STORY TAMU YA JESTINA - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Wednesday, January 29, 2020

STORY TAMU YA JESTINA





Jesca akiwa chooni anaoga ghafla moshi ulianza kutanda chumbani kwake, na ulipotoweka alianza kuhisi maji ni mazito sana na alipoangalia vizuri alijikuta anaoga damu. Alipiga kelele kwa nguvu huku akitoka mbio chooni, alianza kusikia sauti za ajabu ajabu zikinong'ona. "we nani" aliuliza kwa nguvu, "Jesaca siku yako ndio leo" aliiskia ikimjibu, "utalipa kwa ulichokitenda" yalizidi kusikika maneno. "unadhani mi nakuogopa, kama unajiamini jitokeze mbele yangu" aliogea kwa kejeli. ghafla taa zikazimika na kuwaka, mbele yake alisimama Jestina huku damu nyingi zikimtoka. Sasa Jesca aliamini kama ule ni mzimu, alianza kupiga kelele huku akikimbilia mlangoni kwa ajili ya kutoka lakini mlango haukufunguka. "nimekoma nisamehe Jestina" alianza kuomba msamaha, "siku ile wakati unafurahia tukio lile hukujua kama ulikuwa unakosea" Jestina alijibu huku akimsogelea na kumkaba koo. Jesca alianza kutapatapa huku akijaribu kupiga kelele lakini hazikutoka. Kwa nguvu Jestina alimrusha ukutani na kumbamiza, alimsogelea na kumtandika makucha mara kadhaa. Jesca alipoona hali mbaya, alijinyanyua na kukimbilia dirishani. Kwa nguvu alijirusha na kuvunja kioo, kwa vile chumba chake kilikuwa gorofani alianguka mpaka chini na kupasuka kichwa na hapo ndio ukawa mwisho wa Jesca. Hali ilirudi kuwa shwari na Jestina alitoweka huku akiacha ujumbe anaouwacha mara zote baada kufanya mauaji. 
Kishindo kiliskika na majirani pamoja na wazazi wa Jesca walitoka lakini hali waliokutana nayo iliwafanya washangae, Jesca alikuwa chini huku damu nyingi zikitapakaa sehemu alioangukia. Simu zilipigwa polisi na muda si mrefu walifika eneo la tukio, Inspector Hans alifika kuchelewa lakini alifanikiwa kuona mwili kabla haujapelekwa maabara kwa ajili ya uchunguzi zaid. Aliwahoji wazazi wa Jesca kama wanajua lolote kuhusiana na kifo cha Jesca lakini walikuwa hawajui chochote. Basi baada taratibu zote kufanyika mwili wa Jesca uliingizwa kwenye gari na kupelekwa hospitali kwaajili ya uchunguzi zaidi. Vifo hivo viliendelea kuacha gumzo kwa watu wote, hasa watu wa usalama maana kila walipojaribu kuchunguza waliishia kwenye mambo ya mizimu jambo ambalo wengi hawakukubaliana nalo. "jamani sisi tunaonekana wapumbavu sana" aliongea mkuu wa kituo cha inpector Hans, "tukimuacha huyu muuaji atasababisha kuachishwa kazi" aliendelea kuongea. 


"mnajua sisi wote tulikosea mwanzo" aliongea inspecta Hans na kuwashangaza wote, "unamaana gani kusema hivo?" aliuliza mkuu wao kwa mshangao. "nina maana kuwa mauaji yote haya yanahusiana na kesi iliyotokea miaka kumi iliopita" aliendelea kufafanua inspector. "Kwahiyo unamaanisha haki haikuyendeka katika kesi ile au" aliuliza kwa hasira mkuu wake. "kwa kweli mkuu sasa itabidi heshima nieke pembeni sasa maana unataka kunifokea bila msingi, kesi ile ulikabidhiwa wewe na ushahidi wa kutosha kuwa Jestina alibakwa na mwanaume zaidi ya mmoja akiwemo mtoto wa mheshimiwa waziri mkuu Matt, lakini kwa tamaa zako binafsi ukala pesa na kukanusha ushahidi badala yake ukasema kuwa aliebaka ni Alwin. ulifanya hivo makusudi kwa kuelewa kuwa Alwin asingeweza kusema lolote kwa sababu alirukwa na akili. Sasa vyote vinavyotokea leo ujue na wewe umehusika. Na kama nilivokwambia nimekukera basi fanya unalotaka" alimaliza kuongea Inspector Hans na kutoka katika chumba hicho cha mikutano. 
*********************************** 
(miaka kumi iliyopita) 
"asante sana inspector kwa kufika hapa japo nimekushtua" aliongea baba yake Matt, "kwa wewe muheshimiwa hata kama ningekuwa nimelala basi ningeamka na kuja" aliongea inspectar Brandon. "sasa inspecta ni hivi kuna kesi umepewa uisimamie lakini kwa bahati mbaya sana kesi hiyo na mwanangu anahusika" aliongea Waziri mkuu ambae ndio baba yake Matt, "una maanisha kijana wetu Matt anahusika na kifo cha Jestina" aliuliza inspecta kwa mshangao. "ndio inspecta, sasa nataka unisaidie kitu kimoja", "kitu gani hicho". "nataka hiyo kesi ife na ikiwezekana ushahidi upotee kabisa au tafuta yoyote tu umbambikizie" aliongea waziri huku akisogeza bahasha iliovimba. "lakini unajua muheshimiwa kazi hiyo ni ngumu sana" aliongea inspecta huku akiimezea mate ile bahasha. "ah halafu ukifanikiwa kufanya hivyo nitaandika barua rasmi upandishwe cheo" aliongea waziri na kuzidi kutia tamaa inspecta Brandon. kuskia hivo aliinuka haraka na kuchukua ile bahasha kisha akasema "usijali mzee nitahakikisha kesi inakwisha mara moja" na kuondoka. Waziri alitabasamu na kujisemea "hakuna kinachoshindikana mbele ya pesa". 
Inspecta Brandon alirudi kituoni huku akipanga jinsi ya kuizima kesi hiyo, alikuwa na mawazo mengi sana kichwani hasa alipofikiria kupandishwa cheo. Alitumia mbinu zote anazozijua mpaka akafanikiwa kupotosha ukweli wa kesi hiyo na kumsingizia Alwin kuwa ndie aliefanya jambo lile. Habari za kukanushwa kesi hiyo zilimfikia profesa Alexander Harison, alisikitishwa sana lakini hakukuwa na njia nyingine ya kufanya zaidi ya kukubali tu. Wakati wote huo Alwin alikuwa hospitali hajitambui kwa maneno mengine alikuwa amerukwa na akili. Na kutokana na hilo kesi hio ilifungwa moja kwa moja na hivyo Matt na wenzake kuwa huru. Baada ya tukio hilo ndipo waziri mkuu akaamua kumuondoa kwa muda mtotot wake huku Inspecta Brandon akipandishwa cheo na kuwa mkuu wa kituo chake jambo ambalo hata wenzake hawakujua limetokeaje lakini hakuna alieuliza. 
*********************** 
(baada miaka kumi) 
"Profesa tayari wameshaakufa wanne lakini bado hakuna aliekuwa tayari kukubali kuhusika na kifo cha Jestina" alisema Alwin wakati akiwa anaongea na profesa. "tulia kijana madhali hawataki kusema wacha Jestina alipe kisasi kwa kuwauwa mpaka pale watakapokubali kusema ukweli" Aliongea profesa huku akitabasamu. Maongezi yao yaliendelea kwa muda mrefu sana mpaka mwisho walikubaliana wakutane baada wiki moja kujadili tena swala hilo. Baada ya hapo kila mmoja aliondoka na kuelekea nyumbani kwake, lakini Alwin alipita makaburini na kuzuru kaburi la Jestina. "natumai umepumzika kwa amani mpenzi wangu, usijali watalipa kwa kile walichokufanyia" aliongea Alwin na kuweka ua juu ya kaburi la Jestina na kisha akaondoka zake. Jay na wengine waliendelea kumfatilia Alwin wakiamini yeye ndie muuaji na Alwin tayari alishawashtukia hivo kupita kaburini kwa Jestina ilikuwa ni kuwachanganya wanaomfatili pasi na kujua kumbe wao pia wanafatiliwa na Alwin. 
"unajua mke wangu Alwin kabadilika sana siku hizi" aliongea Mr Kelvin kumwambia mkewe, "kivipi mbona mi namuona yupo kawaida tu. "hapana mke wangu mi nakwambia tena Alwin kabadilika sana tokea atoke hospitali ya vichaa" alisitiza Mr Kelvin. "mhh haya lakini mi namuona kawaida tu isipokuwa siku hizi kachangamka sana tafauti na zamani" aliongea mama Alwin huku akiachia tabasamu akionesha kufurahishwa na mabadiliko ya Alwin. Wakati wakiendelea kuongea Alwin aliingia na kuwasalimia, waliitika kwa pamoja na baadae Alwin akaenda zake chumbani kwake. 
Kwa upande wa inspecta Hans baada ya kutoka kwenye kikao alikwenda nje na kutulia huku akili ikitafakari mengi sana, akiwa dimbwi hilo la mawazo aliskia akiitwa na alipogeuka alikutana na mkuu wake wa kituo inspecta Brandon. "nifuate ofisini" aliongea na kuondoka, bila kusita aliinuka nae akamfuata nyuma mpaka walipofika ofisini. "bwana mdogo chunga kauli zako" hayo ni maneno ya kwanza yaliotoka kinywani mwa inspecta Brandon, "wewe hapa kituoni unaongea vile kama nani" aliendelea kuongea kwa hasira. "samahani mkuu, ule ndio ukweli we unadhani dunia bila haki ipo sawa. Hata waliokufa nao wanataka haki zao, we ulielewa fika kama Matt na wenzake wako hatiani lakini ukaibaitilisha kesi na kumuuzia Alwin. Natamani huo mzimu siku moja ukutembelee na wewe uone machungu ya kudhulumiwa" alijibu inspecta Hans bila woga wowote ule. "sasa unaonekana umeota mapembe si ndio" aliongea inspecta Brandon, "kama ndivyo unavofikiri sawa tena makubwa sana" alijib inspecta Hans na hakusubiri neno jingine kutoka kwa mkuu wake aliondoka maana hata yeye hasira zilishaanza kumpanda. Alimuacha mkuu wake akiwa ni mwenye mawazo tele lakini akaona bora apotezee tu. 
Kifo cha Jesca kiliwachanganya wengi miongoni ya waliotenda kosa lile, wapo walioomba usiku usiingie maana walijua Jestina hufanya mauaji yake usiku. Lakini kwa vile hatuwezi kuzuia masaa basi muda uliyoyoma na hatimae kiza kikaana kutanda angani, hatiame usiku uliingia lakini kulikua na mvua kali sana iliondamana na ngurumo pamoja na radi. Usiku huo ulivo ulitosha kuwatisha wengi sana, Mark ndo alikuwa akitoka zake mihangaikononi kwake kuelekea nyumbani kwao ghafla akiwa njiani umeme ukazima. 
Hali hiyoilimshtua kidogo Mark lakini akajipa moyo kuwa ameshaakaribia nyumbani kwao, hivyo basi alianza kukazana huku akiangalia pande zote kama kuna kitu ama mtu anamfuata. Nyumba yao ilikuwa imejitenga kidogo kutoka katika makazi ya wtu wengine, aliacha njia kubwa na kuingia njia ndogo ambayo ilikuwa nampeleka mpaka kwao. Wakati akikazana kwa mbali mbele yake akaona kama mtu kapita mbio. Moyo ulianza kumuenda mbio maana alishaanza kuziona dalili za mauzauza, akiwa anatetemeka ghafla alihisi kama kitu kimepita nyuma yake. Aligeuka kwa kasi lakini hakuona kitu, alipogeuka tena mbele kwa mbali akaona mtu akiwa anakuja upande wake taratibu . Kidogo alipata matumaini na kuanza kukazana kumfata yule mtu. Lakini alivomkaribia mwili ulimsisimka na kuhisi kama hakuwa mtu wa kawaida lakini alipiga moyo konde na kunyongea kwa mendo wa haraka. Ghafla tochi yake ilizima, na ilivowaka alikutana sura ya ajabu sana mbele yake. Aliruka na kuiangusa tochi pembeni, japo kulikuwa na baridi lakini kijasho kilianza kumtoka kwa wingi. "maumivu...." alisikia sauti ikitamka neno hilo kwa sauti a kuning'ona, "leo utahisi maumivu nilioyapata" sauti hiyo iliendelea kuongea huku ikizidi kuwa kali. "unataka nini lakini" aliuliza Mark kwa woga, "nataka roho yako" alijibiwa na wakati huu sauti aliifahamu vizuri sana kama ilikuwa sauti ya Jestina. 
Aliokota tochi yake na kuanza kukimbia, lakini hakufika mbali alishtukia akichezea kofi zito la uso lililomfanya aanze kuona mawenge kidogo na kuanguka chini. Mark alijua kuwa huo ndio ulikuwa mwisho wake, "nisamehe Jestina" alianza kuomba msamaha kwa kilio huku damu zikimoka mdomoni. "leo unalia mshenzi mkubwa wewe, siku ile ulikuwa ukicheka" Jestina aliongea na kumnyanyua Mark. Sasa alifanikiwa kumuona uso kwa uso, macho yalimtoka Mark asijue nini la kufanya. Wakati akiendelea kutumbua macho alirushwa kwa nguvu, kabla hajakaa sawa alichezea makucha kadhaa ya mgongo na kumfanya apige kelele za maumivu. "nimekoma naomba unisamehe" aliongea huku akisimama, "nikusamehe kweli, hivi unajua ni maumivu kiasi gani niliyapata siku ile" Jestina alijibu na kumtokea Mark mbele na kumkaba, kisha sura yake ilianza kubadilika na kuwa ya kutisha sana huku damu nyingi zikichuruzika kutoka machoni mwake kama machozi. Mabadiliko hayo yaliambatana na harufu kali sana ya kuoza, kwa nguvu alimpiga Mark na chini kiasi cha kushndwa kuinuka. "leo utakiona cha moto mpumbavu mkubwa wewe" aliongea Jestina na kisha akamfungua mdomo Mark na kumtia funza. Yeye alikaa pembeni akimuangalia kwa jinsi funza wanavomteketeza Mark. Hawakuwa funza wa kawaida kwani punde baada ya kutiwa mdomoni walianza kutoboa sehemu mbalimbali za mwili wa Mark na kusababisha maumivu makali sana. Mark alipiga sana kelele lakini hakuna msaada wowote alioupata mpaka mwisho alitulia tuli na kuaga dunia. Jestina alipotea eneo hilo akiacha ujumbe wake wa kawaida.




No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa