Ishara 10 za mwanamke anayejitambua - UHONDO KITANDANI

Hot

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa

Monday, February 17, 2020

Ishara 10 za mwanamke anayejitambua


1. Wanaume huchagua wanawake kama vile mtu anachagua yeboyebo zilizotandazwa chini sokoni na kwa mwanaume yeyote ataokota tu zile ambazo ziko karibu yake wakati mwingine hata kama hazimtoshi. Lakini kwa mwanamke anayejitambua na anayejua thamani yake atakuwa sawa na kiatu kizuri ambacho kimetundikwa dukani juu kabisa tena kwenye duka la kioo ambacho hakipatwi hata na vumbi. Anajua thamani yake hivyo atamfanya mwanaume amhangaikie kumfuata dukani na kumchagua kwa heshima, hata jirahisisha na kuruhusu kutandazwa tandazwa chini. 
2. Mwanamke anayejitambua anapaswa kujua kuwa mahusiano yanachangamoto lakini angalau asilimia 8o ya muda wenu muutumie mkifanya mambo yakuwapa furaha, kama mnatumia zaidi ya asilimia ishirini ya muda wenu kugombana basi jua uhusiano wenu hauendi popote, jitathimini kama unamhitaji huyo mtu au la? 
3. Mwanamke anayejitambua hujipenda yeye mwenyewe kwanza kabla ya kumpenda mwanaume, hii ni kutokana na ukweli kuwa, kama hujipendi hata kama ukipendwa vipi huwezi furahia upendo huo. 
4. Mwanamke anayejitambua anajua pia ni kitu gani anakitaka kwa mwanaume na anahakikisha anakipata. Kama hujui unachokitaka kwake hata ukikipata bado utajihisi hujakamilika, hembu jiulize sasa unataka nini kwenye mahusiano uliyonayo sasa. 
5. Mwanamke anayejitambua halinganishi mahusiano yake ya sasa na yazamani, au mahusiano yake na mahusiano ya rafiki yake. Huamua kuwa na furaha sasa bila kujali huko nyuma maisha yalikuwaje, husahau yaliyopita na hahangaishwi na mambo yanayofanywa na wengine. 
6. Mwanamke anayejitambua huchagua aina ya mwaname anayemtaka na si kuchukua tu kila mwanaume kwakuwa tu ni mpweke au anahisi umri umeenda. 
7. Mwanamke anayejitambua hujitoa kimwili kwa mwanaume pale anapohisi kuwa yuko tayari kufanya hivyo na si kwakuwa anaogopa kumpoteza mwanaume, kwani anajua thamani yake na anajua kama mwanaume anamthamini basi hatajali sana kuhusu ngono bali ataangalia upendo wa kweli. 
8. Mwanamke anayejitambua anafahamu kuwa mwanaume si Baba yake, Kaka yake au Bosi wake bali ni rafiki yake, hivyo atamheshimu lakini hatamuogopa na yuko tayari kuongea kuhusu hisia zake. Kwakuwa anajua anachokitaka atamuambia mwenza wake na kwakuwa ni marafiki basi kila mmoja atakuwa huru na mwenzake. 
9. Mwanamke anayejitambua anajua kuwa mapenzi si maisha yake bali ni sehemu tu ya maisha yake, hawezi kusumbuliwa na mwanaume kwakua tu anapenda kwani anajua yuko imara vyakutosha kuvumilia upuuzi wa mwanaume yeyote. Ameiweka mbele furaha yaake kuliko ya watu wengine na anapoona hapati anachokitaka basi hujitoa mara moja kwenye aina hiyo ya mahusiano. 
10. Mwanamke anayejitambua hawezi kupigania mwanaume kwani anafahamu kuwa mwanaume hachungwi na kama mwanaume anampenda basi hawezi kuhangaika hangaika na wengine. Anafahamu kuwa mwanaume anachepuka kwakuwa anataka na si sababu ya mwanamke mwingine hivyo basi humaliza mambo yake na mwanaume wake na hapotezi muda wake kugombana na mwanamke mwingine kwaajili ya mwanaume





No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

https://play.google.com/store/apps/details?id=chumba.cha.wakubwa