STORY TAMU YA JESTINA 11 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Wednesday, January 29, 2020

STORY TAMU YA JESTINA 11


 


Ghafla mrembo huyo alianza kubadilika, naam hakuwa mwengine isipokuwa Jestina. "wewe hujabadilika hata kidogo" aliongea kwa nguvu sana, "yaani bado wewe na yule mshenzi mwenzako mlikuwa mnafikiri kupiga mtungo" aliendele kuongea huku akimsogelea. "Jestina nisamehe" alianza kuomba msamaha, "umechelewa sana" alijibu Jestina na kupiga kofi la uso akimwachia alama za kucha. Alex aliweweseka lakini alipofungua macho hakumuona ila ghafla akamtokea kwa nyuma na kumchana mgongoni. Alex alipiga yowe la kuomba msaada lakini wapi hakuna lolote lilisikilikana nje ya chumba hicho. Jestina akatoweka tena na kumtokea mbel yake ila hakumgusa alimuangalia tu usoni na Alex mwenyewe akaokota kipande cha kioo na kunaza kujichana. Alipiga kelele kwa maumivu lakini alishindwa kujizuia mwisho alianguka chini, hapo Jestina alimsogelea na kumpiga kucha za shingo na kulitoa koromeo, aliacha ujumbe na kutoweka huku Alex akiwa chini akijaribu kuvuta pumzi ambayo haikua na pakupita mpaka mwisho akakata roho. Patrick baada kuona Alex hapigi simu aliamu kutoka na kumfata geto. 
Kwa mwendo wa haraka Patrick alifka geto kwa Alex na kukuta mlango umefungwa lakini kila alipojaribu kugonga haukufunguliwa. Alisubiri kama dakika kumi kumi hivi ila bado kulikuwa kimya, mwisho alikumbuka kuwa ana ufunguo mwengine wa mlango huo lakinialipojaribu kuingiza kwenye kitasa uligoma hiyo ilikuwa ni ishara kuwa kulikua na ufunguo mwingine kwa ndani. Baada kuona jitihada zake zimegonga mwamba aliamua kutoa simu yake na kuandika ujmbe "poa mshkaji wangu tumekubaliana vipi na wewe unafanya nini, mbona mimi nikipata kama hivo tunapiga mtungo safi ila haina noma" aliutuma na kuondoka. Aliondoka na kuelekea nyumbani kwao, baada kufika alivua nguo zake na kwenda kujimwagia maji. Alimaliza na kutoka kurudi chumbani na hapo ndipo aliposhtuka kidogo maana suruali yake chini ilikuwa imeganda damu. Alitahidi kutafuta ni sehemu gani ameumia lakini hakuiona ndipo machale yakamcheza lakini akapotezea na kuingia kitandani. 
Asubuhi mapema aliwahi kuamka nakwenda geto kwa Alex, alipofika alishtuka sana baada kuona michirizi ya damu ikitokea ndani ya chumba hicho. Alipiga kelele na watu wakaja kwa pamoja walisaidiana kuvunjia mlango na hapo ndipo wakakutana na mwili wa Alex umelela sakafuni huku ukiwa umetapakaa damu. Bila kuchelewa walipiga simu polisi na kutoa taarifa, ila alichokifanya Patrick ni kuchukua simu ya Alex na kuufuta ujumbe aliomtumia ili asije akaonekana yupo hatiani. Haukupita muda polisi walifika eneo la tukio na kuanza kufanya uchunguzi na katik tafuta yao walifanikiwa kuipata camera alioitega Alex na kuichukua kama sehemu moja ya ushahidi wao. Walimaliza kufanya uchunguzi na taratibu nyingine zikafuata ikiwa ni pamoja na kuupeleka mwili wa Alex hospitali kwa ajili ya uchunguzi zaidi. 
"tumefanikiwa kupata camera sehemu ya tukio" aliongea polisi mmoja na kumkabidhi Inspector Hans ile camera. Na yeye bila kuchelewa aliunganisha na computer yake na kuanza kuangalia, ilionyesha Alex akitoka chooni na alipofika kitandani alijirusha lakini hakuonekana mtu mwengine katika kitanda hicho. Lakini ghafla alichomoka kitandani na kujigonga ukutani kisha akaonekana kama akiomba msamaha lakini ghafla alipiga kelele na damu kuanza kumtoka. Waliendelea kuangalia video hiyo mpaka walipoona anachukua kioo na kuanza kujikata wenyewe mpaka akaanguka chini na ghafla akaanza kutoka damu shingoni kama ishara kuwa amekachinjwa, yakatokea maandishi ukutani "AMELIPA". Hapo camera ikaingia chenga na kuzima kabisa,askari wengi waliotizama ile video walishtuka sana hasa pale yalipotokea maandshi ukutani. 
"mi si niliwaambia kama mauaji haya hayafanywi na mtu wa kawaida" aliongea Inspecta Hans na kuwaangalia wenzake "sasa mmeamini kama kuna mizimu duniani" aliendelea kuongea lakini alionesha kama kushtuka kidogo na kuamua kurudia kuingalia tena kwa mara ya pili lakini kwa makini zaidi, ndipo akagundua kama shape ya mschana kama iliokuwa inaakisi mwanga. Wenzake walimshangaa na kumuuliza mbona anaangalia tena. "hebu angalieni kwa makini hiyo video kwa mbali sana utaona kama shape ya mschana" aliwaambia na wote wakaikodolea macho ndipo wengi wakagundua kile alichokisema Inspecta Hans. 
Alwin akiwa kwao alifutwa na askari kuombwa aende kituoni kwa ajili ya majadiliano, alikubali bila kinyongo na kuondoka nao. walifika kituoni na kuanza mazungumzo. 


"kijana hebu tueleze kuhusiana na Jestina" 
"mimi sina la kueleza" 
"tunaomba msaada wako maana mauaji yamezidi na yantupa sifa mbaya kama kitengo cha polisi" 
"sasa mimi niwaambie nini wakati kesi yake ilifikishwa kwenu miaka kumi iliopita lakini mkajifanya wababe kuipindisha sheria, kwa kupewa pesa mkanibambikia mimi" 
"tusaidie basi tuweze kumdhibiti" 
"hahaha mna kichaa kweli nyinyi, kiufupi mumechelewa sana amerudi mwenyewe kuja kuiweka sawa sheria na nyinyi hakuna mnaloweza kufanya kilichobaki nyie kaeni tu musubiri kukusanya miili ya atakao waua" 
"kijana unajifanya jeuri si ndio" inpecta Brandon alifoka 
"tena wewe haswaa umo katika list yangu" Alwin aliongea maneno hayo na ghafla alianza kubadilika na kupotea katika mazingira ya kutatanisha. Naam walilipata jibu kumbe hakuwa Alwin bali alikuwa ni mwenyewe Jestina na aliamua kufanya hivo kumpa onyo Inspecta Brandon na polisi wengine juu ya mpango wa kupenda pesa na kupindisha sheria. Kushuhudia hivo Inspecta Brandon alianguka chini na kupoteza fahamu. 
"mimi niliwaambia mkaniona namtetea Alwin, sikusema tu ila yalishaanikuta ndio maana nikawaambia haitasaidia hata kama mtamkamata Alwin kwa sababu Jestina ndie anaejibu ukimwita Alwin" aliongea Inspecta Hans, "unamaanisha nini kusema hivyo" aliuliza askari mwingine. "namaanisha kuwa Jestina anatumia sura ya Alwin, hivyo basi hata ukimhoji utaishia kukipata kama kilichompta Inspecta Brandon muda mfupi uliopita" aliposema hivo ndio wakakumbuka kama mkuu wao ameanguka, haraka walimbeba na kumuwahisha hosptali. 
****************************** 
Ndege ilitua uwanja wa Mashvile, miongon mwa abiria walioshuka alikuwemo binti mmoja mrembo sana. Hakuwa mwengine isipokuwa ni mtoto wa Profesa Alexander Harison, Miryam. Baada ya miaka mingi sasa ndio anarudi nyumbani akitoka kuchukua masters katika udaktari akiwa kama daktari bingwa saikolojia. Alitoka nje ya uwanja na kuonana na baba yake mzazi "karibu nyumbani mwanangu" profesa aliongea huku akitanua mikono kama ishara ya kutaka kumkumbatia mwanae. Miryam kwa furaha aliruka na kumkumbatia baba yake. "umekuwa mkubwa mwanangu" aliongea profesa, "ah kawaida tu baba" Miryam alijibu na kuachia tabasamu na kuufanya uzuri wake uonekane vilivyo. "mie ningapata mtoto kama yule pia nisingefikiria kuoa mke mwengine", "dah yule mtoto ni mkali kupindukia kiasi profesa ampe kila anachotak", "sasa wewe unadhani acheze zawadi kama ile kutoka kwa muumba, kama angekuwa mwanangu angetaka hata dunia ningempa". Hayo ni maneo yalikuwa yakisemwa na walinzi walipokuwa wakimpokea mtoto wa bosi wao. 
Waliingia kwenye gari na safari ikaanza, msafara huo ulikuwa ni zaidi ya ule wa raisi, ulikuwa na gari kumi zote aina Rolls royce nyeusi zikisindikizwa na pikipiki tatu mbele na tatu nyuma. Kwa kweli profesa alimpenda sana mwanae kiasi kwamba hakujali anatumia kiasi gani cha fedha kumhudumia tu. Alimpa kila alichotaka na hakusita kumwambia "WEWE NI LULU YA MAISHA YANGU". Mapenzi yake kwa mtoto wake hayakuwa na hayakufanana na chochote. Ila alijua ipo siku itabidi amkabidhi kwa mtu mwengine ili amlee, akimaanisha kuwa ipo siku mwanae pekee ataolewa na kuondoka nyumbani. Na kila alipoifikiria siku hiyo alihisi kama nusu na robo ya maisha yake atakua kayatoa, kuna baadhi ya wakati alijikuta akibubujikwa na machozi lakini angefanyaje na ndio mfumo wa maisha ulivo. 
Walifika nyumbani na kupokewa kwa shangwe kubwa hasa ukizingatia anapokuwepo Miryam katika nyumba hio kila siku ni skukuu. Maana binti huyo kajaaliwa upendo wa hali ya juu sana kiasi kwamba wafanyakazi wote walikuwa wawazi katika kuongea nae, Ni mschana ambae hakujiona kwa uzuri wake na utajiri aliokuwa nao bali aliishi na watu wote kama sehemu ya familia yake. "Afadhali amerudi", "nakwambia huyu mtoto ni baraka ndani ya nyumba hii", "hata leo profesa aseme hana mshahara wa kutulipa basi mie nitafanya kazi bure ilimradi niwe karibu tu na Miryam". wafanyakazi wa kike hawakuwa nyuma katika kummwagia sifa binti huyo wa profesa maana aliuteka moyo wa kila mtu alikuwa ndani ya nyumba yao. 
Kutokana na machofu ya safari, Miryam alioga na kupumzika. Upande wa Alwin alikuwa hafahamu chochote kuhusiana na ujio wa Miryam na hata profesa alikubaliana na mwanae kuwa asimwambie chochote. 
Sasa kutokana na kilichoonekana kwenye kamera askari wote waliamini kama kuzuia mauaji hayo ni sawa na kuzuia mawimbi baharini. Kila asakri aliamua kushughulika na mambo yake pasi na kuwaza tena njia za kumkamata muuaji, walijisemea "muache auwe tutakwena kukusanya mizoga". Jestina akiwa chumbani kwa Alwin ghafla hali ya hewa ilibadilika ghafla na kutoweka bila yeye mwenyewe kutaka, funga fungua alijikuta yupo kule katika ulimwengu wa waliodhulumiwa. "karibu tena Jestina" aliongea yule malkia, "mbona umenirudisha huku wakati sijamaliza kazi yangu" aliongea akionekana kuchukia kidogo. "kuna jambo nataka nikueleze kwanza ndio utarudi tena katika ulimwengu wa kibinaadamu" baada kusikia hivo kidogo akapoa. "Muda wako wa kukaa huko unakaribia kuisha" aliongea malikia na kumshtuwa kidogo Jestina, "si umenambia muda wangu utakwisha mpaka pale nitakapo wamaliza wote" aliongea Jestina kwa sintofahamu. "ndio, ilikuwa iwe hivyo lakini muda si mrefu utaanza kukutana na kikwazo" alijibu malikia, "na hicho kikwazo kitakufanya upumgukiwe nguvu za kuishi katika ulimwengu wa kibinaadamu", "nambie ni kikwazo gani hicho nikakiondoe mapema" aliaongea Jestina huku akianza kubadilika kwa hasira. "hutoweza kukiondoa hata uwe na nguvu kiasi gani hata mimi pia sikuweza kukiondoa wakati wangu" alijibu malikia akionesha ugumu wa kukiondoa kikwazo hicho. "basi nambie kikwazo chenyewe ni kipi" aliomba sasa Jestina, "MIRYAM" malikia alijibu huku akitetemeka.




No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa