KITUMBUA CHA KIHINDI SEHEMU YA TANO (6) - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Wednesday, February 5, 2020

KITUMBUA CHA KIHINDI SEHEMU YA TANO (6)





ILIPOISHIA
Magosho alivuta pumzi kwa nguvu na kujinyoosha viungo vyake vya mwili na kuchomoa mkono wake kutoka kwenye hifadhi ya zana zake za kivita. Kisha akaendelea kuuchapa usingizi huku akiwa bado amelala chali. Kitendo cha kutoa mkono wake kiliweza kuruhusu umbo la silaha zake kuonekana kupitia kwenye kitambaa laini kilichotumika kuzisitiri.
            Mwanamke yule akajikuta akitetemeka hasa baada ya kuona umbile la vile vitu vya watu ambavyo havikumhusu. Akameza funda kubwa la mate lililosababishwa na tamaa za kimwili. Kwa muda ule mama yule alikuwa amekwisha pagawa na alikuwa tayari kwa lolote ilimradi auridhishe moyo wake.
Bi.Fahreen aliuinua mkono wake wa kuume na kuutazama kwa sekunde chache halafu akawa anaupeleka taratiibu kushika ghala la watu bila ya ruhusa kutoka kwa mwenyewe. Wakati anatua mkono ule akashituliwa na sauti ya mlango wa chumbani kwake ukifunguliwa. Kitendo cha kushituka kilisababisha mkono wake kutua juu ya zana za Magosho kwa nguvu bila kutegemea na kusababisha kijana yule aamke kwa mshituko mkubwa.
ENDELEA…6

“Shiiiiiiiii” Bi.Fahreen alimnyamazisha Magosho huku akiwa ameweka kidole mdomoni kumuashilia asipige kelele.
“Mama unafanya nini hapa!” macho yalimtoka Magosho na kuhoji kwa mshangao.
“Mume yangu iko piga mimi. Kama iko kuje ambie mimi hapana fika hapa?” alisema Bi.Fahreen huku akiingia kwenye kabati la nguo chafu za Magosho. Aliamini kuwa mlango uliokuwa ukifunguliwa ulikuwa ni wa chumbani kwao na Mr.Nakeshiwar alikuwa anamtafuta baada ya kuto muona chumbani. 
Magosho akawa katika mshangao mkubwa kutokana na kile kilichokuwa kikitokea chumbani kwake. Akatulia ili kuona ni kitu gani ambacho kilikuwa kinaendelea. Lakini muda ukapita pasipo kuona chochote. Bi.Fahreen naye alipoona kulikuwa kumetulia akatoka kule kabatini.
“Siku mema toto zuri” Bi.fahreen alisema na kutoka mle chumbani kwa Magosho huku akitetemeka kwa woga. Akanyanta hadi kwenye mlango wa chumbani kwao na kusimama kwa sekunde kadhaa kusikilizia. Alipoona kimya akaushika mlango na kuingia. Alimkuta mume wake amelala akiendelea na zoezi lake la kukoroma mithili ya mashine na kukobolea nafaka. Bi.Fahreen baada ya kufunga mlango alifanikiwa kupanda kitandani pasipo kugundulika. Alimsogelea zaidi mume wake na kumkumbatia ili kuicha dhambi aliyokuwa ametaka kuitenda.
****
Siku zilisogea na kusonga huku mawazo yakiwa yanamsonga Bi.Fahreen juu ya penzi la kijana Magosho. Siku zilivyozidi kusonga mbele ndivyo mwanamke yule wa kihindi alivyojiona akizidi kuchanganyikiwa na kijana yule.
Akiwa amejilaza kitandani huku mto ukiwa kifuani pake ameubana kwa nguvu alijikuta akiubusu mara kadhaa mto ule.
“Lazima pate ile toto zuri leo” Bi.Fahreen alijikuta akizungumza kwa sauti. Akapaza sauti na kumuita Magosho ambaye alikuwa jikoni akifanya usafi.
Magosho aliposikia sauti ya mke wa bosi wake aliwacha kazi na kumfuata. Alipofika kwenye mlango wa chumbani akasimama na kugonga taratibu na kwa unyenyekevu mkubwa. Sauti iliyotokea chumbani ilimruhusu aingie. Magosho akasita na kutamani kugoma kuingia lakini kwakuwa alikuwa ni mke wa bosi wake akaona angeonekana mjeuri. Kwa tahadhari kubwa alishika kitasa cha mlango ule na kusukuma mlango taratibu huku akiwa na wasiwasi moyoni mwake kama vile kibaka.
Magosho alimkuta Bi.Fahreen akiwa amejitandaza kitandani huku amejifunga kanga moja tu kifuani. Magosho akataka kurudi lakini akashituliwa na sauti ya mama yule.
            “Hapana gopa bhanaaa, veve kuje tu” alisema Bi.Fahreen huku akijiinua kutoka pale kwenye kitanda.
Mwanamke yule akajifanya kulikuwa na kitu anakwenda kuchukuwa kwenye kabati. Magosho akawa ametumbua macho kumuangalia mama yule jinsi ambavyo alikuwa akichezesha kwa makusudi ule mzigo wake aliobarikiwa na mola.
            Bi.Fahreen alikuwa akijitambua kuwa alikuwa amebarikiwa. Si kweli kwamba kulikuwa na kitu alichotaka kukichukua kwenye kabati, bali alikuwa akijitembelesha makusudi tu ili kumuonesha Magosho kwamba yaliyomo yalikuwemo kweli na wala hayakuwa yale ya mito na magodoro.
            Weupe wa ngozi ya mama yule ulizidi kung’aa ndani ya ile kanga aliyokuwa amejifunga kifuani na kupelekea miguu yake iliyokuwa imejazia vizuri kuonekana na mvuto mara mbili zaidi. Vijana wanasema mguu wa bia sijui mguu wa nini, Mnh! Haya bwana mie sijui. Magosho aliweza kubaini urembo wa mama yule ambaye alikuwa ameshawahiwa na kumilikiwa na Bwana Nakeshiwar.
            “Duh! Utadhani hakuwahi kuzaa!” alijisemea Magosho huku akiendelea kumtumbulia macho na kumthaminisha mama yule wa kihindi aliyekuwa akijitembelesha mbele ya macho yake kwa uchokozi kabisa.
Bi.Fahreen alipofika pale kabatini akajifanya kupekuwa pekuwa sehemu ya juu ya kabati. Kitendo kile cha kupekuapekua kilipelekea lile zigo lake kutikisika na kutetema kila alipokuwa akijitingisha. Magosho akajikuta akizidi kutoa macho kwa mshangao kijana wawatu na kusahau kabisa kama ile ilikuwa ni mali ya mwenyewe Mr. Nakeshiwar. Yani kama ungepata fursa ya kumuona kijana yule ungesema alikuwa ameona muujiza wa mazingaombwe.
            “Mnh! unaweza ukajikuta unatolewa roho na Nakeshiwar hivi hivi haki ya mungu!” Magosho akajisemea kimoyo moyo huku akihisi jogoo aliyekuwa amefungiwa bandani akiwika. Akapeleka mkono wake haraka sana na kumdaka koo kisha akambana kwa kamba ya lastiki.
            “Haya furukuta sasa” akamuambia jogoo wake kwa sauti ya chini kama vile alikuwa akizungumza na binadamu mwenzake.
            Bi.Fahreen akageuka na kushika kiuno huku akipumua kwa nguvu kama vile kitu alichokuwa akikitafuta alikuwa amekikosa. Magosho akainamisha macho chini kujifanya hakuwa akimuangalia mwanamke yule alipokuwa akileta mafindofindo pale kwenye kabati.
            “Gosoo” aliita Bi.Fahreen.
            “Naam mama” Magosho aliitika na kujianya kushituka kama vile kulikuwa na kitu mbalisana anakiwaza.
            “Mimi taka kupa veve kazi sawa?” Alizungumza Bi. Fahreen kwa
            “Sawa mama” Magosho alijibu na kukwepesha macho kutoka kwa Bi.Fahreen ambaye alikuwa akimtazama kwa jicho lililokuwa limechoka kuangalia.
Bi.Fahreen akakatiza mbele ya Magosho na kwenda kwenye kitanda, alipiga magoti kisha akainamisha kichwa kuchungulia chini ya uvungu.
            “Mama weeee!” Magosho alijikuta akihamaki huku ameweka mikono yake kinywani baada ya mama yule wa kihindi kuinama na kumuachia ule mzigo wake ukiwa umebinuka juu utafikiri breki ya katapila. Bi.Fahreen kama ilivyo kawaida yake, kule chini ya uvungu nako akawa anajitingisha na kufanya zigo kuelemea na kuwa kama vile  likitaka kudondoka.
            “Dah! Kwa kweli Nakeshiwar anafaidi” alisema Magosho kimoyo moyo huku akibana mapaja yake kwa nguvu angalau apate ahuweni kutokana na hali aliyokuwa akiisikia. Baada ya kuona kubana miguu hakumsaidii akapeleka mikono na kujiminya kwa nguvu maeneo ya Pwani ya Afrika Mashariki.
            “Bahati yake ni mke wa Bosi, vinginevyo leo ingefahamika” Magosho alijisemea huku akimeza funda la mate.
            Bi.Fahreen alitoka kule chini ya uvungu bila kitu chochote. Magosho alikuwa na hamu kubwa ya kutaka kukiona hicho alichokuwa akikitafuta mke wa bosi wake. Bi.Fahreen akasimama na kushika tena kiuno chake kuashiria kuwa alikuwa amechoka kutafuta kitu ambacho alikuwa hakioni. Akamtazama Magosho ambaye alikuwa amesimama huku mguu mmoja akiwa ameupitisha mbele ya mguu mwingine ili kuficha mke wa bosi wake asibaini kama alikuwa ameharibikiwa.
            “Sasa veve Goso iko simama tuu, hapana choka veve?” alihoji Bi.Fahreen.
            “Basi mama ngoja mimi niende, halafu utaniita” alisema Magosho huku akipepesa macho kukwepa kuangaliana na mwanamke yule.
            “No! kuje kae hapa kwa tanda yangu” alisema Bi.Fahreen.
Jamani jamani nyie duniani hapa kuna mambo! Sasa Magosho wawatu vilealivyokuwa ameharibikiwa halafu aende akaketi kitandani, ndugu msomaji mbona kama sielewi hivi kwa upande wangu Mnh! Kuna mtego na tego, sasa lile naona lilikuwa nit ego.
            “Hapana mama, ngoja nikae hapa kwenye kochi” alisema Magosho na kuelekea kuketi kwenye kochi lililokuwemo mle chumbani.
Bi.Fahreen akamtupia tabasamu la mahaba lililokuwa limepambwa vyema kwa lipsi zake pana zilizokuwa na wekundu wa asili.
            Mwanamke yule wa kihindi alirudi tena kabatini na kufungua mlango wa chini. Safari hii alitoa nguo kutoka kabatini na kwenda kuzirusha pale kwenye kochi alipokuwa ameketi Magosho. Jamani watu wengine wana vituko! Magosho alipoangalia vizuri nguo zile akabaini kuwa zilikuwa ni nguo za ndani tupu za mama yule. Kichwani akajawa na mshangao na maswali ambayo majibu yake hayakuweza kupatikana kwa wakati ule.
“Inamaana leo napewa nguo za ndani kufua? Hii sasa kali!” Magosho alijisemea kimoyo moyo huku akizitupia jicho la wizi nguo zile.
Bi.Fahreen akamsogele taratiibu huku akirembua yale macho yake. Safari hii alizidisha vituko kwa kijana wa watu ambaye alikuwa amemvumilia kwa muda mrefu. Alipeleka mikono yake na kumshika mabegani. Alitulia kwa sekunde kadhaa akimtazama usoni pasipo kuzungumza neon lolote. Magosho akawa akihangaika kuangalia pembeni kukwepa macho ya mama yule aliyekuwa akimletea mauzauza.
Bi.fahreen akainua mguu wake wa kushoto na kuuweka juu ya mapaja ya Magosho huku akiendelea kumtazama usoni mtoto wa mwanamke mwenzie. Magosho aligutuka baada ya kitendo kile alichofanyiwa na mke wa bosi wake.
“Mama!” alihamaki Magosho.
“Shiii! Mimi taka kupe kazi veve, iko situka nini sasa?” alihoji Bi.Fahreen huku viganja vya mikono yake vikipita pita kwenye shingo ya Magosho ambaye alikuwa ametulia baada ya kunyamazishwa na mama yule.
“Taka veve fua nguo hizo halafu kuje panga kwa kabati. Sawa?” alisema Bi.Fahreen huku ule mguu wake mmoja ukiwa bado kwenye mapaja ya Magosho. Kitendo cha kupandisha ule mguu wake pale kilipelekea ile khanga aliyokuwa amevaa kufunuka upande mmoja na kuzidi kuonesha sehemu kubwa ya mwili wake ambayo haikupaswa kuonekana na Magosho ama mtu mwingine yeyote zaidi na Mr. Nakeshiwar pekee.
Magosho alijikuta akitetemeka kutokana na vitendo vya mama yule mwenye asili ya kihindi. Bi.Fahreen akapeleka mkono wake na kufanikiwa kuzidaka zana zilizokuwa zimefichwa barabara. Magosho akashituka na kujikuta akizidi kutetemeka.
“Lakini mama…!” Magosho alizungumza kwa sauti iliyokuwa ikikwama kwama.
“Nini bhanaaa?...mimi taka onesa kitu veve” alizungumza Bi.Fahreen kwa sauti iliyotokea puani na kuzidi kumchanganya Magosho wawatu kaka wa Ashura.
Kiukweli Magosho alikuwa amepatikana mtoto wa watu wa marehemu mama Ashura. Kama ni ndege basi tungesema alikuwa ameingia mwenyewe kwenye tundu alilokuwa ametegewa na kilichobakia kilikuwa ni kuchinjwa tu na kuliwa.
Sauti ya viatu vya Mr. Nakeshiwar ilisikika ikigonga sakafu ya sebule ya nyumba ile. Bi.Fahreen pamoja na Magosho wakajikuta wakishituka baada ya kusikia vishindo vile. Walikuwa wamechanganyikiwa wasijue cha kufanya. Ilikuwa ni vigumu kwa mtu kutoka pasipo kuonekana. Hivyo walikuwa hawajui wafanye nini ili Mr. Nakeshiwar asiweze kumuona Magosho mle chumbani kwake.
“Naingia huku chooni” alisema Magosho huku akionekana kuchanganyikiwa.
“No! yeye penda ingia humo, kama iko toka kazini” alisema Bi.Fahreen huku akijaribu kuzunguusha macho kutafuta mahali ambapo angemficha Magosho. Mazingira ya chumbani mle ilikuwa ni vigumu kumficha mtu asionekane.
Vishindo vilikuwa vikikaribia kwa haraka kwenye mlango wa chumba kile. Vilipofika mlangoni kitasa cha mlango ule kilishikwa. Pasipo kusubiri chochote Magosho akaingia chooni kujificha ingawa aliambiwa kuwa Mr. yule huwa kila alipokuwa akitoka kazini alipendelea kuingia chooni. Mlango ulifunguliwa na Mr. Nakeshiwar akaingia.
Lilikuwa ni jambo la kuchekesha kama sio kusikitisha. Bi.Fahreen alishindwa kuficha wasiwasi wake kwa mume wake. Alikuwa akitetemeka utafikiri dereva wa trekta. Mr. Nakeshiwar akamtazama kwa jicho la tatu ili kuweza kubaini tatizo alilokuwa nalo mke wake.
“Vipi iko shida yoyote Fahreen?” alihoji Mr. Nakeshiwar
“No problem Darling. Kwanini today iko narudi mapema, any problem?” alihoji Bi.Fahreen huku akijibaraguza kukunja zile nguo zake zilizokuwa kwenye kochi.
            “I come for my files” (Nimefuata mafaili yangu) alisema Nakeshiwar huku akifungua droo ya kitanda na kupekua pekua. Baada ya sekunde kadhaa alionekana kuyapata na kuyatoa. Aliyaweka kitandani kisha akausogelea mlango wa chooni kama ilivyokuwa kawaida yake.
Bi.Fahreen akajikuta akiishiwa nguvu na kulegea huku akishindwa kujizuia kutetemeka. Nakeshiwar alishika kitasa cha mlango wa chooni na kumgeukia mke wake.
            “Leo iko problem” alisema Nakeshiwar akiwa amesimama sawa na mlango.
Kule chooni Magosho alijikuta akijikojolea kwa kitete alichokuwa nacho. Alisikia jinsi kitasa cha mlango ule wa chooni kilivyokamatwa barabara na Mr. Nakeshiwar. Akajikuta akiijutia nafsi yake kwa kukubali kuingia chumbani mle.
            “Masikini mimi ninahukumiwa bila hatia” alijisemea Magosho huku akiwa amejikunyata kwenye pembe ya choo kile kilichokuwa kidogo kiasi cha kukosa pa kujificha.
Magosho alikuwa akimhurumia sana mdogo wake Ashura ambaye angebakia mpweke baada ya kifo chake ambacho kingemkuta muda mfupi uliofuata baada ya kutiwa mikononi na baba yule wa kihindi.
Ghafla kitasa cha mlango ule kilinyongwa na mlango ukaanza kusukumwa ndani taratiibu. Masikini Kijana Maosho akahisi haja kubwa na ndoo zikikaribia kumtoka kwa pamoja. Ndugu msomaji nisikufiche, naandika hadi nahisi kutetemeka mwenyewe kwa tukio hili. Mnh! Mbona kasheshe.
TUKUTANE



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa