STORY TAMU YA JESTINA 8 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Wednesday, January 29, 2020

STORY TAMU YA JESTINA 8





JESTINA-8 

Bado inspecta Hans alikuwa njia panda maana aliona kama Alwin anamchezea mchezo mchafu, baada kufikiria sana bila kupata majibu aliamua kwenda nyumbani kwa Profesa Alexander Harison kwa ajili ya kuripoti alichokiona. Safari yake ilikuwa ni ya dakika kumi tu, alipofika alikaribishwa ndani na kuomba kuonana na Profesa. Haukupita muda aliambiwa aingie katika ofisi, "samahani kwa kuja bila taarifa" aliomba msamaha kwanza, "bila samahani". "ukweli kuna jambo linatitaza, kwa sababu jana nilienda kuongea na Alwin lakini nilipokutana nae msibani alisema hanifahamu na wala hatujaongea kitu" alieleza, " wakati unaongea nae majibu yake yalikuaje" aliuliza profesa. "yalikua yenye chuki ndani yake na baadhi yalikuwa ya mkato" alijibu. "Alwin hana majibu ya mkato, ni kijana ambae majibu yake yanaheshima" aliongea profesa na kumshtua kidogo inspecta Hans ambae sasa alishaanza kuamini kama hakuongea na Alwin, sasa swali lilikuwa aliongea na nani kama si Alwin. "na kuhusu mauaji yanayotokea, mpaka sasa ripoti zinasema kuwa si ya kawaida" alijikaza na kuendelea kuongea. "naweza nikaziona picha za miili yao" aliuliza profesa. "ndio" kisha akatoa fail na kumkabidhi profesa. 
Profesa aliziingiza kwenye mashine fulani hivi kama projecta na kuzima taa zote katika ofisi yake kusababisha kigiza fulani hivi, kisha akaiwasha ile mashine na zile picha zikawa zinaonekana ukutani. Lakini aliganda kidogo akiangalia alama za kucha katika miili yote miwili na kubaini kuwa alama hizo zimepigwa katika mtindo mmoja. Haraka alifungua droo na kutoa picha ya ile michoro alioandikwa Alwin kipindi ambacho allikuwa hayuko sawa na kuanza kulinganisha. "unaona kitu gani hapo inspecta" aliuliza profesa, "mi naona michoro tu" alijibu. "angalia kwa makini" alisisitiza profesa ndipo inspecta Hans aliposimama na kusogea kwenye ukuta na kuanza kuzichunguza kwa makini sana. Aligundua kuna maandishi fulani hivi lakini alishindwa kuyasoma "naona kama maandishi hivi" aliongea inspecta. "ndio katika miili yote miwili kuna jina limeandikwa lakini katika lugha ya kale ya wenyeji wa Mashvile na jina hilo ni JESTINA" aliongea profesa na kumfanya Inspecta kutumbua macho kama mtu aliesakamwa na tonge la chakula kwenye koo. "unataka kunambia kuwa muuaji ni JESTINA au vipi" aliuliza kwa sintofahamu, "ndio inspecta muuajai ni Jestina, hivi umewahi kusikia kama kuna ulimwengu wa watu waliodhulumiwa" alijibu profesa na kuuliza. "ah mi hizo story huwa nazisikia tu lakini siamini kabisa" alijibu inspecta huku akitabasamu, "basi kuanzia leo ndio uamini kama kweli huo ulimwengu upo na mtu akifa kifo cha kudhulumiwa basi hupita hapo kwanza na hukaa kwa muda wa miaka kumi. ikiwa ndani ya kipindi hicho kutakuwa na mtu duniani ambae anaamini mtu huyo amedhulumiwa na haki haijatendeka basi hupata uwezo wa kurudi duniani kuja kuwalipa wale waliomdhulumu" aliongea na kufafanua Profesa "inspecta kazi yako imekwisha sasa kwa sababu hakuna utakalofanya kumzuia Jestina asilipe kisasi. Wewe kazi yako itakuwa ni kushuhudia tu mauaji hayo" aliongea profesa na kuonekana kama kufunga kikao hicho. 
***************************** 
Sauti za huba ziliskika ndani ya chumba kimoja katika hoteli kubwa katika mji wa Mashvile, "James niahidi kama utanioa". "niamini wewe ni wangu na kesho nakupeleka nyumbani nikakutamblishe kwa wazazi wangu" James alijibu huku akionekana kunogewa na penzi la mschana huyo, ndani ya chumba hicho taa zilikuwa zimezimwa isipokuwa taa moja nayo ilikuwa ikitoa mwanga hafifu sana na kukifanya chumba hicho kipendeze. Kuna wakati James alifunga macho kwa raha alioipata, alipofungua alijkuta akimuachia mpenzi wake na kuruka pembeni. Hiyo ni baada kuona sura ya Jestina badala ya mpenzi wake, "James unanini mbona umenikata stimu" aliongea mwanamke huyo kwa kudeka. "ah hamna kitu" alijibu kwa kujibabaisha na kurudi kitandani ili aendelee na mchezo, wakati akiendelea kufanya hivo aliangalia dirishani na kumuona Jestina akimuangalia. "mama" alipiga kelele huku akimsukuma mpenzi wake kwa nguvu na kusababisha ajigonge kichwa kwenye kona ya kitandana na kuanza kutoka damu nyingi na mwisho alitulia tuli. Kicheko kikali kiliskika na kufuatiwa na maneno "na bado utajuta kuzaliwa" kisha kimya kikatawala ndani ya chumba hicho. Alipoona hali imerudi kuwa ya kawaida alimsogelea mpenzi wake na kumtikisa lakini wapi, muda mrefu alikuwa kashapoa. Woga ulimpata na kuamua kuvaa na kuondoka eneo hilo na kuuwacha mwili wa mpenzi wake ukiwa umetapakaa damu. 
Asubuhi mapema akiwa kwao, gari ya polisi ilifika na kuonyesha waraka wa kukamatwa James, hakukuwa na jinsi zaidi ya kukubali na kufikishwa kituoni. Alihojiwa kidogo lakini hakutaka kuonyesha ushirikiano, hivo ikatoka amri awekwe mahabusu mpaka atakapokuwa tayari kusema. Masaa yalikatika na hatimae usiku ulifika bila kukubali kuongea chochote. Akiwa kajilaza kwenye kigidoro kidogo, "James...James...hahaha" aliskia sauti ikimwita lakini hakumuona mtu. "Jestina dadangu naomba unisamehe, ujinga tu ulikuwa ukinisumbua" alianza kuomba msamaha huku akilowanisha suruali yake. "mpumbavu mkubwa wewe nani dadaako, kuna mtu anaeweza kumshika dadaake ili abakwe" Jestina alijibu kwa hasira na kumtokea mbele yake. "mamaaaa nakufa" James aliruka huk akipiga kelele, lakini ghafla Jestina akatoweka na kumtokea nyuma yake. 


Aliinua mkono wake na kumtandika kucha za mgongo na kumfanya apige ukwenzi wa maumivu. Kwa kweli James alijua hicho ndio kiama chake maana kila alivojaribu kujitetea ni kama alikuwa akichochea moto. Jestina aliendelea kumrarua mpaka alipohakikisha amemmaliza kabisa, kuhakikisha haishi tena alikpiga kucha za koromea na kulikata. Kama kawaida yake aliacha ujumbe na kutoweka, siku ya pili asubuhi maaskari waliripoti kifo cha James. Wengi walishtuka hasa waliohusika kwa namna moja au nyingine katika kifo cha Jestina. Hali hiyo haikuwatisha wao tu bali mpaka watu wengine ambao hawakujua chochote juu ya matukio hayo. Kila kukicha vyombo vya habari vilitangaza mauaji mapya yanayofanyika hukua ikiaminika kuwa muuaji ni mtu ambae amebobea na anauwa kwa sababu ya kulipa kisasi. Kama kawaida inspeta Hans alirikodi tukio hilo katika mafaili yake na kuondoka. Sasa hakuumiza sana kichwa kwa sababu alishajua muuaji sikiumbe wa kawaida. 
Upande wa Alwin hali yake ilizidi kutengemaa na sasa mwili wake ulishaanza kurudi na vidonda vidogo vidogo vilishaanza kukauka. Familia yake ilifurahi lakini haikuwa hivyo kwa familia ya Jestina ambayo bado walikuwa ni wenye majonzi sana hasa kwa kumpoteza mtoto wao pekee. Hilo lilimuathri sana mama yake na kupelekea baadhi ya wakati kuzimia kutokana na msongo wa mawazo. Hata baba yake pia ilimathiri na kupelekea kudhoofika kimwili japo si sana. Siku hiyo Alwin alipanga kwenda kuwatembelea ili kuwajulia hali, aliondoka kwao asubuhi mapema na kuelekea kwa Mr Hendrix. Alipofika alikaribishwa ndani vizuri na mfanya kazi kisha akaenda kuitwa Mr Hendrix. Alifurahi sana alipomuona Alwin na kumkumbatia "Mungu ashukuriwe kwa kukupa uzima mwanangu" aliongea huku akijizuia machozi yasitoke. "asante, habari za siku nyingi" Alwin aliuliza, "kama unavoziona mwanangu, kwa kweli tokea Jestina atutoke maisha yetu yamekuwa magumu sana sijui hata kwanini Mungu ametutenda kiasi hichi" Alijibu Mr Hendrix na wakati huu alishindwa kuyazuia machozi na kuyaacha yatiririke kuonyesha machungu alokuwa nayo. 
"hapana mzee wangu usiseme hivo, Mungu hajawatenda ila amekupeni mtihani kama alivowapa wengine tu ili kukupimeni imani. Yeye ndie aliewapa Jestina na yeye ndie aliemchukua kwani kuna ubaya gani mtu kuchukua kilichochake. Nyie jueni tu kama Jestina amepumzika lakini hatopata amani ikiwa bado mtaendelea kumlaumu Mungu kwa kifo chake" Alwin aliendelea kumliwaza Mr Hendrix ambae alikuwa akilia kama mtoto mdogo. "mwangu we huujui uchungu nlokuwa nao, kifo cha Jestina kimepelekea mpaka mamaake kupata maradhi ya kuanguka. Ukweli Alwin naogopa kumpoteza mke wangu" Alwin alivyosikia hivo alishtuka kidogo na kuomba kwenda kumuona. Bila kinyongo Mr Hendrix aliongozana nae mpaka chumbani, alimkuta akiwa amelazwa huku akiwa amewekwa drip. Alwin alisogea mpaka pembeni yake na kukaa kwenye kiti "habari yako mama" aliongea kwa sauti ya chini. "nashkuru sijui wewe Alwin" alijibu mama huyo japo kwa tabu kidogo. "pole kwa yote yaliotokea", "asante mwanangu, kwanini lakini" alijibu huku akilia. ""pole kwa yote yaliotokea", "asante mwanangu, kwanini lakini" alijibu huku akilia. "yote ni kazi ya Mungu na kama tunavojua kazi ya Mungu haina makosa cha msingi mamaangu kukubaliana kama Jestina hayupo tena nasi" Alwin aliongea huku akimshika mkona mama Jestina kwa ajili ya kumliwaza. 
"kwanini waliamua kumfanyia ukatili mwanangu, aliwakosea nini" aliendelea kuongea huku machozi yakimtoka. "usijali mama wote waliohusika na kifo cha Jestina watalipa kutokana na dhambi waloifanya" Alwin aliongea huku hasira zikizidi kumpanda lakini alijitahidi kuzizuia. "nakuahidi mama nitakuletea Jestina mwengine, nipe muda tu mpaka mambo fulani yakamilike" aliongea Alwin na kumfanya mama huyo aachie tabasamu kwa mbali. Waliongea mambo mengine mengi huku kwa muda wakisahau machungu yote ya mambo yaliotokea. Baadae Alwin aliaga na kuondoka na kurudi kwao, moyo wake ulifarijika sana kuonana na familia ya Jestina. Hata wazazi wake waligundua furaha alokuwa nayo na wala hawakujali kumuuliza chochote kile. 
*************************** 
Baada ya kifo cha James waliitana karibu wote wale waliohusika na kifo cha Jestina, "jamani natumai mtakuwa mnajua nini kilichotukutanisha hapa" Jay aliongea baada kikao hicho kilichokuwa na waschana sita na wavulana kumi na moja. "tumeshazika wenzetu watatu, na hatujui atafuata yupi" aliendelea kuongea. "lakini kwa nini tulishiriki kitendo kile" aliongea mschana mmoja alieitwa Christina, "hakuna muda wa kulaumiana saa hivi jambo lile ndo lilishatokea kilichobaki ni kutafuta suluhishi kwa hili linalotukabili sasa hivi" aliongea kijana mwengine alieitwa Mark. "lakini wewe, James, Jay na Matt ndo mloyataka" aliongea mschana mwengine alieitwa Jesca. Walianza kulumbana huku kila mmoja akitafuta wa kumtupia lawama, "sasa mukigombana hivo ndio mtafikia suluhisho, hebu acheni upuuzi wenu" alifoka Jay na wote wakanyamaza kimya. "cha msingi hapa ni kumjua muuaji ni nani" aliongea Jay na kuwashangaza wote. "kivipi wakati muuaji ni mzimuwa Jestina" alijibu Jesca, "kwanza subiri niwaambie kitu, mimi hasa siamini kama mtu akifa anarudi tena duniani eti akiwa mzimu" aliongea Jay. "cha msingi hapa kwanza tuanze kumfatilia Alwin kila anachokifanya, mi nahisi kama si yeye anaefanya mauji basi atakuwa anamjua muuaji ni nani" Aliongea Jay kwa kujiamini.
"oyaa we umekunywa mchana wote huu mtu wangu" aliongea kijana mwengine alieitwa John, "unadhani boya kama yule anaweza kufanya mauaji, hivi we unadhani kuuwa ni kitu cha mchezo" aliendelea kuongea. "hivi nyie hamjiulizi kwanini mauaji haya yameanza baada Alwin kutoka hospitali ya vichaa, kwanini kipindi chote cha miaka kumi hakujatokea matukio kama haya" aliendelea kuongea Jay na sasa maneno yake yalianza kuleta maana ndani ya vichwa vya wenzake. "hapo kidogo inaanza kugonga ndani ya kichwa changu" aliongea Mark kisha akaendelea " sasa tunafanyaje". "hapo ndio kwenye shughuli yenyewe, inabidi tuanze kufanya uchunguzi chini kwa chini mpaka tuapate ukweli" aliongea Jay na kisha wakaanza kupanga mipango ya kuanza kufanya uchunguzi huku kila mmoja akipewa jukumu lake. Baada ya maongezi ya muda mrefu waliagana na kila mtu alikwenda zake kwao. 
**************************




No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa