa baba wadogo mmmh! Inamaana wapo wengi!!"
Kisha akaenda chumbani kwake.

Sabrina alikaa kitandani kwake na kuanza kujiuliza kuhusu Sam kuwa anampenda kweli au hampendi
"Mbona simuelewi jamani!Huyu Sam ananipenda mimi au kuna mtu anayempenda? Na kama hanipendi usiku huu alikuja kufanya nini kwangu? Eti kunisalimia tu mmmh! Na kama ananipenda mbona hajaniambia sasa? Kwanini inakuwa hivi!"
Sabrina alijifikiria sana bila ya jibu la aina yoyote ile.
Akaamua kulala ila bado wazo moja likamjia kichwani na kumfanya kujiuliza swali,
"Kwani Jeff alikuwa na maana gani kunishika vile mpaka Sam kutuona na kuchukia? Ila mi sijaona kama kuna tatizo sababu Jeff ni kama mtoto wangu tu"
Alijiuliza maswali ambayo alijijibu mwenyewe, wakati akiendelea kujiuliza, simu yake ikaita.
Kuangalia ilikuwa ni namba ngeni, kuipokea tu ikakatika pale pale na kumfanya Sabrina ajiulize kuwa ni nani alikuwa akimpigia.
Alipojaribisha tena ile namba ilikuwa haipatikani, ikabidi Sabrina aachane nayo na kuamua kuendelea na mambo mengine kwenye simu yake.
Moja kwa moja akaingia kwenye mtandao wa kijamii, facebook na kukutana na jumbe zaidi ya kumi toka kwa Prince J, Sabrina akatabasamu na kuzifungua kisha naye akamtumia ujumbe Prince J kama kumshtua hivi.
Ila leo ilikuwa tofauti na siku zote kwani Sabrina alishangaa kutokujibiwa ujumbe wake na kuhisi kuwa Prince J amechukia kwani alimuona hewani ila hakujibiwa kitu.
Sabrina akajikuta akimuandikia Prince J,
"Naomba namba yako tafadhari"
Sabrina akautuma ujumbe huo, na muda huo huo akajibiwa na Prince J
"Unahitaji kweli namba zangu?"
"Yeah, mbona jumbe zangu za kwanza hujazijibu?"
"Ulinikera Sabrina"
"Kukukera nini kwani? Mbona sikuelewi!"
"Kwani mi siwezi kuwa mume wako?"
Sabrina akakaa kimya na kuuliza,
"Kivipi na kwanini?"
"Nijibu kwanza, je siwezi kuwa mume wako?"
Sabrina akakaa kimya, kisha Prince J akatuma ujumbe mwingine
"Nakupenda Sabrina, unavyonikalia kimya unaniumiza sana"
"Pole"
"Pole haisaidii"
"Nini sasa itasaidia?"
"Kuonana na wewe ndio itasaidia"
Sabrina akatulia kwanza na kujiuliza kama ataweza kuonana nae, ila alipofikiria sana akaona ni vyema kama ataweza kuonana na huyu Prince J ili awe na uamuzi mzuri juu yake.
Sabrina akaamua kumpa Prince J namba yake ili aweze kumtafuta kwa muda wake wa ziada na kupanga naye ni wapi wataweza kuonana na ni lini siku yenyewe.
Kisha Sabrina akamuaga Prince J na kulala.

Kesho yake asubuhi na mapema, Sabrina akashtuliwa na mlio wa simu yake.
Kuangalia mpigaji alikuwa ni Sam,
"Tafadhari Sabrina nakuomba leo tutoke"
"Sawa haina tatizo"
Kisha Sabrina akakata ile simu na kuanza kujilalamisha,
"Yani huyu Sam hana cha weekend wala nini, hajui hata kama leo ni Jumapili natakiwa kupumzika yani yeye asubuhi asubuhi kunipigia simu eti nakuomba tutoke. Dah! Ana bahati sana nampenda lasivyo ningekuwa namkatalia, kunitongoza kwenyewe hanitongozi yani mwanaume huyu loh"
Ikabidi Sabrina ainuke tu kitandani na kwenda kuoga ili aweze kujiandaa mapema.

Alipotoka sebleni akamkuta Jeff akiandaa chai, na kumuuliza
"Mbona mapema sana mamdogo wakati leo Jumapili?"
"Namngoja Sam, kasema twende tukatembee"
"Mmmh!"
"Nini sasa unaguna?"
"Umtambulishe kabisa basi kwangu mamy"
" Nenda zako na wewe, nimtambulishe nini"
Sabrina akaona kuwa Jeff anamletea mada zisizokuwa na msingi kwa wakati huo.
Alipokaa muda kidogo Sam akawasili, wakasalimiana tena na kutoka.
Jeff akawaangalia tu huku moyo wake ukimuuma.

Sabrina na Sam wakiwa njiani, wakamuona Joy ambaye ni ndugu wa Sam akiwa ameongozana na rafiki yake.
Ikabidi Sam asimamishe gari kuwasalimia.
Sam na Sabrina wakashuka na kuwasimamisha Joy na rafiki yake, kisha wakasalimiana halafu Joy akamtambulisha rafiki yake kwa Sam,
"Huyu ndio yule rafiki yangu uliyekuwa ukimsikiaga nikimtaja, anaitwa Agness"
"Aaah! Kumbe Agness ndio wewe, nashukuru sana kukufahamu"
Kisha wakapeana mikono, ila Agness naye akasema
"Usijali Sam, mi nakufahamu kitambo sana"
Wakaendelea kufurahiana, muda wote huo Sabrina alikuwa kimya tu ila yule Agness alimuangalia Sabrina na kumuuliza,
"Wewe sio Sabrina kweli?"
Sabrina akashangaa na kujiuliza kuwa huyu dada amemfahamia wapi,
"Ndio ni mimi, kuna mahali umewahi kuniona?"
"Nahisi ila sikumbuki ni wapi, lakini ni vyema kufahamiana nafurahi kukuona"
"Nafurahi pia"
Kisha Sam na Sabrina wakawaaga Joy na rafiki yake na kupanda gari na kuondoka.
Ndani ya gari Sabrina akamuuliza Sam,
"Kwani yule mtoto wa mjomba wako yule Joy anafanya kazi gani?"
"Mwalimu yule, tena ni mwalimu mzuri sana. Hutoa pia ushauri nasaha kwa wanafunzi"
"Basi ni vizuri, nimemuona amechangamka sana. Yani alinifahamu kwa siku moja tu ila ameshanizoea"
"Ni mwepesi sana kuzoea watu yule ila ukikaa nae hutaipenda tabia yake moja tu"
"Tabia gani hiyo?"
"Ni mmbea sana, na marafiki zake wote wambea kwahiyo ni wakumzoea tu"
Sabrina akacheka na kuendelea na maongezi mengine huku safari yao ikiendelea.

Joy na rafiki yake Agness wakajikuta wakiwajadili Sabrina na Sam, alianza Agness kwa kumuuliza Joy
"Kwani yule Sabrina ndio mwanamke wa Sam?"
"Nahisi maana kila sehemu wako wote. Kwanza niambie yule Sabrina umemjulia wapi?"
"Mmh shoga yangu, kama kaka yako ana mahusiano na yule binti basi kaumia"
"Kheee! Kaumia! Kivipi?"
"Yule binti si amesoma nje yule!!"
"Ndio, niambie vizuri basi ameumia kivipi?"
"Yule binti ni muathirika shoga yangu, chuo alichokuwa anasoma wote wanamjua"
"Mmh! Wewe umepata wapi hiyo khabari wakati nje hujawahi kwenda? Mipakani tu hujawahi kufika lakini eti una khabari ya chuo alichosoma Sabrina mmh!"
"Umbea si kazi shoga yangu, kazi ni kusutwa. Kuna mtu ana picha za huyo Sabrina na ndiye aliyenipa khabari zake. Usimuone na uzuri huo ni mgonjwa huyo."
Joy akaishia kushangaa na kumsikitikia kaka yake kuwa ameangamia.

Sam alimpeleka Sabrina kwenye hoteli ambayo ilikuwa ufukweni ili waweze kupumzika hapo.
Sabrina alitulia huku akiamini kuwa leo ameletwa huku na Sam ili kumwambia anavyompenda, wakati wanazungumza simu ya Sabrina ikaita.
Kuangalia mpigaji alikuwa ni Sakina, na kumfanya Sabrina apokee kwa tabasamu
"Jamani mdogo wangu nimekukumbuka sana"
"Usijali dada, nitakuja kukutembelea"
"Vipi huyo mwanangu naye hajambo? Hebu mwambie aje anitembelee mama yake"
"Sawa dada, ngoja nimwambie"
Sabrina akakata simu na kutaka kumpigia Jeff ila kabla hajapiga Sam akamkatisha na kumuuliza,
"Unataka kumpigia nani?"
"Nampigia Jeff ili umwambie nini?"
"Nimwambie kama mama yake kamkumbuka na anamtaka aende kwao kumsalimia"
"Tena umwambie akakae huko huko kwao"
Sabrina akacheka na kumpigia simu Jeff na kumwambia kuhusu kwenda kwao kusalimia, urahi sana,
"Kwakweli nafurahi kuonana na wewe, ila naomba nikutafute ili tuweze kuongea vizuri zaidi"
"Usijali Jeff, wee nitafute tu"
Kisha akaagana nae , na kuondoka zake.
Alipoondoka tu, akafika rafiki wa mwalimu yule
"Nani yule ulikuwa unaongea naye hapo?"
"Anaitwa Jeff, ni mwanafunzi wangu. Nilikuwa mwalimu wake kipindi anasoma"
"Ni kazuri hako"
"Mmh na wewe kwa kupenda watoto hujambo, hebu acha mambo yako. Yule ni kijana mdogo sana, yani urefu tu ule unamzuzua"
"Hata kama, ila ni mzuri acha nimpe sifa yake. Mabinti walikuwa hawajigongi kwake kweli!"
"Yule kijana katulia sana yani huwezi amini, mabinti wengi alikuwa akiwapotezea"
Walijikuta wakimjadili tu Jeff kwa muda huo, hata Sam hakukosea kusema kama wanatabia ya umbea kwani hawa walikuwa ni Joy na mwenzie Agness.

Jeff alipofika kwao alimkuta mama yake akiwa ametulia kabisa na kumsalimia kisha kuongea nae mawili matatu.
"Mwanangu, kale kabinti kazuri kale kanakokupendaga kalikuja hapa jana"
"Nani huyo?"
"Yule Zuwena mwanangu"
"Mi hata simtaki mama"
"Kwanini sasa mwanangu? Yule binti ni mzuri sana tena ana heshima zake, tafadhari mwanangu usikatae bahati ya kuwa naye"
"Sasa mi simpendi, nitakuwaje naye sasa? Yupo mwanamke ninayempenda mama"
"Nani huyo? Ni mwanamke gani huyo? Kuwa makini mwanangu, magonjwa ni mengi ila Zuwena ni binti mzuri kwako"
"Jamani mama, simpendi huyo Zuwena kwakweli. Nampenda....."
"Nani huyo? Mtaje"
"Nitakutajia tu usijali, ila leo naenda kuonana nae. Kwahiyo badae nitaondoka"
"Mmh sikuwezi wewe mtoto"
Sakina alitamani kujua mwanamke ambaye anapendwa na mtoto wake ila hakufanikiwa kumjua.

Sam na Sabrina wakaendelea na maongezi, Sabrina akamuomba Sam simu yake na kuingia nayo kwenye mtandao wa kijamii ili kuona kama kuna ujumbe wowote aliotumiwa ila hakukuta ujumbe wowote ule, akajisemea kimoyo moyo
"Mmh leo Prince J hata hajanikumbuka"
Kisha akamrudishia Sam simu yake, wakaendelea kuongea na kuagana.
Sam akamrudisha Sabrina nyumbani kwake.

Sabrina alipokuwa nyumbani kwake akaamua kuingia tena kwenye mtandao wa kijamii, moja kwa moja akakutana na ujumbe kutoka kwa Prince J
"Tafadhari naomba tuonane leo mpenzi"
Sabrina hakuwa na pingamizi kabisa kwavile alihitaji kumfahamu kwa sura na kumjua ni nani.
Kwahiyo akapanga naye muda wa kuonana.

Muda ulipofika Sabrina alijiandaa ili kwenda kuonana na Prince J.
Alipofika eneo la tukio, akaangaza macho ili aweze kumuona Prince J.
Macho yake yakagongana na watu wawili mbele yake, Sam na Jeff.

Itaendelea



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa