JE HAYA NI MAPENZI!! 16: - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Sunday, February 16, 2020

JE HAYA NI MAPENZI!! 16:





Sabrina alishtuka kwani mama yake alikuwa
kamavile mtu aliyewehuka na alipomuona tu
Sabrina, akaacha kusema na kuanguka chini huku
akitapatapa.
Sabrina akashtuka zaidi na uoga kumjaa, akaanza kupiga makelele na yeye ili aweze kupata msaada zaidi ila mwisho wa siku akagundua kuwa kelele zake hazisaidii kitu kwani atajaza watu bure tu.
Akaona njiabora ni kwenda kwa yule mmama wa njiani aliyemkimbia ili akamuombe msaada kwani hakujielewa kitu.

Akamuangalia Francis na kumuomba abakie pale na mama yake ili yeye akachukue msaada
"Sabrina, sasa utaondokaje na kumuacha mama yako katika hali kama hii?"
"Ningoje tu Francis, acha niende kwani nimfataye ndio uzima wa mama yangu"
Kisha akatoka nje na kujaribu kukimbia ili aweze kuwahi lile eneo ambalo alikutana na yule mmama.
Sabrina alikuwa anahema sana na giza nalo lilishaanza kuingia ila Sabrina hakuacha kukimbilia eneo la tukio ili aweze kuwahi.

Alipofika lile eneo, akauona ule mbuyu ila hakuona vitambaa vile alivyoviona jana yake.
Akajihisi kuchanganyikiwa, akakaa chini ya ule mbuyu huku akili yake ikikosa muelekeo.
Akiwa amejiinamia vile, akapita mtu mmoja na kumshika kichwa Sabrina, kisha Sabrina akainua kichwa na kumuangalia mtu huyo ni nani.
Alikutana na mzee wa makamo aliyekuwa amevaa nguo ndefu mpaka chini aina ya kanzu na kikofia kidogo kichwani.
Yule mzee akamuuliza "Unafanya nini hapo na giza hili binti?"
"Kuna kitu nangoja"
"Unangoja nini? Mashetani au?"
"Kuna mtu namngoja"
"Unamngoja mtu chini ya mbuyu binti yangu? Hivi unajua kama mibuyu ni nyumba za majini?"
Sabrina akashtuka sana kusikia ni nyumba za majini na kuanza kuogopa.
Yule mzee akamwambia tena Sabrina,
"Mtumainie mwenyezi Mungu, hayo mambo ya kukaa chini ya mibuyu hayatakusaidia"
Kisha yule mzee akaondoka na kumfanya Sabrina ainuke kwenye eneo lile alilokuwa amekaa.

Sabrina akaanza kuondoka taratibu huku akiangalia lile eneo labda apate kumuona tena yule mmama ili aweze kupata msaada.
Akafika mbele na kusimama huku macho yake yakiwa katika eneo lile la mbuyu na akiamini kuwa yule mmama atatokea kumpa msaada.
Wakati amesimama vile, ni kweli yule mmama akatokea ila alikuwa amekasirika sana, lakini Sabrina alishukuru huku akiamini kuwa mama yake atakuwa mzima.

Sabrina akaanza kumfata yule mmama, ila yule mmama alianza kuongea kwa hasira sana,
"Mmeniudhi sana nyumbani kwenu nyie"
Sabrina alimuangalia tu yule mmama kwani hakuelewa ni kitu gani kingendelea
"Nakwambia kwenu mmeniudhi sana, rudi nyumbani kwenu na ukawazuie yote wanayoyafanya"
"Kwani ni nini?"
"Tena uwazuie uwezavyo lasivyo mimi nammaliza mama yako"
Sabrina akaogopa sana kwani hakujua ni kitu gani kinaendelea nyumbani kwao.
Akiwa bado amesimama kwa kusitasita, yule mmama akampazia sauti
"Nammaliza mama yako, nenda wee mwanakwenda"
Ile kauli ya nammaliza mama yako ikamtisha zaidi Sabrina na kumfanya Sabrina apige magoti kwa yule mmama na kuanza kumuomba kuwa asimdhuru mama yake
"Hivi wewe mtoto una akili kweli? Watakaomdhuru mama yako ni hao waliopo nyumbani kwenu, nenda ukawazuie ili mama yako nimuachie lasivyo nammaliza leo leo"
Sabrina aliwaza kuwa ni watu gani hao wanaozuia uponyaji wa mama yake na kuamua kuanza kukimbilia maeneo ya nyumbani kwao ili akawawahi watu hao na kuwazuia ila hakujua kuwa ni watu wa aina gani.

Wakati Sabrina ameondoka kwaajili ya kumfata yule mmama kule kwenye mbuyu, huku nyumbani kwao alifika yule mchungaji ambaye alipigiwa simu asubuhi ili aweze kuja kuongea na Sabrina.
Na muda huo, Francis nae alikuwa amempigia simu mchungaji aliyekuwa anamfahamu na kuomba afike eneo hilo. Kwahiyo wale wachungaji walijikuta wamefika wote wawili kwa muda mmoja, na kwavile hali ya Joy ilikuwa mbaya waliamua kuingia kwenye maombi moja kwa moja na kuanza kukemea roho ya mapepo wakati huo Joy alikuwa hajitambui kabisa, kwani alikuwa akitapatata tu huku na kule.
Ila kadri walivyokuwa wakiomba ilionyesha Joy akipatwa na unafuu fulani.

Sabrina alipofika nyumbani kwao aliwakuta wale wachungaji wakiendelea kufanya maombi, moja kwa moja alienda kati yao na kuanza kuwazuia
"Muacheni mama yangu, hakuna anayehitaji maombi hapa"
Ila wale wachungaji waligundua wazi kuwa Sabrina anaendeshwa na mapepo kwahiyo sio akili yake inayomfanya awazuie na kufanya wazidi kufanya maombi.
Francis alibaki kushangaa kuwa kwanini Sabrina amekuwa vile na kumfata pale alipokuwa akiwazuia wale wachungaji, ila Sabrina hakuelewa wala kusikia na kumfanya apatwe na wazo lingine la kwenda kumuita yule mmama tena.
Sabrina akatoka pale kama chizi kwani alikuwa akikimbia na kumfanya Francis atake kumkimbiza ili aweze kumrudisha lakini wale wachungaji walimzuia Francis na kumwambia
"Mwache tu atarudi, Mungu ni mwaminifu"
Francis alimuacha Sabrina huku roho ikimuuma sana.
Ila wale wachungaji waliendelea na maombi ya kumuombea Joy.

Sabrina alipokaribia kufika alipokuwa anakimbilia, aliona giza zito sana yani giza ambalo huwezi hata kuona chochote kile na kumfanya aanze kuogopa.
Kisha akasikia sauti ikimkaripia kwa nguvu,
"Toka Sabrina tokaaaaaa.... Na kamwe hutokuja kupata mtoto kamwe katika maisha yako, na kila mwanaume utakayelala nae lazima afe na wewe upate kesi ya mauaji. Tokaaa Sabrinaaa....!"
Ile sauti ya mwisho ikagongana na mwangwi na kumfanya Sabrina aogope zaidi.
Ila alipiga magoti eneo lile huku machozi yakimtoka kamavile anaomba kupunguziwa ile adhabu kwani ilikuwa ni kubwa sana.
Ile sauti ikasema tena,
"Na mama yako lazima nimmalize na ba......"
Kabla hajamalizia kusema, mara ukimya ukatanda na gafla ilisikika ile sauti ikipiga ukelele wa nguvu,
"Aaaaaaaaaaaaaahhhhh.........!!!!!"
Na ikakatika gafla na kumfanya Sabrina ashtuke pale alipopiga
 magoti na kuanza kuangaza macho yake ambapo yalikutana na mwanga mkali wa ajabu na kumfanya ashindwe kustahimili kuuangalia kwani alihisi ule mwanga ukimchoma choma.
Sabrina alipata nguvu ya ajabu na kuanza kukimbia huku akielekea kwao, ila kila alipokimbia ule mwanga ulizidi kumfata.

Alipofika kwao alikuwa anahema sana na moja kwa moja akaanguka mlangoni na kuzimia.
Wakambeba na kumuingiza ndani kwani hali yake haikuwa sawa, na muda huo mama yake alikuwa mzima kabisa huku akisimulia aliyokuwa akiyaona wakati ule aliokuwa akitapatapa.
Francis alikuwepo muda wote akisikiliza yaliyojiri ila walimshukuru sana Mungu kwa kuwasaidia kwa hilo na kwa kuweza kumponya mama huyo.
Ingawa muda ulikuwa umekwenda ila hakutamani kuondoka na kumuacha Sabrina akiwa amezimia vile.
Wale wachungaji walimuhakikishia kuwa hapatakuwa na tatizo lolote kwani Mungu amewakomboa tayari.
"Hapana, mi nitakuwa nao hapa hadi kesho ili niendelee kuona hali zao kwani hapa walipo wapo wenyewe"
Basi wakakubaliana na Francis kisha wale wachungaji wakaaga na kuondoka na kuahidi kuendelea kufanya maombi hata watakapokuwa makwao.

Francis alisaidiana na Joy kumkokota Sabrina na kumpeleka chumbani kwake ili akapumzike kwani wameambiwa kuwa ataamka mwenyewe tu muda ukifika kwahiyo wasiwe na wasiwasi.
Kisha Francis akaenda kulala sebleni.

Kulipokucha, Sabrina aliamka akiwa amechoka sana hata asielewe kilichokuwa kimetokea.
Alijiona akiwa na uchovu mwili mzima, hivyobasi akaenda kuoga na huko ndipo alipokumbuka swala la kamba yake ya kiunoni na kumfanya ajiulize maswali,
"Kamba yangu iko wapi? Inamaana imeyeyuka au ni kitu gani?"
Ni wazi Sabrina alijihisi kusahau kila kitu kilichomtokea.
Alipotoka kuoga, alienda na kukaa kitandani kwake huku akitafakari na kukosa jibu.
Akavaa na kwenda sebleni kwao, alishangaa kumuona Francis pale kwao na kumuuliza kwa mshangao,
"Francis, asubuhi yote hii unafanya nini hapa kwetu?"
"Khee, Sabrina kwanza niambie unaendeleaje?"
"Naendelea vizuri, kwani nilikuwa naumwa?"
Mama yake nae akatoka ndani na kumfanya Francis aage kwani usiku ulishapita na tayari palishakucha.
"Mama, mimi naenda ila kama kutatokea tatizo lolote msisite kunipigia simu na badae nitakuja kuwatembelea tena"
"Asante sana mwanangu, umetusaidia sana hapa. Mungu akubariki"
Kisha akaaga na kuondoka, na kumfanya Sabrina azidi kupatwa na maswali kuwa ukaribu wa hivyo wa Francis na mama yake umetoka wapi? Ila hakuwa na kumbukumbu kabisa kwa yaliyotokea siku ya jana.
Katika akili yake alijua wa kumpa majibu yote ni Sakina tu, hivyo akataka kwenda kwa Sakina.
Mama yake alikuwa akiingia chumbani kwake na kwake na kumwambia Sabrina,
"Nisubiri hapo mwanangu nikupe ushuhuda"
Kisha akaingia chumbani ila Sabrina hakutaka kujua hizo khabari za ushuhuda, kwani alichotaka kujua kwa wakati huo ni juu ya kamba yake ya kiunoni kuwa imekwenda wapi.
Pale pale aliinuka na kufanya safari ya kwenda nyumbani kawa Sakina.

Alimkuta Sakina akiwa amelala kwenye kochi ndani kwake, tena alionekana kuwa ni mtu aliyechoka sana.
Kisha Sabrina akamuamsha Sakina na kumfanya ashtuke sana kutoka kwenye ule usingizi.
"Utaniua kwa presha Sabrina, mambo gani hayo ya kushtuana kiasi hicho?"
"Sio hivyo dada ila nimepatwa na maajabu"
"Maajabu gani hayo?"
"Ile kamba yangu ya kiunoni imeyeyuka"
"Imeyeyuka! Kivipi?"
"Leo nimeamka asubuhi sijaikuta kwenye kiuno changu"
"Hebu acha uwehu Sabrina, wakati ile kamba jana ulikatwa na mama yako"
Sabrina akashtuka sana na kumfanya Sakina amkumbushe jinsi ilivyokuwa na kumfanya Sabrina akumbuke kila tukio ambalo lilitokea siku ya jana na kumfanya atetemeke,
"Hivi nilikuwa ni mimi au ni nani?"
"Mbona sikuelewi Sabrina?"
Ilikuwa ngumu kwa Sakina kumuelewa Sabrina kwavile matukio mengine hakujua kama yalitokea.
Sabrina aliinuka na kumwambia Sakina,
"Ngoja nikamuulize mama vizuri kama atakuwa na kumbukumbu na kuweza kunieleza"
"Hebu ningoje twende wote"
Sakina nae aliinuka akiwa na hamu ya kujua kwani hakumuelewa Sabrina hata kidogo.

Walimkuta Joy akiwa ametulia huku akisikiliza nyimbo tu.
"Yani hapa mtoto kweli sina, sikuamini kama nikitoka ndani sitakukuta mwanangu!"
"Nisamehe mama, ila kuna mambo ambayo yalinichanganya ndiomana"
Kisha akasalimiana na Sakina huku Sakina akiwa na hamu ya kujua kuwa ni mambo gani yalitokea.
Joy aliamua kuwapa ushuhuda wake juu ya mambo ambayo yalimtokea kwa siku ya jana.
"Unajua kile kitendo cha mimi kuona kamba kwenye kiuno cha mwanangu kilinisikitisha sana na ndiomana nilipatwa na hasira na kuikata, ninachoshukuru ni kuwa baada ya tukio hilo nikapata wazo la kuwapigia simu watu wa Mungu"
Sabrina akdakia kabla hata mama yake hajamaliza,
"Na ndio hapo ulipoharibu mama"
"Sijaharibu chochote, hujui tu ni jinsi gani wameifanya kazi kubwa hapa sababu ya hayo mashetani yako."
Hapo Sakina na Sabrina walitulia kumsikiliza ataongea vitu gani, Sabrina akashangaa kuona mama yake akimsimulia mambo aliyokuwa  akikumbana nayo kule kwenye mbuyu, kumbe mama yake alikuwa akiyaona yote wakati ameanguka na kutapatapa,
"Ile kamba ilikuwa inakupa mwanangu uwezo wa kuwaona wachawi na kumbe ilitaka pia uwe mchawi, kule kwenye mbuyu ambako ulikimbia mara ya kwanza, walitaka wakupe uchawi ila machale yakakucheza mwanzoni na kukimbia. Ila uliponikuta mimi nikihangaika ndipo ujinga wa kwenda kumsujudia pepo ulipokupata mwanangu na kusahau kuwa Mungu ndio kila kitu"
Joy pia akasimulia jinsi Francis alivyomsimulia kwa hali aliyomkuta nayo na jinsi alivyowasiliana na yule mchungaji mwingine.
Sabrina akamuuliza mama yake,
 "Inamaana Francis anajua kila kitu?"
"Ndio anajua, na yeye amesaidia kumuita mchungaji"
"Mmmh huyo Francis bibi yake ni mkubwa wa wachawi, eti leo ndio amekuitia mchungaji mama mmh!"
"Hata kama bibi yake ni mchawi wa kuzimu, kumbuka yeye yupo tofauti"
Kwa upande mwingine Sabrina alijisikia vibaya kwani akiyafikiria mambo aliyoyafanya jana na kuambiwa kuwa Francis alikuwepo alijionea aibu sana na kuhisi kamavile Francis atakuwa akimfikiria vibaya.
Joy alifanya kazi ya ziada ya kumtaka Sabrina na Sakina wamtumainie Mungu kwani aliona wazi kuwa wanaamini ushirikina zaidi ya Mungu.
"Mungu amekuokoa mwanangu, unatakiwa uanze kufanya ibada sasa"
Sabrina alikubaliana na mama yake nusu nusu kwani kwa fikra zake alihisi kuwa yale mambo yatajirudia tu.

Jioni ya siku hiyo, Sabrina akapigiwa simu tena na Japhet.
"Kuniweka jana ndio nini?"
"Naomba unisamehe tafadhari"
"Basi naomba leo nije nikufate hapo kwenu, kuna mahali ningependa twende wote"
Sabrina akakubali na kukata simu, kisha akaanza kujiandaa kwaajili ya hiyo safari.

Alipomaliza tu kujiandaa, akasikia mtu akibisha hodi pale kwao. Moja kwa moja akahisi ni huyo Japhet kaja kumpitia, ila alipoto kufungua alimkuta Francis na Fredy, hakuwa na cha kufanya zaidi ya kuwakaribisha tu.
Ile wanaingia ndani tu, Japhet naye akawasili.

Itaendelea



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa