PETE YA KIKE Sehemu Ya 4 - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Saturday, February 1, 2020

PETE YA KIKE Sehemu Ya 4





"we fadhila, hebu Jieshim.. Ile pete anataka anipe mimi kwa njia hio.. Sasa wewe wataka kujua ili iweje"
"kwani wewe umekuja na pete wewe"
"si nimekwambia anataka anipe"
"lakini Mwanaidi... Mwalimu kaanza kazi leo.. Ushaanza kumtamani jamani"
"weeeee, najua hapa kuna mbwa mwitu, nikichelewa tu sina changu.. Si unakumbuka mwalimu Shabani.. Nilimpenda nikajifanya kuchelewaa.. Mpaka zaina akamchukua... Ina na hiyu nichelewe?? Hapana.. Wacha nikachukue Pete kama zawadi yangu toka kwake..."
"mmhhj haya mwaya"
"sio haya... Najua anaogopa kunipa mbele yenu mana kuna miaka 30 jela.. Hivyo ananipa kiujanja ujanja.. We si unaona hakuna aliotoka"
Aliongea Mwanaidi huku akinyanyuka kwenye meza yake kuelekea mbele ili kuchukua ile pete... Na wakati huo maimati anaangalia tu, Mwanaidi anavyokwenda kuchukua ile pete

ENDELEA.......

Suria ni mtoto wa pili katika familia ya mzee Rashidi, mtoto wa kwanza akiwa ni mwanamke mwenye jina ASHA, mzee Rashidi alipenda sana uzao wa kiume kwani ndio anajua unaweza kumsaidia,.. Suria alipendwa sana na baba yake, na baba yake akaamua kumsomesha suria kwa gharama zake zote,.. Mzee Rashidi alikua na mifugo lakini yote ilikwisha kwa kumsomesha suria,.. Asha hakuipata nafasi hio kwani baba alipenda kuendeleza upande mmoja, asha aliishia kidato cha nne lakini suria alizunguka Tanzania nzima kuhakikisha anapata ilemu ya juu isio na mfano... Mana vyuo vyote vikubwa vikubwa kasoma ili hali tu kudokoa dokoa hapa na pale..

Baada ya kuhitimu elimu yake yote, suria Anaanza kutafuta kazi ilio endana na elimu yake,.. Lakini anakutana na vikwazo vya hapa na pale katika hali ya kutafuta kazi...

Suria hakukata tamaa, aliendelea kitafuta kazi, hasa ile alio shauriwa na baba yake... Lakini kwa bahati nzuri, suria anapata msaada kutoka kwa kiumbe mwenye asili ya ujini...

Maimati aliweza kumsaidia suria mpaka kupata kazi, tena siku hio hio akaanza kazi rasmi... Lakini sasa maimati naye ni msichana na ana asili mbili, asili ya kibinadamu na asili ya ujini,.. Katika dunia hii hakuna binadamu wala kiumbe ambacho hakina hisia,... Sifa alizotaka murati sabaha, suria anazo lakini sasa mbaya zaidi hata maimati anataka mwanaume wa aina hio,... Hivyo moja kwa moja tujue jina maimati kampenda suria, na sio kampenda kwa niaba ya Murati sabaha,.. Bali kampenda yeye kama yeye...

Kwakua suria yupo ndani ya moyo wa maimati,.. Basi jini huyo aliweza kuvua pete yake ambayo ni PETE YA KIKE, kwani ina urembo wa kike, japo ni pete ya gharama kubwa... Mana ni dhahabu tupu... Pete hio ina kazi Nne pale binadamu anapo ivaa...

1). KUMLINDA BINADAMU ASIFUATWE NA SHETANI AU JINI MAHABA KWA NJIA YEYOTE ILE.... HIVYO UKIVAA HIO PETE, KAMA ULIKUA MALAYA UNASAHAU NA HUTOFANYA TENA KIPINDI UNAPO KUA NAYO....

2). BINADAMU ANAPOIVAA PETE HIO, HUMUONGEZEA RIZIKI KATIKA KAZI YAKE,... YAANI KAMA NI DUKANI, BASI WATEJA UTAWACHOKA MWENYEWE

3). BINADAMU ANAPOIVAA PETE HIO, HUMUONGOZA KUFANYA MAZURI TU... YAANI KAMA ULIKUA UNAZULUMU WATU, UKIIVAA HIO PETE HUWEZI KUZULUMU TENA.. LAKINI UKIIVUA UNARUDI KATIKA HALI YAKO ILE ILE YA UZULUMISHI

4). BINADAMU ANAPOIVAA PETE HIO, HAWEZI KUKUBALI KISHAWISHI KIBAYA CHA AINA YEYOTE ILE, YAANI KAMA KUNA MTU ANATAKA KUKUSHAWISHI KUFANYA JAMBO, BASI HUEZI KUKUBALI..

Sasa maimati kampa anampa suria pete kwa niaba ya wale wanaomtamani wasikubaliwe.... Afu pia anampa ili jini mahaba au shetani asiwezi kumsogelea pale anapo sahau kuomba dua,... Hivyo suria akiivaa hio pete, hakuna kibaya kitakacho mkuta yaani hata huyu maimati mwenyewe, hawezi kumwingilia kimwili katika ndoto mana wapo majini wema ambao nao huja usiku kwa wanaume wanao wapenda,... Hivyo hata yeye hatoweza kama akitaka kumjia katika ndoto...

Sasa maimati alipoirusha pete ile suria aliona, lakini kwakua ni pete ya kike, aliwaarifu wanafunzi wake kua kuna pete hapo chini hivyo alio idondosha aweze kupita mbele aichukue...

Ni shule ya sekondari inayosemekana kua na maadili mazuri, lakini kwa upande wa wasichana walikuepo ambao wanaweza kumtamani mwalimu wao, na hio ndio sababu kubwa ya maimati kutoa pete yake na kumpa suria... Fadhila na Mwanaidi wao walikua kipaumbele kumpenda suria, kitendo ambacho maimati alikasirika sana lakini hakuweza kuwafanya lolote...

Sasa Mwanaidi alipofika mbele, alishangaa haoni pete,... Hivyo akamuuliza mwalimu tena kwa upoleee wa taratibu sana...
"hensam ticha?.. Iko wapi hio pete"
Aliuliza Mwanaidi lakini suria alishangaa kuskia anaitwa hensam ticha,...
"umeniitaje"
Suria alimuuliza kwa sauti kubwa
"ticha, nimekuuliza taratibu, sasa mbona wapaza sauti hivyo"
Aliongea Mwanaidi tena huku akijinengua flani hivi,.. Suria akashangaa ina maana kaingia choo cha kike, kapata kazi lakini kazi ina mitihani mingine juu yake.. Na achana na wanafunzi wa sekondari ni hatari kwa visura vyao na makusudi yao pale wanapo amua...
"kama umeshachukua pete yako, rudi kaketi"
Aliongea suria, na Mwanaidi akatii amri ya mwalimu... Lakini Mwanaidi alihisi hakukua na pete ila ni Janja ya mwalimu ili amuone vizuri... Yaani Mwanaidi bado anajipa matumaini juu ya suria.. Na ni leo tu hata siku haijaisha... Sasa jiulize hio ni shule au balaa..

Maimati alitoka zake hapo shuleni baada ya kuona mambo ni shwari kwa upande wa suria... Alipotoka aliwasiliana na shaimati ambaye yeye shaimati yupo huku kwa faima

Sasa tukija huku kwa faima akiwa na shaimati,.. Na faima bado hajajua kuwa hapo anaongea na kiumbe cha aina gani... Shaimati alikua akimbembeleza faima ampe muelekea huyo jini alipo,... Lakini faima hakutaka kusema kwani anajua ataibiwa mpenzi wake, na mpaka sasa hatujui mpenzi wa faima ni nani...sasa shaimati baada ya kujua kuwa faima hataki kusema,.. Alianza kumuuliza qarena wa faima
"Qarena?"
"ndio"
"niambie anapoishi mchumba wa pacha wako"
"anaishi pongwe"
"nyumba namba ngapi"
"namba 40 majengo ya mkoloni"
Sasa papo hapo shaimati akiwa anazungumza na qarena,.. Aliweza kupata mawasiliano kutoka kwa maimati, hua wanasikilizana hata wakiwa umbali kiasi gani,.. Na hawatumii simu kama sisi binadamu, shaimati alisogea kwa pembeni ili faima asigundue, mana akimwona anaongea afu hana simu, itakuwa tabu

"shaimati"
Maimati aliita kisha shaimati akaitika
"yeeeeeeeeee"
"vipi, umefanikiwa kupata hata Msafi mmoja"
"kuna ambaye namfuatilia sasa hivi, ili niweze kumfahamu"
"wacha nije tumfuate wote"
"sawa, tukutane pongwe majengo ya mkoloni"
"sawa"
Shaimati alimfuata faima na kumwambia,..
"sawa umekataa kuniambia"
"ndio, mana sikuamini... Wewe ni mzuri, je ukienda kumteka mchumba wangu"
"siwezi.. Basi kwaheri"
Shaimati alimuaga faima kisha huyoo akaondoka zake,.. Alitoka hapo kwa mguu lakini alipofika mahali pa Kujificha aligeuka kuwa upepo na kupotea papo hapo,...

Jioni nyakati za saa kumi na moja, faima akiwa anapanga nguo ambazo ni mzigo ulio ingia sasa hivi, hivyi kachana beli kisha anazipanga... Hilo ni duka la ngu za Kiislamu tu, kama tunavyojua shamra shamra za mkoani tanga zilivyo za mavazi ya heshima, mana asilimia kubwa ya wanawake hupenda kuvalia hijabu, na wanaume huvaa kanzu... Faima akiwa bize ghafla alimuona mchumba wake akiwa na furaha sana...
"waoooooo, mume wa mie huyoo"
Aliongea faima kwa furaha kubwa mno, kwa kumwona mchumba wake, na mchumba mwenyewe sii mwingine bali ni suria...
"Assalam Aleykh mke wa mie"
Suria alimsalimia faima, huku wakiitana mke na mume kama vile wameona, na hio ni ishara ya lazima waoane,.. Na mpaka sasa kinacho mkwamisha suria kuoa ni kazi, mana kuona sii jambo la mzaha.. Kwanza mungu anasema, kama huna uwezo wa kumlisha mke basi usioe mpaka pale utakapo pata uwezo wa kumlisha mke,..
"waaleykh msalam, haz wangu"
Faima anampenda sana suria, yaan hapo kasahau mpaka kazi kwa kumuona suria alio mtembelea kwa nyakati hizo...
"sasa naona leo upo bize... Nikuache kidogo"
"hapana... Wewe ndie unaenifanya mimi kua bize... Surian, nakupenda sana sua wangu"
"nalijua hilo na kunipenda si tatizo tatizo dhumuni kutimia"
"heeee hilo lazima kwa uwezo wa Allah"
"kweli eee"
"yes.... Afu Surian,.. Mbona leo kama una raha hivi, niambie Tufurahi sote"
Aliuliza faima huku suria akitabasamu na kusema...
"mwenyezi Mungu kaniwekea mkono wake... Nimepata kazi ya ualimu"
Aliongea Suria huku faima akitabasamu mno kwa furaha
"waooooo... Surian mpenzi wangu.. Sasa naona ndoa yetu hiiooo imefika"
Aliongea faima huku akizidi kumkumbatia suria,..
"hata mimi naona inakaribia.... Lakini?"
"lakini nini tena haz wangu"
"wale wanafunzi hawana maadili.... Kuna mwanafunzi kaniita hensam ticha... Kiukweli wananipa mitihani"
Aliongea suria na faima akajua tu, wanafunzi wamesha anza kumtamani Surian wake.... Lakini faima hakuogopa hilo, tena alizidi kumpa nguvu
"haz (Husband) wangu.. Najua uzuri wako umekua tabu kwa wasichana wengi hasa hasa mimi... Lakini hebu nikuulize... Toka umezaliwa, humjui mwanamke,.. Umediriki mpaka kuachana na mpenzi wako wa zamani aliokua anakufosi kufanya mapenzi, ukamuacha.. Umezunguka vyuo vingapi hapa Tanzania?.. Umeona wazuri wangapi huko vyuoni?"

"wengi tu"
"sasa iweje leo utikiswe na watoto wa juzi tu"
Aliongea faima (fey) kama kumtia nguvu asiache hio kazi
"unajua nimeshangaa kua.. Shule inasifika kua na maadili, iweje wanafunzi wanze tamaa kwa walimu zao"
"nakuomba sana haz wangu.. Usiache hio kazi.. Jitahidi kuwakwepa na uwaambie ukweli ikiwezekana nenda kashtaki kwa walimu wengine"
"mmmhhh Kiukweli nitavumilia lakini vikinishinda naacha"
Aliongea suria mana hapendi kufanya kazi huku akitegwa,... Acha na tabia ya mwanafunzi pale anapo amua kufanya jambo lake,... Basi kwakua ni jioni suria alimuaga faima anaelekea nyumbani
"chukua basi hii weka mfukoni"
Faima alimpa suria elfu kumi na tano,
"faima.. Kila siku unanipa.. Hii imezidi sasa.. Fanya kazi jiwekee fedha zako kulingana na kazi yako... Mimi bado nipo nyumbani"
Aliongea suria huku faima naye akiongea
"kwani mimi naishi peke yangu?.. Hata mimi naishi kwetu.. Nimeshakupa na nitakupa na sintochoka kukupa.."
Aliongea faima kisha akaingia ndani kuendelea na kazi...

Sasa huku mtaani kwa akina suria.. Maimati na shaimati wapo katika mti mmoja, wakimsubiria kijana mwenye sifa anazo zitaka Murati sabaha... Lakini sasa maimati yeye hajui kama wanae mtega ndio yule aliomsadia kupata kazi, na nzuri zaidi tayari yupo moyoni mwake... Shaimati nae yeye kapata muelekea kuwa mtaa huo una kijana ambaye wanamtafuta.. Sasa wamekuja kuweka kambi kwenye mti mmoja hivi.. Ila walikua wakionekana na kila mtu, lakini hata uwaone huezi jua kama ni majini.. Sasa shaimati yeye anaangalia nyumba namba 40, mana yeye ndie anajua kijana huyo anaishi nyumba namba ngapi...

Punde sii punde suria akiwa anaendesha baiskeli yake kurudi nyumbani,... Sasa maimati ndio anamuona suria,..
"kumbe huyu mwanaume Msafi anaishi huku"
Alijiuliza maimati, japo hajui kua ndio mtu wanaye msubiria hapo... Mara shaimati akanyanyuka na kusema
"yeeeeeee, itakua ni yule"
Aliongea shaimati, lakini maimati alimshika shaimati mkono kua waondoke waachane na huyo mtu
"maimati mbona sikuelewi lakini"
"huyo kijana ni mchafu achana nae"
Aliongea maimati ili shaimati aachane na suria...
"hapana, niache niongee na qarena wake"
Aliongea shaimati huku maimati akikasirika sana..
"shaimatiiiiiiiii...."
Maimati alimuita mwenzie kwa hasira, mpaka shaimati akashangaa leo ndugu yake ana nini....
"wewe, mbona leo sikuelewi?... Hii ndio kazi tuliotumwa huku duniani... Leo nataka nimjue kama ana sifa.. Afu wewe hutaki una maana gani"
Aliuliza shaimati na kuachana na suria.. Wakati huo suria keshaingia kwao...
"ni kweli shaimati... Huyo mwanaume ni Msafi, ila nilisha mwona tokea asubuhi.... Ana sifa zote za kuishi ndani ya himaya yetu... Lakini sifa alizonazo huyo mwanaume, hata mimi nazitaka... Hivyo sipo tayari nimpeleke kwa murati sabaha... Tafadhali sana shaimati... Naomba tutafute MWANAUME MSAFI mwingine, ila sio Surian"
Aliongea maimati tena kwa kumuomba shaimati
"maimati, hivi una akili wewe... Hivi umejisahau kuwa upoje... Yule ni binadamu na wewe ni jini... Inawezekanaje kwa hilo"
"nikifuata taratibu zote.. Naweza kuwa nae"
"hata kama... Lakini huyu mwanaume ni lazima afike kwenye himaya ya Murati sabaha... Na nitampeleka mimi kama wewe hutaki"
"sasa tutaona... Mimi na wewe nani zaidi.... Surian haendi popote"

Itaendelea...............






No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa