JE HAYA NI MAPENZI!! 92: - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Thursday, February 20, 2020

JE HAYA NI MAPENZI!! 92:





Kisha akamkumbatia Sabrina ila Sabrina bado
alimshangaa na kufanya Jeff ajaribu kujieleza kwani
alikuja kwa kushtukiza tena bila taarifa kamili.
Ila kabla Jeff hajajieleza, akashangaa kumuona
Sabrina akianguka na kuanza kutapatapa.
Ikabidi Jeff aite msaada ambapo mama Sabrina alitoka ndani kisha kuanza kusaidiana na Jeff cha kufanya.
Kwavile gari ya kukodi aliyopanda Jeff ilikuwa bado haijaondoka ikabidi waitumie gari hiyo kumuwaisha Sabrina hospitali.

Walifika hospitali na moja kwa moja Sabrina akapelekwa kwa daktari kwahiyo Jeff na mama Sabrina walitulia wakingoja majibu.
"Na wewe Jeff, kwanini unakuja kwa kushtukiza kiasi hiki? Kwanini hukusema kama unarudi?"
"Nilisema kama narudi ila tu sikusema kama narudi leo"
Ikabidi pale wampigie simu na Sakina na kumtaarifu kuwa wako hospitali.

Sakina alikuwa nyumbani kwake na kushangaa tu hadi kuongea peke yake,
"Yani huyu Jeff, hata kusema kuwa anarudi hakuna. Na huyu Sabrina kapatwa na nini jamani?"
Ikabidi ajiandae na kumuaga Dorry kisha kuelekea kwenye hospitali aliyoelekezwa na mtoto wake.

Dorry pale nyumbani baada ya Sakina kuondoka akaona wazi kuwa hali itakuwa mbaya sana pale ambapo Jeff atakuwa amerudi na mama yake, alichokifanya na yeye ni kuingia chumbani kwa Sakina na kuchukua kiasi fulani cha pesa kisha kupanga mizigo yake na kumuita dereva wa gari za kukodi kisha kuondoka mahali pale.

Sakina alifika hospitali na mtu wa kwanza kumuona alikuwa ni mwanae na kumkumbatia kwa shauku yote kisha kumuuliza kilichotokea.
Jeff akamueleza mama yake kama ilivyokuwa,
"Ila wewe Jeff una matatizo sana mwanangu loh! Yani wewe badala ufike kwenu kwanza ukaona ni vyema upite kwa bibi yako. Unaona sasa majanga uliyosababisha?"
"Mama, hii ni bahati mbaya tu na wala sikuwa na nia mbaya. Sabrina atapona, nilimkumbuka sana na ndiomana nikaanzia pale"
"Ulimkumbuka sana!! Yani ulimkumbuka kushinda mie mama yako? Wewe mtoto akili yako wewe loh!"
Akafika na mama Sabrina ikabidi waanze kuongelea hali ya Sabrina huku wakingoja majibu ya daktari kumuhusu Sabrina.

muda kidogo daktari akatoka na kitanda cha kubebea wagonjwa akiwa amebebwa Sabrina na kufanya wote waanze kufatilia kwa nyumba ambapo Sabrina alipelekwa moja kwa moja kwenye chumba kingine na wao kuzuiwa nje ya chumba hicho.
Kisha daktari akawafata pale nje na kuwauliza,
"Mume wa huyu dada yuko wapi?"
Pale nje wakatazamana kwa zamu na kumfanya mama Sabrina aulize,
"Kwani anaumwa nini jamani na mume wake wa nini?"
"Kwani yuko wapi? Kama mnaweza mpigieni simu aje."
Kisha daktari akaingia tena kwenye kile chumba na kuwafanya pale nje watazamane tu,
"Tutampata wapi Sam?"
Na muda huo akawasili baba wa Sabrina na kuwakuta wakijadiliana kuhusu kumpata Sam,
"Tumpigieni simu jamani, hakuna namna nyingine hapa"
"Mumpie simu nani?"
"Tunataka tumpigie simu Sam maana daktari amesema tumuite mume wa Sabrina"
"Sitaki kusikia huo upuuzi kabisa, mwacheni huyo Sam aendelee na miujinga yake. Msimuite hapa"
Baba wa Sabrina hakutaka kuelewa wala kutambua kuhusu huyo Sam kwani alienda kukaa tu kwenye moja wapo ya mabenchi pale hospitali na kuwaacha Sakina na mama Sabrina wakijadili ambapo nao waliamua kutoka nje ili wajue cha kufanya.

Jeff aliyekuwa kaganda pale pale, aliamua kujitoa muhanga na kumfata daktari kisha akamwambia kuwa yeye ndiye mume.
"Na mbona wakati naulizia hukujitaja? Haya twende"
Daktari akatoka kwenye chumba chake na kumpeleka kwenye chumba alichopelekwa Sabrina.
"Huyu mkeo kashikwa na kifafa cha uzazi ila kuna mengi yameingilia kati, mi ni daktari ila huwa naona mambo mengi sana. Nimemleta huku ili tumfanyie operesheni ili tuokoe maisha yake ila kuna kengele ha hatari imegonga kichwani mwangu kuwa kuna uwezekano wa kumpoteza mama na mtoto kwa muda mmoja. Sasa ninachokuomba ni wewe kuweka mkono wako wa kuume chini ya tumbo lake na uombe kuwa ajifungue vyema"
Jeff alishangaa haya mambo kuyakuta hospitali ila alifanya kile alichoelekezwa na daktari huyo.
Baada ya muda mfupi tu akamuona Sabrina akitulia kule kutapatapa kwani pale hospitali alifungwa mikono na miguu ili asiweze kuanguka na kuumiza kiumbe kilichopo tumboni.
Kisha daktari akamwambia tena Jeff akamshike Sabrina kwenye paji la uso ambapo Jeff akafanya kama alivyoelekezwa.
Muda kidogo Sabrina alirejewa na ufahamu na kuweza kujifungua kawaida kabisa.

Sakina na mama Sabrina walikuwa nje na kukubaliana kumpigia simu Sam ambapo walipiga sana ila simu yao haikupokelewa wala nini na kufanya wajadiliane kitu kingine cha kufanya ukizingatia baba wa Sabrina hakuwa na msaada nao kabisa.
Wakati wako pale nje, kuna manesi wawili wakapita wakizungumza,
"Yani huyu daktari ana mambo ya kishirikina sijapata kuona jamani loh!"
"Huyu ndio alivyo, mi nahisi kachanjiwa huyu"
"Ona sasa, yule mgonjwa mule tumemfunga tu eti hadi mume wake aje loh huyu daktari jamani mmh!"
"Na hapo asipokuja huyo mumewe hali itakuwa mbaya, yani huyu daktari bora angekuwa mganga wa kienyeji tu"
Wakaendelea na safari yao huku wakiongea tu.
Sakina na mama Sabrina wakahisi wazi kuwa anaeongelewa pale ni Sabrina tu.
Wakajikuta wakiangaliana bila ya majibu yoyote.
Kisha wakaulizana tena,
"Sasa tutafanyaje?"
"Hakuna namna hapa ila kwasababu Jeff yupo itabidi atusaidie"
"Atatusaidiaje?"
"Itabidi tumuombe akamuangalie Sam ofisini na nyumbani, akimpata aje nae"
Mama Sabrina akaona kuwa lile ni wazo jema na kuamua kwenda kumuangalia Jeff ili wamwambie wazo lao.
"Mungu atusaidie akubali jamani"
"Jeff hawezi kukataa hilo"
Walifika pale walipomuacha Jeff ila hawakumuona, ikabidi wamfate baba Sabrina na kumuuliza kwani alikuwa amekaa tu pale bila wasiwasi wowote.
"Eti Jeff yuko wapi?"
"Nilimuona anazunguka zunguka na daktari, sijui hata walipoishia"
"Kwahiyo hata hujamuuliza daktari kuhusu maendeleo ya mtoto wetu?"
"Kama kungekuwa na chochote angetuambia tu"
Mama Sabrina alimuangalia mumewe na kumuona kuwa ni mtu asiye na faida hapo.
Wakajaribu kupiga simu ya Jeff ila haikupatikana.

Muda kidogo wakamuona Jeff akitoka na kuwafuata, ila kabla hawajamwambia chochote akawapa taarifa njema ya kujifungua kwa Sabrina.
"Amejifungua mtoto wa kiume, tumepata dume sasa"
Wote walionekana kusahau habari ya kumuhusu Sam huku wakifurahia kujifungua kwa Sabrina.
Ilikuwa ni furaha sana kwao na walikuwa wanangoja sasa hitimisho la daktari kama atawaruhusu kuondoka na Sabrina wao.

Sam alikuwa nyumbani kwake muda huu, alishika simu yake sasa na kukuta ni wengi waliompigia ila aliamua kumpigia mmoja tu kati yao ambaye alikuwa ni Sia.
"Khabari Sam?"
"Nzuri tu, mambo vipi?"
"Poa, si ulisema kuwa unaishi Mbezi? Mi nipo hapa stendi, itakuwa ni vizuri kama ukija kunichukua hapa ili nipafahamu kwako"
Ikabidi Sam amuulize vizuri kisha kwenda kumchukua alipo.

Sam alifika stendi na kumkuta Sia kisha akaenda nae nyumbani kwake ambapo walijikuta wakiongea mambo mengi sana.
"Vipi Sam una mke?"
"Hiyo ni historia ndefu labda tuongelee mengine. Kwani wewe una mume?"
Sia hakujibu hilo swali bali aliweka stori zingine na kusahau hayo kabisa.
Jioni ilipoingia, Sam akaamua kuondoka pale na Sia kisha wakaenda hotelini kula halafu akamrudisha kwenye mitaa yao kisha akampa hela kidogo huku akimwambia kuwa ni ya vocha, kitendo hicho kilimtia ushawishi zaidi Sia na kujikuta akifurahi sana huku akisema,
"Hawa ndio wanaume sasa, sio mwanaume hata hela ya bodaboda hana. Huyu nimeenda kwake, kanipeleka kula hotelini na kanipa pesa, eti elfu hamsini ya vocha mmh akinipa ya nguo je itakuwaje? Uwiii msichana wake anafaidi sana, natamani niwe mimi"
Sia alifikiria sana na kutamani kumjua mwanamke wa Sam kwani aliona wazi kuwa atakuwa anapata raha sana ya kuwa na mwanaume kama Sam.

Sam alirudi nyumbani kwake na kujiuliza kuwa kwanini Sakina na mama Sabrina walikuwa wanampigia, akajipa jibu
"Watakuwa walitaka kuniambia habari za Sabrina tu, hata hakuna jipya hapa"
Ila alijifikiria kwa upande mwingine na kujiona na upweke sana kwa kumkosa huyo Sabrina.
Akafikiria sana hadi alipolala.

Hospitali nako wakawaambia ndugu wa Sabrina kuwa Sabrina ataruhusiwa kesho kwahiyo ikabidi warudi nyumbani kwanza ili wawahi kesho asubuhi.
Hakuna aliyejua kuwa Jeff ndiye aliyejifanya kuwa mume wa Sabrina kwani wote walikuwa wamefurahi juu ya habari ya kujifungua kwa Sabrina.

Kulipokucha, Sam alijikuta akiamka huku akiwa na mawazo sana.
Alijikuta akimfikiria Sabrina, akakumbuka jinsi ambavyo alikuwa akilala nae na kuamka nae, akamkumbuka mtoto wao.
"Cherry mwanangu, lazima atakuwa amenikumbuka sana baba yake."
Akapatwa na wazo la kwenda kumuona Sabrina ila aliamua kwenda ofisini kwake kwanza halafu ndio aende kwakina Sabrina.

Neema katika hali yake ya ugonjwa vilevile alijikuta akikumbuka mambo mengi sana na kumuomba Mungu amsamehe kwa yote aliyokosea.
Aisha alikuwa pembeni kama kawaida akimuhurumia ila leo alimuuliza,
"Dada, kwani yule mkaka anayekujaga hapa ndio shemeji?"
"Alikuwa, ila sio shemeji yako tena. Kwanza ni mume wa mtu yule. Usiku uliona kuna karatasi nachoma?"
"Nilikuona ndio ila sikuelewa ni kwanini ulikuwa unazichoma"
"Nilikuwa najutia mambo niliyoyafanya, ni mimi ndiye niliyemuachanisha yule mkaka na mkewe"
"Kivipi dada?"
"Ni historia ndefu, ila kwa kifupi ni kuwa nilimfanyia dawa kwa mganga amsahau mkewe. Sasa yale makaratasi niliyochoma jana ni baadhi ya masharti tu niliyopewa niyatunze na yule mganga. Sasa mimi nimeamua kuyachoma ili roho yangu ibaki nyeupe. Sitaki maumivu ya zaidi ya haya niliyonayo, hata kama nikifa basi nife kwa amani"
Aisha alimuonea huruma sana Neema kwa maneno yale.
"Pole sana dada yangu, ilimradi umetambua kosa basi jua kwamba Mungu naye atakusamehe dada yangu"
"Nashukuru sana Aisha, ila ipo siku nitakupa siri kubwa sana kuhusu yule mwanaume. Ila sio kwasasa, ngoja kwanza nikamilishe toba zangu"
Neema alihofia sana kusema kwani aliogopa kifo, alijua wazi kuwa akisema basi ataishia kama rafiki yake Rose kwahiyo akawa kimya katika kuitoa siri hiyo.

Sam nae alienda moja kwa moja ofisini kama alivyopanga na kuwakuta wafanyakazi wake pale kama kawaida.
Akaweka mambo sawa, kisha akawaaga na kutoka kwani mawazo yake kwa muda huo yalikuwa juu ya Sabrina na mtoto wao Cherry.
Wakati anatoka ofisini akamuona Sia akikatisha pale na kuamua kumuita, kisha wakasalimiana.
"Ndio unapofanyia kazi hapo?"
Huku akionyesha ile ofisi,
"Yeah, ndio ofisi yangu hiyo"
"Hongera sana, sasa unaenda wapi maana unaonekana kama unatoka!"
"Nataka nikamuone mke wangu kidogo"
"Kheee kumbe una mke? Mbona jana hukuniambia?"
"Nilikwambia ni stori kidogo, hata hivyo sijaonana nae kwa miezi kadhaa nashangaa leo nimejikuta nikimkumbuka sana"
Sia akajikuta akijawa na wivu sana moyoni mwake kwani alitamani Sam asingekuwa na mke yani angekuwa hajaoa ili aweze kumpata kirahisi ila hakuwa na jinsi zaidi ya kumtakia safari njema tu.
"Basi nitakupigia simu badae, nenda salama na umsalimie sana huyo mkeo"
"Nashukuru Sia"
Kisha Sam akaingia kwenye gari yake na kuondoka pale ofisini kwake.

Sakina alijikuta akimwambia Jeff upuuzi uliofanywa na Dorry jana yake,
"Huyu binti ni mpumbavu sana, yani kachukua na pesa zangu na kuondoka nazo"
"Hapo ndio utajifunza siku nyingine mama kuwa usipokee watu usiowajua hovyo"
"Nawe unanilaumu tu badala ya kunielekeza vizuri"
"Nitakuelekeza tu mama, ila ngoja tuwahi hospitali. Sabrina atakuwa mpweke saizi"
Sakina alimuangalia  mwanae na kujiuliza maswali ila hakupata jibu na kuamua kuondoka nae ile asubuhi kuelekea hospitali ambako walimkuta baba na mama Sabrina tayari wako pale.

Muda kidogo wakaruhusiwa na daktari kumuangalia Sabrina na kwenda naye nyumbani.
Kisha daktari akamwambia Jeff,
"Hapa sasa lazima uwe na uhakika kuwa ni mwanao maana asingekuwa wako lile zoezi lingebuma"
Jeff akamtazama daktari kwa jicho kama la kumkataza kwani alijua kuwa ataharibu.
Mama Sabrina naye akamtazama daktari na kumwambia,
"Tunashukuru sana dokta, umetusaidia sana"
"Msinishukuru mimi tu, mshukuruni na mumewe pia hapa"
Huku yule daktari akimtazama Jeff na kufanya wote wamtazame Jeff.

Itaendelea



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa