JE HAYA NI MAPENZI!! 15: - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Sunday, February 16, 2020

JE HAYA NI MAPENZI!! 15:





Akamfata karibu, kisha akachukua mkasi
uliokuwepo kwenye meza ya Sabrina na kuikata
ile kamba.
Sabrina akapigwa na butwaa kwani kilikuwa ni kitendo cha gafla kwa mama yake kuikata ile kamba.
Alitamani apige makelele kwa kulia kwani aliona mambo yake yote yakiharibika, hakutegemea kama mama yake angefanya vile alivyofanya.
Sabrina alikaa chini huku machozi yakimtoka
"Yani unalia sababu ya hii kamba Sabrina? Mbona unaniletea mambo ya ajabu wewe mtoto jamani!"
Sabrina alikuwa kimya kabisa huku machozi yakimtoka, ila Joy hakujua ni kwanini mtoto wake alikuwa akitokwa na machozi kiasi kile, hakujua kama ile kamba ilikuwa na maana kubwa sana kwenye kiuno cha mwanae.
"Sabrina, hivi wewe mtoto una kichaa au ni kitu gani jamani? Unajua sikuelewi! Yani sikuelewi kabisa. Eti unalia na kulia sababu ya huo uchafu nilioukata, mtoto mwehu kweli wewe"
Joy akatoka chumbani kwa mwanae na kwenda kuendelea na kazi zake zingine.

Sakina alipoona muda unapita tu bila ya Sabrina kutokezea, akaamua kwenda kumfata mwenyewe.
Na alipofika alikaribishwa na Joy, wakasalimiana na kumuulizia Sabrina.
"Asubuhi yote hii Sabrina wa nini?"
"Kuna mahali nilipanga nae kwenda ila sijamuona hadi sasa"
"Wewe si ndio msiri wake! Nenda huko chumbani kwake ukamuangalie anavyolia lia"
Sakina akashangaa kumuona Joy akiongea kwa jazba kiasi kile, akajua kwa vyovyote vile lazima kuna kitu Joy amekijua kuhusu Sabrina.
Akaongoza moja kwa moja mpaka kwenye chumba cha Sabrina, alimkuta kajifunga khanga huku amejiinamia na machozi kumtoka.
"Nini tatizo Sabrina mdogo wangu jamani?"
Sabrina akamuonyesha Sakina ile kamba pale chini na kumfanya Sakina nae ashtuke kisha akamuuliza kuwa imekuwaje.
"Mama kaikata na mkasi"
"Ameionaje?"
Sabrina akamuelekeza Sakina ilivyokuwa
"Nilijua tu kuwa mama yako akijua itakuwa balaa kama hivi, yani mamako kaongeza tatizo juu ya tatizo hata sijui itakuwaje jamani!"
"Nisaidie dada, nitafanyaje mimi jamani!"
"Basi ngoja tufanye kitu, najua wewe haupo sawa kwasasa. Hivyobasi ngoja mimi niende mahali kuulizia vizuri kuwa tufanyaje kisha nitakwambia kila kitu mdogo wangu. Punguza mawazo, mimi nipo kukusaidia Sabrina"
"Basi nitashukuru dada"
Sakina akampooza pale Sabrina kisha akamuaga na kuondoka.
Kufika nje, akamuaga na Joy ili aende zake
"Nenda mama, ya kiunoni nimeikata. Nenda ukamletee ya shingoni sasa ili niione vizuri na nitaichoma moto"
Sakina alimuangalia tu Joy kwani alielewa wazi kama akiamua kubishana nae basi atabishana nae hadi siku ya pili.
Akamuaga tena na kuondoka.

John baada ya kusikia mkasa alioufanya mpenzi wake kwa Sabrina akajihisi vibaya na kuamua kumpigia simu Sabrina ili aweze kumuomba msamaha.
Ila ile simu iliita tu bilawake na ndiomana hakutaka kuwasiliana nae tena bila kujua kwamba Sabrina alikuwa na matatizo mengine yaliyomsumbua akili yake tayari.

Sabrina hakujisikia vizuri kabisa siku ya leo, kila alipofikiria masharti ya ile kamba ya kiunoni iliyokatwa hakujua itakuwaje. Hakujua mama yake atapatwa na janga gani baada ya kumkata ile kamba.
Alijihisi vibaya na moyo kumuuma sana kwa mawazo.
Aliisikia simu yake ikiita ila hakujisikia kuzungumza na mtu yeyote wala kumjibu ujumbe mtu yeyote kwahiyo alikuwa akiitazama tu simu yake wakati inaita.

Joy alikaa na kujifikiria sana, alihisi kuwa mwanae ana mapepo na ndiomana amekuwa akifanya mambo ya ajabu.
Akaamua kumpigia simu mchungaji wao na kumueleza matatizo ya mtoto wake.
"Nimekuelewa mama James, nadhani jioni nitafika hapo na nitapenda kuzungumza na huyo binti yako"
"Hakuna tatizo mchungaji, utamkuta tu hapa nyumbani"
"Ila kuna huduma nafanya, kwahiyo itakuwa ni jioni sana"
"Hakuna tatizo, cha muhimu ni ufike tu"
Joy akaona itakuwa afadhari kwa binti yake kuzungumza na huyo mtumishi wa Mungu, kwakuwa matendo yake yalimdhihirishia wazi kuwa mwanae ana mapepo kwani yale mambo ya kujifunga kamba za kichawi kiunoni hayakuwa ya kawaida.
"Yani mtoto wangu ni wa ajabu huyu mmh! Maombi kwake mwiko, yeye na ushirikina tu hata sijui kajifunzia wapi!"
Joy alikuwa akijilalamisha mwenyewe tu bila ya muafaka wa anachokilalamikia kwa muda huo.

Sabrina akaona kujifungia ndani ni kuzidi kujipa mawazo tu, kwahiyo akaona ni vyema hata atoke na kutembea tembea kidogo ili kupoteza mawazo mpaka pale Sakina atakaporudi.
Alitoka na kumuaga mama yake kuwa anaenda kutembea tembea kidogo
"Umepata nguvu ya kuzurulia sasa eeeh!"
"Sio hivyo mama"
"Nini sasa?"
"Siendi mbali mama, nafika hapo kwa rafiki yangu Sia tu"
"Haya wee nenda tu, naona leo hata wakina Sia wamekumbukwa ila uwahi kurudi tu"
"Sawa mama"
Sabrina akaondoka na kwenda kwa huyo rafiki yake.

Alipofika alimkuta rafiki yake na kufurahi sana, walikaa na kuongea mambo mengi sana.
"Sabrina, hivi yule kaka yangu Japhet unamjua?"
"Ndio namjua, kafanyaje kwani?"
"Jamani Sabrina, kaka yangu anakupenda yule yani kafa kaoza kwako"
"Mmh Sia ya kweli hayo!"
"Mie nitakudanganyaje wewe shoga yangu jamani! Kaka yangu anakupenda, tena anakupenda sana Sabrina"
Sabrina alijikuta akitabasamu kwa furaha kwani alikuwa na tatizo kubwa moja, yani yeye akisikia kuwa anapendwa alijihisi kama kupagawa wakati zamani alikuwa hataki hata kusikia kuhusu mapenzi ila siku hizi akiambiwa anapendwa basi anajihisi kama ni malkia pekee kwenye dunia.
Kwahiyo swala la Sia kumwambia kuwa anapendwa na kaka yake lilimfanya asahau matatizo yake kwa muda na kujisikia vizuri,
"Nimpe namba zako? Maana aliniomba mawasiliano yako ili akwambie mwenyewe"
"Mpe tu namba zangu, hakuna tatizo"
"Mmh Sabrina! Je na wewe utampenda?"
"Sijui"
Na kuanza kucheka, Sia akapata jibu kuwa lazima Sabrina nae atakuwa anampenda kaka yake huyo ila tu hakuweza kusema.
Wakaongea mengi sana, na mwisho wa siku Sabrina akaaga na kuanza safari ya kurudi kwao.

Akiwa njiani kuelekea nyumbani kwao, alipita karibu na mti wa mbuyu.
Mti ule ulikuwa umefungwa kwa pembeni kitambaa chekundu na cheusi, halafu chini yake kulikuwa na kiwembe kimoja na yai ambalo lilikuwa limechorwa chorwa kwa maandishi mekundu.
Sabrina akaogopa sana kupita na kuanza kurudi nyuma nyuma, alipofanikiwa kufika nyuma akaanza kukimbia kwa uoga kwani hakutegemea ile hali kwakweli, hakutegemea kukutana na vitu vya aina ile pale njiani.
Alipofika mbele alisimama na kuhema sana, mara akapita mmama mmoja ambaye hakuwahi kumuona yani ndio ilikuwa mara yake ya kwanza kumuona.
Yule mmama akamwambia Sabrina,
"Kilichokukimbiza ni nini wakati wewe ni jasiri!"
Sabrina akamuangalia huyu mmama bila ya kumjibu kitu chochote na kuendelea na safari yake, ila yule mmama akamuita Sabrina kwa nguvu
"Wee Sabrina!"
Sabrina akaogopa kuona huyu mama kamuita kiasi hicho, inamaana anamjua. Na kama anamjua basi anamjuaje!
Sabrina akasita kugeuka na kuendelea kutembea kwa nguvu, akaisikia sauti ya yule mmama ikisema
"Unajifanya kiburi eeh!! Utaona sasa"
Sabrina akaogopa sana na kumfanya aanze kukimbia ili aweze kupotea kwenye eneo hilo aliloona kuwa linampa maajabu tu.

Akakimbia sana na kutokea katika mitaa ya kwao, moja kwa moja alirudi nyumbani kwao na kumkuta mama yake akiwa ametulia tu
"Leo umewahi kurudi kweli!"
"Ndio mama, nimekuwa mtoto mzuri"
"Haya, mmbea mwenzio katoka hapa sasa hivi anakutafuta"
"Nani huyo mama?"
"Nani mwingine zaidi ya Sakina! Kasema uende kwake haraka uwezavyo"
Basi Sabrina alivyoambiwa hivyo hakutaka kupoteza muda na kugeuka ili aende ila kabla hajaondoka mama yake akamwambia
"Na nilijua tu baada ya ujumbe huo hutotoka hata kuingia ndani na kunywa maji tu, basi uwahi kurudi sababu kuna mtu wa muhimu sana anakuja leo kuzungumza na wewe"
"Sawa mama"
Sabrina alimuitikia mama yake ila bado alikuwa na kinyongo kikubwa sana dhidi yake kutokana na ile kamba ambayo aliikata siku hiyo na kumfanya akose raha ya maisha kwa siku nzima.

Alipofika kwa Sakina, alimkuta nyumbani kwake kama kawaida.
Na moja kwa moja Sakina alianza kumuelezea Sabrina aliyoenda kuyakuta huko alipotoka
"Mwenzangu Sabrina kuna makubwa"
"Niambie dada, si unajua nina matatizo! Sasa unaponiambia hivyo unazidi kunitisha jamani"
"Yani ile kamba haikutakiwa kukatwa na mtu yoyote yule, kwavile mama yako kaikata basi kuna majanga yatampata"
"Mmh majanga gani hayo?"
"Tena kuna mawili, anaweza akapona au asipone kabisa na kama atapona basi kunatatizo litajitokeza kwani anaweza akapararaizi"
Hii habari ilimuumiza sana Sabrina, alijihisi atanywea sasa
"Sasa nitafanyaje dada katika kumnusuru mama yangu?"
"Mmh hata mi mwenyewe sielewi ila..."
Kabla hajaendelea, simu ya Sakina ikaita na kumfanya apokee simu ile na kukatisha yale maongezi huku Sabrina akiwa na hamu ya kujua kitu kwani ile ila ya Sakina ilimfanya ahisi kuwa kuna njia ya wao kukomboka na yale majanga.

Sakina alipomaliza kuongea na ile simu, akamuangalia Sabrina kwa makini sana na kumuuliza swali moja tu
"Ulikuwa wapi leo?"
"Nilikuwa kwa rafiki yangu Sia"
"Ni kitu gani kimekutokea?"
Huku akimuangalia Sabrina kwa makini sana na kumfanya aanze kuingiwa na uoga huku akimuelezea yaliyomtokea wakati anatoka kuonana na Sia.
"Kwahiyo huyo mama aliyekuita hukuweza kumsikiliza?"
"Hata kama ungekuwa wewe dada usingeweza, alikuwa akiniita kwa ukari sana na kuniambia maneno ya kejeli"
"Sasa kwa taarifa yako tu ni kuwa yule mmama ndio alikuwa mtu pekee wa kukusaidia wewe na hilo tatizo lako"
Sabrina akashtuka na kushangaa kuwa mtoa msaada gani anakuwa mkali kiasi kile!
"Mmmh dada, mbona leo unanipa maajabu zaidi?"
"Sio maajabu ila wewe umeshindwa kupata msaada kwa ujinga wako mwenyewe. Kwanini hukutaka kumsikiliza?"
"Basi tena dada, hakuna la kufanya nimeshakosea tayari"
"Kwahiyo kirahisi tu hivyo unaitikia kuwa huna la kufanya kwavile umeshakosea tayari! Hivi unajua matatizo vizuri wewe Sabrina? Angalia jinsi ya kumuokoa mama yako, maana hapa muathirika sio wewe tu bali na mama yako pia"
Sabrina alihisi kichwa chake kuvurugika kwani hakujua ni vipi anapata msaada ikiwa wazi huyo mmama alimkimbia, alijua ni wale washirikina waliokuwa wakimsumbua.
Wakaongea mengi sana na Sakina ila hawakupata muafaka wa jambo lolote lile zaidi ya kuongea tu.

Sabrina alitulia kimya akitafakari cha kufanya na hali ya mama yake pia.
Simu ya Sabrina ikaita, na akaipokea kwa unyonge sana kwani alishakuwa na mawazo tayari
"Japhet naongea hapa"
"Aaah! Mambo vipi?"
"Poa tu, je tunaweza kuonana muda huu?"
Sabrina akajifikiria kidogo kumjibu, kisha akakubali kuonana nae na kupanga pa kukutana na huyo Japhet, kisha akakata simu.
Akamuangalia Sakina na kumuaga
"Unaenda wapi sasa Sabrina?"
"Kuna mahali nataka kwenda nikatulize akili yangu"
"Ila kwa ushauri wangu mie ni bora uka...."
Kabla hajamaliza, simu ya Sabrina iliita tena, naye akapokea
"Francis anaongea hapa"
Akajua moja kwa moja kuwa anataka kumpa hali ya Fredy tu,
"Eeh niambie"
"Nipo hapa kwenu naomba uje haraka"
Halafu akakata ile simu, Sabrina akamuangalia Sakina na kumwambia
"Huyu mwanaume ana wazimu nini? Eti uje haraka, halafu anipe nini! Ngoja nikaonane na huyo Japhet kwanza"
"Ila si yupo kwenu huyo!"
"Ndio yupo nyumbani"
"Basi nakuomba uende nyumbani kwenu kwanza kwani kuna kitu nahisi kuwa hakipo sawa huko"
Sabrina akajiona kama yupo njiapanda, na kuamua kurudi kwao huku akiwa amenuna kabisa.

Alipofika kwao, alimkuta Francis akiwa nje ya nyumba yao, naye alipomuona tu akamkimbilia Sabrina na kumwambia
"Siielewi hali ya mama yako"
Sabrina hakutaka kusikiliza zaidi na kukimbilia ndani kwao ambapo alimkuta mama yake amekaa huku ametambaliza miguu yake na kurudia rudia maneno
"Kamba, kamba, kamba, kamba...."
Sabrina alishtuka kwani mama yake alikuwa kamavile mtu aliyewehuka na  alipomuona tu Sabrina, akaacha kusema na kuanguka chini huku akitapatapa.

Itaendelea



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa