STORY TAMU YA JESTINA 10 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Wednesday, January 29, 2020

STORY TAMU YA JESTINA 10






Asubuhi taarifa ya kwanza ilikuwa ni kifo cha Mark, huku ikisema bado mauaji hayo hajulikani yanasababishwa na nani. Lakini kilichowashtua watu ni kwamba wote waliokufa walikuwa ni marafiki tokea zamani sana, hivo kukaibua maswali mengi sana. Kituo kimoja cha televisheni kiliomba kufanya mahojiano na mwalimu mkuu wa shule ambayo inaaminika kuwa wote waliokufa wamesoma pale. 
"habari yako mwalimu" 
"nzuri nashkuru" 
"kwa jina naitwa Anita ni mwandishi wa habari kutoka J76 news chanel" 
"mimi naitwa Anthon Dickson, ni mwalimu mkuu hapa" 
"naam mwalim unazungumziaje matukio haya ya mauaji yanayoendelea hapa mjini hasa ukizingatia wote walipoteza maisha mpaka sasa ni wananfunzi wako" 
"kwa kweli ni vigumu kueleza" 
"kivipi mwalimu" 
"unajua ndugu Anita hapa kulitokea kesi kubwa sana ya ubakaji kama utakuwa unakumbuka, ni takriban miaka kumi sasa imepita na inavosemekana kuna wananfunzi wamehusika na tukio hilo" 
"unaweza kuwataja" 
"hapana siruhusiwi kufanya hivo" 
"na kwanini hasa ukawa unahisi kama mauaji yanayofanyika sasa ya uhusiano wowote na kilichotokea miaka kumi nyuma" 
"Unajua tulivokuwa wadogo, tulikuwa tukisimuliwa mambo mengi sana ambayo wengi wetu hatuyaamini" 
"kama yapi" 
"kwa mfano najua utakuwa umesimuliwa kuhusu ulimwengu wa watu waliodhulumiwa" 
"ndio lakini hizo ni hadithi za kufikirika tu" 
"hapo ndio kwenye utata sasa na hilo ndilo linalotokea saa hivi, baada kufanyika tukio lile kesi ilipelekwa mahakamani lakini cha ajabu ilizimwa haraka na watuhumiwa wakaacha huru, kwa sababu haki haikupatikana, sasa aliedhulumiwa amerudi kuja kuitafuta haki kwa mikono yake kama tunavojua HAKI ISIPOPATIKANA KWA AMANI BASI ITAPATIKANA KWA VITA. Na hii ni vita ambayo hakuna mtu yoyote kati yetu anaeweza kuizua na kama huamini kama mizimu ipo heebu jaribu siku moja kuuwa halafu uachiwe huru uone kama hutokipata walichokipata hawa vijana walikufa" 
Mwalimu mkuu alimaliza kuongea na kuomba kuondoka akaendelee na majukumu mengine ya kawaida. Na kwa sababu kipindi hicho kilikuwa hewani live kila mtu alishuhudia, "ni bora wafe tu ili watu wajue kama haki ya mtu ni mali", "pumbavu nani atakaa aamini upumbavu ule". "mmmh makubwa mi nlijua ni hadithi tu za kufikirika", hayo ni baadhi ya maneno yaliokuwa yakisemwa na baadhi ya watu kila pahali. Kwa kweli story ilikuwa ni hiyo tu kila kona unayopita, Alwin ni miongoni mwa watu waliokiona kipindi hicho na kufurahia sana majibu ya mwalimu, yalitosha kupeleke ujumbe kwa wote ambao wanacheza na haki za watu. 
"jamani hali imezidi kuwa mbaya sasa" Jay aliongea katika kikao kifupi cha dahrura kilichoitisha baada ya kifo cha Mark. "sasa tunafanyaje" aliuliza Monica, "ah hatuna la kufanya, sisi tulitenda uovu huku tukifurahia bila kufikiria ni kiasi gani tulichowaumiza wengine" Jay aliongea akionekana kujuta sasa. "akah! we vipi sasa unajuta nini, mi nasema hapa cha msingi ni kumuua Alwin maana nahisi yeye ndie anetufanyia mchezo huu" alifoka Alex kwa hasira. "sasa umeona ulivokuwa huna akili unataka kurekebisha kosa moja kwa kutenda jingine" Jay alimjibu akionekana kuchukizwa na maneno ya Alex. "mi nlikwambieni huyo boya ni mtoto wa mama" aliongea Alex na kumkejeli Jay, "sawa mi ni mtoto wa mama, lakini mi naona bora tujiandae kufa tu maana hatujui anefuata ni nani" Jay aliongea na kuinuka kisha akaanza kutoka nje, "nenda huko na leo utakufa wewe, Jestina kama unanisikia leo Jay amejianda ukamuue sawa" aliongea Alex na kufanya mzaha. 
Jay hakujibu kitu,wakati anatoka aliingia unyonge wa ghafla na kupatwa na homa kali sana iliomfanya aanguke barabarani. Wasamaria wema walipiga simu hospitali na punde gari ya kubebea wagonjwa ilifika na kumuawahisha hospitali. Alipofika tu alipatiwa huduma ya kwanza na kupelekwa chumba cha wagonjwa mahututi kutokana na hali yake kuwa mbaya sana. Familia yake ilifka akiwemo mkewe na mwanae wa kike mwenye umri wa miaka minne, lakini hawakuruhuisiwa kumuona kutokana na kuwa hali yake haikuwa nzuri. Hali hiyo ilimtia simanzi mkewe kumuona mumewe yupo katika hali mbaya sana lakini angefanyaje na alitakiwa kusubiri. 
Walisubiri mpaka jioni lakini hali yake haikuchanganya hico wakaambiwa waondoke na warudi kesho kwa ajili ya kumuangalia walikubaliana na daktaru na kuondoka. Kiza kilianza kuingia lakini bado hali ya Jay haikutengemaa kabisa "kwa kweli tumejaribu kadri ya uwezo wetu sasa ni muda wa kumuachia Mungu atende muujiza" aliongea daktari mmoja na wenzake wakamuunga mkono. Walizima vifaa vyote na kumuhamisha chumba, huko walimuunganisha na mashine ya kupumulia kwa ajili ya msaada maana hata pumzi ilikuwa ni ngumu kuvuta. Baada ya hapo walitoka wote na kumuacha chini ya uangalizi wa manesi. 
"Jay.....amka" alisikia sauti ikimuamsha huku akitingishwa, kwa uvivu alifungua macho na mbele yake alikuwa Jestina amesimama akiwa na sura yake ya kawaida, sio ile ya kutisha. "najua umekuja kulipiza" aliongea Jay huku akiitoa mashine ya kupumulia, "lakini nina ombi moja tu kwako, naomba uniache mpaka kesho angalau nimuone mwanangu kwa mara ya mwisho kabla ya kuaga dunia" aliongea Jay kwa masikitiko makubwa. "kwanini ulikubali kushuhudia unyama ule" aliuliza Jestina huku uso wake ukianza kubadilika na kuwa wa kutisha. "kwa kweli siku ile sikutegemea kama kungetokea tukio kama lile" alijibu Jay kiunyonge, "lakini wakati linafanyika ulikuwa na uwezo wa kuzuia lisifanyika" aliongea Jestina akizidi kutisha. "hilo ndio linalonijutisha mpaka leo" aliongea Jay huku machozi yakianza kumtoka, "najua kama nimekukosea na niko tayari kulipa kwa nilolitenda, lakini naomba unipe siku moja tu japo nimuone mwanangu na mke wangu kisha njoo unimalize" Aliendelea kuongea Jay huku kilio kikipamba moto, alijaribu kujifuta lakini aliposusha mkono Jestina alikuwa kashaatoweka. "asante kwa kunikubalia ombi langu" aliongea huku akijiweka vizuri kitandani na kuendelea kulala. 



Asubuhi mapema familia yake ilifika kumuona, "nini kimekusibu baba Sophia" aliongea mkewe huku akimuangalia kwa huruma, "hata mimi mwenyewe sijui, homa tu ilinishika ghafla" alijibu huku akilazimisha kutabasamu. "pole mume wangu" aliongea mkewe kumpiga busu katika paji la uso, "pole dady utapona" sauti ya Sophia iliskika huku akimpa pipi baba yake. Sophia alikuwa kafanana sana na baba yake, na alimpenda sana. "Sophia baby njoo nkwambie kitu" Jay alimuita mwanae na kumnong'oneza kitu, Sophia alitabasamu na kumrukia baba yake kisha akasema " wewe ni baba mzuri kuliko wote". Muda wa kutizama wagonjwa uliisha na familia yake iliaga na kuondoka huku wakiahidi kurudi kesho yake kwa ajili ya taratibu za kwenda nae nyumbani. Aliagana nao huku machozi yakimtoka maana alielewa hiyo ilikuwa ni siku yake ya mwisho duniani. Kutokana na hali yake kuimarika mashine za msaada wa kupumua ziliondolewa na kupelekwa chumba cha wagonjwa wa kawaida tu. Aliendelea kupata matibabu madogomadogo, lakini akilini mwake alikuwa akiwaona kama madaktari wanatwangaa maji kwenye kinu maana usiku wa siku hiyo ni usiku wa kifo chake. 
Usiku hatimae ulifika na Jay alikuwa tayari kwaajili ya kufa tu maana alielewa kabisa ni aina gani ya mauaji anayofanya Jestina. "Jay, naona uko tayari kwa adhabu yako" alimsikia Jestina akimwambia wakati akiwa amepumzika. "ndio niko tayari kwa chochote" alijibu Jay huku akitetemeka, "Kwa vile umelitambua kosa lako na kulijutia, mimi sikuja hapa kukuuwa maana kwanza una mke anaekuthamini sana na pili una mtoto ambae bado anahitaji malezi yako na upendo wako kama baba yake" aliongea Jestina na kujitokeza mbele ya Jay akiwa katika umbile la kibinaadamu "lakini nataka ufanye kitu kimoja, usijaribu kutoa ushahidi kokote pale na pia nakupa siku tatu uondoke Mashvile na familia yako yote, nenda mbali sana na uwe baba mwema kwa mwanao na pia mume mwema kwa mkeo. Na jengine asijue hata mmoja miongoni mwa marafiki zako waliohusika na kifo changu. Mimi nimekusamehe na nakutakia maisha mema na yenye amani tele lakini kumbuka ukitovukwa adabu nitakurudia" alimaliza kuongea Jestina na kuoweka. Jay hakuamini kama kasamehewa maana alielewa kabisa kuwa Jestina alikuwa hataki masihara, alilala usingizi mzuri huku akijiapiza kufanya yote aliyoambiwa. 
******************* 
Mapema siku ya iliyofuata familia yake ilifika na taratibu za kutoka hospitali zikafanyika, baada ya kufika kwake alimueleza mkewe kuwa anataka kuhama Mashvile kwani amepata kazi nzuri nchini Italy. Aliwaeleza pia wazazi wake swala hilo na kwa vile yeye ndie aliekuwa analisha familia hakuna aliempinga, maandalizi ya safari yalifanyika kimya kimya bila hata rafiki yake mmoja kujua. Jioni yalikuwa yamekamilika na wote waliondoka mjini Mashvile "nakuahidi Jestina nitatekeleza yote ualionambia" aliongea maneno hayo kimoyomoyo wakati analipita bango liliandikwa KWA HERI MASHVILE. 
"Oya Alex mtu wangu mbona tokea jana sijamsikia Jay" Patrick alimuuliza Alex ambae alikuwa bize akijaribu kumchora mwanadada mmoja ambe alionekana kudance vizuri sana, "ah mara mwisho niliskia kalazawa hospitali, lakini nahisi Jestina atakua kashampitia tayari" alijibu Alex na kuinuka kulekea katika ulingo wa kudance lakini nia na madhumuni yake ilikuwa ni kwa ajili ya yule mschana. "habari yako mrembo" 
"safi tu" 
"Mimi naitwa Alex sijui mwenzangu" 
"ahaa mimi naitwa Jessie" 
"jina lako zuri, tunaweza tukasogea pembeni tukaongea mawili matatu" 
"hamna shida" 
basi walisogea mpaka counter na Alex akaagiza vinywaji kisha wakaanza kuongea, waliongea sana mwisho walionekana kukubaliana "oya Patrick wacha mi nitoke na shemeji yako" Alex alimuita Patrick na kumwambia, "oya mwanangu mtoto huyo mkali, kama vipi tupige tungo" Patrick alimnong'oneza Alex. "tulia mtu wangu mi naenda nae geto nikimaliza kula asali na kutwangia na wewe uje kuonja mtu wangu" aliongea na wakakubaliana. 
Patrick alirudi kwenye dance floor huku Alex akiondoka na Jessie, "tunaenda wapi sasa" aliuliza Jessie, "ah nyumbani kwangu si mbali na hapa" alijibu Alex na kuzungusha mkono wake kwenye nyonga ya binti huyo. Mwendo ulikwa wa dakika tano tu hatimae walifika geto na kumkaribisha ndani. "kaa kitandani hapo nakuja" aliongea Alex na kuingia chooni, kumbe alikwenda kutega camera ili ajirikodi anavomkuna mrembo huyo. Alirudi na kumkuta tayari ameshavua nguo na kubakia mtupu, tamaa ya ngono ilimpanda Alex kujikuta anamvamia lakini kabla hajafikisha mdomo wake kwenye midomo ya mrembo huyo alijikuta akirushwa kwa nguvu.




No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa