PETE YA KIKE Sehemu Ya 10 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Saturday, February 1, 2020

PETE YA KIKE Sehemu Ya 10





Na ni kweli,... Sasa maimati anakuja tena kwa kupaa, kwani alishajua kuwa kuna tatizo juu ya mtu ampendaye, lakini sasa mbaya zaidi aliokua na suria ni huyo malkia wao.. Sasa huku chumbani, murati Sabaha nae anashtuka kwa kuhisi kuna jini mwenzake anatumia nguvu za uhalisia wake,.. Wakati huo surian ndio anafika mshindo lakini Murati keshajitoa saa mingi sana katika mwili wa suria kana kwamba uchafu unaomtoka surian hautakiwi umguse jini yeyote na ndio mana mwanaume akiamka asubuhi, anakuta kajitandika bao la kisigino.. Sasa Murati anakuja kustuka anashangaa kuna jini mwenzie naye anakuja katika chumba hicho hicho... Murati akapotea na hapo hapo maimati anaingia, tena alikuja akiwa anaonekana live bila chenga.... Alimkuta surian anajikamua kumalizia utamu wake... Ndipo maimati akaamua ku...

ENDELEA........

Katika ulimwengu huu kuna viumbe vingi sana, lakini tukija katika ulimwengu wa majini, kuna aina 360 za majini, na hapo hapo kuna wazuri na wabaya.. Majini wabaya ndio hao mashetani wenyewe, ambao huwatakia wanaadamu kufanya mabaya na kuacha kutii amri za Mwenyezi Mungu,... Lakini pia wapo majini wazuri ambao wao hawapo kwa ajili ya kumfanyia kibaya binadamu wala wanyama... Yaani hao wapo kimsaada zaidi pale wanapo kupenda kuwa nao,... Na wapo majini wa kike walio olewa na binaadam, lakini ndoa hizi hua zinajulikana ni za kawaida, hivyo hakuna atakae jua kuwa mwanaume fulani kaoa jini, ila yeye mwenyewe ndio anajua kaoa jini au pia hata mume huenda asijue kama kaoa jini, mana majini yana uwezo wa kuwa kama binadamu na hata maisha Anaweza kuishi kama binadamu... Yaani kila anachokifanya binadamu hata jini Anaweza kukitekeleza vilevile, hivyo upo uwezekano wa mwanaume kuoa jini bila ya yeye kujua... Lakini katika majini hao kuna majini wenye asili mbili, kuna majini wenyewe ambao hawana asili mbili... Yaani baba na mama ni majini.... Sasa kuna wale majini ambao walioshiriki tendo la ndoa na binadamu.. Wale ndio walituletea majini ambao wana uwezo wa kubadilika kuwa kama binadamu wa kawaida na usijue mpaka kufa kwako.. Na mwisho wa siku wakipata watoto, jini huchukua watoto wake... Hivyo kukawa na jamii ya majini wenye asili mbili... Ambao majini hao wakiingia duniani huezi jua kama ni jini.. Kwani utamuona ni mvulana mzuri tu... Utamuona ni msichana mrembo na mwenye tabia njema... Na pia hakuna mipaka juu ya kufanya mapenzi pale utakapo amua... Tuchukue mfano wa wanyama na binadamu... Hapo hakuna mipaka ya kufanya mapenzi na mnyama, lakini hairuhusiwi kufanya lakini pia hapo hapo unaweza ukafanya kwa akili yako jinsi ilivyo kutuma kufanya mapenzi na mnyama lakini hairuhusiwi lakini pia hakuna mipaka, kwahio ni hivyohivyo hata kwa majini wanaotaka kufanya mapenzi na binadamu hua hakuna mipaka sema sasa mtu akijua kuwa huyu ni jini ndio hairuhusiwi lakini hakuna mipaka juu ya mapenzi, Ilimradi jini mwenyewe kakubali kulala na binadamu, hapo hakuna mipaka....

Lakini sasa hawa majini wenye asili moja wao hawana uwezo wa kuonekana kama binadamu pindi wawapo duniani,... Hivyo jini huyu akija duniani hawezi kuonekana... Na akionekana basi unaweza kumkuta ana mguu wa ng'ombe au farasi... Au ukamfunua katika sehemu za siri ukakuta hakuna njia, kote kuna nywele.... Kwasababu hana asili mbili, na wao wakitaka kuoana na binadamu, basi ni lazima binadamu akaishi katika falme za majini, kule ndio atakua kama binadamu, ila akija duniani atakua kituko.... Sasa na hawa wa asili mbili, wao wakitaka kuoana basi hawaruhusiwi kuishi katika falme za majini, hivyo wanatakiwa kuishi duniani na sio chini ya maji... Hivyo kwakua maimati alimpenda surian, hivyo hakutaka aje huku majini, kwani yeye maimati alikua tayari kwenda kuishi duniani kwa ajili ya surian....

Sasa huyu Murati sabaha yeye ni jini mwenye asili moja,.. Na happ alipo hajawahi kufanya mapenzi live, na ili aweze kufanya mpenzi live na jini mwenzie au binadamu, ni lazima wafunge ndoa kwanza.... Lakini jini Murati sabaha alishikwa na tamaa ya mapenzi na kumjia surian katika ndoto kisha akafanya nae tendo la ndoa, lakini hapo haikutoa bikra yake kwani ndoto sio kitu cha uhalisia... Na hua sio akili ya mwanaume kufanya mapenzi pasina kutumia akili yake....

Sasa kitendo hicho kilimkwaza sana maimati, kwani anampenda sana surian, sasa iweje awe anaingliwa kila wakati na Murati sabaha....

NDUGU WASOMAJI,... NIMETOA MAELEZO MENGI KWANI SITAKI KUKUACHA NA MASWALI MENGI JUU YA SIMULIZI HIII.... HIVYO TUENDELEEE

Maimati Alimkuta surian anajikamua kumalizia utamu wake... Ndipo maimati akaamua kuondoka katika himaya hio kwani asingeweza kugombana na mkuu wake,... Wakati huo surian anajiskia aibu kwani kuna mwanamke kamuona live akiwa anamalizia bao lake,... Hivyo alijiskia aibu hata siku hio hakutaka kutoka nje ili asije kuonana na maimati, na hapo surian hajui kama yupo katika falme za majini, bali anajua yupo dubai kikazi,.... Na hata hawezi jua nani kafanya nae tendo la ndoa katika nfoto kwani jini hapendi ajulikane hivyo akikujia hua anakuwekea taswira ya mwanamke yeyote yule, ili usijue wewe binadamu

Surian aliingia bafuni na kufua nguo zake, ila jini aliomwingilia sio jini mbaya.....

Maimati alimfuata shaimati na kumfokea sana kwani yeye ndio sababu ya surian kuja huku....
"sasa umefanya nini?... Umeleta mtu afanye kazi au aingiliwe na Sabaha"
Aliongea maimati huku shaimati akishangaa sana kuwa Murati sabaha kafanya jambo hilo ambalo hata wafuasi wake hawakuweza kulifikiri kabla...
"unasemaje"
"nakulaumu sana wewe... Nilikwambia, sitaki surian aje huku"
Aliongea maimati kisha akaruka na kupotea,... Kumbe huku huku falme ya majini kuna wazazi wa kila jini, hivyo maimati alikwenda kwao,... Ikumbukwe kuwa kuna himaya yao ambapo ndipo ufalmeni kwao.. Na pia kuna kwao ambako ndipo alipo zaliwa.... Na kule kwao jini ni mama yake, ila baba yake ni binadamu wa kawaida na mtoto waliopata ni huyo maimati na mwingine mdogo alie itwa zubinati (zubeda) ... Majini ya majini bwana lazima yaishie na neno (ti)... Maimati alilalamika sana kwa wazazi wake, lakini wazazi walimshauri, kama kampenda kijana huyo basi ampe pete yake ili imlinde mana hawezi kugombana na Murati sabaha...
"mamiii, pete ipo duniani"
Aliongea maimati huku mama yake akishangaa kuwa pete kaiacha dunia wakati walipo kwenda kutafuta kijakazi wa kiume,...
"unasemaje we maimati"
"ndio mamii, dada yake suria ndio kaivaa pete hio, na toka aivae hakuivua"
"akili zako haziko sawa muna... Unaachaje pete duniani"
"nitakwenda kuichukua mamii"
Alijibu maimati huku akilia kwani kitendo alicho kifanya Murati sabaha hakikumpendeza maimati....

Siku zilizidi kwenda, surian kila siku asubuhi yeye ni kufua nguo zake baada ya kuingiliwa na Murati sabaha, hata suria anajiuliza ana inakuwaje, mana Amezoea kuwa hali hio humjia kila mwezi au miezi kadhaa kwa mara moja.. Lakini mbona huku dubai anachafuka kila siku,... Anasoma dua ya kulalia kila siku lakini wapi,... Na dua hio haiwezi kuzuia kwani tayari upo katika himaya yao,... Sasa yapata mwezi mmoja toka surian kuja katika falme za majini, lakini bado hajajua kuwa hapo sio dubai... Maimati kila siku anashuhudia jinsi surian anavyo fanya mapenzi na Murati sabaha... Na mpaka hapo kalipwa jiwe la thamani kama mshahara wa kazi yake,... Kwa sasa maimati yupo karibu sana na surian na hapo suria bado hajui kama maimati anampenda,
"sasa hivi umezoea mazingira ya dubai"
Aliongea maimati huku suria akijibu kua
"ndio,... Sio mbaya sana"
Alijibu suria lakini huku akiona aibu mana maimati alishamkuta suria kama mara tatu hivi akimalizia utamu wa ndoto... Lakini maimati akiwa hapo, ghafla alipata ishara ya kuvuliwa kwa pete, Kiukweli alishtuka sana mpaka suria naye akashtuka kutokana na sauti za mshtuko alizo zitoa maimati
"mbona unanitisha dada maimuna"
Aliuliza suria huku maimati akiwa hamjibu na badala yake alizunguka nyuma ya nyumba kisha akatoweka katika mazingira ya kutatanisha...

Huku duniani, baada ya mwenzi mmoja kupita asha sasa anamiliki saluni kubwa,.... Sasa hapa ni kabla hajaivua pete,.. Kuna mteja aliokuwa akimuosha nywele baada ya kumpaka dawa zao wenyewe wanazijua... Sasa yule mteja alikuwa akilalamika kutokana na pete, kwani pete hio ilikua ikishika nywele za huyo dada hivyo kumsababishia maumivu wakati wa kuoshwa nywele, ndipo asha akadiliki kuvua pete hio na kuiweka pembeni... Hata kidole chake kilikua na alama ya pete kana kwamba pete hio haikuwahi kuvuliwa toka kuvaliwa kwake.... Sasa maimati yupo njiani kuja kuichukua pete hio mana hairuhusiwi kumpokonya ikiwa kidoleni, bali ni mpaka aivue

Huku nyumbani kwa akina faima,... Faima kwa sasa hakua akiuza duka la nguo tena kwani mawazo juu ya surian yalizidi hadi kufikia hatua ya kuikosa kazi yake, mana kila wakati ni yeye na mawazo tu...
"hivi faima... Huli, hulali... Kutwa kucha wewe ni mtu wa mawazo tu, hivi huyo suria ni mungu wako"
Alikua ni dada yake na faima ndio aliemwambia faima maneno hayo,..
"dada hujui tu, mimi naona uniache tu"
"siwezi kukuacha.... Umeshapoteza kazi yako nzuri tu, kisa mwanaume"
"dada ZAMINA, mbona unaongea sana... Mimi nampenda surian ndio mana sitaki akosekane moyoni mwangu"
Aliongea faima huku zamina akirudia kwa kubana pua
"eti nampenda staki akosekane moyoni mwangu... Kwa mwanaume gani, pamoja na elimu yake lakini kazi hapati... Akaona bora atoroke akaishi mbali na familia yake... Kama angelikua anakupenda hata simu si angekupigia?"
Aliongea zamina huku wazazi wao wakiwasikiliza tu, mana hata mama yake hapendi mapenzi ya surian na fsima kwani wanapotezeana muda tu

"asha atakuwa kamuua ndugu yake... Ona mjengo anao jenga"
Hao walikua ni marafiki wa asha, wale akina amina na Fatuma ambao hawaamini mafanikio ya asha yalikujaje na hata asha mwenyewe pia hajui kuwa pete hio ndio sababu ya mafanikio yake...
"heeee amina... Kamuuaje mdogo wake"
Alishangaa fatuma baada ya maneno ya amina kumtoka
"hivi wewe fatuma, huoni kabisa hizo ni pesa za haraka... Hebu ona ndani ya mwezi mmoja tu, saluni kubwaaa... Angalia ile nyumba anayo jenga pale bondeni, na ni mwezi mmoja tu"
"lakini kama kweli Fatuma, ila we umejuaje"
"kwani mimi si mtu mzima nimeweza kuchuja akili yangu"

Katika saluni ya asha, maimati ndio anaingia,... Wateja walikua wamevaa nguo fupi sana kuliko asha kwani asha alibadilika kutokana na pete hio,.. Maimati alichukua pete yake na kuondoka zake, kwani alikuja kama upepo tu, hakutaka kuonekana... Sasa ile asha anageuka haoni pete,
"hii pete imeenda wapi tena"
Aliuliza asha lakini hajui kuwa pete hio ina thamani gani katika mafanikio yake,..
"si uliiweka hapa"
"ndio, niliiweka hapa kwenye kioo, sasa mbona haipo"
"wewe niwashie mashine utaitafuta baadae"
Aliongea mteja wake aliokuwa tayari katumbukiza kichwa chake katika draya wanayoitumia kuseti nywele...
Sasa asha alijua ataiona tu, kwani haitokua mbali...

Ilipofika jioni wateja hakuna hata mmoja, asha alianza kuitafuta ile pete kwani aliipenda sana kutokana na urembo wake, na ilimpendeza sana katika kidole chake,... Aliitafuta sana lakini hakuweza kuipata.. Hivyo yeye aliipenda pete hio kwakua ilimpendeza sana...

Huku nyumbani kwa akina surian, wazazi wamesha kata tamaa juu ya ujio wa surian kwani ni mwezi sasa umepita toka surian kupotea...
Ghafla asha katokea hapo nyumbani,
"Shikamooni"
Alisalimia asha huku wazazi wakiitikia na kumuuliza
"asha mwanangu, hujasikia sikia hata fununu za ndugu yako huko"
Aliongea mama yake asha huku asha akigeuka
"mama,... Huyu mtu keshawatoroka tayari.... Alishapigiwa simu ya kazi anakwenda kulipwa milioni kumi,.. Aache kwenda kula na wanawake aje ale na nyie"
Aliongea asha, ikiwa ni maneno ya uongo kwasababu ile pete inayo kataza uongo, hana tena katika kidole chake....
"asha, mbona humpendi ndugu yako lakini"
"mama, sio kuwa simpendi.... Mumemsomesha elimu ya juu, mimi mkaniacha, sasa ndio nataka niwaonyeshe kuwa hata mtoto wa kike ana uwezo.... Nyumba inakwenda kuisha, tutahamia... Na hata yeye akija ataishi tu... Pamoja na elimu yake kuwa juu lakini haniwezi kimaendeleo"
Aliongea asha huku wazazi wakiwa kimya, mana kweli asha kaishia kidato cha nne tu,... Lakini mambo yake kwa sasa ni zaidi ya huyo aliesoma mpaka kumaliza maktaba nzima....

Sasa tukija huku kwenye falme ya majini,... Surian alikuwa katulia ndani ikiwa ni asubuhi baada ya kufua nguo,... Ikumbukwe kuwa kule duniani sasa ni jioni, lakini huku ni asubuhi... Na sasa suria keshazoea katika swala la ndoto za mapenzi.... Yaani mpaka sasa kateua mpaka nguo ya kulalia iwe hio hio.... Lakini akiwa kakaa hapo, mara Murati sabaha akaja mbele zake
"habari yako kijana"
Suria alishtuka na kusimama kwa heshima, mana huyo ndio malikia wa eneo hilo,... Na huyo ndie anaye mwingilia suria usiku, lakini suria hajui
"salama boss, Shikamoo"
"ahsante, ila unaonekana kuchoka sana... Njoo upate supu"
"hahaha hakuna shida boss"
sasa wakati huo huo, maimati naye anatokea
"usijali njoo utoe uchovu"
Aliongea Sabaha mana anajua kweli ana uchovu mana kila siku anamuingilia....
"hakuna tabu boss"
"sawa basi, na kama unajiskia uchovu... Pumzika ndani"
"ahsante boss"
Sabaha aliondoka kisha maimati naye akaingia,... Lakini sasa Murati Alianza kuwa na wasiwasi na maimati kwani yupo karibu na suria muda wote... Murati aliingia chumba kimoja hivi,.... Lakini sasa kumbe Murati sabaha naye kuna jambo alikua akilifanya ndani ya chumba hicho.... Ni chumba chake, na juu ya Meza yake palikua na pete ya kiume, na hio pete ilikua ni spesho kwa ajili ya surian,... Murati kaichukua pete ile ya kiume kisha akaja nayo pale alipo surian, na hata maimati bado yupo na surian, alafu maimati kaja kumpa surian pete ya kike, na Murati sabaha naye analeta pete yake ya kiume ili surian aivae... Sasa wote nia yao ni moja, kinachotakiwa ni pete ivaliwe na pete ya mmoja wapo ikivaliwa na suria, basi hakuna atakaye msogelea
"surian?.... Nina zawadi nataka nikupe leo"

Je? Nani kasema maneno hayo?? Na je? Pete ya nani itavaliwa na surian??












No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa